Uamuzi wa CHADEMA dhidi ya madiwani: "A Big Mistake!"

Mkuu Pasco niruhusu nizirejee hoja zako kama ilivyozileta nikiwa na mawazo huru yasiyofungamana na siasa za upande wowote au kuwa na ushawishi. <br />
Hoja # 1:Ni kweli sheria hiyo si sahihi kwasababu ulizozitaja. Mahakama kuu ilitoa hukumu nadhani kesi ya Mtikila(Judge Rugakingira RIP). Serikali ilikata rufaa na suala hilo bado lipo mahakamani na sijui kwanini mahakama imeamua kulikalia kimya, pengine ni kutokana na <i>conflict of interest</i> kati ya wateule wa mahakama. Chadema inawajibika kwa sheria za nchi hata kama haikubaliani nazo hadi itapokuwa vinginevyo. Sisi wananchi tuna jukumu la kushinikiza kuhusu mabadiliko hayo. Labda ungesema Chadema walipaswa kuonyesha mfano tofauti ,lakini pia inategmea matokeo ya majadiliano kama ulivyoyaleta katika <i>update</i> yako.<br />
<br />
#2: Bado tunarudi pale pale kuwa sheria zetu zina utata sana na sio kwa Chadema tu. Chama kinapokudhamini ni sawa na mwajiri wako wa zamani anapokupa <i>reference letter </i>na ukishaajiriwa ndio mwisho wa i<i>nfluency</i> yake. Ndivyo ilivyo kwa madiwani, wabunge n.k mwajiri wao ni wananchi na wanawajibika kwao, lakini ni sheria hiyo hiyo inayosema chama kinauwezo wa kumvua uongozi mchaguliwa bila kumpa haki mwajiri (mwananchi) kumvua uongozi. Kwa mazingira yaliyopo Chadema ilikuwa na uamuzi unaolingana na sheria zetu, kama ni sahihi au la hilo ni jambo lingine,lakini je walifanya kulingangana na taratibu zetu, jibu ni ndiyo. Hapa ndipo tunatakiwa tuangalie upya wakati wa kujadili katiba mpya.<br />
<br />
#3: Nadhani waliitwa katika vikao halali na hawakuwa condemned.Rejea <i>update</i> yako.<br />
<br />
#4: Chadema haina sababu ya kufuata mipangilio ya CCM, na inadhima kubwa sana ya kubadilisha mwelekeo wa watu kuhusu uchaguzi ili watu wachague sera za chama na si mtu au watu. Kosa hilo limefanywa na CCM na linawagharimu ni vema Chadema wakalitafutia dawa.<br />
<br />
#5: Haa! yaani makosa yaliyofanywa na CCM ndiyo yarudiwe na Chadema! CCM kinameguka kwasababu kiliacha misingi ya uongozi (<i>principles</i>) na kukumbatia haiba(<i>personalities</i>). Uamuzi wa Chadema ni wa kuonyesha njia kuwa wao wanaweza na hakuna zaidi ya Chama. Kuendelea kuwalea watovu wa nidhani ni kufuga na kuzalisha vi-EL na vi-RA au vi-CH vidogo vidogo na vitakapo ota mbawa ndipo yatawakuta ya CCM. Kinga ni bora kulilo kuponya.<br />
<br />
#6: Uamuzi sahihi ni ule unaofaa kwa muda muafaka. Igunga ni jimbo moja tu na pengine RA asingejiuzulu tusingekuwa na uchaguzi. Ni bora Chama kikajijengea imani ya kuaminika bila hofu ya uchaguzi kwani chaguzi zipo nyingi na zitakuja lakini<i> credibility </i>ya chama hutengenezwa kwa miaka mingi na kuharibika kwa saa moja. Hakuna haja ya kuogopa maamuzi magumu kama yanayoisumbua CCM na serikali yake kwa hofu ya jimbo moja au mawili, gharama za<i> credibility</i> ya chama ni kubwa sana.<br />
<br />
#7: Siasa za Tarime ni <i>very complicated</i>, Mwera alipotemwa Chadema akarudi CCM huyu hakuwa muumini wa sera bali tumbo lake. Nashukuru mh Mbowe alikwenda Tarime na kuwapasha ukweli. Kwa hali yoyote lazima tukubali siasa za Tarime ni <i>beyond politics, ideology na policy</i>.<br />
<br />
#8: Nakubaliana na wewe kuwa bado uwanja wa mapambano si sawa(level), kuhusu kuunda <i>coalition </i>nadhani una maanisha na wapinzani wengine, labda tujiulize Mrema ba Cheyo ni wapinzani? CUF yenye uhusiano wa karibu na CCM ni wapinzani. Nadhani ili tuwe na uwanja mzuri agenda ya katiba mpya lazima ipewe kipaumbele , ichukuliwe na Chadema kabla ya mwaka kesho.<br />
<br />
Hitimisho<br />
Uamuzi wa Chadema kuwavua uanachama ni sahihi kwasababu hakuna mtu au watu au Organization iliyowahi kufanikiwa bila nidhamu. <br />
Ni nidhamu inayowatesa CCM sasa hivi. <br />
<br />
Nilishawahi kuwaonya Chadema kuwa suala la Arusha lilikuwa la kitaifa na zaidi, na kuliachia madiwani ilikuwa kosa kubwa sana. <br />
Hata baada ya kutangazwa muafaka niliwasihi watoe msimamo cha kushangaza walikaa kimya kwa wiki mbili. <br />
Hii inaonyesha kuwa Chadema hawana vitengo vya kutathmini hali ya kisiasa na kufanya maamuzi ya haraka na busara. <br />
Hili lilipelekea <i>political base' </i>kuwa <i>demoralized</i>.<br />
<br />
Mkuatano wao wa Arusha na maoni juu ya uamuzi wao katika blogs na vijiwe unatetea hoja yangu kuwa wapenzi na wanachama walikereka sana na mwenendo wa Chama chao na kwamba maamuzi magumu waliyochukua wame <i>excite base </i>yao tena.<br />
<br />
Ingawaje naunga mkono maamuzi ya CC lakini nadhani kuna mapungufu ambayo hayaelezeki kwa njia ya kawaida.<br />
Uongozi wa mkoa na wilaya ulihusika vipi katika sakata zima na je hakuna uzembe miongoni mwao. <br />
Najua uongozi wa wilaya umejikosha kwa kufanya mabadiliko lakini CC ya Chadema inapaswa kutoa kauli kuhusu ushiriki wao.<br />
<br />
Pili, je mbunge wa Arusha anahusika vipi na amechukuliwa hatua gani. Kama uwajibikaji wake akiwa mjumbe wa Halamshauri ya jiji la Arusha ungekuwa sahihi mambo yasingefikia hapo yalipofikia. Yeye angekuwa kiungo muhimu sana kwa mawasiliano kati ya makao makuu na madiwani.<br />
Nadhani inabidi CC itolee kauli kuhusu ushiriki wake vinginevyo itakuwa ni <i>double standard</i>.<br />
<br />
Mwisho, je muundo wa Chadema upo kamilifu? Vinginevyo habari hizi zisingekuwa za mshtuko, na hii inapelekea niamini kuwa kuna vitengo ndani ya chama haviwajibiki. Utamaduni wa kuunda tume ni ishara ya uzembe kama tunavyoona ndani ya CCM na serikali yake.<br />
<br />
Haiwezekani chama chanye sekretariati na CC vishindwe kuelewa nini kinaendelea katika <i>political sphere</i> hasa mambo ndani ya chama chao.<br />
Kuna umuhimu wa Chadema kurejea utendaji wa vitengo vyake na wawepo watu makini zaidi. Chama hakiendeshwi na tume bali <i>facts and principles<br />
<br />
</i>Ahsante
Mkuu Nguruvi3 , nimependa sana mchango wako huu, haswa objectivity na impartiality yako. Kwa maoni yangu, Chadema hivi sasa kinahitaji washauri wa calibre yako more than any other time watakao wapa mtazamo wa outside the box. Najua kwenye safu yao kuna line-up nzuri ya watu makini wenye vision na mission ila naona bado hawana right strategies to hit the bull on time na kwa vile watu hawa ni part and parcel, dhana ya collective resiponsibility ina wa blind kutoona mapungufu yao.

Kwa maoni yangu bado wako kwenye stage ya beating around the bush for too long. CCM wameshajua suala la katiba mpya ni crucial na threat kwa mustakabali wake kuendelea kuitawala nchi hii kwa kutuswa kama kondoo hivyo delaying tactics its their only weapon hivyo katiba hiyo itacheleweshwa mpaka eleventh hour such that Chadema will dance to its tune by the time they realise the games people play, it will be too little too late to do anything worthwhile.

Nguruvi nashauri for the sake of this nation, put your idears in black and white, wape ushauri wa bure in confidence. Wakimeza au wakitema itakuwa ni shauri yao but you'll have clear concious that "they were told!".
 
Mimibaba;2362755Kwanza nilitegemea nione "[U said:
declared interest[/U]" yako kwenye hili swala kwa sababu unatumila lugha yenye madaraka makubwa.Pili kwa baadhi yetu kutokana na uzoefu uchambuzi ungetambua "Risks na Assumptions" katika mchakato na utaratibu mzima wa kufikia maamuzi. Kwa maoni yangu Risk kubwa ilitokana na CCM kutaka kuhodhi mustakabali wa hili suala. Assumption kubwa ilikuwa pande zote zilikuwa na dhamiri njema. Singependa kukufanyia uchambuzi ila ebu zijaribu (test) risk na assumption uone unabakia na option zipi?
Mwisho facts na principles ni guiding factors kwa ajili ya kufikia conclusion fulani. Kwa maoni yangu CDM walichukua tahadhali na muda muafaka kuona dot zina connect vipi.
Mimi nilishiriki kwenye madaraka, uhuru na jamhuri wa nchi hii; nimeona jinsi siasa zilivyogeuzwa na kubadirika kuwa mchezo mchafu. Sasa sijui utailamu timu yako au timu unayocheza nayo ili ufikie lengo?
Ahsate Mimibaba kwa maoni yako. Siajkuelewa vema kuhusu declared interest uliyosema, labda nieleze kama nilivyoielewa. Mimi naamini kuwa siasa makini ni moja ya nyenzo za kutuondoa hapa tulipo kuelekea miaka 100. Ni ukweli kuwa uwepo wa vyama vya upinzani umekuwa sehemu muhimu sana ya jamii yetu. Tumeweza kujielewa na kuelewa yale yanayofanyika nyuma ya pazia, na upinzani umeku karibu nasi hata kuwavuta watawala wa nusu karne kutufikia. Enzi hizo kuwasiliana na kiongozi wa serikali lilikuwa kama kosa la jinai, tukiwaona kama wanadamu wenye fursa pekee duniani. Walipokuja akina mh Mbowe, Dr Salaa, Zitto n.k kuchanganyika nasi tunajisikia kama sehemu ya uongozi wa nchi, sasa hata wale waliobweteka wanatufikia.

Kwa mantiki hiyo uimara wa siasa ni muhimu bila kujali mrengo. Nimekuwa nachelea yaliyokikuta CUF yasije kujirudia ndio maana huwa nakuwa mkweli kwa vyama vyote ili tuwe na mfumo imara na si wa misimu. Pengine hilo ndilo linapelekea kuwa muwazi zaidi na lugha kuonekana ya madaraka makubwa.

Nashukuru umeniasa kuwa lugha imekuwa ya madaraka makubwa pengine ukinitahadharisha kuhusu maandiko yangu. Nitajaribu kuwa katika lugha ya kiraia ambayo ndiko niliko, nisichoweza ni kubadili ukweli kwasababu naamini spade ni spade not a big spoon. ha ha ha.

Kuhusu Risk na assumption nakubaliana na wewe kuwa ni vema kuviangalia vitu hivi, si baada ya, lakini kabla ya.
Wakati uongozi wa Chadema unakwenda Arusha kwa nguvu zote walitakiwa watambue hiyo ni risk na walitakiwa wawe na assumption na options a,b,c. Nadhani walifanya hivyo na njiani kukawa na communication breakdown.

Yalipotokea mauaji risk iliongezeka zaidi na hapo walitakiwa kuwa waangalifu wa kila hatua. Sina tatizo na kile walichoamini wanasimamia na ukweli unabaki kuwa kuna nyakati CCM inaweza kulazimisha mtu au watu kuchukua hatua zisizotarajiwa.

Tatizo lipo namna suala lilivyoshugulikiwa. Haiwezekani kuwa uongozi ulikuwa haujui muafaka wa madiwani tukizingatia kuwa kuna madiwani, wabunge, mbunge, uongozi wa wilaya na mkoa. Suala lililochukua taswira ya kitaifa na kimataifa haikuwa muafaka kuliacha liende kwa nguvu za asili. Sikatai kuwepo kwa muafaka kama hilo ni jema kwa Chama na wanachi wameridhia, lakini je kulikuwa na ridhaa ya wanachama na wapenzi wa Chadema? Je, political analysts, pundits na obsevers wa chadema waliweza kufanya riks assessment kwa kuangalia base yao?

Muafaka ulipofikiwa tulitegemea viongozi watoe ufafanuzi. Halikutokea na kiongozi wa CCM labda kwa asumption kuwa ataeleweka na wanachama na wapenzi wa Chadema ndiye aliyesimama na kulitolea taarifa. Katika mchanganyiko huo watu wakahoji, je suala zima lilikuwa umeya wa watu 2?
Ikachukua wiki mbili, licha ya maoni mbali mbali kuwa uongozi utoe kauli. Hakuna kilichotokea na hii ikaongeza mfadhaiko miongoni mwa wana Chadema. Iliponekana wazi kuwa CCM walitumia muafaka kuifedhehesha Chadema ndipo kazi ikaanza.

Kazi ikaanza kwa kuunda tume! na kwa utamaduni wa nchi yetu tume ni kichaka cha kupooza hasira na kuficha maovu kama tulivyorishishwa na CCM na serikali yake, na ndivyo ilivyopokelewa na wana Chadema. Walihoji tume inachunguza kitu gani chama isichokijua? Tumepata majibu kuwa chama kilikuwa na taarifa, kwahiyo ni ukweli kuwa maana halisi ya tume hata kama ilikusudia kuwa tofauti na za CCM ilikuwa adulterated.

Maamuzi yamefanyika kwa taratibu za chama, jambo jema. Excitement iliyotokana na maamuzi ni ushahidi kuwa wana Chadema na wanachi wengine hawakupendezwa na mwenendo mzima wa mambo yalivyokuwa handled.

Ni vema limefanyika lakini lisichukuliwe kama dhalili bali somo ili lisijirudie. Je, maamuzi yaligusa sehemu husika, jibu ni ndiyo na hapana.
Ni ndiyo kwasababu walioleta mtafaruku na wakashindwa kuafikiana na Chama walichukuliwa hatua.
Ni hapana kwa sababu hili halikuwa suala la kata au mji liligusa wilaya na mkoa hadi taifa Kichama, je hapo kati kati hakukuwa na uzembe uliolazimu kuundwa tume, kama upo hatua gani zimechukuliwa na kama haupo je imefafanuliwa?

Nafahamu Chadema wana watu makini sana na utaratibu makini, lakini wao ni wachezaji, je si vema sisi watazamaji tukatoa maoni yetu hata kama hayapendezi lakini yakasikika.

Namalizia kwa kusema Chadema imejifunza lolote kuhusu mwenendo wa mambo ya kisiasa nchini!
Je, Chadema wana political analysts wanaofanya risk assessment. Je, kuna communication inayoridhirisha kati yao wenyewe na political base.
Je, wanaelewa kuwa katika siasa saa moja au kali moja inaweza kuwa na big political ramification achilia mbali siku 14.
Je, kama chama mbadala wamejijnga kwa majukumu na utayari inapotokea hali ya kisiasa na dharura kama ya Arusha.

I wonder if the party is aware that politics is the dirty game, the existence in political sphere depends on viable and vibrant political base. Unnecessary flactuation of moral in political base is the last thing any party would like to see.

senti thumuni,

Ahsante
 
Ahsate Mimibaba kwa maoni yako. Siajkuelewa vema kuhusu declared interest uliyosema, labda nieleze kama nilivyoielewa. Mimi naamini kuwa siasa makini ni moja ya nyenzo za kutuondoa hapa tulipo kuelekea miaka 100. Ni ukweli kuwa uwepo wa vyama vya upinzani umekuwa sehemu muhimu sana ya jamii yetu. Tumeweza kujielewa na kuelewa yale yanayofanyika nyuma ya pazia, na upinzani umeku karibu nasi hata kuwavuta watawala wa nusu karne kutufikia. Enzi hizo kuwasiliana na kiongozi wa serikali lilikuwa kama kosa la jinai, tukiwaona kama wanadamu wenye fursa pekee duniani. Walipokuja akina mh Mbowe, Dr Salaa, Zitto n.k kuchanganyika nasi tunajisikia kama sehemu ya uongozi wa nchi, sasa hata wale waliobweteka wanatufikia.

Kwa mantiki hiyo uimara wa siasa ni muhimu bila kujali mrengo. Nimekuwa nachelea yaliyokikuta CUF yasije kujirudia ndio maana huwa nakuwa mkweli kwa vyama vyote ili tuwe na mfumo imara na si wa misimu. Pengine hilo ndilo linapelekea kuwa muwazi zaidi na lugha kuonekana ya madaraka makubwa.

Nashukuru umeniasa kuwa lugha imekuwa ya madaraka makubwa pengine ukinitahadharisha kuhusu maandiko yangu. Nitajaribu kuwa katika lugha ya kiraia ambayo ndiko niliko, nisichoweza ni kubadili ukweli kwasababu naamini spade ni spade not a big spoon. ha ha ha.

Kuhusu Risk na assumption nakubaliana na wewe kuwa ni vema kuviangalia vitu hivi, si baada ya, lakini kabla ya.
Wakati uongozi wa Chadema unakwenda Arusha kwa nguvu zote walitakiwa watambue hiyo ni risk na walitakiwa wawe na assumption na options a,b,c. Nadhani walifanya hivyo na njiani kukawa na communication breakdown.

Yalipotokea mauaji risk iliongezeka zaidi na hapo walitakiwa kuwa waangalifu wa kila hatua. Sina tatizo na kile walichoamini wanasimamia na ukweli unabaki kuwa kuna nyakati CCM inaweza kulazimisha mtu au watu kuchukua hatua zisizotarajiwa.

Tatizo lipo namna suala lilivyoshugulikiwa. Haiwezekani kuwa uongozi ulikuwa haujui muafaka wa madiwani tukizingatia kuwa kuna madiwani, wabunge, mbunge, uongozi wa wilaya na mkoa. Suala lililochukua taswira ya kitaifa na kimataifa haikuwa muafaka kuliacha liende kwa nguvu za asili. Sikatai kuwepo kwa muafaka kama hilo ni jema kwa Chama na wanachi wameridhia, lakini je kulikuwa na ridhaa ya wanachama na wapenzi wa Chadema? Je, political analysts, pundits na obsevers wa chadema waliweza kufanya riks assessment kwa kuangalia base yao?

Muafaka ulipofikiwa tulitegemea viongozi watoe ufafanuzi. Halikutokea na kiongozi wa CCM labda kwa asumption kuwa ataeleweka na wanachama na wapenzi wa Chadema ndiye aliyesimama na kulitolea taarifa. Katika mchanganyiko huo watu wakahoji, je suala zima lilikuwa umeya wa watu 2?
Ikachukua wiki mbili, licha ya maoni mbali mbali kuwa uongozi utoe kauli. Hakuna kilichotokea na hii ikaongeza mfadhaiko miongoni mwa wana Chadema. Iliponekana wazi kuwa CCM walitumia muafaka kuifedhehesha Chadema ndipo kazi ikaanza.

Kazi ikaanza kwa kuunda tume! na kwa utamaduni wa nchi yetu tume ni kichaka cha kupooza hasira na kuficha maovu kama tulivyorishishwa na CCM na serikali yake, na ndivyo ilivyopokelewa na wana Chadema. Walihoji tume inachunguza kitu gani chama isichokijua? Tumepata majibu kuwa chama kilikuwa na taarifa, kwahiyo ni ukweli kuwa maana halisi ya tume hata kama ilikusudia kuwa tofauti na za CCM ilikuwa adulterated.

Maamuzi yamefanyika kwa taratibu za chama, jambo jema. Excitement iliyotokana na maamuzi ni ushahidi kuwa wana Chadema na wanachi wengine hawakupendezwa na mwenendo mzima wa mambo yalivyokuwa handled.

Ni vema limefanyika lakini lisichukuliwe kama dhalili bali somo ili lisijirudie. Je, maamuzi yaligusa sehemu husika, jibu ni ndiyo na hapana.
Ni ndiyo kwasababu walioleta mtafaruku na wakashindwa kuafikiana na Chama walichukuliwa hatua.
Ni hapana kwa sababu hili halikuwa suala la kata au mji liligusa wilaya na mkoa hadi taifa Kichama, je hapo kati kati hakukuwa na uzembe uliolazimu kuundwa tume, kama upo hatua gani zimechukuliwa na kama haupo je imefafanuliwa?

Nafahamu Chadema wana watu makini sana na utaratibu makini, lakini wao ni wachezaji, je si vema sisi watazamaji tukatoa maoni yetu hata kama hayapendezi lakini yakasikika.

Namalizia kwa kusema Chadema imejifunza lolote kuhusu mwenendo wa mambo ya kisiasa nchini!
Je, Chadema wana political analysts wanaofanya risk assessment. Je, kuna communication inayoridhirisha kati yao wenyewe na political base.
Je, wanaelewa kuwa katika siasa saa moja au kali moja inaweza kuwa na big political ramification achilia mbali siku 14.
Je, kama chama mbadala wamejijnga kwa majukumu na utayari inapotokea hali ya kisiasa na dharura kama ya Arusha.

I wonder if the party is aware that politics is the dirty game, the existence in political sphere depends on viable and vibrant political base. Unnecessary flactuation of moral in political base is the last thing any party would like to see.

senti thumuni,

Ahsante

Nashukuru sana kwa kupanua hoja na ufafanuzi wako. Nilichokiona hapa interest yako kubwa ni mabadiriko kutokana na mwenendo mzima wa maendeleo ya nchi yetu kisiasa, kijamii na zaidi zinavyogusa maisha yetu ya kila siku kuchumi.

Maoni yako nayapa changamoto mbili.

1. Ni kweli issue hapa ni CDM ndiyo maana risks na assumption ulizozijadiri zinahusu CDM (Ya internal to CDM) ingawaje sina uhakika kama umezimaliza. Nilitarajia angalau upate mrejesho toka ndani ya CDM

2. Kisayansi risks na assumptions za ndani ni manageable; failure of which ni udhaifu dhahiri wa ndani. Nilitegemea kusoma external risks na assumptions, mifano role ya CCM na Dola katika mchakato na mgogoro mzima. Ni matarajio yangu utaendelea kuchangia angalau kurespond kwenye observations zangu kwa faida yetu wote.

Maoni yangu ni kuwa situation/scenerio nzima inawezekana hatuijui undani wake ndiyo maana matokeo ya maamuzi ya CDM yanaungwa mkono na baadhi ya watu walio wengi. Pili ninaona role ya external elements nje ya CDM ni kubwa ambayo bila kuzingatia mchango na michagizo yao kwenye suala hili tunaweza kufikia temporary conclusions na solutions. Kwangu hiyo ni greatest risk kwa sababu kama ulivyojadili kuna uwezekano CDM au vyombo vyake vilizembea mahali fulani, kwa upande mwingine tunaweza tukawa tunaona na kutatua dalili za tatizo bila kujiridhisha na kuondoa chanzo chenyewe.

Shida yangu nyingine ni kwamba naamini kabisa humu kwenye forum kuna wahusika wa pande zote ambao hawachangii kutujuza ili michango yetu ijikite kwenye mustakabali (Way Foeward) badala ya kwenye changamoto

Thanks again
 
Ndugu yangu Mimibaba, sitarajii kupata usuli (feedback) kwasababu yapo mambo ya chama yasiyotakiwa kujadiliwa hadharani. Hili la Arusha lina embarrassment kubwa kwahiyo uchangiaji wa wahuisika wa 'pande zote' kama ulivyosema unakinzana na maslahi ya leo au baadaye.
Tulijadili katika kiwango cha mawazo huru na changamoto.

Mgogoro wa Arusha kwa external risk ulikuwa nazo nyingi kutoka CCM na Serikali. Kumbuka Jiji la mwanza lipomikononi mwa Chadema, Mbeya inaelekea huko, Dar es Salaam ndio hofu ilipo-Chadema imepenyeza katika hot spot na gome ya Iringa imeanguka, Singida tayari kuna uasi.
Mahali Salama kwa CCM ni Mtwara, Lindi, Songea, Tanga, Morogoro, Dodoma.
Kuiachia Arusha ni jambo la mwisho na wangetumia mbinu iwe ya moto,ushirikina au ulaghai ili kubaki na kiti cha AR.

CCM wanajua kuwa Mwanza na Arusha zikiongozwa na Chadema kwa mafanikio ya Karatu na Tarime itakuwa ugonjwa unaosambaa.
Wanajua rasilimali za AR, umuhimu wake kama makao ya EAC na ushawishi wa AR kwa mikoa jirani.

Chadema walijua hili ndio maana kampeni yao ilivuka hadi mikoani. Kinachoshangaza walikubalije ulaghai wa CCM kuingia muafaka kwa kutumia madiwani! Walijua lengo ni kuweka Meya wa CCM sio maendeleo ili kuizima Chadema kisiasa,wakakubali mazungumzo.

CCM walipofanikiwa wakatangaza muafaka(jambo jema), halafu wakaanza kampeni za kupaka matope Chadema kuwa ni watu wa vurugu, hawajui wanadai nini, wanakiuka taratibu n.k Pressure ikawepo kutoka katika base ya Chadema iliyokasirishwa sana na muafaka wa kumpa mtu 1 unaibu meya na mwingine mkuu wa kamati kwa gharama kubwa sana ya miasha na ulemavu wa watu.

'External elements' zimekuzwa kwasababu ya internal weakness. Ukitaka kuona udhaifu ni pale kamati kuu inapowasiliana na madiwani moja kwa moja, hatujasikia uongozi wa wilaya au mkoa na ushiriki wake. Maana yake ni kuwa structure haipo sawa. Sijui kama ndio muundo wa Chadema lakini network ya kutoka mwenyekiti Taifa na kuwasiliana na m/kiti wa kata, mhh! naliona tatizo naweza kuwa panaoic, ila ni tatizo.

Hivyo kukawa na external na interna pressure. Siku zote Chadema ni wazito sana wa ku react kwenye political issues! pengine huwa wanatafuta umakini, lakini unapokuwa na suala nyeti kama la Arusha ukaliacha siku 14 lijiulize na kujitolea majibu unasababisha damage kubwa sana.
Hawakufanya damage control katika kipindi cha wiki mbili wakajikuta wanafanya crisis management kwa kuunda tume, ambayo kimsingi haikuwa na sababu ya kuwepo! politically imefanikiwa lakini kimantiki sina uhakika!

Wanachama na wapenzi wamefurahia maamuzi ya CC ya Chadema kwa kuangalia mambo haya;
1. Muafaka haikuwa lengo la maandamano, vifo, ulemavu ili tu mtu awe naibu meya
2. Ilionekana kuwa imewadhalilisha mbele ya umma hasa kwa kejeli za CCM
3. Madiwani wamechukuliwa hatua stahiki kwa utaratibu stahiki na wakati muafaka
4. Chama kimeonyesha njia ya maamuzi magumu hata pale yanapokinzana na masilahi.

Pamoja na excitement iliyopo, inabidi Chadema walichukue suala la Arusha kwa kujitathmini katika mawasiliano, muundo wa chama, damage control startegy na chochote kilichojiri katika sakata zima.

Msimamo wangu ni kuwa sina tatizo na kile Chadema ilichoamua kusimamia Arusha wala sina tatizo na maamuzi. Tatizo nilionalo ni kuwa handling ya ile issue nzima ikiwa ni pamoja na hukumu kwa baadhi, haikuwa katika viwango.
 
Msimamo wangu ni kuwa sina tatizo na kile Chadema ilichoamua kusimamia Arusha wala sina tatizo na maamuzi. Tatizo nilionalo ni kuwa handling ya ile issue nzima ikiwa ni pamoja na hukumu kwa baadhi, haikuwa katika viwango.

Ni matumaini yangu michango yako kwa pamoja imetoa vidokezo muhimu kama ulivyosema tuchangie kwa uhuru na ku focus kwenye changamoto zinazojitokeza. Nakushukuru na kukupongeza
 
Tumekuwa tukiliongea suala la Chadema na maamuzi magumu waliyoyafanya dhidi ya madiwani wao. Nimewahi kuonya kuwa kuwaachia madiwani wawe juu ya mamlaka zao ni kujenga chama kwa haiba na si kwa misingi.

Kuna kijana wa ANC Julius Malema ambaye ni mshiriki mzuri wa siasa za kumuondoa Thabo Mbeki akiwa na Zuma. Siku za nyuma aliwahi kutoa maneno yaliyoashiria ubaguzi, na chama chake kwa aibu kikamuonya bila kumchukulia hatua za nidhamu. Malema ambaye ni maarufu alijiona kuwa yeye ni zaidi ya chama na kwamba alikuwa anaogopwa kwa ushawishi wake. Madhara yake sasa yanaonekana, soma habari ifuatayo

ANC ya Afrika Kusini kumuadhibu Malema
Mkutano mkuu wa chama tawala cha ANC nchini South Africa umeamua kumuadhibu kiongozi wa vijana Julius Malema kwa kuchafua sifa ya chama hicho.

Tuhuma za hivi karibuni zinatokana na kauli zake kuwa Umoja wa Vijana wa ANC utafanya uwezalo kuanzisha mabadiliko ya utawala wa nchi jirani ya Botswana.

Bw Malema alikuwa &#8216;akipanda mbegu za mgawanyiko' ndani ya chama, ANC imesema.
Ni kiongozi mashuhuri Afrika Kusini lakini maoni yake kuhusu kutaifisha madini na mashamba yamesababisha hisia tofauti kutoka kwa umma.

"Komredi Julius Malema amekuwa akituhumiwa kwa matukio kadhaa ya kuvunja katiba ya ANC ikiwemo kuiingiza ANC katika migogoro kupitia kauli na matamshi yake kuhusu Botswana na kupanda mbegu za mgawanyiko katika uongozi wa Chama," Chama hicho kilisema katika taarifa yake.

ANC kinasema suala lake sasa limo mikononi mwa Kamati ya Maadili ya ANC, ambayo itaamua tarehe, mahali na muda wa kusikiliza tuhuma hizo.
Mapema wiki hii, Bw Malema amekiomba radhi ANC kwa kusema kuwa utawala wa serikali ya Botswana ni wa vibaraka na ni
 
Uchaguzi wa Igunga upo mbioni na vyama vyote vinapigana kulitwaa jimbo hilo. Uteuzi wa wagombe umeshaanza ama kukamilika.
Vyama vya CCM,Chadema na CUF vinategemewa kuwa na mchuano mkali.
Ni mapema mno kutathmini mwenendo mzima wa uchaguzi na si kutenda haki kutoa maoni kwa jambo linaloendelea( unfolding)

Pamoja na hayo lipo jambo la kuangalia kwa siku za usoni. CCM kwa ukongwe wake kina mazingira ya kupata wagombea wanaokubalika kwa urahisi kwa sababu kipo madarakani muda mrefu na bado watu wengi wanadhani ni njia rahisi ya kupata madaraka hata kama imani zao zinapingana na sera na matendo ya chama. Wanafahamu kuwa uchakachuaji unaosimamiwa na vyombo vinavyopaswa kuwa 'neutral' hauwezi kukemewe achilia mbali kutenguliwa.

Chama cha Chadema kimesekana kumzuia Erasto Tumbo kwa hoja kuwa itaonekana ametumwa kutoka makao makuu kulingana na wadhifa wake. Erasto Tumbo kwa historia, umaarufu na jina vingeweza kukisaidia chama kupata mgombea mwenye mizizi ndani ya jimbo.

Uamuzi wa Chadema umefanywa kwa busara ya hali ya juu na hata Tumbo kukubali maamuzi hayo ni ukomavu wa kisiasa. Kwa hili inabidi niwapongeze Chadema kwa umakini na jinsi walivyoweza kusoma mazingira ya wapiga kura wao. Ni uamuzi uliolenga kuimarisha chama si kwa uchaguzi huu bali siku zijazo. Ni uamuzi uliompa ugombea mtu asiyejulikana katika medani za kisiasa lakini kwa kuzingatia demokrasia.

Chadema wanatakiwa wasiishie hapo bali wajifunze kwa siku za usoni. Kama wanakubali kuwa mgombea anaweza kutoka katika jimbo bila kuwa na jina kisiasa (jambo zuri kabisa) ni vema wakaangalia namna ya kuweza kuwaandaa wagombea wao siku za usoni kutoka huko huko kwa wapiga kura. Tuna mifano mizuri kuwa wapiga kura wanawafahamu wagombea wao vema kuliko uongozi mzima wa chama.

Felix Mkosamali wa NCCR ni kijana mdogo lakini amefanya vema katika jimbo lake. Zitto amekulia ndani ya chama na sasa ni moja ya viongozi katika ngazi ya taifa. Mnyika hata baada ya kushindwa uchaguzi aliendelea kuwa mshiriki wa jimbo lake na sasa ni mbunge. Halima Mdee alijikita katika jimbo moto na kukulia huko akipigana vikumbo na magwiji na kuibuka kidedea.
Regia Mtema pamoja na Chadema kutokuwa na mizizi Kilombero ameingia huko na kulijenga jina lake, leo au kesho akirudi Kilombero si mgeni tena miongoni mwa wananchi wa Kilimbero. mifano ni mingi.

Vijana wanaokulia ndani ya chama chao wanakuwa na nidhamu kuliko kusubiri watu walioachwa na vyama vingine kama akina Shibuda.
Muda wa kuwaandaa wagombea wa baadae wanaokubalika na wenye mapenzi ya nchi na chama ni sasa. Chadema ianze na mkakati wa kuwalea viongozi wa baadaye kadri wanavyoweza na kutambua 'potential zao' sasa ili kuepuka ima kuchukua makapi au mgombea anayeuzika kwa shida.

Ni kwa mantiki hiyo Chama kifanye mkakati wa makusudi wa kuwafikia watu wote hata kule kunakoaminika hakuna matumaini kichama.
Hakuna aliyejua kuwa Dar es Salaam shina la CCM lingemeguka na kuwa na wabunge wawili. Ni makosa kufikiri Lindi, Mtwara, Tanga au Songea hilo haliwezi kutokea. Linaweza lakini je kuna maandalizi ya muda mrefu? kuna mbegu zilizopandwa?

Tutafakari
 
Ahsate Mimibaba kwa maoni yako.
Kwa mantiki hiyo uimara wa siasa ni muhimu bila kujali mrengo. Nimekuwa nachelea yaliyokikuta CUF yasije kujirudia ndio maana huwa nakuwa mkweli kwa vyama vyote ili tuwe na mfumo imara na si wa misimu. Pengine hilo ndilo linapelekea kuwa muwazi zaidi na lugha kuonekana ya madaraka makubwa.

Nitajaribu kuwa katika lugha ya kiraia ambayo ndiko niliko, nisichoweza ni kubadili ukweli kwasababu naamini spade ni spade not a big spoon. ha ha ha.

Kuhusu Risk na assumption nakubaliana na wewe kuwa ni vema kuviangalia vitu hivi, si baada ya, lakini kabla ya.
Wakati uongozi wa Chadema unakwenda Arusha kwa nguvu zote walitakiwa watambue hiyo ni risk na walitakiwa wawe na assumption na options a,b,c. Nadhani walifanya hivyo na njiani kukawa na communication breakdown.

Yalipotokea mauaji risk iliongezeka zaidi na hapo walitakiwa kuwa waangalifu wa kila hatua. Sina tatizo na kile walichoamini wanasimamia na ukweli unabaki kuwa kuna nyakati CCM inaweza kulazimisha mtu au watu kuchukua hatua zisizotarajiwa.

Tatizo lipo namna suala lilivyoshugulikiwa. Haiwezekani kuwa uongozi ulikuwa haujui muafaka wa madiwani tukizingatia kuwa kuna madiwani, wabunge, mbunge, uongozi wa wilaya na mkoa. Suala lililochukua taswira ya kitaifa na kimataifa haikuwa muafaka kuliacha liende kwa nguvu za asili. Sikatai kuwepo kwa muafaka kama hilo ni jema kwa Chama na wanachi wameridhia, lakini je kulikuwa na ridhaa ya wanachama na wapenzi wa Chadema? Je, political analysts, pundits na obsevers wa chadema waliweza kufanya riks assessment kwa kuangalia base yao?

Muafaka ulipofikiwa tulitegemea viongozi watoe ufafanuzi. Halikutokea na kiongozi wa CCM labda kwa asumption kuwa ataeleweka na wanachama na wapenzi wa Chadema ndiye aliyesimama na kulitolea taarifa. Katika mchanganyiko huo watu wakahoji, je suala zima lilikuwa umeya wa watu 2?
Ikachukua wiki mbili, licha ya maoni mbali mbali kuwa uongozi utoe kauli. Hakuna kilichotokea na hii ikaongeza mfadhaiko miongoni mwa wana Chadema. Iliponekana wazi kuwa CCM walitumia muafaka kuifedhehesha Chadema ndipo kazi ikaanza.

Kazi ikaanza kwa kuunda tume! na kwa utamaduni wa nchi yetu tume ni kichaka cha kupooza hasira na kuficha maovu kama tulivyorishishwa na CCM na serikali yake, na ndivyo ilivyopokelewa na wana Chadema. Walihoji tume inachunguza kitu gani chama isichokijua? Tumepata majibu kuwa chama kilikuwa na taarifa, kwahiyo ni ukweli kuwa maana halisi ya tume hata kama ilikusudia kuwa tofauti na za CCM ilikuwa adulterated.

Maamuzi yamefanyika kwa taratibu za chama, jambo jema. Excitement iliyotokana na maamuzi ni ushahidi kuwa wana Chadema na wanachi wengine hawakupendezwa na mwenendo mzima wa mambo yalivyokuwa handled.

Ni vema limefanyika lakini lisichukuliwe kama dhalili bali somo ili lisijirudie. Je, maamuzi yaligusa sehemu husika, jibu ni ndiyo na hapana.
Ni ndiyo kwasababu walioleta mtafaruku na wakashindwa kuafikiana na Chama walichukuliwa hatua.
Ni hapana kwa sababu hili halikuwa suala la kata au mji liligusa wilaya na mkoa hadi taifa Kichama, je hapo kati kati hakukuwa na uzembe uliolazimu kuundwa tume, kama upo hatua gani zimechukuliwa na kama haupo je imefafanuliwa?

Nafahamu Chadema wana watu makini sana na utaratibu makini, lakini wao ni wachezaji, je si vema sisi watazamaji tukatoa maoni yetu hata kama hayapendezi lakini yakasikika.

Namalizia kwa kusema Chadema imejifunza lolote kuhusu mwenendo wa mambo ya kisiasa nchini!
Je, Chadema wana political analysts wanaofanya risk assessment. Je, kuna communication inayoridhirisha kati yao wenyewe na political base.
Je, wanaelewa kuwa katika siasa saa moja au kali moja inaweza kuwa na big political ramification achilia mbali siku 14.
Je, kama chama mbadala wamejijnga kwa majukumu na utayari inapotokea hali ya kisiasa na dharura kama ya Arusha.

I wonder if the party is aware that politics is the dirty game, the existence in political sphere depends on viable and vibrant political base. Unnecessary flactuation of moral in political base is the last thing any party would like to see.

senti thumuni,

Ahsante
Mkuu Nguruvi3 , kwanza naendelea kukushukuru, pia namshukuru na Mimi baba, kwa kuku-provoke ukaileta hazina hii uliyoihifadhi moyoni mwako. Kiukweli mimi nilipenda siasa tangu shule ya msingi, nikasoma journalism nikajikita kwenye political programs, nikajiunga chuo kikuu, UDSM, kusoma something else huku nikijiaminisha siasa tayari naijua, lakini sasa, kupitia michango yako humu, ndio sasa najirealise kumbe mimi siasa siijui, ni sifuri kabisa katika siasa!. Kupitia michango yako, sio tuu naiona Chadema katika mwanga mpya, bali sasa ndio nauona uchambuzi wa kisiasa wa ukweli na unaotokana na hard facts na sio hisia au mapenzi tuu ya siasa za mrengo fulani.

Kwa vile thread ilianza kwa mtazamo hasi (a big mistake), nadhani wahusika wakuu Chadema na wapenzi wao, hawasomi anything negative kuhusu chama chao, lakini naamini michango yako hii ni muhimu sana kwao than anyone else. Naomba ama uicompile na kuianzishia mjadala neutral ili Chadema wenyewe wasome.

Nimetamani niicompile mimi mwenyewe lakini tayari wamesha ni label, "nina langu jambo dhidi yao", hivyo chochote nitakachoandika kuhusu Chadema, kinaweza kuattract a bad impact tukakosa michango objective kama hii.

Pasco.
 
Nguruvi3, kwanza naendelea kukushukuru, pia namshukuru na mimi baba kwa kuku-provoke ukaileta hazina hii uliyoihifadhi moyoni mwako. Kiukweli mimi nilipenda siasa tangu shule ya msingi, nikasoma journalism nikajikita kwenye political programs, nikajiunga chuo kikuu kusoma something else huku nikijiaminisha siasa tayari naijua. Kupitia michango yako, ndia sasa najirealise kumbe mimi ni sifuri kabisa katika siasa. Kupitia michango yako, sio tuu naiona Chadema katika mwanga mpya, bali sasa ndio nauona uchambuzi wa kisiasa wa ukweli na unaotokana na hard facts na sio hisia au mapenzi tuu ya siasa za mrengo fulani.

Kwa vile thread ilianza kwa mtazamo hasi (a big mistake), nadhani wahusika wakuu Chadema na wapenzi wao, hawasomi anything negative kuhusu chama chao, lakini naamini michango yako hii ni muhimu sana kwao than anyone else. Naomba ama uicompile na kuianzishia mjadala neutral ili Chadema wenyewe wasome.

Nimetamani niicompile mimi mwenyewe lakini tayari wamesha ni label, "nina langu jambo dhidi yao", hivyo chochote nitakachoandika kuhusu Chadema, kinaweza kuattract bad impact tukakosa michango objective kama hii Pasco
Awali niwashukuru wote wachangiaji,wasomaji na wale wanaotukosoa au kutupongeza. Jambo zuri sana na linalonifurahisha katika thread hii ni ukomavu wa kubadilishana mawazo bila kuwa na hisia za kejeli, dharau au vinginevyo. Utulivu huo ndio umetuwezesha tujifunze mengi,tukubaliane au tupingane kwa hoja. safi sana!

Pili, Pasco hapo nilipopigia mstari '......kumbe ni sifuri katika siasa' sikubaliani na wewe kwasababu unapoanzisha mjadala kwa mawazo yako huru na ukapata wachangiaji wenye mitizamo tofauti ni sehemu kubwa sana ya uelewa na fikra. Si muhimu wangapi wanakubaliana na wewe na wangapi wanahitilafiana, muhimu ni je mjadala umeamsha hisia na mitazamo tofauti? Hicho ndicho kipimo muhimu na upo njia sahihi sana ndugu yangu.

Katika suala la thread ingawaje sikuona tatizo kubwa na iliyopo,kwa kuheshimu mitazamo yenu napendekeza tuwe na thread itakayozungumzia mambo neutral kwa uhalisia wake. Tuiite 'Duru za siasa'.

ahsanteni
 
Kweli Iza!
Nimependa sana conclussion ya hii thread na mtiririko wote...
Kwa muda nimekuwa naipitia tu bila kutia neno zaidi...
Heshima zaidi kwa Pasco, Mimibaba, Nguruvi3 na wewe Iza!
Viva JF.

Kila nilipokuwa nikiandika kitu nadelete naona kama vile napoteza flow ikabidi niwaachie magwiji,ila kama Nguruvi3 alivyoshauri ni vyema hiyo 'Duru za Siasa" ikaanzishwa lakini ikiwa strictly ni hoja tupu iwe ni ya kuunga mkono au kupinga kama matusi au kejeli Mods waziondoe ASAP..
 

Uandishi huu unatia shaka kwani mwanzoni ulionyesha kuwa hauna upande lakini baadaye unaonyesha dalili za kuwa upande fulani. Huu ni unafiki na wahenga wanasema ni Afadhali ya mchawi kuliko mnafiki.

Nadhani CDM wamefanya kile kitu ambacho wenzao wa CCM wameshindwa kukifanya hadi wakafikia kutishiwa na watuhumiwa. Nadhani mnakumbuka waliodai "ukimwaga ugali tutamwaga mboga". Je, hayo ndiyo anayokumbatia Pasco?

Inabidi akumbuke hata ingekuwaje nidhamu ni jambo muhimu sana kwenye uongozi-mengine yanafuata.
 
Wanabodi,

Kitendo cha Kamati Kuu ya Chadema kuwavua uanachama madiwani wake wa Arusha, is "A Big Mistake"!, and there is a price to pay, so Chadema must pay the price which is very high!.

1. Ile sheria ya kulazimisha wawakilishi wa wananchi, lazima wadhaminiwe na vyama, its a bad law, na inakwenda kinyume cha Katiba ya JMT inayotoa uhuru kwa kila raia kushiriki katika uongozi wa serikali tangu ya mitaa hadi serikali kuu, hadi mahakama kuu ilishatoa rulling hicho kipengele kuwa ni 'unconstitutional' na kiwe struck out from the books of law!. Naamini Chadema hilo wanalifahamu, hivyo kitendo cha kutumia kipengele hicho hicho ambacho ni bad law, to its advantage, is "A Big Mistake!".

2. Ukishachaguliwa, Diwani au Mbunge, hata kama ulidhaminiwa na chama, wewe, unakuwa umechaguliwa na wananchi, na unakuwa ni mtumishi wa watu na kule kwenye ngazi za maamuzi, Baraza la Madiwani na Bungeni, unawakilisha maslahi ya wananchi waliokutuma, na sio maslahi ya chama kilichokudhamini, japo katika uwakilishi wako, pia maslahi ya chama yatazingatiwa. Kitendo cha chama kuwafukuza wawakilishi halali wa wananchi kwa maslahi ya chama, is "A Big Mistake!".

3. Sisi ambao hatuna vyama, lakini tuna shauku ya kuona Tanzania inaongozwa na chama mbadala, tumekuwa na imani kubwa sana na Chadema kama ndicho chama pekee mbadala ambacho kimethibitisha kikiaminiwa, kinaweza kuleta mabadiliko ya kweli. Hivyo tunategemea Chadema kitafanya maamuzi yanayofuata misingi ya haki. Kitendo cha kuwavua uanachama madiwani wake hawa, waliochaguliwa na wananchi, (sio chama) bila kuwasikiliza, ni kuwa "condem Unheard", which is against principles of Natural Justice, and this is a "A Big Mistake!"
Nafanya tuu rejea ya baadhi ya makosa ambayo Chadema imeyafanya na ikavuka salama!, ila hili la kumtumua Zitto, sio kosa, ni zaidi ya kosa!, its a blunder!, Chadema imefanya blunder na haitavuka salama!.

Pasco.
 
Mkuu Mkandara Nikushukuru kwa ujenzi wa hoja zako. Nipitie baadhi kwa kiasi nitakachojaaliwa.

1. Suala la Kafulila ZZK hakupinga kufukuzwa kwasababu ya kupoteza jimbo. Motive behind Kafulila ilikuwa ni uongozi wa kikanda na ukabila ili Zitto apate mwanya.

Tuhuma hizo zilipaswa kukemewa na ZZK kabla ya kupinga hatua. Zitto hakuzikemea ikimaanisha alikubaliana. Leo tunajua ule ulikuwa mwanzo wa 'waraka' ingeshangaza Zitto kuwatosa vijana wake.

Kafulila alipinga kubadilishwa nafasi,mabadiliko yaliyolenga kuondoa chokochoko kwa mtindo wa kuvumiliana. Mwisho Kafulila akaona hana namna nzuri ya kuishi CDM akajitoa na wala hakufukuzwa.

Chama kinachopigania kuondoa uzembe na kuchukua hatua kikimewanyooshea kidole CCM hakipaswi kuogopa kupoteza jimbo kwasababu ya mtu fulani.

Ni kutokana na hilo pengine watanzania wakaona CDM ni mbadala wa CCM na kukiunga mkono katika maeneo mengine ambako CDM ilikuwa haijulikani.

Kusema kuwa kuna kupoteza jimbo na kusahau kuwa hiyo ni sehemu ya political investment sidhani kuwa ni sahihi.

Marehemu Sokoine alipendwa si kwasababu aliwakumbatia wenzake bali alisimama kidete kwa kilicho sahihi. Kuendelea kuishi na watu wasioamini katika kile wanachokisema au kukitetea ni aina ya unafiki.

2. Lowasa hakuachwa CCM kwasababu ya kulinda chama. Ameachwa CCM kwasababu ya kulindwa na swahiba wake.

Kikao cha NEC Butiama kilichowashirikisha marais wastaafu ukiacha mkapa, mawaziri wakuu wa zamani, wadhamini wa CCM kiliazimia kuwafukuza akina Lowasa. Mkutano wa kwanza uliotoa azimio ulikuwa wa Makongoro na wenyeviti wa mikoa.

Aliyeahirisha kikao ni mwenyekiti wa CCM na aliyepiga hoja dana dana alikuwa mzee Ngunge na Yusuph. Dhana kwamba walimwacha ili kulinda siri zao si sahihi, aliachwa na mwenyekiti ili kulinda siri zao kwasababu 'hawakukutana barabarani'

Haya unayoyasikia ya akina Nape na Mangula ni 'pre-lude' ya kile kinachokuja siku za karibuni. Yote ya akina Lowasa yataibuka upya kwasababu ni jipu lililovia, bado lina usaha na halijatumbuliwa.

3. Kwamba kamati kuu imekurupuka hilo nakubaliana nalo.
Kulihitajika umakini zaidi. Kwa mfano, kulikuwa na sababu gani za Slaa na Mbowe kwenda Kigoma na Mwanza wakati gogoro linaunguruma na bila suluhisho.

Kuwavua uongozi ilikuwa hatua ya mwanzo ingawa iligubikwa na jazaba.
Hata hivyo lazima tukumbuke kuwa Zitto hakutaka kuhudhuria kikao jambo lililo wa provoke zaidi wajumbe na pengine kupoteza mwelekeo.

Hoja yangu siku zote ni kuwa ili kumaliza gogoro ilitakiwa tume huru kwani ingekuja na ukweli. Hilo halikuzingatiwa na kutoa nafasi kwa mahakama ambapo mambo mengi zaidi yatajitokeza.

4. Kwamba Zitto yu 'ICU' na hivyo anapigania roho yake kisiasa hilo sikubaliani nalo.
Zitto yupo mtaani anadunda kwa kasi kubwa tu. Angekuwa ICU asingekwenda kwenye vyombo vya habari na mikoani kuhutubia mikutano.

Pengine ukimya ungesaidia zaidi watu kurudisha nyoyo zao na kusema kijana anakua 'aachwe abalehe'. Lakini uniambie yu ICU wakati anazidi kubomoa CDM! Huko ICU watu wanapumulia mashine, yeye anatembea na mashine, ICU gani hiyo Mkandara!

5. Kuhusu hoja za Mzee Mwanakijiji kumtaka ajivue uanachama, kama nilivyomuelewa kwa tafsiri yangu binafsi ni kuwa ZZK yupo 'mahututi kisiasa'

Utaalam unaonyesha yupo katika vegetative state, kwamba mwili wa kisiasa upo lakini brain imekufa. Mwanakijiji anamaanisha ZZK wa vegetative state sasa ni wakati akubali life support iondolewe.

Mantiki ni kuwa kila mtu 'anapigania roho yake' akiwa wodini, lakini kwa hili la ZZK, manesi, madaktari, ndugu jamaa na marafiki hata wanaokuja kusalimia wagonjwa wa jirani wamechoka kuuguza.
Wanasema mgonjwa sasa ni wakati aondoke ili 'bwana atoe bwana atwae' maisha yaendelee.

5. CDM ndio waliopiga ngoma za kupunga mapepo na wachawi wamekuja. Kama wasingepiga madebe wachawi wasingesogelea.

Kuwalaumu wachawi wanaofuata ngoma za mapepo ni makosa, kwanini asilaumiwe mpiga zumari na ngoma kwa kuita wachawi ili hali walijua ngoma za mapepo huvuta wachawi?

Ngoma ikipigwa kila atakaye kucheza hucheza, lakini kila ngoma ina mwenyewe na mwenye ngoma ya sasa ni Zitto.

Tabia yake ya kutembea na manyanga, kukutwa na viungo, kuvaa vibwenda usiku japo hajawahi kukamatwa na kidhibiti ni ushahidi kuwa ngoma inayoleta wachawi anaijua na kamba utaalamu huo anao.

Ushanfahamu mkubwa!
 
tukakanyaga katiba yetu, Huu ni uongo wa mchana Katiba ya CHADEMA imeandikwa 2006 na kufanyiwa marekebisho mwaka 2016 na mwaka 2019 muda wote huo hakuna ilipowahi kukanyagwa. Labda ututhibitishie ni kifungu gani kiliwahi kukanyagwa na kwa dhumuni lipi.
Na Yericko Nyerere
Mkuu Yericko, nimekusoma mahali, kuwa Chadema haijawahi kukanyaga kifungu chochote cha katiba yake.

Utaratibu wa kufukuza uanachama Chadema unatawaliwa na kifungu No. 5.4.6
Tangu fukuza fukuza ya wanachama wa Chadema, jee kuna hata mara moja mmewahi kukifuata?

Na kwa faida ya wasiofahamu utaratibu wa kufukuza wanachama kwa mujibu wa katiba ya Chadema ni huu

QUOTE="Pascal Mayalla, post: 5404773, member: 17813"]
  • Kwa mujibu wa katiba ya CHADEMA, ili kumvua mtu uanachama kuna mlolongo wa kanuni na taratibu za kufuatwa na miongoni mwake ni hizi nitakazo ziorodhesha hapa chini, jee zilifuatwa?.
  • Kuandaa Hati ya Mashtaka kwa maandishi yenye tuhuma zote ambazo mtuhumiwa anakabiliwa nazo. Jee hati hizi za mashitaka kimaandishi ziliandaliwa?.
  • Hati hiyo ya mashitaki kimaandishi inatakiwa ikabidhiwa kwa mtuhumiwa kwa "despatch" ili kuthibitisha imemfikia, jee hili lilifanyika?, nimesikia kuna watu waliitwa kwa simu, jee huu ndio utaratibu kwa jambo zito kama hili?.
  • Mtuhumiwa atatakiwa kuzijibu tuhuma za mashitaka hayo ndani ya kipindi cha siku 14 tangu tarehe aliyopokea barua ile ili apate muda wa kutosha kutafakari, jee hili lilifanyika?.
[/QUOTE]
Mkuu Yericko, unakumbuka madiwani hawa walifukuzwaje?, utaratibu ulifuatwa?.
P
 
Naitafakari sana jinsi Chadema inavyofanya mistakes mwaka wa uchaguzi!, haswa CC ya Chadema kutoa maamuzi ya kutimua wanachama wake kidikiteta. Katiba ya Chadema ipo, imeweka utaratibu wote wa nidhamu kwa kila ngazi, kwanini hawafuati katiba yao?.
Nilianza kuwalalamikia hapa
Uamuzi wa CHADEMA dhidi ya madiwani: "A Big Mistake!" - JamiiForums
Nikaja hapa,
Wito: CHADEMA Watendeeni Haki Wanachama Wenu Ili Kuwatendea Haki Watanzania 2015! - JamiiForums
Na baada ya kumtimua Lwakatare, nimewaeleza
Haya.
Je, wajua kuwa hatma ya CHADEMA ipo mikononi kwa Lwakatare?. Baada ya CHADEMA kumwaga ugali, Lwaka akiamua kumwaga mboga, CHADEMA Kwishney! - JamiiForums

Mwenye masikio na masikio.
P
 
Naitafakari sana jinsi Chadema inavyofanya mistakes mwaka wa uchaguzi!, haswa CC ya Chadema kutoa maamuzi ya kutimua wanachama wake kidikiteta. Katiba ya Chadema ipo, imeweka utaratibu wote wa nidhamu kwa kila ngazi, kwanini hawafuati katiba yao?.
Nilianza kuwalalamikia hapa
Uamuzi wa CHADEMA dhidi ya madiwani: "A Big Mistake!" - JamiiForums
Nikaja hapa,
Wito: CHADEMA Watendeeni Haki Wanachama Wenu Ili Kuwatendea Haki Watanzania 2015! - JamiiForums
Na baada ya kumtimua Lwakatare, nimewaeleza
Haya.
Je, wajua kuwa hatma ya CHADEMA ipo mikononi kwa Lwakatare?. Baada ya CHADEMA kumwaga ugali, Lwaka akiamua kumwaga mboga, CHADEMA Kwishney! - JamiiForums

Mwenye masikio na masikio.
P
Mayalla: Bado naamini wewe ni mwaandishi mahiri sana. Kasoro ni kuwa uliamua kujitoa ufahamu kwa maslahi ya CCM.

Baada ya kugundua uchonganishi wako wa wapinzani kwa serikali hakukusaidii ushauri wangu mdogo rudisha ufahamu sasa tuendelee kufaidi uwezo wako uliopewa na Mungu.

Hata madiwani waliofukuzwa au kununuliwa unajua kilichowapata.
 
Wanabodi,
Hili ni bandiko la wito kwa Chadema na ushauri wa bure, kiwatendee haki wanachama wake, ili ifikapo Octoba 2015, Watanzania waiaminie Chadema kuwa itawatendea haki Watanzania. Kitendo cha kutowatendea haki wanachama wake, kutapelekea wanachama hao kunyanyasika na kulia machozi ya ndani kwa ndani, hayo machozi ya ndani kwa ndani, yanabeba karma liability kubwa sana, hivyo mbele ya safari, Chadema itakuja kukumbwa na majanga makubwa ya ajabu ambayohawatajua chanzo chake, kumbe ni matokeo tuu ya matendo yake chenyewe.

Ushauri huu lengo lake ni kutuaminisha sisi Watanzania wengine tusio wanachama wa CHADEMA, kuwa Chadema ni chama cha haki na kinafanya maamuzi yake kwa haki kufuata misingi ya sheria, taratibu na kanuni za haki, hivyo kutupa matumaini kuwa CHADEMA inaweza kuaminika na kukabidhiwa nchi mwaka 2015!, vinginevyo kwa mambo haya kama yalivyo sasa, na kama CHADEMA haitabadilika, then kwa 2015 CHADEMA itakuwa bado haijakomaa kiasi cha kutosha kuaminika na kukabidhiwa nchi!.

Naomba Kuwasilisha.

Pasco
CHADEMA mnazani watanzania ni wajinga?

Yaaani mnaongoza harakati za kudai Katiba Mpya ya nchi wakati nyie kwenye chama chenu hakuna Haki wala demokrasia.

Mtatushawishi vipi wakati nyie wenyewe chama chenu kinaendeshwa na sauti ya mtu mmoja.
Mkuu Ritz , angalia tarehe ya bandiko hili, nilisema nini na nilishauri nini!.
Haki ni jambo la msingi sana, hata hawa Wabunge 19 wa Chadema alikuwa wasipo tendewa haki, karma lazima itaendelea kuitembezea Chadema kichapo cha bakora za jumla jumla za karma kwa Chadema kama chama, huku viongozi wake individually nao wakila bakora zao individually according to the roles they play, kama kiongozi ame play a big role, anatandikwa bakora kubwa, na kama ameplay a small role ana tandikwa fimbo ndogo.

Tatizo la bakora za karma, ni hazina specific time frame, tangu ufanye uovu ni muda gani utapita kabla hujalipwa ulichofanya, sometimes it's instant tit for tat, hivyo unaweza kujua, sometimes unapita muda mrefu sana hata miaka kabla karma haijakulipisha, hivyo wakati unalipa unakuwa hukumbuki tena ulifanya nini!. Chama kilichokuwa na wabunge zaidi ya 50 tena majimbo ya haja na majiiji , leo kina Mbunge mmoja tuu wa jimbo!.

Hii sii kawaida!, hakuna mtu anayekumbuka ya nyuma Chadema ilifanya nini, au kinachowakuta viongozi wa Chadema individually, no one can connect the dots, wanahesabu ni majanga tuu, kumbe ndio karma yenyewe!.

P
 
Katika suala la thread ingawaje sikuona tatizo kubwa na iliyopo,kwa kuheshimu mitazamo yenu napendekeza tuwe na thread itakayozungumzia mambo neutral kwa uhalisia wake. Tuiite 'Duru za siasa'.

ahsanteni
Mkuu Nguruvi3, where is "Duru za Siasa"?. Nimekamisha mchakato wa kuanzisha kipindi kipya cha TV cha political discussion kiitwacho " Kwa Maslahi ya Taifa", demo za kipindi hicho zitaanza kuruka TV mbalimbali this week, mfano leo Saa 3:00 usiku on TBC, kesho Saa 3:00 usiku on ITV, Jumapili Saa 3:30 usiku on Channel Ten.

I would like to look for you in one of these programs ili tuyatumie madini yako kulisaidia taifa, na ikitokea ukakubali, kule kwenye TV program, sitakutaja kuwa wewe ni fulani kule JF.

Pia I know kuna watu wanapenda kulisaidia taifa under animosity bila kujulikana kama Bhakhresa anavyosaidia watu, hutakaa usikie, hivyo ukiamua kuendelea kusaidia taifa kupitia jf only, pia nitauheshimu msimamo wako.

Thanks in advance
Paskali
 
Back
Top Bottom