Ubabe wa Magufuli unavyozidi kumharibu kisiasa

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,884
Magufulii(8).jpg


KWA WANANCHI KIGAMBONI ALIONGEA HIVI:

Kauli inayodaiwa kuwaudhi wananchi hao ni ile iliyotolewa na Waziri Magufuli Januari Mosi, mwaka huu, alipozungumza na wananchi wa Kigamboni kuhusu nauli hiyo mpya na kuwaambia kuwa


asiyetaka kulipa nauli hiyo
  • apige mbizi baharini
  • kuzunguka Kongowe kuingia katikati ya jiji au
  • arudi kijijini akalime.

KWA WAANDISHI WA HABARI ALIONGEA HIVI
Pia baadaye siku hiyo hiyo, akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za wizara hiyo, alisema

yeyote asiyetaka nauli hiyo mpya kutozwa,

anunue kivuko chake na akitaka akipe jina la chama chake cha siasa kisha atoe huduma hiyo kwa Sh. 100 au bure ilimradi aende kwake (waziri) kupata kibali cha kutoa huduma hiyo.

Mtazamo wangu juu ya Magufuli
Nilivyokuwa namfikiria Magufuli kwa sasa nimeanza kubadili msimamo, maana mambo ya uongozi si shauri ya kufanya utakavyo na kutojali wananchi unaowatumikia. Na mtazamo wake kila kinachopingwa anasukumia vyama vya siasa kama alivyoongea na waandishi wa habari. Huu ni upeo wa kidikteta, Magufuli ni mwanaharakati wa mfumo wa kidikteta.
 
Nilikua namheshimu sana Magufuli lakini kwa hili heshima yangu kwake imeondoka kabisa. Kama kiongozi wa umma unapaswa uchuje kauli zako kila sekunde. Ni sawa na ule upuuzi wa waziri wa fedha kipindi kile aliyesema hata kama ni majani itabidi watanzania wale lakini ndege ya rais lazima itanunuliwa.
 
Nilikua namheshimu sana Magufuli lakini kwa hili heshima yangu kwake imeondoka kabisa. Kama kiongozi wa umma unapaswa uchuje kauli zako kila sekunde. Ni sawa na ule upuuzi wa waziri wa fedha kipindi kile aliyesema hata kama ni majani itabidi watanzania wale lakini ndege ya rais lazima itanunuliwa.

Tatizo hawa viongozi wa CCM wanajisikia wako huru na kufanya cho chote watakacho na hakuna hatua itakayochukuliwa, hali hiyo ndiyo inayowapa kiburi cha hali ya juu na kufikia hatua ya kuwadhalilisha wananchi waliowachagua.
 
Hii ndiyo design ya viongozi tunaotaka kwa sasa kila sehemu. Waziri wa fedha naye angetoka na single yake ya walipa kodi/tax! wasiotaka kulipa ushuru wa bidhaa wafunge biashara zao. Mbona tutasonga mbele, na hiyo 200 ya magufuli itakubalika mbona. Tatizo hapa ni hizo wizara zingine kutofanya kazi zao vizuri ndiyo maana mnamuona Dr kama mnaa hivi.
 
kwani mlikua hamumjui magufuli??hata kwake mke wake na watoto hawana uhuru wowote...huyu ajateleza ndo alivyo anafanya mambo kiumwamba ila mimi sioni shida coz wakazi wa dar ni mazezeta ngoja wapelekwe..dar kama jiji kongwe tulitegemea iwe chachu ya mabadiliko lakini ndo wamekuwa wakwanza kuvaa kofia na tshirt za ccm...kazi kwao sie tunamsubiri kijijini kwetu akija kubomoa nyumba...HATUTAKI MCHEZO KWANI SIE BARABARA ILITUFATA NA TUKO MPAKANI MWISHO WA NCHI....AJE ATATUKUTA ILA AJUE ATUTAKI UPUUZI
 
Samahani jamani, najua mtaniita MKABILA, ila naomba niwakumbushe kitu hapa:

Hivi Maghufuli anatoka wapi hapa Tz??

Si mnazifahamu tabia za walio wengi watokao kule??

typical, isn't it???

