Ubahili kwenye ndoa

carmel

JF-Expert Member
Aug 24, 2009
2,836
262
...........Najua hii mada ishaongelewa sana hapa JF hata kama siyo direct kama navyotaka kuipresent case niliyoipata hivi karibuni! Kuna mdada kaolewa ana kama miaka mitatu kwenye ndoa sasa, anasema mumewe ni bahili sana kutoa matumizi ya kawaida kwa mkewe, hajawahi hata kumnunulia nguo wala kiatu, wala zawadi ya birthday wala anniversary! eti hata outing ni za manati sana na kwamba siku za kwanza jamaa hata pesa za mahitaji ya home alikuwa anabana sana akitegea mkewe atoe. Dem akashtuka akaona hatendewi haki akatia mgomo bariri kwenye hilo. Ila life yake yuko upset every time, anadai haoni umuhimu wa kuolewa kama anachoshare na mumewe ni kitanda lakini mahitaji yake yeye, shida zake na worries zake zote mumewe hataki kuhusika. Hata hajui mumuwe ana plan gani katika maisha maana yuko kivyake sana. Kinachomuumiza ni kwamba si kwamba hubby wake huyo hana pesa, ana kazi nzuri tu na analipwa vizuri sana, na akaunti zake (anadai anazionaga ki bahati mbaya) zina salio la kutosha tu. Ila ni bahili!
Sasa kwa wenye ndoa, waume kwa wake toeni views zenu, is it fair? I mean, inakuwaje unaoa mke hata kama ana kazi wewe unajitoa kabisa kwenye ishu zinazomhusu mkeo? Mimi ni ardent believer wa kusaidiana between mke na mume but does this allow mume ajitoe kabisa?
Hebu toeni experience tofauti hapa tupate mwafaka wa kila upande, kiumeni na kikeni!:rolleyes:
 
...........Dem akashtuka akaona hatendewi haki akatia mgomo bariri kwenye hilo. !:rolleyes:

Hivi Carmel huu ndo mgomo gani jamani?
Na nyie wanawake jifunzeni kujitegemea sio kila kitu unamtegemea mwanaume akufanyie.
 
eeeeh jamani huyo mwanaume ana matatizo ya kisaikolojia hivi haoni hata bible imeandikwa enyi wanaume watunzeni wake zenu na enyi wanawake wapendeni waume zenu..hayo maneno yana utofauti kabisa ingawa sometimez tunasaidiana kukidhi maisha
Huyu dada hatakiwi kukaa kimya kwani tatizo litakuwa sugu na atakapoamua kusema itakuwa too late ..itabidi amuite mme wake na aongelee hayo yanayomkwaza ili wapate muafaka amwambie mmewe vile anavyojisikia na anaona kama hatendewi haki
Kuna watu wengine wanafumbuliwa macho kwa kuambia..Je anamuogopa mme wake ???????
 
eeeeh jamani huyo mwanaume ana matatizo ya kisaikolojia hivi haoni hata bible imeandikwa enyi wanaume watunzeni wake zenu na enyi wanawake wapendeni waume zenu..

Endeleeni kutegemea waume zenu bila kujishughulisha akifilisika familia inateteleka na wengi wenu ndo hapa napo wachukia wanawake ukisha fulia tu basi mwanaume unakimbiwa na mke na ndo kama ni mzuri basi inakuwa balaa anahamia kwa wenye fweza wewe unabaki kukomaa sura tu.
 
eeeeh jamani huyo mwanaume ana matatizo ya kisaikolojia hivi haoni hata bible imeandikwa enyi wanaume watunzeni wake zenu na enyi wanawake wapendeni waume zenu..hayo maneno yana utofauti kabisa ingawa sometimez tunasaidiana kukidhi maisha
Huyu dada hatakiwi kukaa kimya kwani tatizo litakuwa sugu na atakapoamua kusema itakuwa too late ..itabidi amuite mme wake na aongelee hayo yanayomkwaza ili wapate muafaka amwambie mmewe vile anavyojisikia na anaona kama hatendewi haki
Kuna watu wengine wanafumbuliwa macho kwa kuambia..Je anamuogopa mme wake ???????
Sijui kama anamuogopa mwenzie au ni nini, ila mimi hainiingii akilini kabisa yani. ni kweli mwanaume ukimzoeza tu imekula kwako, ila hii kesi naona iko to the extreme jamani.
 
Ndio ubahili unaozungumziwa hapa. Ubahili si kwenye pesa tu hata kwenye huduma! Unapoacha kutoa huduma badala yake unatoa talaka, nayo ni sehemu ya ubahili. LOL!
ha ha haaa binamu bwana, lakini unadhani anavyofanya mwenzenu ni sawa?
 
Hata ambao hawajaoa si wana maGF/BF? na hata walioach/achwa wanayo opinion i gues

Duh sasa mm nilikuwa natoa 70,000/= kwa wiki huduma ya nywele bado naambiwa bahili unaichukuliaje hili? Maana nilikuwa najinyima kunywa Safari nikawa nakunywa Bingwa ili kumfurahisha yeye lakini nimeambulia patupu.
 
Sijui kama anamuogopa mwenzie au ni nini, ila mimi hainiingii akilini kabisa yani. ni kweli mwanaume ukimzoeza tu imekula kwako, ila hii kesi naona iko to the extreme jamani.

Hivi kama ni mmeo Carmel utasema kumzoea inabidi muwe marafiki hapo ndo utaweza kujiexpress mwenye lakini ukimchukulia kama kituo cha police iko kazi
 
...........Najua hii mada ishaongelewa sana hapa JF hata kama siyo direct kama navyotaka kuipresent case niliyoipata hivi karibuni! Kuna mdada kaolewa ana kama miaka mitatu kwenye ndoa sasa, anasema mumewe ni bahili sana kutoa matumizi ya kawaida kwa mkewe, hajawahi hata kumnunulia nguo wala kiatu, wala zawadi ya birthday wala anniversary! eti hata outing ni za manati sana na kwamba siku za kwanza jamaa hata pesa za mahitaji ya home alikuwa anabana sana akitegea mkewe atoe. Dem akashtuka akaona hatendewi haki akatia mgomo bariri kwenye hilo. Ila life yake yuko upset every time, anadai haoni umuhimu wa kuolewa kama anachoshare na mumewe ni kitanda lakini mahitaji yake yeye, shida zake na worries zake zote mumewe hataki kuhusika. Hata hajui mumuwe ana plan gani katika maisha maana yuko kivyake sana. Kinachomuumiza ni kwamba si kwamba hubby wake huyo hana pesa, ana kazi nzuri tu na analipwa vizuri sana, na akaunti zake (anadai anazionaga ki bahati mbaya) zina salio la kutosha tu. Ila ni bahili!
Sasa kwa wenye ndoa, waume kwa wake toeni views zenu, is it fair? I mean, inakuwaje unaoa mke hata kama ana kazi wewe unajitoa kabisa kwenye ishu zinazomhusu mkeo? Mimi ni ardent believer wa kusaidiana between mke na mume but does this allow mume ajitoe kabisa?
Hebu toeni experience tofauti hapa tupate mwafaka wa kila upande, kiumeni na kikeni!:rolleyes:


hapo kwenye red jamani sio asubirie atolewe outing tu, na yeye ajitoe mwenyewe pia, kama mie mr kusema ile outing kivile sio sana ni mara moja moja,sasa ninapoona naboreka tu kwanini nicjitoe mwenyewe na wakati huo yeye yupo kwenye stuli ndefu na ma frnds zake?...hapo kwenye blue mie nasemaga hata acponihudumia mie kama mie, yaani zawadi cjui na nini lakini kwa mambo ya familia(huduma za familia) acjaribu kuyumbisha, afanye yote huduma kwa wanae hasa c jambo la kuuliza, mie nitajifanyia mwenyewe kama hajickii kunifanyia.....huyo mdada ambane huyo mr wake kwenye huduma za ki familia yeye kama anaona vipi ajihudumie mwenyewe tu jamani na haya mambo ya kuachiana huduma za kifamilia sio kabisa, kwanini amuachie mama na yeye anaweza? mnawaendekezaga kuanzia mwanzo matokeo yake ndio haya.
 
U know what i dont understand about ladies is 1 thing,if u have a job and ur getting paid what financial assistance do you need????kama kila ki2 in the house your provided with,unataka nini tena????apart from that,kama unataka upewe assistance then what is your salary for???? Msaada always upo,but strictly kwa mambo muhimu,co unadai hadi hela za kuendea saluni..............
 
Ulijaribu kumwuliza huyo dada kabla ya kuoana huyo kaka alikua na hizo tabia au zimeanza baada ya kuoana?maana inawezekana hata wakati wa uchumba labda alikua hampi kitu chochote hata aouting hazikuwepo na mdada aliridhika kabisa,sasa inakuwaje waingie kwenye ndoa aanze kulalamika,mwulize vizuri hizo huduma kabla hawajaoana zilikuwepo? maana isije kuwa analilia kitu ambacho hata kabla hakikuwepo.
 
kwa wale ambao hamjaoa, mtahangaika enz ya uchumba kutafuta kiwanja na process nzima mpaka nyumba kuisha then mtasema kweli uhusiano wetu ni wa maana tuoane sasa, mkishaoana tu ile nyumba utaambiwa si yenu tena ila ya kwake mwanamke na atakuambia ukitaka tuachane hata sasa hivi!,number 2 hata ukijitahidi kujibana mkeo apate elimu zaidi au gari yake binafsi kwa asilimia 85 mbona utakoma hapo baadae, akipata cheo au fedha zaidi ndio utajuta kuzaliwa (i stand to be corrected) sasa ufanye nini? OMBA KILA SIKU MUNGU AWAPE UELEWA NA BUSARA KUBWA NA ZINGATIA YALIYOANDIKWA KWAMBA UNATAKIWA KUISHI NA MWANAMKE KWA AKILI!! and no 3 kuhusu ubahili si kawaida kwa mwanaume kukataa kutoa matumizi ya nyumbani kwake lazima kuna tatizo kubwa KAA NAE CHINI ASEME!!
 
mumewe ni bahili sana kutoa matumizi ya kawaida kwa mkewe[/COLOR], hajawahi hata kumnunulia nguo wala kiatu, wala zawadi ya birthday wala anniversary! eti hata outing ni za manati sana na kwamba siku za kwanza jamaa hata pesa za mahitaji ya home alikuwa anabana sana akitegea mkewe atoe. Dem akashtuka akaona hatendewi haki akatia mgomo bariri kwenye hilo. Ila life yake yuko upset every time, anadai haoni umuhimu wa kuolewa kama anachoshare na mumewe ni kitanda lakini mahitaji yake yeye, shida zake na worries zake zote mumewe hataki kuhusika. Hata hajui mumuwe ana plan gani katika maisha maana yuko kivyake sana.

Nguo, birthday, anniversary,outing!!! Yaani, hizi ndio ameona priority kwenye ndoa yao? Yeye amewahi kumfanyia nini mumewe hata kwa hicho kidogo anachokipata? Upendo ni kutoa zaidi ya kusubiri kupokea!
 
Back
Top Bottom