Uanaume,emotions na ushoga

Ubumuntu

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
14,316
10,782
Salaam wana JF!

Kuna hili suala la 'uanaume' na 'emotions'. Yaani kuna shule ya hisia ambayo inaamini kwamba mwanaume hapaswi kua "too emotional" katika suala la mahusiano,urafiki na mapenzi. Kwamba mwanaume alie "too emotional" ana kosa 'uanaume'.

Sasa kwa wanaume walio "too emotional" shule hiyo inawafafanua kua na chembechembe 'hormones' za uanauke. Hapo suala la ushoga ndipo linaingia. Kwamba wanaume walio "too emotional" katika MMU uwa ni mashoga.

Ndio maana hata katika tasnia ya muziki,wanamuziki kama John Legend,Neyo n.k. wamekua wakihusishwa na ushoga kutokana kuimba kwa "emotions" za kupitiliza juu ya MMU, kinyume na 'uanaume'.

Mimi naamini kwamba binadamu (wanaume kwa wanawake) tuna 'emotions' katika masuala ya MMU. Lakini mwanaume ukiwa "too emotional" katika masuala ya MMU,wasiwasi unaanza kujitokeza.

Ni hayo tu.
 
Ni makuzi tu haya! Unaona watoto wakiwa wadogo! Mtoto wa kiume akilia anambiwa "wacha kulia bwana unakuwa kama mwanamke"? mtoto wa kike anafundishwa tangu mtoto kujali watoto wenzake na kuwalea - anakatazwa kukwea miti ama kusema kwa kupayuka payukia.

Kimsingi, binadamu kamili wanahisia, wakati mzuri ni wakati wa misiba. Utasikia wanaume wanaambiwa "Jikaze wewe ni mwanaume bwana" Futa machozi. Lakini wanawake wanapiga ukunga mpaka kesho. Matokeo yake wanaume wanakuwa frustrated kwani wanachemka tu ndani kwa ndani
 
Jiulize kwa nini asilimia kubwa kwa nini mashoga wapo mijini tu vijijini hawapo? Wanaume wanaokuwa mashoga ni wale wanaopenda maisha mazuri wakati hawana uwezo kwa hiyo wanaongozwa na tamaa ya vitu kufanya ushoga.
 
Ukikariri kwamba ugali huliwa na mchuzi pekee siku ukipewa samaki mkavu utakataa katu katu HAIWEZEKANI.
 
Ni makuzi tu haya! Unaona watoto wakiwa wadogo! Mtoto wa kiume akilia anambiwa "wacha kulia bwana unakuwa kama mwanamke"? mtoto wa kike anafundishwa tangu mtoto kujali watoto wenzake na kuwalea - anakatazwa kukwea miti ama kusema kwa kupayuka payukia.

Kimsingi, binadamu kamili wanahisia, wakati mzuri ni wakati wa misiba. Utasikia wanaume wanaambiwa "Jikaze wewe ni mwanaume bwana" Futa machozi. Lakini wanawake wanapiga ukunga mpaka kesho. Matokeo yake wanaume wanakuwa frustrated kwani wanachemka tu ndani kwa ndani


Sawa.
Lakini pamoja na malezi,hili suala pia lipo kiasili zaidi.

Binadamu wa kiume kama wanyama hiyo ndio asili yao. Hawapaswi kua "too emotional" katika MMU,kwani kwa kuwa hivyo kunaweza kumuathiri katika kufanya shughuli zake za kumwezesha kutunza familia. Ndio maana mwanamume anaweza gombona na mke wake nyumbani,lakini kazini akapiga kazi kama kawaida,tofauti na mwanamke.
 
hata mwanamme ni mtu jamani.


Sawa. Lakini kuna mtu wa kiume na mtu wa kike.

Sasa kwa mtu wa kiume 'emotions' zikiwa "too much" anakua hana tofauti na mtu wa kike. That's nature. Tukienda kinyume na nature matokeo yake ndio mabadiliko ya tabia mtu.
 
Sawa. Ila katika mtu,kuna mtu wa kiume na mtu wa kike.

Sasa kwa mtu wa kiume, ikiwa "too much" anakua hana tofauti na mtu wa kike!

Ulipoanza kuandika umesema hatakiwi kuwa "emotional". . huku unajifanya hatakiwi kuwa "TOO emotional". . .kuwa na msimamo. Wasichotakiwa kuwa nacho ni hisia kama mawe yalivyo ama hisia kupita kiasi?
 
