TV za dini kuanzishwa.Hii inaashiria nini?

Mtego wa Noti

JF-Expert Member
Nov 27, 2010
2,592
1,599
Leo nimeangalia kwenye taarifa ya habari channel ten kuwa kanisa la Mch. Rwakatare wanataka kuanzisha Television yao itakayoitwa Ebenezer Tv. Naona kila kanisa liko ize kuanzisha Tv kila kukicha, hii ina maana gani wanaJF, kwamba ndio tunakaibia mwisho wa dunia hivyo wanatumia kila njia kufikisha ujumbe ili baadae Mungu asiwalaumu aliowatuma kuongoza kondoo wake? Naomba majibu wanaJF...nawakilisha...
 
Kueneza neno la mungu kwa watu wengi zaidi na biashara pia.
 
Kueneza neno la mungu kwa watu wengi zaidi na biashara pia.
kwa hyo ina maana kama kila kanisa wakiwa na tv yao hizi wanazozitumia kwa sasazitadoda maana hazitapata wateja, kwa mfano chanel ten kuna lusekelo, rwakatare, kakobe na wengineo. wakiwa na tv zao si kule watu wataanza kuhisi njaa?
 
kwa hyo ina maana kama kila kanisa wakiwa na tv yao hizi wanazozitumia kwa sasazitadoda maana hazitapata wateja, kwa mfano chanel ten kuna lusekelo, rwakatare, kakobe na wengineo. wakiwa na tv zao si kule watu wataanza kuhisi njaa?
Ndio maana yake............na huenda wanaanzisha TV stesheni ili kupunguza gharama za kurusha matangazo kwenye tv stesheni nyingine.
 
Hivi Tanzania kuna tv station ya kiislamu? Nimeuliza tu ili nijue wakuu.
 
Mara nyingi hizi tv ni mahsusi kwa mijini tu ambako ndiko kwenye biashara kubwa kubwa. Vijinini haitalipa na kawaida mungu wa dini huangalia masilahi zaidi. Vijinini kuna nafsi nyingi lakini hazina uchumi kigezo ambacho kimemsababisha asiwekeze huko.
.
 
Mara nyingi hizi tv ni mahsusi kwa mijini tu ambako ndiko kwenye biashara kubwa kubwa. Vijinini haitalipa na kawaida mungu wa dini huangalia masilahi zaidi. Vijinini kuna nafsi nyingi lakini hazina uchumi kigezo ambacho kimemsababisha asiwekeze huko.
.
ok, ndio maana huku vijijini tuko doro..hata hivyo vijijini hakuna umeme, kw hiyo ni ngumu kuendesha tv
 
Hii ni biashara tu inayolengwa wala sio kulitangaza neno la Mungu. TV zitasaida kupeleka watu kwenye majumba yao ili wakachange zaidi kwa ajili ya kuwaneemesha wachungaji. Kuhusu TV zingine bado zitapata watu kama sisi maana kwangu ni marufuku kuangalia huo uongo.
 
Waislam wapo dis organized hivyo kuanzisha tv ni ngumu ingawa matajiri wakubwa tanzania ni waislamu!bakwata ipo kutuliza amani si social developments
 
hawana vita bali chombo kilichopewa dhamana na serikali bakwata is not there for muslims!hakuna hata hospital moja ya waislamu etc!
 
kwa kuwa wameamua kuanzisha tv zao na hii itayumbisha hizi zilizop kimapato, hamuoni kuwa hizi zilizopo zinaweza kujitahidi kuweka vikwazo kwa hizi mpya kuanzishwa ili biashara yao isidorore? hebu imagine kakobe, rwakatare, lusekero, mwakasege, wote hawa wakianzisha tv zao, biashara si itakuwa ngumu kwa hizi zilizopo??
 
Mkuu hebu jaribu siku moja kuangalia hizo tv, utaona hawapo kibiashara kabisa kama unavyo dhania.
 
hivi hawa jamaa wa hizi tv wanapataje faida? maana sionagi matangazo ya biashara kwenye tv zao...ufafanuzi plz
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom