Uamuzi wa CHADEMA dhidi ya madiwani: "A Big Mistake!"

Sheria hiyo kandamiziambayo hata mimi siiungi mkono inawanyima wananchi haki ya kuendelea kupata huduma ya mwakilishi wao waliyemchagua, sheria hiyo haiwaelekezi madiwani kutotii maamuzi yaliyotolewa na viongozi wao wa chama, nadhani uchore mstari kati ya hivyo viwili.

Najaribu kutaka kuelewa pendekezo lako ni lipi kwa hali kama hii iliyotokea kwa madiwani kukaidi maelekezo ya kamati kuu. Labda kwa ufupi tu,unaweza kuniambia wewe kwa mtazamo wako kamati kuu ya chadema ilipaswa kutoa uamuzi gani?
TLP ilikuwa na Mbunge mmoja tuu bunge lililopita, ni Benedict Mutungurehi (RIP), (Biharamulo), mara tuu baada ya uchaguzi, wakatibuana na M/Kiti wake Mrema, Mrema kamfukuza uanachama, aliopokwenda mahakamani, uamuzi ule ulisitishwa, ila wananchi wa Biharamulo, walikosa uwakilishi kwa miaka minne.

Hivi ndivyo nilivyosema kuhusu TLP.

Pamoja na yote aliyoyafanya Mrema, Mutungurehi bado ni mwanachama halali wa TLP na ni Katibu Mwenezi, kwa sababu zoezi zima limekiuka Katiba ya TLP, na kama kweli wajumbe waliridhia, basi TLP hakuna Chama.
Kwa kufuata principles of natural justice, 'No one is condemmed unheard', Mrema alipaswa kumuelekeza Katibu Mkuu wake kuitisha Kikao cha dharura cha Secretarieti ya Nec ya TLP na kuwasilisha agenda hiyo ya kumfukuza Mutungurehi, azmio la secretarieti hiyo ndilo lenye mamlaka ya kuitisha kikao cha dharura cha Nec ya TLP na kuijadili hiyo ajenda iliyo mbele yake, halafu Mutungurehi, angepaswa kuitwa na kuhojiwa kabla ya kufukuzwa. Hata kama angekataa, basi mamlaka ya kikao hicho ni kumsimamisha uanachama na kupeleka azimio hilo Mkutano Mkuu ambao ndio wenye mamlaka ya kikatiba ya kufanya hivyo.

Mrema yeye ndiye Mwenyekiti wa TLP, na Katibu ndiye Yeye, Kamati Kuu ni Yeye, Sectarieti ya TLP pia yeye, Halmashauri Kuu ni yeye na amejifanya pia ndiye Mkutano Mkuu kumfukuza Katibu Mwenezi ili awe yeye!. Huu ni udikiteta wa hali wa juu na naamini Msajili wa vyama halalifumbia macho hili, yaani chama chote kiko mfukoni!.
 
Pasco kama unasomea sheria na uko ndani ya nchi hii hii lakini hujafanya jitihada za kujua ni kwa kiasi gani hao jamaa walipewa nafasi namuda wa kusikilizwa, basi nina shaka kwamba unaweza kuhitimu na kupata cheti cha sheria lakini isikusaidie sana wewe binafsi na taifa kwa ujumla wake.

Kamati ya marando ilikwenda arusha na ikawasikiliza madiwani wote wa arusha, na bado jana kabla ya kufikiwa uamuzi huumadiwani wakaidi waliitwa dodoma na kupewa nafasi nyingine tena ya kusikilizwa. Sasa unaposema hiyo principle of natural justice haikuzingatiwa basi hapo ndo napata mashaka na uelewa wako wa hiyo principle of natural justice.

Mwita Maranya, nimekuambia sheria, nimefuta tongotongo.

Ndivyo ulivyoambiwa Kamati ya Marando iliwahoji madiwani wote?. Hivi ilizikia sababu zao kuitunishia misuli CC yao?.

Kama Marando unafahamiana naye kwa karibu, muulize vuzuri. Nilikuwa nae hoteli moja hapa Dodoma, na leo asubuhi wanakati ana check out, kuna kitu nimezungumza nae, hebu muulize nimemwambia nini kuhusu uamuzi huo?.
 
bOSS,

YOU PICKED A VERY WRONG EXAMPLE... RAILA NI JAMBAZI, NA KWA MTIZAMO WA CCM, YULE JAMAA KAMA NI BONGO WANGESHAMUUA TENA KABLA HAJAFIKISHA HATA MIAKA 45

GIVE US ANOTHER EXAMPLE

mkuu nimetoa mifano ya obama na reagan sijui umeiona???????
 
Labda tu nimkumbushe Pasco kusoma ile habari ya hawa jamaa kufukuzwa.

Mmoja hakufukuzwa kwa sababu tu hakufika kwenye mkutano. Pamoja na kujua hatima ya yatakayomfika kwa kitendo cha yeye kukwama kufika, wamemuweka kiporo. Pasco, PULIZI.

By the way: Umesema Wapinzani wakiingia Ikulu watanyonga watu?! Je huoni hata wana CCM ambao wao wanatangaza kabisa kunyonga? Mbona mnakuwa mnaegemea upande mmoja hadi kila mtu anaona?
Deo Filikunjombe, Mbunge wa Ludewa (CCM) anasema umefika wakati kwa serikali ya chama hicho kutoa adhabu kali kwa makada wake na watendaji wa serikali wanaobainika kushiriki katika ubadhirifu ikiwezekana wanyongwe.

Kutoka: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-makundi-na-chuki-kuelekea-urais-2015-a.html

Pasco kama unasomea sheria na uko ndani ya nchi hii hii lakini hujafanya jitihada za kujua ni kwa kiasi gani hao jamaa walipewa nafasi namuda wa kusikilizwa, basi nina shaka kwamba unaweza kuhitimu na kupata cheti cha sheria lakini isikusaidie sana wewe binafsi na taifa kwa ujumla wake.

Kamati ya marando ilikwenda arusha na ikawasikiliza madiwani wote wa arusha, na bado jana kabla ya kufikiwa uamuzi huumadiwani wakaidi waliitwa dodoma na kupewa nafasi nyingine tena ya kusikilizwa. Sasa unaposema hiyo principle of natural justice haikuzingatiwa basi hapo ndo napata mashaka na uelewa wako wa hiyo principle of natural justice.
 
TLP ilikuwa na Mbunge mmoja tuu bunge lililopita, ni Benedict Mutungurehi (RIP), (Biharamulo), mara tuu baada ya uchaguzi, wakatibuana na M/Kiti wake Mrema, Mrema kamfukuza uanachama, aliopokwenda mahakamani, uamuzi ule ulisitishwa, ila wananchi wa Biharamulo, walikosa uwakilishi kwa miaka minne.

Hivi ndivyo nilivyosema kuhusu TLP.

[/COLOR]

Kwanza kabisa kabla sijaenda mbali nikukumbushe tu kwamba Benedict Mutungirehi hajwahi kuwa mbunge wa biharamulo, hakuawhi mbunge katika bunge lililopita na kubwa zaidi huyu bwana hajafa.

Bila shaka unamchanganya na marehemu Phares Kabuye, ndiye alikuwa mbunge wa biharamulo na alifariki wakati akifuatilia rufaa yake baada ya mahakama kuu kutengua ushindi wake, na pia hakuwahi kuwa na ugomvi na mrema hadi kufikia kuvuliwa uanachama.

Aliyekuwa na ugomvi na mrema ni Mutungirehi ambaye bado yuko hai.

Ni vizuri ukumbuke kwamba staili ya mrema kufanya maamuzi kwa mgongo wa kamati kuu ama NEC ya TLP ni tofauti sana na chadema ambao utaratibu mzima wa kiutendaji umezingatiwa. Hawa madiwani wamevuliwa uanachama na kikao halali cha chama kilichoitishwa pasipo na ujanja ujanja ujanja wowote na taratibu zote zilizingatiwa. Kwahiyo jaribu kutenganisha siasa za mrema na tlp/nccr mageuzi na chadema, ni taasisi mbili tofauti kabisa.
 
TLP ilikuwa na Mbunge mmoja tuu bunge lililopita, ni Benedict Mutungurehi (RIP), (Biharamulo), mara tuu baada ya uchaguzi, wakatibuana na M/Kiti wake Mrema, Mrema kamfukuza uanachama, aliopokwenda mahakamani, uamuzi ule ulisitishwa, ila wananchi wa Biharamulo, walikosa uwakilishi kwa miaka minne.

Hivi ndivyo nilivyosema kuhusu TLP.

[/COLOR]

Nadhani ulimaanisha Phares Kabuye,Mutungirei alikuwa mbunge wa Karagwe na bado yupo hai.
 
Mwita Maranya, nimekuambia sheria, nimefuta tongotongo.
Ndivyo ulivyoambiwa Kamati ya Marando iliwahoji madiwani wote?. Hivi ilizikia sababu zao kuitunishia misuli CC yao?.
Kama Marando unafahamiana naye kwa karibu, muulize vuzuri.
Nilikuwa nae hoteli moja hapa Dodoma, na leo asubuhi wanakati ana check out, kuna kitu nimezungumza nae, hebu muulize nimemwambia nini kuhusu uamuzi huo?.

Sidhani kama ninahitaji kumuuliza marando ulimwambia nini. Nina kila sababu ya kuamini kwamba hata kile ambacho hukumwambia umekisema hapa.

Suala la msingi hapa hata kama mtu hujafuta matongotongo ya sheria, unahitaji kutumia common sense kujua kwamba hawa jamaa wamepewa nafasi na muda wa kutosha wa kusikilizwa, na ndio maana utaona kuna mmoja ambaye hakwenda dodoma kamati kuu haijatoa uamuzi wowote juu yake, sasa unataka uambiwe nini uridhike kwamba jamaa walisikilizwa??

Kinachoonekana hapa ni kutaka kulazimisha watu wakuamini kwamba kamati kuu haikuwatendea haki hawa jamaa kwa kutowapa nafasi ya kusikilizwa, kitu ambacho sio sahihi. Katika hili Pasco sihitaji kusomea sheria ili nijiridhishe kwamba jamaa walipewa nafasi ya kusikilizwa labda useme jingine. Wacha niendelee kusema na vyuma tu kwani pamoja na kusema nayo bado naweza kuelewa principle of natural justice bila kwenda darasani.
 
Nadhani ulimaanisha Phares Kabuye,Mutungirei alikuwa mbunge wa Karagwe na bado yupo hai.

Mkuu nimeipenda sana contribution yako,

Bado namsubiri mtaalam wa politics the boss na mchambuzi wa siasa za bongo Pasco waendelee kutufahamisha ni jinsi gani chadema ingewa-handle madiwani wakorofi.
 
Mkuu nimeipenda sana contribution yako,

Bado namsubiri mtaalam wa politics the boss na mchambuzi wa siasa za bongo Pasco waendelee kutufahamisha ni jinsi gani chadema ingewa-handle madiwani wakorofi.

Mbona nimeshasema hapo kuwa ilihitajika politics tupu hapo slaa na wenzie wangeenda arusha na kuwashawishi tu, na sio kufanya mambo kimahakama na kamaushahidi wa rushwa uikuwa hakuna, wangewaomba radhi na kuwaambia msimamo wa chama
ni upi ufuatwe.......kisiasa bila vitisho
 
Hihiiiii Boss bana :) Ananifurahisha kwelikweli.

Obama hajui siasa: Ilitosha kwenda Pakistan kuongea na Osama. Si alijua wapi anaishi?

Bush hajui siasa: Ilitosha kuchukua pipa na kwenda kwa Sadam Husein. Wangeyaongea yakaisha.

Nyerere hajui siasa: Ilitosha kabisa kwenda Uganda kwa Nduli na wakapata pamoja bia na mambo yakaisha........

Kuna mtu anaweza kuongeza Wanasiasa wasiojua SIASA?

Kama kuongea, si walienda hadi kwa Mtei? Mbona wengine hawakuhitaji kumsubiri Slaa? Kitendo cha jamaa kutunisha msuli kwenye TV ilikuwa ni ishara tosha kuwa jamaa WANAJUA WANACHOKIPANDA. Ni sawa uwe ni kisherehe hapo Dar na wazee wa Clouds waje kuivuruga. Hata ukifanya vipi kuwashawishi wasifanye fujo, wao lazima watembeze kibano kama vijana wa Green Guard wa CCM.
mbona nimeshasema hapo kuwa ilihitajika politics tupu hapo
slaa na wenzie wangeenda arusha na kuwashawishi tu
na sio kufanya mambo kimahakama
na kamaushahidi wa rushwa uikuwa hakuna,wangewaomba radhi na kuwaambia msimamo wa chama
ni upi ufuatwe.......kisiasa bila vitisho
 
Wanabodi,

Kitendo cha Kamati Kuu ya Chadema kuwavua uanachama madiwani wake wa Arusha, is "A Big Mistake"!, and there is a price to pay, so Chadema must pay the price which is very high!.

Mkuu huwa naheshimu comments zako lakini kwa hili, I beg to differ. Kwanza kusema kwamba uamuzi uliofikiwa ni biggest mistake, inaonyesha kuwa you are afraid of making bold decision in your life whether they are right or wrong. There may be a biggest price to pay including kupoteza hivyo viti vya udiwani kwenye uchaguzi mdogo ujao. Hata hivyo, kwenye institution yoyote whether chama or not, ni bora to pay such a price kuliko kuwa na wanachama ambao hawafuati kanuni na taratibu mlizojiwekea. Kuwa na watu kama hao inaweza kuua kabisa the very foundation of the institution including its aims an objectives.

Kwa mfano, tunaona yanayondelea CCM kwa sasa. Wametangaza kujivua gamba na kuwapa muda baadhi ya wanachama wajivue nyadhifa zao. Mpaka sasa hakuna kulichofanyika. CCM imeshindwa kuchukua maamuzi magumu kuwafukuza hao wanachama kwa sababu inaogopa to pay a price for that. Instead wamewaongezea mwezi mmoja tena. Kitendo cha wao kutochukua hayo maamuzi baada ya zile siku 90 juisha, is probably the biggest mistake kwa chama.

Mkuu the biggest mistake we make in your lives ni kutofanya maamuzi magumu because we are afraid of the price we will have to pay. Sometimes, you will have to make bold decision, which may seem as a mistake to other, but good for the success of your organisation in the future. Ukiangalia matatizo mengi tulioyo nchini, yanatokana na serikali kushindwa ku make bold decions kwenye mambo mbalimbali. Lowasa mwenyewe alilisema hili bungeni kuwa we are afraid to make bold decisions ndio maana tuko hapa tulipo. Kwa Chadema, it would probably have been the biggest mistake, kama wasingefanya a bold decision. They may have to pay a price for their bold decision, but I hope they looked beyond that.

1. Ile sheria ya kulazimisha wawakilishi wa wananchi, lazima wadhaminiwe na vyama, its a bad law, na inakwenda kinyume cha Katiba ya JMT inayotoa uhuru kwa kila raia kushiriki katika uongozi wa serikali tangu ya mitaa hadi serikali kuu, hadi mahakama kuu ilishatoa rulling hicho kipengele kuwa ni 'unconstitutional' na kiwe struck out from the books of law!. Naamini Chadema hilo wanalifahamu, hivyo kitendo cha kutumia kipengele hicho hicho ambacho ni bad law, to its advantage, is "A Big Mistake!".

Mkuu hapa nafikiri argument yako ina utata mkubwa. Kweli Katiba inatoa uhuru kwa kila raia kushiriki katika uongozi wa serikali tangu ya mitaa hadi serikali kuu. Lakini Katiba hiyo hiyo inasema kuwa hao wawakilishi ni lazima wadhaminiwe na vyama vya siasa. Kwa maana nyingine hatuna independent candidates. Na Mahakama hivi karibuni imesema kuwa hatuna independent candidates Tanzania. Nashangaa sana unapo-quote kesi ambayo hai-apply kwenye hili suala.

Kila mwananchi anao uhuru kushiriki katika uongozi wa serikali tangu ya mitaa hadi serikali kuu. Katika kushiriki huko, anatakiwa akubali na afuate taratibu zilizowekwa na chama chake. Kama hatafuata hizo taratibu, chama kinaweza kumchukulia hatua kulingana na taratibu walizojiwekea. Hapo kwa mujibu ya sheria ya sasa hakuna kosa.

Cha maana ni kukumbuka kuwa Katiba yetu inakupa haki kwa mkono wa kulia, then inaichukua haki hiyo hiyo kupitia mkono wa kushoto. Kwa maana nyingine, wakati Katiba inampa kila mwananchi uhuru kushiriki katika uongozi wa serikali tangu ya mitaa hadi serikali kuu, Katiba hiyo hiyo inasema kuwa lazima ushiriki kupitia chama cha siasa. Kwenye hicho cha chama cha siasa itakubidi ukubali na kuziheshimu kanunu na taratibu ambazo chama kimejiwekea. Ukishidwa unatimuliwa na chama na kwa mujibu wa Katiba huwezi tena kuwa tena mwakilishi kwa vile sio tena mwanachama wa hicho chama.

2. Ukishachaguliwa, Diwani au Mbunge, hata kama ulidhaminiwa na chama, wewe, unakuwa umechaguliwa na wananchi, na unakuwa ni mtumishi wa watu na kule kwenye ngazi za maamuzi, Baraza la Madiwani na Bungeni, unawakilisha maslahi ya wananchi waliokutuma, na sio maslahi ya chama kilichokudhamini, japo katika uwakilishi wako, pia maslahi ya chama yatazingatiwa. Kitendo cha chama kuwafukuza wawakilishi halali wa wananchi kwa maslahi ya chama, is "A Big Mistake!".

Hapa mkuu ndio umechemsha kabisa. If that is the case, wananchi watawafukuzaje watumishi ambao wameshindwa kutekeleza majukumu waliojiwekea? Wewe unaweza kumfukuza mbunge wako uliomchangua? If so, kwa sheria ipi? Katiba inasema wazi kuwa an MP shall cease to be a Member of Parliament when s/he ceases to be a member of the party to which he belonged when he was elected or appointed to be a Member of Parliament. Natumaini hii huwa inatumika kwa madiwani pia. Chama kikikuvua uanachama unapoteza na uwakilishi wako hapo hapo.

Kwa mujibu wa Katiba ya sasa mwananchi wa kawaida hawezi kumwondoa madarakani mbunge. Kasome vizuri ibara ya 71 ya Katiba. Hii inatumika pia duniani kote. Hata huko Ungereza wanatafuta njia ya mpiga kumwajibisha mbunge aliyechaguliwa kupitia chama cha siasa. Mkuu huwezi kuacha kufuata kanuni za chama chako, on the ground kuwa wewe ni mtumishi wa wananchi hivyo hautachukuliwa hatua na hicho chama, isipokuwa wananchi tuu. Hilo lipo wazi kabisa unless labda uwe uligombea as independent candidate bila kupitia kwenye chama.

3. Sisi ambao hatuna vyama, lakini tuna shauku ya kuona Tanzania inaongozwa na chama mbadala, tumekuwa na imani kubwa sana na Chadema kama ndicho chama pekee mbadala ambacho kimethibitisha kikiaminiwa, kinaweza kuleta mabadiliko ya kweli. Hivyo tunategemea Chadema kitafanya maamuzi yanayofuata misingi ya haki. Kitendo cha kuwavua uanachama madiwani wake hawa, waliochaguliwa na wananchi, (sio chama) bila kuwasikiliza, ni kuwa "condem Unheard", which is against principles of Natural Justice, and this is a "A Big Mistake!".

Bado umerudia kosa lile lile. Una maana kwa kuwa wamechaguliwa na wananchi then, they are exempted from being punished by their party wanapovunja kanuni za chama? Kwa mfano leo, CCM ikiamua kuwatimua hao waliokataa kujivua gamba, then uta argue kuwa kwa vile wamechaguliwa na wananchi, then wananchi pekee ndio wanaweza kuwatimua. If so kivipi? Nipe tararibu ambazo zinaruhusu diwani au mbunge kusimamishwa na waliomchagua kama zipo.

Mkuu vyama vya siasa ni kama associations nyingine. Vina katiba zao ambazo wanachana inabidi wazifuate. Wakati ya kujiunga unaridihia kuiheshimu, kuizingatia hiyo katiba. Kama ukishindwa kufanya hivyo, then chama kwa kufuata katiba hiyo hiyo kina haki ya kukuchukulia hatua kwa kufuata taratibu zilizowekwa na kukubaliwa na wanachama wote.

Kama Chadema, wakati wakifanya hao maamuzi, hawakufuata kanuni na taratibu, kama vile kuwapa haki ya kusikilizwa watuhumiwa, then watakuwa wamevunja taratibu. They should be given the right to be heard and those who reached the decision should give reasons for their decision. Kama hawakufanya hivyo nina imani Chadema itakuwa na taratibu za hao hao waliofukuzwa kukata rufaa.

4. Uzoefu wa siasa za Kanda ya Kaskazini, watu wanachagua watu na sio vyama, ndio maana CCM wanajua wazi kuwa, wao CCM, kuanzia Mwenyekiti wao, sekretariat yake, CC yao na NEC nzima ya CCM, hata wakapige kambi Moshi mjini, wakeshe kwa siku 30 mfululizo usiku na mchana huku wakipiga kampeni ya nguvu kwa kutumia mabilioni yao wanayofisidi, na kuwavisha wanamoshi wote, zile T.Shirt na kofia, pamoja na kulisha pilau la nguvu siku zote 30, Ndesa hawatamng'oa!. Kitendo cha Chadema kuwavua uanachama watu wa watu mjini Arusha, it's "A Big Mistake!".

Mkuu watu wanachagua watu na sio vyama lakini hao wanaochaguliwa kwa sheria ya sasa ni lazima wapitie kwenye vyama vya siasa. Huwezi kugombea udiwani au ubunge bila kupitia kwenye chama. Bado hatuna independent candidates. Kwa vile utagombea kupitia kwenye vyama, itakubidi kwanza ukubaliane na kanuni na tararibu zilizowekwa na chama husika. Kama ukishindwa kufuata hizo kanuni, chama, as an association, kina haki ya kukuchukulia hatua ikiwa ni pamoja na kukufukuza uanachama, hata kama umechaguliwa na wananchi. Hilo sio tatizo la Chadema pekee. Hili ni tatizo la Katiba yetu. Katiba inawanyima wapiga kura haki kuwaadhibisha waliowachagua.

Hata kama katiba ya Chadema ingeruhusu, hilo lisingekubaliwa, kwa sababu Katiba ya nchi hauruhusu. Ndio maana watu wengi tunadai independent candidates. Hii itasaidia sana kwa vile wananchi, na sio vyama, ndio watakuwa na mamlaka ya kuwaadabisha wawakilishi wabovu. Kwa sasa wananchi hawawezi kuwaadabisha wawakilishi wao kwa sababu hakuna huo utaratibu.

5. Wenzao CCM walipokuja na makelele ya kujivua gamba, nilisema CCM, kuanzia Mwenyekiti wao, na kelele zote za Nape na Chiligati, hawana ubavu wa kuwavua uanachama hao watuhumiwa wa ufisadi kwa kuhofia retaliation ya watu wao, ndio maana mtashuhudia kwenye kampeni za Igunga, CCM lazima impigie magoti RA. Amini nakuambia, hawawezi kuwafanya lolote EL na AC, sana sana watawabembeleza kujiudhuru nyadhifa zao, lakini sio kuwavua uanachama, kwanini Chadema, chama cha matumaini, kifanye makosa ambayo CCM iliyochokwa, haiwezi kuyafanya, ya kuwavua uanachama wachaguliwa wa wananchi?!. That is "A Big Mistake!".