Samahani
 
asiyetaka kulipa nauli hiyo
  • apige mbizi baharini
  • kuzunguka Kongowe kuingia katikati ya jiji au
  • arudi kijijini akalime.

anunue kivuko chake na akitaka akipe jina la chama chake cha siasa kisha atoe huduma hiyo kwa Sh. 100 au bure ilimradi aende kwake (waziri) kupata kibali cha kutoa huduma hiyo.

Kimtokacho mtu ndicho kimchafuacho, kimwingiacho hakimchafui mtu. Aliyoropoka Magufuli ndiyo mtazamo wake kwa wananchi, kiongozi mzuri hawezi kutoa matamshi ya dharau, kejeli, na ubabe kama ailivyofanya. Kwa kifupi hana hulka ya kujali utu wa mtu, na kwa vile anajiona yuko juu anajiona yuko juu ya wote na walio chini yake nikuitikia hewalahewala, ule mfumo dume wa utwa na utwana ndo hulka ya Maguvuli.

Hii si kutokana na haya yaliyotokea juzi tu, ila kuna mlolongo mrefu ambao amewahi kushikwa koti na Waziri Mkuu Pinda na Rais Kikwete, huu ni ushahidi tosha. Hata alipohamishwa wizara hii ya sasa katika awamu iliyopita huenda kuna kitu ambacho ni siri ya ikulu.
 
Samahani jamani, najua mtaniita MKABILA, ila naomba niwakumbushe kitu hapa:

Hivi Maghufuli anatoka wapi hapa Tz??

Si mnazifahamu tabia za walio wengi watokao kule??

typical, isn't it???

Samahani

Nimekuelewa, lakini ndio maana tuna madarasa na vyuo ambavyo kwa miaka kadhaa inatusaidia kujiweka sawa kufanya yale ambayo yanatazamiwa na kumbuka yeye ni Dr. Huyu huyu anaopoomba kura anagaagaa mavumbini na nakumbuka last time alimpeleka Kikwete kijijini kwake kuonana na mama yake kama si shangazi yake kama sijachanganya, lakini anachofanya leo si kile alichoonyesha wakati anaomba kura.
 
Hii ndiyo design ya viongozi tunaotaka kwa sasa kila sehemu. Waziri wa fedha naye angetoka na single yake ya walipa kodi/tax! wasiotaka kulipa ushuru wa bidhaa wafunge biashara zao. Mbona tutasonga mbele, na hiyo 200 ya magufuli itakubalika mbona. Tatizo hapa ni hizo wizara zingine kutofanya kazi zao vizuri ndiyo maana mnamuona Dr kama mnaa hivi.

Hata kama msimamo wake ni kuwa ongezeko la bei litabaki lilivyo kuna namna ya kuongea na kutetea msimamo huo. Si kwa lugha ya dhihaka na kebehi namna alivyofanya Magufuli. Kwa nchi ambayo sovereignty katika maana yake halisi iko kwa wananchi sasa hivi tunavyoongea Magufuli angekuwa nje ya kibarua aidha kwa kuresign mwenyewe ama kufutwa kazi na boss wake.
 
Nilikua namheshimu sana Magufuli lakini kwa hili heshima yangu kwake imeondoka kabisa. Kama kiongozi wa umma unapaswa uchuje kauli zako kila sekunde. Ni sawa na ule upuuzi wa waziri wa fedha kipindi kile aliyesema hata kama ni majani itabidi watanzania wale lakini ndege ya rais lazima itanunuliwa.

Usiwe na heshima kwa kufuata matukio, kwani kesho akifanya jambo jema ina maana utarudisha heshima yako kwake.
 
Mimi nadhani ''ukitafakari kauli yake' inayoonekana kuwaudhi wabunge wa Dar! kwa 'mapana' zaidi......Mh. Magufuli alikuwa anawapa taarifa wananchi wa tanzania kuwa kwa sasa kila mtu ajijue kivyake(hasa wa kipato cha chini) atakavyo jiwezesha kijikwamua na hali ngumu ya maisha, maana serikali iliyoko madarakani haipo tena katika kuwasaidia wananchi wa kipato cha chini kujikwamua. Aliona hiyo ndiyo njia sahihi kufikisha ujumbe ili watu waelewe kinachoendelea. Bahati mbaya sana watanzania tulio wengi hatukumuelewa.

