M-bongotz
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 1,734
- 405
Hii ni hoja binafsi....
Kwa kweli nasikitishwa sana na hili 'jeshi' la mgambo wa jiji.,sipingi uwepo wao kwani limetoa ajira kwa vijana wengi tu wa Tanzania.,kinachonikwaza mimi ni utendaji wao wa kazi, sina hakika kama wanapatiwa mafunzo ya kutosha ikiwa ni pamoja na hata basic knowledge ya sheria na haki za binadamu au ndio wanaokotwa tu hovyo hovyo na baada ya siku mbili tatu wanapewa magwanda na kuingia mitaani.
Hawa jamaa naona wao ndio wanakuwa kero badala ya kutusaidia kupunguza kero hapa jijini.,sina shaka kuwa ni mambumbumbu wa sheria ndiyo maana utendaji kazi wao una walakini sana hebu angalia jinsi wanavyowavamia wafanya biashara na kuwapora vitu vyao, ona jinsi wanavyobeba masufuria ya mama lishe na hata wasiyafikishe huko ofisi za jiji badala yake wanazunguka kona na kula chakula chote.,wale wanaozunguka na breakdowns ndio usiseme wananuka rushwa kupita kiasi.
Nahisi walioanzisha 'jeshi' hili hawakujipanga vizuri, ndio maana wala hawaheshimiki, inabidi waangalie upya hii kada ambayo naona ikitumiwa vizuri inaweza sana kusaidia walau kuwapunguzia mzigo polisi.,naomba tu Mungu wakuu wasijiloge wakawapa hawa jamaa bunduki tutaisha wote huku mitaani.
Nawasilisha.
Kwa kweli nasikitishwa sana na hili 'jeshi' la mgambo wa jiji.,sipingi uwepo wao kwani limetoa ajira kwa vijana wengi tu wa Tanzania.,kinachonikwaza mimi ni utendaji wao wa kazi, sina hakika kama wanapatiwa mafunzo ya kutosha ikiwa ni pamoja na hata basic knowledge ya sheria na haki za binadamu au ndio wanaokotwa tu hovyo hovyo na baada ya siku mbili tatu wanapewa magwanda na kuingia mitaani.
Hawa jamaa naona wao ndio wanakuwa kero badala ya kutusaidia kupunguza kero hapa jijini.,sina shaka kuwa ni mambumbumbu wa sheria ndiyo maana utendaji kazi wao una walakini sana hebu angalia jinsi wanavyowavamia wafanya biashara na kuwapora vitu vyao, ona jinsi wanavyobeba masufuria ya mama lishe na hata wasiyafikishe huko ofisi za jiji badala yake wanazunguka kona na kula chakula chote.,wale wanaozunguka na breakdowns ndio usiseme wananuka rushwa kupita kiasi.
Nahisi walioanzisha 'jeshi' hili hawakujipanga vizuri, ndio maana wala hawaheshimiki, inabidi waangalie upya hii kada ambayo naona ikitumiwa vizuri inaweza sana kusaidia walau kuwapunguzia mzigo polisi.,naomba tu Mungu wakuu wasijiloge wakawapa hawa jamaa bunduki tutaisha wote huku mitaani.
Nawasilisha.