TVT, Star TV washinikizwa kutoonyesha Bunge

Mwafrika wa Kike,

Nilichosema ni kwamba mpaka mtu anihakikishie kwamba hizo component zote zilikuwa sawa wakati huo... ndio naweza... ku-bai (buy) hizo tetesi zenu... kama sina hilo... siwezi -ku-buy ingawa ni posibility... tatizo lenu mnasema almost with authority kwamba kituo cha TBC1 kiliwafanyia hujuma... kama hakuna ushahidi hakuna haja ya kusema hivyo.


NB: Hakuna kitu kinaitwa TVT siku hizo... guys it is TBC

Asante kwa correction....I meant TBC,

Mkuu, umepata statement yoyote toka TBC inayosema kwa nini hawakuweza kurusha hii kitu live? Je hili jambo sio muhimu ya kulitolea maelezo.

Kasheshe,

Mimi na wewe wote tunajua spin kwa hiyo katika hili tunaweza hata kusema kuwa technician alipatwa na stroke... kwa vile ni Tanzania, hakuna mwenye kudai uthibitisho.

Mimi ninachosema ni kitu kimoja, whatever the reason, uamuzi wa kutorusha hotuba ya Slaa kwa TV zote mbili (kama ilivyoelezwa hapa) sio mzuri kisiasa na kiutendaji.

Ifikie wakati maslahi ya taifa yawe mbele zaidi ya masilahi ya vyama.
 
Mwafrika wa Kike,

Nilichosema ni kwamba mpaka mtu anihakikishie kwamba hizo component zote zilikuwa sawa wakati huo... ndio naweza... ku-bai (buy) hizo tetesi zenu... kama sina hilo... siwezi -ku-buy ingawa ni posibility... tatizo lenu mnasema almost with authority kwamba kituo cha TBC1 kiliwafanyia hujuma... kama hakuna ushahidi hakuna haja ya kusema hivyo.


NB: Hakuna kitu kinaitwa TVT siku hizo... guys it is TBC

Kasheshe Inamaana na mawasiliano mengine ya TTCL kutoka dodoma mpaka DAR es Salaam unamaanisha yalikuwa yanamatatizo?

Au ni kituo tu cha TBC kilikosa mawasiliano na TTCL?
 
Kasheshe Inamaana na mawasiliano mengine ya TTCL kutoka dodoma mpaka DAR es Salaam unamaanisha yalikuwa yanamatatizo?

Au ni kituo tu cha TBC kilikosa mawasiliano na TTCL?

Yaani acha tu,

Thread inasema hapa kuwa vituo vyote viwili - TBC na Star TV havikuonesha... do the math.
 
Yaani acha tu,

Thread inasema hapa kuwa vituo vyote viwili - TBC na Star TV havikuonesha... do the math.

Huo unaitwa usanii.
Ninachojua ni kwamba kutoka Dar mpaka dodoma TTCL wanalink moja. Sasa sijui tena na Star TV ni ilikuwaje?

Na haya yote yalitokea wakati wa DR Slaa
 
Siasa ni game chafu. Dont hate the players; hate the game. Tatizo la upinzani Tanzania ni kulialia sana bila kuwa na jinsi mmbadala wa kutatua matatizo.

FP nadhani kama inavyoonyesha signature yako inaonekana inasema kinyume chake yaani 'Negative thinker' Maana hivi kwa nini nyie wanachama wa Chama cha mijizi statement zenu ni hizo hizo kila siku?
Hivi kweli mbadala unaochangiwa humu hamuuoni kwa sababu ya wizi wenu?
Macho yenu yameshapofuka na masikio kuziba, maana hamsoi nini kinazungumzwa hapa ni vipi tutatue matatizo yetu?
Maskini pole kwa upofu wenu.
 
Ni mali ya serikali na hence wananchi. Lakini recently imekuwa ya kibiashara zaidi. Sio ya kijamaa.

Kwahiyo viongozi wa serikali wanapewa umuhimu zaidi kwasababu wanawahudumia wananchi wote officially.

Mie sioni tatizo lipo wapi kwenye hili suala. Bado nasisitiza mngelipia muonekane live.

Kidumu chama cha mapinduzi!
nASHIBDWA KUKUELEWA UNAPOSEMA VIONGOZI WA KISIRIKALI WANAPEWA UMUHIMU.SASA MBONA VIKAO VYA BUNGE VILIVYOFUATA WANAONYESHA LIVE?MWAMBIE JAMAA AKO TIDO AACHE UBAGUZI ATI
 
Huo unaitwa usanii.
Ninachojua ni kwamba kutoka Dar mpaka dodoma TTCL wanalink moja. Sasa sijui tena na Star TV ni ilikuwaje?

Na haya yote yalitokea wakati wa DR Slaa

Physical link moja; Different Channels!!! Hope this explains your concerns. Also remember you have receivers etc....
 
Kasheshe Inamaana na mawasiliano mengine ya TTCL kutoka dodoma mpaka DAR es Salaam unamaanisha yalikuwa yanamatatizo?

Au ni kituo tu cha TBC kilikosa mawasiliano na TTCL?

Guys, sikusema matatito ya TTCL au Provider mwingine, nilichosema ... vyote ni moja ya potential points of failures... ambazo husababisha stesheni ya Luninga husika kutoonyesha... LIVE....

Mfano mzuri wa kuonyesha kwamba LIVE sio kitu kirahisi kama munavyodhani... Wandugu washabiki wa Soka,,, mliokuwa mnafuatilia mechi ya Germany na Turkey... nini mulishuhudia kupitia kwenye Super Sport 3....

Guys amkeni... sio kwamba na mtetea mtu... nazungumza vitu vinavyoweza tokea..
 
Guys, sikusema matatito ya TTCL au Provider mwingine, nilichosema ... vyote ni moja ya potential points of failures... ambazo husababisha stesheni ya Luninga husika kutoonyesha... LIVE....

Mfano mzuri wa kuonyesha kwamba LIVE sio kitu kirahisi kama munavyodhani... Wandugu washabiki wa Soka,,, mliokuwa mnafuatilia mechi ya Germany na Turkey... nini mulishuhudia kupitia kwenye Super Sport 3....

Guys amkeni... sio kwamba na mtetea mtu... nazungumza vitu vinavyoweza tokea..

Mkuu Kasheshe,

Darasa zito sana hili, nimekusikia mkuu!
 
Jamani,

Mnaweza kutofautiana nami bila names calling. Naungana na Kasheshe kuwa mpaka sasa ni speculations hatujajua kwanini hawakuionyesha, labda kulikuwa na kitu kingine muhimu sana wakati huo.

Mwafrika wa kike, nami ningependa sana irushwe. Ninachokataa ni kuhitimisha kuwa ni HUJUMA. Hapo tu mzee wangu. Napenda kabla ya kuamua jambo tutafiti kabla.

Wengine, CCM ina mapungufu yake na hayo mapungufu yanasababishwa na baadhi ya wanachama, so is Chadema, CUF, NCCR etc. Kuhitimisha kuwa CCM ni chama cha mijizi na mafisadi sio sahihi. Sahihi ni kusema CCM ina baadhi ya wanachama mafisadi na mijizi.

Na kama ni mijizi kiasi hicho; mbona wanaendelea kupeta mitaaani?. Mahakama pekee ndio ina mamlaka ya kuamua nani ni Fisadi au mwizi.
 
TBC na Star TV zinamilikiwa na hao hao hata wasipoonyesha sishangai. Uhuru wa vyombo vya habari kubanwa kwa kigezo cha maslahi ya taifa ni upotoshwaji wa demokrasia.
 
TBC na Star TV zinamilikiwa na hao hao hata wasipoonyesha sishangai. Uhuru wa vyombo vya habari kubanwa kwa kigezo cha maslahi ya taifa ni upotoshwaji wa demokrasia.

You are entitled to your opinion. Tatizo ni pale anapokuja mtu kusema vinginevyo. Inabidi tukomae kisiasa!. Ila hotuba ya Dr Slaha haikuonyeshwa live.
 
Jamani,

...Naungana na Kasheshe kuwa mpaka sasa ni speculations hatujajua kwanini hawakuionyesha, labda kulikuwa na kitu kingine muhimu sana wakati huo.

... nami ningependa sana irushwe. Ninachokataa ni kuhitimisha kuwa ni HUJUMA. Hapo tu mzee wangu. Napenda kabla ya kuamua jambo tutafiti kabla.

Vipi kama Tanzania press ni hafifu na tunaweza tusijue ni kwa nini vitu vimefanyika?
 
Ndio maana huwa tunasisitiza kusema "kama ni kweli...au kama katamka" kabla ya kushutumu/kukosoa.

Lakini pointi yangu ililenga zaidi kusema kwamba kuna wakati haiwezekani hata kufanya huo utafiti wa habari kwa sababu -kilioa changu cha kila siku - Tanzania hakuna press.

Naomba nitoke nje ya mada dakika moja.

Leo Zitto kaniambia hapa lile swala la Harare kuita balozi wao nyumbani analijua kwa sababu yuko kwenye kamati maalum ya Bunge. Tungekuwa na press za maana, waandishi wangemrukia baada tu ya kumaliza spichi yake ili waje kuiambia Tanzania, jamani eeeh, Zimbabwe wameita balozi wao. Hii ni stori kubwa, kubwa mno. Lakini umeiona magazetini?

Kwa hiyo hizi speculations na guesswork moja ya vyanzo vyake ni usiri wa Sirikali na kutokuwepo na press.
 
Physical link moja; Different Channels!!! Hope this explains your concerns. Also remember you have receivers etc....

Kwa uzoefu wangu katika masuala ya transmission ambapo najua stesheni nyingi na mawasiliano ya masafa malefu huwa wanatumia TTCL kwa sababu wana capacity ya kutosha na kwa TBC hawawezi kuwa na provider tofauti.


Labda Mkuu sikiliza hapa ninachojua, hapa ni kwamba TTCL kutoka Dodoma kwenda Bongo wana Link moja ambayo ina channels(SDH-E1 kama 60 hivi), same applied to Dodoma Mwanza.

Sasa katika suala lako la msingi la kusema haya mawasiliano yalishindikana kwa star TV (Mwanza-Dodoma) at the same time kwa TBC/TVT- DAR-DOdoma ni kitendo ambacho si rahisi.


Halafu uzoefu wangu kama kuna nia na ikatokea kuwa matangazo hayakuwezekana huwa Mara nyingi kama imezoeleka huwa wanatangaza. Kama hakuna response yoyote na jambo lilikuwa technical ambalo lilikuwa haliko kwenye uwezo wao basi hakukuwa na uwezekano wa kuwa siri.
 
Guys, sikusema matatito ya TTCL au Provider mwingine, nilichosema ... vyote ni moja ya potential points of failures... ambazo husababisha stesheni ya Luninga husika kutoonyesha... LIVE....

Mfano mzuri wa kuonyesha kwamba LIVE sio kitu kirahisi kama munavyodhani... Wandugu washabiki wa Soka,,, mliokuwa mnafuatilia mechi ya Germany na Turkey... nini mulishuhudia kupitia kwenye Super Sport 3....

Guys amkeni... sio kwamba na mtetea mtu... nazungumza vitu vinavyoweza tokea..

Hapa unachokisema kinaweza kuwa sawa kuwa kuonyesha Live siyo rahisi lakini suala la msingi baada ya kuangalia link ya Dodoma-Dar na Mwanza-Dodoma Je utakubaliana na mimi kuwa labda kwa sababu DR. Slaa alitaka kurusha Data zake, labda receiver/transmitters ziliminywa kama kitendo kile cha kuzima Kamera ktk jengo la bunge wakati mweshimiwa akifanya vitu vyake?

Kwa sisi tutaendelea kufikiria kuwa ni hujuma mpaka hapo majibu mazuri/ya ukweli yatakapotoelewa.
 
Mkuu Kasheshe,

Darasa zito sana hili, nimekusikia mkuu!

Kasheshe hana shule yoyote katika maswala haya isipokuwa anajua hata yeye kuwa anasaidia watu wake kuleta usanii.

Lakini nina uhakika katika hili atakwama na mwisho atakimbia tu, mpaka Star Tv na TBC watakapo toa majibu ya kutosha na siyo ya kasheshe.
 
Back
Top Bottom