Ubadhirifu mkubwa Benki ya Posta

Ndivyo ilivyo kwa mashirika ya Umma kutumiwa kwa masilahi ya wanasiasa na marafiki zao. Mfano mwingine ni TANESCO.

Ili Watanzania waweze kupona kuna umuhimu mkubwa sana kwa haya mashirika ya umma yawe na uwazi mkubwa sana. Nadhani usiri mkubwa sana katika shughuli za haya mashirika ya Umma ndio tatizo kubwa sana, ambapo wanasiasa na mafisadi wenzao wanatumia kwa manufaa yao.

Hatuna haja ya kuuza mashirika yetu eti tumeshindwa kuyaongoza. Mazingira ya mashirika ya umma ndo yanatakiwa kubadilishwa, hasa hasa kwenye kuripoti shughuli zake kwa jamii ikiwa ni pamoja na mahesabu yake.

Tunaweza kuiga uwazi uliopo kwenye mashirika yaliyokuwa listed kwenye masoko ya hisa, kwamba pamoja na wale viongozi wa mashirika kuongoza mali zisizo zao, zinazomilikiwa na umma (general public), lakini sheria zimewekwa kusaidia kuyaongoza mashirika hayo kwa ufanisi na pia kuepusha wizi na ubadhirifu unaoweza kufanywa na viongozi.

Mimi nadhani hilo ndo litakuwa moja ya suluhisho kubwa la matatizo ya mashirika yetu ya umma.

Wenye ufumbuzi mwingine tafadhali tuchangie.....
 
Hii ndio Danganyika bwana,nchi ambayo ufisadi na embezzlement ni sehemu ya maisha
 
Kajula sasa anatesa NMB na huko wakizinduka atakua amewalamba kama alivyofanya, CRDB na Postal Bank
 
Huu ni wakati muafaka kabisa wa hii habari kuwa kwenye front pages za nyumbani wakati uchunguzi wa kina ukiendelea hapa.

Serikali ya Kikwete ni dhaifu mno na imegubikwa na ufisadi na sidhani kama kuna lolote hapa litafanyika..... aibu kabisa kwa ccm na serikali yake
 
..hivi bado kuna mashirika ya umma kama haya? kumaliza wizi wizi kama huu ni kuyauza tuu.
 
kwanza wangeiacha hii bank ijitegemee coz itakua na unfair advantage kwenye industry.hii kitu kua chini ya serikali ndo inachangia sana wizi.watu wanakua na confidence za kujichotea mihela, isingekua serikalini sidhani ka kihwele angekua na power namna hiyo hata ya ku-intimidate kufanya mchezo wa primary(kumpigia kura aliyeiba kompasi)
 
Hili nalo inaonekana linahitaji kuundiwa tume.

Tanzania inaliwa na wenye meno.... yego masatu aliwahi kusema kuwa Tanzania ni shamba la bibi... kazi kweli kweli!
 
Hili nalo inaonekana linahitaji kuundiwa tume.

Tanzania inaliwa na wenye meno.... yego masatu aliwahi kusema kuwa Tanzania ni shamba la bibi... kazi kweli kweli!
Tatizo ni pale itakapoundwa tume ya 'kishkaji' na ikawabeba watuhumiwa.

Believe me or not; baadhi ya tume zinazoundwa huwa ni namna nyingine ya kufanya 'makamuzi' ya ziada kwenye kashfa husika. Watuhumiwa wakiwa ni wenye fedha hizi chafu huzitumia bila huruma kuhakikisha wenye 'njaa zao' (walio kwenye tume) wanawanyenyekea na kupindisha ukweli. Kuzipata kama zile za kina Mwakyembe (I mean strong and firm ones) ni ngumu!

Crying for my nation!
 
Hii hapa kweli inatupa picha ya kwa nini Tanzania bado ni maskini. Sijui ni sheria? Sijui ni uongozi? Kila shirika na taasisi zote zinanuka rushwa.

Lakini cha kushangaza watu wanapiga kelele wahusika wanapeta tu hivi viongozi wa juu huwa hawapati miskendo hii?

Hii hata akipelekewa mtoto mdogo akaelezwa kichoandikwa lazima atie mtu kwenye vyombo vya sheria, lakini Tz yetu sasa hivi nina hakika watu watakuwa wanahaha kutafuta nani katoa information za ulaji huu.
 
.... lakini Tz yetu sasa hivi nina hakika watu watakuwa wanahaha kutafuta nani katoa information za ulaji huu.
Ndiyo Tanzania ya leo. Fedha chafu daima huishia katika matumizi machafu. Wakifumbiwa macho wanaweza kuzitumia visivyo.

Tunahitaji wataalamu toka nje kugundua jinsi nchi inavyoliwa. Safari ni ndefu lakini naamini taratibu tutafika tu
 
Tuhuma nzito Benki ya Posta....UPUPU UMEMWAGWA KUNA MTAFUTANO BODI YAENDELEA NA KIKAO SI CHA KUTAFUTA UKWELI WA TUHUMA BALI NI CHA KUMTAFUTA ALIYETOA TUHUMA LA...WANATARAJIA KUIPIGA CHINI MENEJIMENT YOTE,WANAAMINI NI MENEJIMENT TU INAYOJUA UFISADI HUO NA KUUTUO.... HAKIKA WANAWAONEA KABISAA....
 
Sms Za Vitisho Kwa Wakurugenzi Wanodhaniwa Kutoa Habari....wana Jf Tukemee.tuhuma Zinakanushwa Kwa Kuutoa Ukweli Na Si Kumtafuta Mtoaji.....
 