Mkuu kasome vizuri katiba ya CCM. CCM inaweza kabisa kumwachisha uanachama mwanachama yoyote kama amevunja kanuni za chama. Na akiachishwa uanachama, kama ni mwakilishi, automatically anapoteza na nafasi yake ya uwakilishi. Kwa Katiba yetu ya sasa, huwezi kumfukuza mtu uanachama halafu utegemee andelee kuwa mbunge au diwani. Kwa kigezo gani wakati wanawakilisha wananchi kupitia vyama? Narudia tena hatuna independent candidates. CCM kuogopa kuwatimua wanachama wake haina maana Katiba ya CCM hauruhusu. CCM wanaogopa ku make a bold decision because they are afraid to pay the price associated with it. Lakini kuto make a bold decision, CCM are making the biggest mistake ever.

6. Chama makini kama Chadema, is expected to do the right thing, at the right time. Hatua hii, ya kuwavua uanachama madiwani pendwa Arusha, hata kama it was the right step, imekuja at the wrong time!, wakati wakitafuta justification ya kulitwaa jimbo la Igunga, ndio chama kinaanzisha tifu kanda ya Kaskazini ambako ndiko kwenye mizizi yake, mimi sijui, Chadema, imeyafanya hayo kwa kutegemea nini?.

Mkuu you gonna have to make a bold decision regardless of what lies ahread. Kigezo cha kuwa kutakuwa na uchaguzi Igunga should not bar Chadema from making bold decisions. It is better to make long term based decision, that the short term one. Compare with CCM who are afraid of making bold decisions because of what lies ahead. Mkuu kama kuna tatizo you will have to resolve it immediately. The longer you entertain the problem, ndivyo linavyokuwa sugu.

Kwa maoni yangu, kama Chadema wamefuata kununi na taratibu walizojiwekea na kukubaliwa na waliovuliwa uanachama, then sidhani kama kuna tatizo. Tatizo litakuwepo tuu kama Chadema hawakufuata kanuni na taratibu ambazo zimewekwa na kubaliwa na wana Chadema wote including hao waliofukuzwa. Kama waliofukuzwa wanaona wameonewa, the kuna taratibu za kukata rufaa. Otherwise, uamuzi uliofikiwa na Chadema ni fundisho kwa CCM. Kwamba sometimes, you will have to made bold decisions despite the price you have to pay. Making bold decisions is not the biggest mistake. Rather, the biggest mistake is to avoid making bold decions.

My comments was inspired by Mwanakijiji's comments he made in another thread on this matter. It is time for not only the political parties but also the government to make bold decisions if we really want to resolve the problems we are facing. Tuache kuogopana. Tuache kuogopa kufanya maamuzi magumu na mazito kwa kuogopa what lies ahead.
 
Hihiiiii Boss bana :) Ananifurahisha kwelikweli.

Obama hajui siasa: Ilitosha kwenda Pakistan kuongea na Osama. Si alijua wapi anaishi?

Bush hajui siasa: Ilitosha kuchukua pipa na kwenda kwa Sadam Husein. Wangeyaongea yakaisha.

Nyerere hajui siasa: Ilitosha kabisa kwenda Uganda kwa Nduli na wakapata pamoja bia na mambo yakaisha........

Kuna mtu anaweza kuongeza Wanasiasa wasiojua SIASA?

Kama kuongea, si walienda hadi kwa Mtei? Mbona wengine hawakuhitaji kumsubiri Slaa? Kitendo cha jamaa kutunisha msuli kwenye TV ilikuwa ni ishara tosha kuwa jamaa WANAJUA WANACHOKIPANDA. Ni sawa uwe ni kisherehe hapo Dar na wazee wa Clouds waje kuivuruga. Hata ukifanya vipi kuwashawishi wasifanye fujo, wao lazima watembeze kibano kama vijana wa Green Guard wa CCM.

nilkuwa nakuheshimu mno mpaka leo aisee, ina maana hao madiwani ni sawa na osama, saddam na iddi amin?

Hizo ndo mentality za chadema kumbe?
 
TLP ilikuwa na Mbunge mmoja tuu bunge lililopita, ni Benedict Mutungurehi (RIP), (Biharamulo), mara tuu baada ya uchaguzi, wakatibuana na M/Kiti wake Mrema, Mrema kamfukuza uanachama, aliopokwenda mahakamani, uamuzi ule ulisitishwa, ila wananchi wa Biharamulo, walikosa uwakilishi kwa miaka minne.

Hivi ndivyo nilivyosema kuhusu TLP.

Mkuu Pasco...

Kama hata hili dogo unashindwa kuliweka vizuri sembuse kuichambua Katiba ya JMT,za Vyama Vya Siasa pamoja na wawakilishi wao? Kama hata hujui kuwa Mtungirei hawakuwa wa Bunge lililopita na wala sio wa Biharamulo alikni kubwa zaidi sio marehemu na bado ni mwanachama wa TLP. Yaani hata Phares Kabuye ulikuwa humfahamu pamoja na kazi yako yote yan uchambuzi wa siasa kama unavyojiita utawezaje kutenganisha wawakilishi (Rais,Wabunge,Madiwani,Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji) na nguvu ya chama.

Duniani kote unapokuwa kwenye chama cha siasa hata ukiwa nani lazima ufuate katiba na kanuni za chama hicho..Chama ndio kinakupitisha kwanza kabla hujachaguliwa na wananchi. Mambo haya yakutokuwa na nidhamu ndio maana Serikali yetu inapata kigugumizi kuruhusu mgombea binafsi kwakuwa hali itakuwa mbaya sana nadni na nje ya Bunge,kila mmoja atafanya analotaka kwakuwa hakuna wakumuwajibisha moja kwa moja.

Niheri kupoteza kata zao zote kuliko kuwa na madiwani wasiofuata Katiba ya Chama.Muafaka unapaswa kuwa a chama na sio watu binafsi, Halmashahuri zote zinazoongozwa na CHADEMA ziko chini ya chama sio ya Madiwani wa eneo husika,Wabunge wote wa CHADEMA wako chini ya chama. Kwa katiba yaeu hii ambayo haina mgombea binafsi hakuna aliye juu ya chama.. Walikuwepo, wameondoka, tumepokea wengine na watakuja wengine safari itaendelea.. Kamati Kuu ya CHADEMA inaviongozi na wajumbe Makini tena wa level zote za elimu ya msingi mpaka PHD na wote walikuwepo na wachambuzi walifanya chambuzi zote unazisema wewe hapa.

Hakuna mistake iliyofanyika ila Madiwani wenyewe ndio walijichanganya. Walibembelezwa kupita maelezo..

Cheers!
Regia
 
obama aliposhinda urais na chama chake kuwa na nguvu kubwa,
alikuwa na option ya kumuondoa joe lieberman kwenye kamati za congres
lakini ali compromise na kumuacha tu,licha ya joe lieberman kuungana na republicans kumponda obama wakati wa uchaguzi.....
chadema ni kama mtoto mdogo anaejaribu ku prove kuwa yeye ni mtu mzima
mwisho hufanya madudu tu mengi.....
ukiwa mtu mzima huitaji ku prove anything.....
itwacost mno hiiiii,mark my words

Mkuu ndio maana unaona Obama anavyosumbuka sasa. Reputation yake inazidi kupungua because of compromises he made when he came into power. Angekuwa makini angefanya maamuzi mazito ya kumtimua Joe Lieberman kwenye kamati za congress. Kitendo cha yeye ku compromise ndio kinam cost sasa. In my view, he should not have even appointed Hillary Clinton as Foreign Secretary. Obama ali base zaidi kwenye short term solutions za wakati ule, Angekuwa ameangalia mbali yasingemkuta yanayomkuta sasa.

The Boss, politicians need to be bold enough to make tough decisions and reforms. The word "bold" is key here. A bold decision requires courage and guts due to the fact that what is being decided upon has complex implications and, in some cases, has even a risk element. It is this kind of scenario that normally makes a person or an institution hesitate to decide on an issue, opt to compromise or play ostritch and leave matters to providence.

In other words, not all decisions made in one's life or by the government are bold ones. Most of them are routine. We need to change this. In any institution, we need a leader who can make bold decisions. In the case of state governance, a decision to form a government of national unity in Zanzibar was a bold one. So, is the decision to write a new constitution, assuming it is genuine.


 


Mkuu ndio maana unaona Obama anavyosumbuka sasa. Reputation yake inazidi kupungua because of compromises he made when he came into power. Angekuwa makini angefanya maamuzi mazito ya kumtimua Joe Lieberman kwenye kamati za congress. Kitendo cha yeye ku compromise ndio kinam cost sasa. In my view, he should not have even appointed Hillary Clinton as Foreign Secretary. Obama ali base zaidi kwenye short term solutions za wakati ule, Angekuwa ameangalia mbali yasingemkuta yanayomkuta sasa.

The Boss, politicians need to be bold enough to make tough decisions and reforms. The word "bold" is key here. A bold decision requires courage and guts due to the fact that what is being decided upon has complex implications and, in some cases, has even a risk element. It is this kind of scenario that normally makes a person or an institution hesitate to decide on an issue, opt to compromise or play ostritch and leave matters to providence.

In other words, not all decisions made in one's life or by the government are bold ones. Most of them are routine. We need to change this. In any institution, we need a letter who can make bold decisions. In the case of state governance, a decision to form a government of national unity in Zanzibar was a bold one. So, is the decision to write a new constitution, assuming it is genuine.




how is it that hillary was a mistake
hebu explain hapo kwanza
 
how is it that hillary was a mistake
hebu explain hapo kwanza

Simply because they have different opinions on policy issues that matter to the Americans. For example, the abortion issue. During his campaign and even after being elected as President, Obama spoke of finding "common ground" on abortion policy. However, his personnel picks such as Hillary Clinton precluded this policy. Hillary Clinton has a 100% pro-abortion voting record in the U.S. Senate. Her Presidential candidacy was heavily supported by EMILY's List, the nation's leading pro-abortion women's organization. How Obama will find a common ground on this issue?