Ulipoanza kuandika umesema hatakiwi kuwa "emotional". . huku unajifanya hatakiwi kuwa "TOO emotional". . .kuwa na msimamo. Wasichotakiwa kuwa nacho ni hisia kama mawe yalivyo ama hisia kupita kiasi?


Umesoma kimalizio cha main post?

Hisia kua nazo ni sawa. Lakini zikizidi sana mwanaume huyo anakua hana tofauti na Eva. Hiyo ndio asili.
 
HATING IS BAD!!
Hiyo chuki uliyonayo itumie kufanya mambo yako binafsi utafanikiwa sana kulijo kuchukia watu wasikuongezea wala kukupunguzia chochote kile.
 
jiulize kwa nini asilimia kubwa kwa nini mashoga wapo mijini tu vijijini hawapo? Wanaume wanaokuwa mashoga ni wale wanaopenda maisha mazuri wakati hawana uwezo kwa hiyo wanaongozwa na tamaa ya vitu kufanya ushoga.


ahahahaahahahaahahaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Umesoma kimalizio cha main post?

Hisia kua nazo ni sawa. Lakini zikizidi sana mwanaume huyo anakua hana tofauti na Eva. Hiyo ndio asili.

Nimesoma sana. . .
Umetumia "emotional" 3 times na "too emotional" once. Again onyesha msimamo wako. Kama mwanaume kuwa na hisia kunamfanya shoga then hata wewe unaweza ukawa shoga maana sidhani tangu umekua na akili zako hujawahi kukasiriki ama kuumia kwa lolote. Ila tukienda kwenye kuwa na hisia zilizopitiliza hata mimi nakubali kwamba haipendezi kwa mwanaume japo kwa kiasi flani haina uhusiano na mtu kuwa ama kutokua gay.
 
Wasichotakiwa kuwa nacho ni hisia kama mawe yalivyo ama hisia kupita kiasi?


Hisia za kupitiliza katika MMU kwa upande wa mwanaume si sawa.

Sawa na mwanamke hasiye na hisia katika MMU ambavyo watu umfafanua kama jikedume.
 
Mkuu_kweli hawa watu wanaudhi sana,ila punguza kidogo hasira kiongozi wangu,..ila ukianza hiyo kampeni ya kimya kimya nitonye.
 
Hisia za kupitiliza katika MMU kwa upande wa mwanaume si sawa.

Sawa na mwanamke hasiye na hisia katika MMU ambavyo watu umfafanua kama jikedume.
Sasa tumia "hisia zilizopitiliza" maana hisia hata mbwa anazo, achilia mbali binadamu.
 
HATING IS BAD!!
Hiyo chuki uliyonayo itumie kufanya mambo yako binafsi utafanikiwa sana kulijo kuchukia watu wasikuongezea wala kukupunguzia chochote kile.

Mimi nimeshadeclare interest mashoga kwangu ni maadui hawawezi kukaa karibu na mimi. Niambie ni kijiji gani hapa Tanzania umeenda umemkuta shoga, vijana wa mjini hapa na tamaa tamaa zao kutwa kujificha kwenye madanguro ya kike.
 
Kama mwanaume kuwa na hisia kunamfanya shoga then hata wewe unaweza ukawa shoga maana sidhani tangu umekua na akili zako hujawahi kukasiriki ama kuumia kwa lolote.

Ila tukienda kwenye kuwa na hisia zilizopitiliza hata mimi nakubali kwamba haipendezi kwa mwanaume japo kwa kiasi flani haina uhusiano na mtu kuwa ama kutokua gay.


Kukasirika na kuumia kupo. Lakini si kwa kiwango cha kupitiliza hadi unaanza kulialia na kutamani kujitoa roho au kujidhuru kwa aina yoyote ile.

Mbona mwanamke anajifanya 'mgumu' wa hisia katika MMU uhusishwa na ujikedume? Jibu ni kwamba,kiasili wanawake wanapaswa kua ndio wenye hisia kali katika MMU na si wanaume!
 
Jiulize kwa nini asilimia kubwa kwa nini mashoga wapo mijini tu vijijini hawapo? Wanaume wanaokuwa mashoga ni wale wanaopenda maisha mazuri wakati hawana uwezo kwa hiyo wanaongozwa na tamaa ya vitu kufanya ushoga.

Kama kuwa na hasira kali nayo ni "too emotional" kwa muktadha wa thread hii basi inaonekana Nitonye uko too emotional. Unafikiria kuua kimya kimya ndugu yangu?
 
Back
Top Bottom