Tuhuma nzito Benki ya Posta....UPUPU UMEMWAGWA KUNA MTAFUTANO BODI YAENDELEA NA KIKAO SI CHA KUTAFUTA UKWELI WA TUHUMA BALI NI CHA KUMTAFUTA ALIYETOA TUHUMA LA...WANATARAJIA KUIPIGA CHINI MENEJIMENT YOTE,WANAAMINI NI MENEJIMENT TU INAYOJUA UFISADI HUO NA KUUTUO.... HAKIKA WANAWAONEA KABISAA....

Hayoooo yameisha anza walaji wanatafuta watoa info. PCCB kwa nini wasifukuzwe wote kazi? Mpaka leo bado wako wanavizia maakimu? na wale wanaotoa shilingi elfu moja? na matraffic?
 
Kwa kweli nadhani huu ni wakati wa kuiambia PCCB isifanye mchezo na mali za Watanzania. Kama kweli kuna vyombo vya dola hapa ndipo mahali pa kuanzia na sijui hawa waandishi (wahandisi) wa habari wanafanya kazi gani. Kuna habari kwamba mwandishi wa habari mmoja ambaye sasa amehamia katika fani ya "PR" alipata kufuatilia tuhuma hizi muda mrefu kidogo na sasa ni "MTEJA" mzuri wa Benki ya Posta, maana amepata "MKOPO" mnoni wa benki hiyo na "anaaminiwa" kuchukua na kuhamisha fedha anavyotaka, hatumii tena benki nyingine kwani hapo mambo yake yananyooka kabisa, na sitoshangaa kusikia naye amefutiwa deni. Hii si kusema kwamba waandishi wengine nao waende kujipendekeza kwa MAFISADI, bali nawatahadharisha mambo ya KIBENKI huwa hayana siri kabisa kila kitu kiko wazi, watakaojipeleka mambo yatakuwa hadharani na watajikuta ZINAWATOKEA PUANI hizo fedha za "MIKOPO" ya kiaina. Tuhakikishe PCCB, IKULU, BoT, Wizara ya Fedha, Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma (POC) na wabunge wote wanapata nyaraka zote husika.
 
Trafiki adakwa na PCCB (kaongwa elfu tano, hivi kweli mkuu wa PCCB ana PhD?, anatuma wafanyakazi wake wafuatilie elfu tano wakati vitita vya mamilioni vikiliwa na wajanja?)

teeeh, teeeh, kweli waongezewe marupurupu.

Source: Alasiri ya jana
 
Sms Za Vitisho Kwa Wakurugenzi Wanodhaniwa Kutoa Habari....wana Jf Tukemee.tuhuma Zinakanushwa Kwa Kuutoa Ukweli Na Si Kumtafuta Mtoaji.....
Nilitoa mimi na waje wanifuate, pambaf kabisa hawa jamaa. wanadhani upuuzi huo unabebeka tena nyakati hizi? Na wakiisimamisha kazi menejimenti nzima tutafanya ambacho hawakutarajia. Kudadadeki wanaigeuza Tanzania kuwa yao sio? Mtu akiwa mzalendo hawa mapimbi wa akili wanaanza kumgeuza asusa. Kudadadeki tushachoka na hawa watu. PCCB kwanini wasifanye kazi yao? Bado kuna kulindana hadi wakati huu?
 
Nimesoma! Nimetishika! Nimebabaika kuona haya! Y

Zaidi nimeogopa sana kusikia eti Benki ya Posta imesimamisha sehemu ya watu wa management sio kwa tuhuma hizo la!Ila kwa kudhaniwa ndio waliotoa hizo habari wakati ni siri za kibenki. Hapo ndio nchi hii ilipofika!

Uchunguzi unaanza, SI WA UKWELI WA TUHUMA HIZI, bali WA NANI KAZITOA TUHUMA HIZI!!!
Hii maana yake ni wamba kila kilichosemwa ni sahihi ila mafisadi wametahayari no wanauliza "Hee wamejuaje?"

Nikiulizwa mahala wewe ni mtanzania leo, nitashawishika kusema La hasha! Sitaki kuhusishwa na watanzania wenye uchu, na upumbavu na jeuri ya Benki ya Posta..sitaki kuhusishwa na wezi hawa. Hivi hawana hata mwanasheria uchwara wa kuwapa mlengo wa kufata..au naye ni miongoni mwao?/..hivi mtuhumiwa napounda chombo kujichunguza sio kiini macho na kusaka uchawi. Watanzania wa leo ni wajinga kiasi hicho?!

Busara ndogo, ambazo nadiriki kusema waliopitisha maamuzi hayo hawana, zinaelekeza hivi: awali unaunda tume kuchunguza ukweli/uongo wa tuhuma, (tume huru kabisaa, tena hata BOT(!?) au reputable Audit company); then baada ya report, ikiainisha ni uongo, ndio unakuwa na base ya kutafuta mzushi mwenyewe; na ukikuta ni kweli, unadeal na MAFISADI hao!

Tufanyeje? tuache genge la watu liendelee kufanya maasi ya kifisadi? wakati ni huu...tuwaanike, na wakati huu sasa tuongezee nguvu kulisemea hili! wenye dhamana na kulifanyia kazi wasipolifanyia kazi, basi tuchukue hatua zaidi: tuliwakilishe kunakohusika..kwa nguvu zote..
 
Back
Top Bottom