Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Tunapoendelea kutafakari miaka hamsini ya Uhuru wa Tanzania bara hatuna budi kupitia mojawapo ya kurasa nyeti sana za taifa letu - uamuzi wa kuondokana na mfumo wa vyama vingi na kuwa rasmi nchi ya chama kimoja. Uamuzi huu kwa wengine ndio uliomthibitisha Nyerere kuwa ni dikteta kwani "alifuta vyama vingi". Bahati mbaya sana watu wenye kuelezea uamuzi huu wanaangalia kwa mwanga ambao ukiufikiria sana ni vigumu sana kuuelewa kuwa demokrasia ni "vyama vingi" kwamba nje ya vyama vingi hakuna demokrasia. Hili kwa haraka linaonekana ni kweli.
Na kutokana na hilo wapo wanaoamini kuwa vyama vingi vinaharakisha maendeleo na ya kuwa kama tungeendelea kuwa na vyama vingi labda tungepiga hatua za haraka za maendeleo. Kutokana na hili wapo wanaoshangaa kwanini wananchi walipoulizwa mwanzoni mwa miaka ya 1990 kama tuingie kwenye vyama vingi waliopata kutoa mawazo yao asilimia 80 walitaka kuwa na chama kimoja. Matokeo ya chaguzi mbalimbali bado yameonesha kuaminiwa kwa chama kimoja kwa muda mrefu kiasi kwamba sasa tunajua kabisa kuwa CCM kama kweli ingetaka kutawala vizuri na kuliongoza taifa kwenye maendeleo ingeweza kwani wananchi waliamini kweli na wapo ambao waliamini kuwa demokrasia iliyokuwemo ndani ya chama kimoja ilikuwa na nguvu zaidi kuliko demokrasia ya vyama vingi.
Kuelewa hiyo kauli yangu hapo juu hatuna budi kurudi kwa miongoni mwa wanadharia wa kwanza wa CCM na mmoja wa viongozi walioamini kabisa Ujamaa Dr. Will Kleruu. Wengi wanamkumbuka zaidi kutokana na kifo chake - aliuawa kule Iringa na risasi ya Mwamindi na labda wimbo wa kwanza wa kumsifia kiongozi aliyependwa Tanzania ukiondoa Nyerere ulitungwa na Mbaraka Mwinshehe ule wa kumuaga Dr. Kleruu - "Dr. Kleruu ukalale pema kiongozi wetu shujaa, mwanamapinduzi".
Kwanini tuliingia kwenye chama kimoja? Je ni kweli Nyerere aliamua tu kufuta vyama vingine? Je, kulikuwa na hoja gani zilizotolewa za kulipeleka taifa kwenye chama kimoja na je hoja hizo zingewa kupingwa vipi? Hapa basi, Dr. Kleruu ameandika kitu ambacho tunaweza kuita ni propaganda za TANU za kuhalalisha chama kimoja kwa kutumia hoja za kiakili (rational arguments). Je hoja zake nani angeweza kuzipinga wakati ule? Je leo ukizisoma hoja hizi ni ipi unaweza kuipangua na kusema hapa Dr. Kleruu alikosea?
Pamoja na kijitabu cha Dr. Kleruu cha "Serikali ya Chama Kimoja" nimeambatanisha vile vile maelekezo ya Rais Nyerere kwa Tume ambayo ilitakiwa kubuni mfumo wa demokrasia ya chama kimoja iwe vipi. Ndani ya maelezo hayo kuna mambo ambayo aliyasimamia kama taifa kwamba bila kujali tuko kwenye chama kimoja au vingi kuna mambo ambayo ni lazima yawepo katika Tanzania - nina uhakika ukiyasoma utasisimka kwani ndiyo yaliyotufanya Watanzania tuwe Watanzania (rejea Utetezi wangu wa Tanzania sehemu zote mbili). Na kama burudani kwa wazee wenzangu na vijana ambao hawajahi kusikia wimbo huu, ninawakumbushia wimbo wa Mbaraka Mwinshehe wa buriani ya Dr. Kleruu.