It is well known that Obama awarded such a prize plum to Hillary as a sop to her aggrieved fan base. But she does not have credentials for that position. Aside from being a mediocre senator, Hillary has a poor track record as both a negotiator and a manager. Hillary will do a good job but she will do it for herself, not for Obama.

Well, this is merely an obiter dictum, so let's concentrate on the subject matter of this thread.
 
Simply because they have different opinions on policy issues that matter to the Americans. For example, the abortion issue. During his campaign and even after being elected as President, Obama spoke of finding "common ground" on abortion policy. However, his personnel picks such as Hillary Clinton precluded this policy. Hillary Clinton has a 100% pro-abortion voting record in the U.S. Senate. Her Presidential candidacy was heavily supported by EMILY's List, the nation's leading pro-abortion women's organization. How Obama will find a common ground on this issue?

It is well known that Obama awarded such a prize plum to Hillary as a sop to her aggrieved fan base. But she does not have credentials for that position. Aside from being a mediocre senator, Hillary has a poor track record as both a negotiator and a manager. Hillary will do a good job but she will do it for herself, not for Obama.

Well, this is merely an obiter dictum, so let's concentrate on the subject matter of this thread.

mkuu sioni a bigger problem hapo
obama mistakes zake zipo kwenye uchumi
alipaswa kumuweka larry summer treasury ni sio geithner
geithner hafai so far
 
Ni bora kuwa na wanachama watatu katika chama lakini wenye nidhamu kuliko kuwa na wanachama miilioni wasio na nidhamu. Ni heri CDM ikose hizo nafasi tano za madiwani huko Arusha katika uchaguzi mdogo utakaorudiwa, kuliko kuwa na hata madiwani wote wa mkoa ambao ni mzigo na maadui wa maendeleo ya chama. Kama chama, huo ndo ulikuwa uamuzi pekee wa busara kwa maslahi ya chama na wananchi wa Arusha.

Hata Roma ilianguka kutokana na kuibuka kwa falme ndogondogo katikati ya ufalme mkuu. Hatuwezi tukawa na viongozi wa CHADEMA taifa, halafu kukawa na viongozi wengine somewhere ambao wanamaamuzi sawasawa na wale wa Taifa.

Chadema walishasema tangu mwanzo, no body is above the party. Hakuna na hatatokea aliye maarufu kupita chama. Hilo litabaki hivyo na linapaswa liheshimiwe. Anayetafuta umaarufu unaokizidi chama aende CCM, huko ndiko mtu mmojammoja anaweza kuwa maarufu kukishinda chama according to Makamba.
 
Mimi naona walichofanya chadema ni kuonyesha tu nani ana nguvu kuliko mwingine, hivi ingetokea yule jamaa wa chadema aliyekuwa anagombea unaibuka spika ameibuka mshindi na kuwa msaidizi wa mama Makinda angelazimika kujiuzulu au ingekuwaje?

Off the topic: hivi wataitisha uchaguzi mdogo wa madiwani kwenye hizo kata? Na kama ni ndio naona hawa jamaa wanaojiuzulu na kufukuzana kwenye vyama kisha uchaguzi mdogo ufanyike wanatuongezea umaskini tu, wanachezea sana kodi zetu, ningekuwa mimi ndo mwamuzi (bahati mbaya sio mwamuzi) jimbo/kata linaloaachwa wazi kwa mbunge/diwani kujiuzulu au chama chake kumfukuza hakuna kufanya uchaguzi tena ama tuache nafasi iwe wazi ama tuchukue mtu aliyeshika nafasi ya pili na awawakirishe wananchi maana ni matumizi mabaya ya kodi zetu.
 
pasco, kwanza kabisa naomba ieleweke kwamba "a mistake is not a alwayz a failure" nikikusoma vizuri maandishi yako ni kama vile unasema CDM have made wht you classifiy as a "big mistake" and therefore they will fail.

Mtizamo huu ndio haswaa unaowafanya CCM waendelee kuhangaika with their "kabuki" kujivua gamba huku wakiogopana ogopana mara siku 90, mara 120, mara ooh hii ni ajenda ya NEC and you wonder walianzanje kuijadili huko CC. Ni msimamo huu ndiyo umeifikisha Tanzania hapo ilipofika na ni msimamo huu unaofamfanya Kikwete mara nyingi kujikuta kwenye conflicting positions mfano wakati ule wa Dowans, na hii juzi kwenye kikao chao cha CC. Ni misimamo ya aina hii ambayo watendaji wa serikali ya bongo wanaitumia and that is why niliwahi kuanzisha thread kwa jina la "TZ:Taifa la kusikilizia"

All in all what was needed was to do a "right thing", which I believe is wht CDM did na it doesn't matter hata kama inakuwa opinionated as u have said "big mistake" lakini is absolutely not a failure and never will.

A point to note though "Sometimes losing one battle helps you win the war"
 
Back
Top Bottom