Wabunge wa Dar wamemuelewa sana Waziri Magufuli alichokuwa ana maanisha hasa hawa kutoka CCM(chama tawala) ndio maana kwa kuona mwenzao anajaribu kumwaga mboga sasa wao(Wabunge wa Dar) wanataka kuhakikisha mboga hiyo inamwagikia yeye(Mh. Magufuli).
 
Leo amefafanua kauli zake. Tegeni masikio radioni ama kwenye Runinga

Umeona tatizo la viongozi hawa kufafanua kauli yake maana yake kujenga utetezi juu ya aliyowadhalilisha wananchi. Ingekuwa busara kama angewaomba radhi wananchi heshima yake ingerudi, lakini kutoa ufafanuzi ni kuzidi kujenga ufa aliouanzisha kwa wananchi.

Leo hii mawaziri wengi wanaishi mahotelini na wafanyakazi wengi wa umma wanaostahili kupata nyumba serikali wanaalazimika kulipa gharama kubwa ya kupanga kwa sababu ya ubabe wa Magufuli aliofanya awamu ya Mkapa kuuza nyumba za watumishi wa serikali. Kwa mtazamo huo Magufuli hakuona mbali zaidi ya kwa nini zilijengwa nyumba za watumishi halafu yeye kiulaini aishie kuziuza, na kama Mkapa singemshtukia tungebaki na ikulu tu.
 
Samahani jamani, najua mtaniita MKABILA, ila naomba niwakumbushe kitu hapa:

Hivi Maghufuli anatoka wapi hapa Tz??

Si mnazifahamu tabia za walio wengi watokao kule??

typical, isn't it???

Samahani

Kalale ofile! Katamila omuguta! na cjuhi kwanini ww housekeeper umeruhusiwa kuwa humu muda huu wakati unatakiwa kuwa jikoni! inawezekana huna ufahamu wa hali ya nchi na uchumi ulivyo! hivi nauli ya dalax2 kituo hadi kituo unajua bei yake? ukitoka fire hadi kariakoo au kutoka Akiba hadi Posta au kutoka posta mpya hadi ya zamani unalipa bei gani? ukijibu swali hilo nina imani utaacha kufikiri kwa makalio kama Wabunge wako wakiongozwa na Mtemvu! Magufuri ni waziri makini sana na hiyo nauli ni ndogo sana kwa hali ilivyo kwa sasa! Nilifikiri Mnyika angeendelea na kutatua kero za maji kuliko kujihusisha na ujinga kama huu! ckutegemea kuona wabunge wanatafuta umaarufu kwa shs 100, bac kama ndo hivyo kwa nini hawataki kuutafutia kwenye shs 200,000 za posho? shame on them! Kwetu Iringa nahisi unaweza kuwa beki tatu wa Luhanjo ww maana ndo familia zinazotumia makalio kufikiri!
 
Mimi nadhani ''ukitafakari kauli yake' inayoonekana kuwaudhi wabunge wa Dar! kwa 'mapana' zaidi......Mh. Magufuli alikuwa anawapa taarifa wananchi wa tanzania kuwa kwa sasa kila mtu ajijue kivyake(hasa wa kipato cha chini) atakavyo jiwezesha kijikwamua na hali ngumu ya maisha, maana serikali iliyoko madarakani haipo tena katika kuwasaidia wananchi wa kipato cha chini kujikwamua. Aliona hiyo ndiyo njia sahihi kufikisha ujumbe ili watu waelewe kinachoendelea. Bahati mbaya sana watanzania tulio wengi hatukumuelewa.

Wabunge wa Dar wamemuelewa sana Waziri Magufuli alichokuwa ana maanisha hasa hawa kutoka CCM(chama tawala) ndio maana kwa kuona mwenzao anajaribu kumwaga mboga sasa wao(Wabunge wa Dar) wanataka kuhakikisha mboga hiyo inamwagikia yeye(Mh. Magufuli).

Pamoja na we kumjengea tafsiri nzuri Magufuli bado haijalishi ukweli wa hali halisi ya maisha, maana hapo inavyoonekana ingekuwa mara yake ya kwanza tungejaribu kumsafisha, lakini amezoeleka hivyo.
 
Back
Top Bottom