Uamuzi wa CDM kuonana na Kikwete ulianzia wapi?

Sizinga

Platinum Member
Oct 30, 2007
9,100
6,022
Nimesikia kwenye gazeti la MwanaHalisi(leo) kwamba Uongozi wa Juu wa Chadema umekanusha vikali kauli ya Zitto kabwe kwamba Plan ya Chadema kuonana na Rais kuzungumzia Suala la Katiba Mpya kwa mara ya kwanza lilitolewa na Regia Mtema(R.I.P).

Wamesema si kweli kwani plan ya kuonana na Rais ilitolewa ndani ya Sekretariati Kuu ya Chadema na Muh Regia sio mjumbe wa Tume hii. Upii ukweli hapa?? Na iweje Zitto aliseme hili ilhali haikuwa kweli kwa kadri ya madai hayo ya viongozi wa JUU??
 
Hilo ni jambo dogo sana lisituumize vichwa.


Si jambo dogo hata kidogo. Kwanza Zitto ni Naibu Katibu mkuu wa Chadema. Kutoka katika vyombo

vya habari na kusema jambo ambalo si la kweli maana yake nini? Hilo amelisema kwa Regia aliyetutoka,

je anasema mangapi ambayo hayajanaswa? Kwa mfano Mbowe au Dr Slaa wakaitwa mbele ya haki

yeye atasema mangapi? Nadhani ni jambo la kufanyiwa kazi na Mnyika atuweke sawa. Na tatizo

ninaloona kwa Zitto sasa kujaribu kufanya 'balanced politics'. Awapendezeshe CCM kidogo, NCCR

kidogo, CDM kidogo, Wananchi Kidogo nk nk nk. As of now I cant define him anymore regardless of

whether kasema hili au lah. And soon he will be lost in politics. You can count on my words!
 
Mkuu kaa kimya ni kitu kidogo sana .Hapa kuna mgomo naposho mkuu na Katiba na wizi wa TBS .Hili la Zitto liache tu si wamesha sema sowhat ?Unataka nini au nani aseme nini ?
 
Mi nadhani tuwekane sawa ili jambo liwe dogo kuna vitu vingine vinatakiwe vichukuliwe maanani moja mazingira ya jambo lenyewe nitoe mfano mtu umekwanda msibani kutoa pole baada unathubutu kuwaambia wanafamilia acha afe manake naye kaugua sana utaonekana mwehu kwa kuwa Mazingira hayakuruhusu la pili ni msemaji wa jambo
lenyewe mathalan Kauli wanazotoa Mawaziri Bungeni au Wakuu wa taasisi mbali mbali hawezi tu Waziri akatoa kauli na kuwaaminisha Watz juu ya kauli yake halafu kesho ikawa ndivyo sivyo then wenzie wanasema ni jambo dogo kwa kweli huu utakuwa ni upuuzi uliotukuka.

Sasa waungwana mnaong'ang'ana kusema eti hili ni jambo dogo haliwezi kuwa dogo bata kidogo yani tukukuruke vipi hili si la mzaha kabisa manake Zitto pamoja na kuwa hakulizungumzia kama Naibu ila watu walimwamini kwa cheo chake na vile vile yale mazingira yalikuwa ya msiba hivyo watu waliamini hawezi kudanganya sasa leo tuelewe kipi halafu tunasema ni jambo dogo!!!!!

Hili linahitaji tamko toka kwa wahusika si la kupuuzia aidha Chama au Zitto mwenyewe waweke sawa jambo hili tuache mambo ya kishabiki manake kama litabaki bila ufafanuzi wengine watabaki na notion ya kwamba Zitto kadanganya jambo ambalo litamchafulia jina lake na wengine watahisi kuwa Chama kina matatizo.
 
Nimesikia kwenye gazeti la MwanaHalisi(leo) kwamba Uongozi wa Juu wa Chadema umekanusha vikali kauli ya Zitto kabwe kwamba Plan ya Chadema kuonana na Rais kuzungumzia Suala la Katiba Mpya kwa mara ya kwanza lilitolewa na Regia Mtema(R.I.P).

Wamesema si kweli kwani plan ya kuonana na Rais ilitolewa ndani ya Sekretariati Kuu ya Chadema na Muh Regia sio mjumbe wa Tume hii. Upii ukweli hapa?? Na iweje Zitto aliseme hili ilhali haikuwa kweli kwa kadri ya madai hayo ya viongozi wa JUU??

Kwani gazeti linatoa sauti mpaka usikie au kuna mtu amekupa hii habari na wewe ukaileta kama ilivyo?
 
Kwani gazeti linatoa sauti mpaka usikie au kuna mtu amekupa hii habari na wewe ukaileta kama ilivyo?

Labda mleta thread amesikia mtangazaji wa TV akisoma habari hii ktk kipindi cha magazeti asubuhi. Unashangaa nini mkuu?
 
Si jambo dogo hata kidogo. Kwanza Zitto ni Naibu Katibu mkuu wa Chadema. Kutoka katika vyombo

vya habari na kusema jambo ambalo si la kweli maana yake nini? Hilo amelisema kwa Regia aliyetutoka,

je anasema mangapi ambayo hayajanaswa? Kwa mfano Mbowe au Dr Slaa wakaitwa mbele ya haki

yeye atasema mangapi? Nadhani ni jambo la kufanyiwa kazi na Mnyika atuweke sawa. Na tatizo

ninaloona kwa Zitto sasa kujaribu kufanya 'balanced politics'. Awapendezeshe CCM kidogo, NCCR

kidogo, CDM kidogo, Wananchi Kidogo nk nk nk. As of now I cant define him anymore regardless of

whether kasema hili au lah. And soon he will be lost in politics. You can count on my words!

Calnde, kwani mangapi huyu Mh aliyasema wakakana lakini mwisho ikadhihirika ni kweli? Shida ni hivi, anakuwa anajua ukweli kuhusu jambo fulani, basi yeye analitumia kisiasa na ndivyo wanasiasa wengi wanavyofanya, yawezekana kabisa ni Mh Rejia alitoa wazo hilo ila tu haipendezi kubinafsisha hoja badala ya kuifanya ya Chama hasa hoja sensitive kama hii. Mh Zitto anajua ni Mh Rejia aliisema/alipendekeza, wazee wakaona ni la busara wakaamua kulifanya official ndani ya vikao halali, basi wakalipitisha. Sasa ndani ya vikao huwezi kuliita la Mh Rejia hata kama yeye ndiye aliyemshauri Katibu Mkuu au Mwyneykiti kabla ya kikao, na hata kama yeye haingii kwenye vikao. Alichosema Mh Zitto ni kweli ila Kichama halina mantiki na linapotosha uzito wa jambo lenyewe na kulifanya binafsi na si la chama. Ukiangalia swala la Posho, Mh Zitto nadhani alikuwa amesha teta na vyanzo vya uhakika. Hakuna kitu kizuri kama mwanasiasa ukiwa wa kwanza kubreak news hata kama ni contraversial.
 
Ndipo hapo sasa watanzania mjiulize CHADEMA ni chama au NGO? maana kila mtu anasema atakalo muda wowote bila ya kujali. Viongozi wa CHADEMA jengeni mahusiano ndani mtakiuwa chama! Ushauri wangu Acheni ubabe, Ubaguzi, Ukabila na kujiona kuwa MBowe ndiye mwenye akili peke ya kujua baya na zuri kwa Chadema. DR Slaa mbona hapo umekuwa BUTUUUU?
 
nimeshangaa sana kona gazeti ninalo liamini limeweka hii habari kipaumbele cha kwanza eti

'' ZITO AMZUSHIA MTEMA ''


sidhani kama hii ni issue kihivyo ya kumfanya mtu atumie Tsh 500/= kuisoma ilihali kuna mambo mengi sana ktk nchi hii ya kuyajadili mfano ajenga za vikao bunge kwa hivi sasa na mgomo wa madaktari + walimu wa ....
 
Mwanahalisi ni gazeti la Udaku linalotumiwa na wanasiasa wachache kwa maslah yao.Nimeacha kusoma gazeti hili.
 
Ndugu,

Kwa kawaida mkikaa kwenye kikao, mmoja wenu akaleta hoja, ikajadiliwa kwa mapana na mwishowe hoja hiyo ikapitishwa au ikakataliwa uwa SIO nani kakubaliwa au kakataliwa bali kikao kimekubali au kimekataa.


Jambo la muhimu katika hoja ya CHADEMA kwenda kuonana na Rais ni moja tu walifanya jambo la maana au la! Nani alitoa hoja, nani alimuunga mkono au nani aliguna si jambo la kuumiza vichwa ila la maana hapa ni kwamba walipoenda kuonana na Rais walifanikiwa katika hoja zao au la. Kikao kiliamua kuonana na Rais basi.
 
Nimesikia kwenye gazeti la MwanaHalisi(leo) kwamba Uongozi wa Juu wa Chadema umekanusha vikali kauli ya Zitto kabwe kwamba Plan ya Chadema kuonana na Rais kuzungumzia Suala la Katiba Mpya kwa mara ya kwanza lilitolewa na Regia Mtema(R.I.P).

Wamesema si kweli kwani plan ya kuonana na Rais ilitolewa ndani ya Sekretariati Kuu ya Chadema na Muh Regia sio mjumbe wa Tume hii. Upii ukweli hapa?? Na iweje Zitto aliseme hili ilhali haikuwa kweli kwa kadri ya madai hayo ya viongozi wa JUU??
......ulianzia kwa cdm na wana cdm wenyewe, ww unataka aliyeanzisha hoja au hoja yenyewe?
 
Zitto alishaachana na CHADEMA siku nyingi..na kwenye akil zake chama sio muhimu tena! akitoa hotuba zake..humsikii hata siku moja akitaja CHADEMA au UPINZANI...
 
Back
Top Bottom