SWALI: Je, ni kweli demokrasia inajengwa peke yake kwa vyama vingi? Je, yawezekana kubuni mtindo wa kuwa na demokrasia ndani ya Chama kimoja? Faida na hasara za mifumo yote miwili ni nini hasa? Dr. Kleruu anajaribu kujibu. Kwa upande wetu leo hii tunatakiwa kujiuliza je Demokrasia ya vyama vingi imefanya yale ambayo tuliambiwa itaweza kufanya? Vietnam na China ni nchi zenye mfumo wa chama kimoja kwanini zinapiga hatua ya haraka ya maendeleo kuliko sisi?
Do Enjoy!!
MMM
Na kutokana na hilo wapo wanaoamini kuwa vyama vingi vinaharakisha maendeleo na ya kuwa kama tungeendelea kuwa na vyama vingi labda tungepiga hatua za haraka za maendeleo. Kutokana na hili wapo wanaoshangaa kwanini wananchi walipoulizwa mwanzoni mwa miaka ya 1990 kama tuingie kwenye vyama vingi waliopata kutoa mawazo yao asilimia 80 walitaka kuwa na chama kimoja. Matokeo ya chaguzi mbalimbali bado yameonesha kuaminiwa kwa chama kimoja kwa muda mrefu kiasi kwamba sasa tunajua kabisa kuwa CCM kama kweli ingetaka kutawala vizuri na kuliongoza taifa kwenye maendeleo ingeweza kwani wananchi waliamini kweli na wapo ambao waliamini kuwa demokrasia iliyokuwemo ndani ya chama kimoja ilikuwa na nguvu zaidi kuliko demokrasia ya vyama vingi.
Kuelewa hiyo kauli yangu hapo juu hatuna budi kurudi kwa miongoni mwa wanadharia wa kwanza wa CCM na mmoja wa viongozi walioamini kabisa Ujamaa Dr. Will Kleruu. Wengi wanamkumbuka zaidi kutokana na kifo chake - aliuawa kule Iringa na risasi ya Mwamindi na labda wimbo wa kwanza wa kumsifia kiongozi aliyependwa Tanzania ukiondoa Nyerere ulitungwa na Mbaraka Mwinshehe ule wa kumuaga Dr. Kleruu - "Dr. Kleruu ukalale pema kiongozi wetu shujaa, mwanamapinduzi".
Kwanini tuliingia kwenye chama kimoja? Je ni kweli Nyerere aliamua tu kufuta vyama vingine? Je, kulikuwa na hoja gani zilizotolewa za kulipeleka taifa kwenye chama kimoja na je hoja hizo zingewa kupingwa vipi? Hapa basi, Dr. Kleruu ameandika kitu ambacho tunaweza kuita ni propaganda za TANU za kuhalalisha chama kimoja kwa kutumia hoja za kiakili (rational arguments). Je hoja zake nani angeweza kuzipinga wakati ule? Je leo ukizisoma hoja hizi ni ipi unaweza kuipangua na kusema hapa Dr. Kleruu alikosea?
Pamoja na kijitabu cha Dr. Kleruu cha "Serikali ya Chama Kimoja" nimeambatanisha vile vile maelekezo ya Rais Nyerere kwa Tume ambayo ilitakiwa kubuni mfumo wa demokrasia ya chama kimoja iwe vipi. Ndani ya maelezo hayo kuna mambo ambayo aliyasimamia kama taifa kwamba bila kujali tuko kwenye chama kimoja au vingi kuna mambo ambayo ni lazima yawepo katika Tanzania - nina uhakika ukiyasoma utasisimka kwani ndiyo yaliyotufanya Watanzania tuwe Watanzania (rejea Utetezi wangu wa Tanzania sehemu zote mbili). Na kama burudani kwa wazee wenzangu na vijana ambao hawajahi kusikia wimbo huu, ninawakumbushia wimbo wa Mbaraka Mwinshehe wa buriani ya Dr. Kleruu.
SWALI: Je, ni kweli demokrasia inajengwa peke yake kwa vyama vingi? Je, yawezekana kubuni mtindo wa kuwa na demokrasia ndani ya Chama kimoja? Faida na hasara za mifumo yote miwili ni nini hasa? Dr. Kleruu anajaribu kujibu. Kwa upande wetu leo hii tunatakiwa kujiuliza je Demokrasia ya vyama vingi imefanya yale ambayo tuliambiwa itaweza kufanya? Vietnam na China ni nchi zenye mfumo wa chama kimoja kwanini zinapiga hatua ya haraka ya maendeleo kuliko sisi?
Do Enjoy!!
MMM
Attachments
Last edited by a moderator: