TZ Embassy in DC Web

Jim

Member
Mar 7, 2008
70
4
Kwenye website yenu, kuna link inayosema "Balozi Message". Uki-click hiyo link inakupeleka kwenye page yenye kichwa "Ambassodor's Biography", ambazo sina hakika kama ni kitu kimoja au vipi?

Lakini mimi nilitaka kusoma message ya balozi na badala yake nikalazimika kusoma kwamba Balozi alisoma Mzumbe, ana post-graduate certificate na ana watoto 2, which is fine but misplaced.
 
Wewe unashangaa web page!..hata kile choo pale chini hakina sabuni,toilet paper na taa haiwaki! duu sijui hata hao wageni wanajisikiaje!

Wembe
 
Wewe unashangaa web page!..hata kile choo pale chini hakina sabuni,toilet paper na taa haiwaki! duu sijui hata hao wageni wanajisikiaje!

Wembe

Unajua "rest room" wanagundua wachache, but this one is a world wide web where everyone has access to.
 
Kingine, biography ya Balozi imemtaja Mkapa mara saba, haijatulia. Sio kwamba ina mapungufu ya kitaaluma au uzoefu, ila imejaa uhusiano wake wa karibu na Mkapa, mshutumiwa wa high crimes in high places. Hawa watu kuna vitu fulani vya public relations hawajaamka kuvijua bado. Mkapa sasa hivi ni persona non grata. Hata kama ni ndugu yako inabidi hadharani usimtaje taje Rais Mstaafu anayetaka kushtakiwa kwa kujiuzia migodi. Barabarani Mkapa kazomewa. Vivyo hivyo, mitandaoni Mkapa sio popular, kama Uswahilini ambako akijichanganya bila ulinzi atapigwa matofali!

Bio inasema Balozi alikuwa "personal assistant with added responsibilities" wa Mkapa (wanajua wenyewe hayo majukumu ya ziada). Sasa unafikiri Rais alipokuwa anafanya dili za kununua migodi alikuwa anaenda mwenyewe kwenye minada? Ni hawa "personal assistant with added responsibilities" zisizo julikana ndio walikuwa wanatumwa labda.

Hiyo ni labda. Cha uhakika ni kwamba hata kama walikuwa hawaendi kwenye minada kwa niaba ya Mkapa, at the very least, walijua madili yake. Hawa ndio wanabeba brief case la Mkapa, ndio wanatoa photocopy ma document ya Rais, ndio ma liaison wa idara ya Usalama Ikulu. Hata wasipoenda nae kwenye dili, wanajua amelalia wapi, ameamkia wapi. Kwa hiyo, kama we ni mjanja, huwezi ku advertise kwenye Bio yako hicho ki wasifu cha kubeba mkoba wa master key ya mwizi, kama anavyo shutumiwa. Ni kirekodi kichafu. Huyu balozi lazima atakuwa hana public relations/political savvy masikini. Labda ni mtupu huyu.

Viongozi wetu, masikini weeee!
 
jana nimeona kwenye daily news mkapa amepoteza hati ya kiwanja kiko kigamboni, mwenye kuiona airudishe kw aassistant registrar of titles kabla ya siku 21, otherwise huyu jamaa atampatia nyingine, wakuu nitawekeeeni phptocopy hapa, hii ni issue ndogo lakini sijaelewa alipotezea wapi, isije ikawa....
 
Aliyepoteza hati ni Benjamini Mkapa huyu rais mstafuu au mwingine?? Maana haya majina huko masasi ni kama kwetu kule ukisema magadula tu wanaweza kuja hata 40....kama ni yeye yawezekana mishe mishe zilipamba moto katika kuweka deal sawa ikadondoka....aliyeokota wala asirudishe na tutafatilia tujue kama hicho kiwanja alikipata kifisadi au vipi lazima kitakuwa super low density si kama vya kwetu kule kiburugwa....
 

Kwenye website yenu, www.tanzaniaembassy-us.org, kuna link inayosema "Balozi Message". Uki-click hiyo link inakupeleka kwenye page yenye kichwa "Ambassodor's Biography", ambazo sina hakika kama ni kitu kimoja au vipi? Lakini mimi nilitaka kusoma message ya balozi na badala yake nikalazimika kusoma kwamba Balozi alisoma Mzumbe, ana post-graduate certificate na ana watoto 2, which is fine but misplaced.

Mkubwa ndio hivyo tena tunajikongoja na maisha haya ya Sayansi na teknolojia na umakini. Ni kweli na mimi ni shuhuda wa haya maana nilishayaona. Wahusika najua wapo makini na JF watalirekebisha nadhani.
 
Nami nimeshuhudia hilo. Ila mambo mengine bwana, inabidi kucheka tu! Hapo hapo kwenye Home page ya Ubalozi wa TZ Marekani pana ka-title ka Regional Corporation, ukienda kwenyewe unakuta title bado ni hiyo hiyo Regional Corporation lakini ukisoma content unaona Kinachoelezwa ni Regional Co-operation!!! Huu ndo uzembe wa kupasua kichwa cha mgonjwa wa mguu na kupasua mguu wa mgonjwa wa kichwa!!!!
 
Hongera ubalozi. Naona sasa link ni "Balozi Bio".

Fanyeni proof reading ya mambo mengine sasa na hasa hilo la Corporation badala ya Cooperation.

Goodluck!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom