Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Baada ya Mengi kuwatosa wananchi wanyonge waliokuwa wanamuona ni alama (symbol) ya kupambana na mafisadi, hasa baada ya ujasiri wake wa kuwataja mafisadi papa, sasa wanyonge tutampata wapi mwingine kama yeye?
Kwa umiliki wake wa vyombo muhimu vya habari – radio, TV na magazeti – Mengi alikuwa ni mtu muafaka sana katika kazi hiyo, na wengi tuliona jinsi mafisadi walivyokuwa wakipata kiwewe kutoka kwake. Lakini ghafla ameamua kuwatosa, na vyombo vyake vya habari havigusii kabisa masuala ya ufisadi.
Alipowataja mafisadi papa, CCM na serikali yake walimpa msukosuko mkubwa sana lakini alipata faraja kutoka kwa wananchi ambao walikuwa nyuma yake. What went wrong?
Hata katika kipindi cha ITV cha mapitio ya magazeti, hayasomwi magazeti yale yenye habari kuu ukurasa wa mbele kama inahusu ufisadi wa viongozi wa chama tawala.
Tunajua yeye ni CCM na anapenda kuona chama hicho kinashinda – ingawa twashangaa ni kitu gani kinamfanya aamini kama CCM inaweza kupambana kweli na ufisadi, kama tunavyoona sasa hivi jinsi JK anavyowakumbatia waziwazi mafisadi.
Lakini kupambana katika vita vya haki ilipasa kuwa muongozo wake, hata kama vita hiyo ni ajenda kuu ya chama cha upinzani – Chadema. Kwa nini anawaona Chadema adui – na hivyo kuyatelekeza mapambano yenye lengo jema – na hivyo kuwatosa mashabiki wake?
Tunaomba Mzee Mengi ajifikirie tena kuhusu hili. Kuna hatari naye ataambiwa ni fisadi kama vile wale aliowatuhumu miaka miwili iliyopita.