Tuzo tunazopewa tanzania zinatia shaka

Avocado

Member
Aug 23, 2010
97
4
Namekuwa nikifuatilia sana vyombo vya habari na hii ni mara ya pili katika kipindi kisicho pungua mwaka mmoja nimesikia Tanzania ikitunukiwa TUZO kwenye nyanja za ELIMU na AFYA,kwa kweli nimeakuwa na mashaka sana juu ya hao wanao toa, na wanaopokea hizo TUZO kwa kweli sijui vinatumika vigezo gani kupewa TUZO hizo,ukiangalia jinsi waziri wa mambo ya nje Mh Membe anavyokuwa kifua mbele kuzizungumzia TUZO hizo utadhani kuna kitu kikubwa sana kimefanyika hapa Tanzania,wiki mbili zilizopita kulikuwa na taarifa kuwa dawa mseto za malaria zimeadimika nchini na ilisemekana kuwa kuna vigogo wameziuza nje ya nchi,na uhaba huo wa dawa pia waziri alikiri kuwa upo, lakini akajitetea kuwa bajeti ni kidogo ! Na akasema wanahitaji kama dola milioni mia tano($500M.) kupitia bajeti ijayo ili kupata dawa za kutosha, Malaria ni ugonjwa unaua zaidi kuliko magonjwa mengi,na kwa kifupi hili ni janga na janga ni vita, je tutahitaji kusubiri bajeti ijayo kuingia vitani ? Wakati tunaisubiri bajeti hiyo maisha ya watanzania wakawaida hasa vijijini tunayaweka wapi ? Mimi nilidhani JK alipozindua kwa mbwembwe ile kampeni ya MALARIA HAIKUBALIKI alikuwa amejipanga ! Kumbe hata dawa hakujua zipo au hazipo !!
Hili la TUZO ya ELIMU ambayo Tanzania aliipata mwaka jana sijaelewa vizuri naomba wadau mnisaidie, ilikuwa ni TUZO ya uwingi wa majengo ya shule au ubora wa taaluma ? na kwanini pia tukubali kupewa TUZO ambazo hazina Tija ?Kuna sifa gani kupewa TUZO ya kuandikisha wanafunzi wengi halafu mwisho wa siku wote wanafeli ? Hebu angalieni matokeo ya kidato cha nne mwaka 2010 ni AIBU napenda kumshauri aliyepokea ile TUZO ya ELIMU airudishe alikoitoa ''we don't deserve that shit '' ! Na hiyo ya MALARIA pia wairudishe,vingozi wetu wanafanya propaganda huko nje ya nchi ili kukidhi matakwa yao ya kiutawala na kuwapendezesha hao wafadhili huko nje lakini hali halisi ni kinyume kabisa hapa nchini,hakuna haja ya kuwaonyesha jirani zako kuwa wewe na familia yako mna Good time kumbe njaa kali ,ni heri ieleweke mna njaa ili msaidiwe kwa hali na mali. Viongozi wetu waache kupenda sifa za kimataifa wakati kitaifa hali ni mbaya. Unasifiwa kuwa umezaa watoto wengi unafurahi na unachukua zawadi,jiulize mwisho wa siku, inakuwaje ?
Mungu tusaidiae !!
 
Kwa kweli katika hili tupo pamoja mzee. Hebu angalia kila siku takwimu za vifo juu ya Malaria inaongezeka na hata dawa za uhakika za kutibu malaria hazipatikani katika zahanati, vituo vya afya na hata hospitali zetu za Serikali. Hatuna haja ya hiyo tuzo isiyo na maana Irudi tu ilikotoka.

Kwangu mimi sera nzuri ya kuboresha huduma za afya ni hii; Expand, Equip and Renovate na tukikamilisha suala hili hakika tutastahili tuzo kwa maana tutakuwa tumepunguza vifo vya kinamama na watoto na pia umbali wa kutoka ktuo kimoja cha tiba hadi kingine na kwa kufanya hivyo tutakuwa tumemsaidia mtanzania.

Expand:- Tunahitaji kuvipanua vituo vya Afya vilivyopo ili viweze kutoa huduma bora za upasuaji wa dhalura, kuweza kuongeza damu kwa wanaohitaji na hata kuweza kutoa Oxygen kwa watoto na hata watu wazima wanaohitaji huduma hizo.
Na si kujenga kituo cha afya kila kijiji wakati nvilivyopo vimetushinda kuviongoza ili vitoe huduma bora.

Renovate:- Tunahitaji kukabati kama si kufanya ukaravati kwa kila zahanati iliyopo ili kuwe na mazingira rafiki kwa kina mama na hata wahitaji wengine wa huduma za afya. Kwa kufanya hivi akinamama wajawazito watajifungulia hospitali badala ya kwenda kwa mkunga wa jadi na vifo vya kinamama na watoto wachanda vitapungua kwa kiasi kikubwa.

Equip:-Tunahitaji kila Hospitali, Kituo cha Afya na kila Zahanati iwe na Wataalamu wa kutosha, Vifaa bora na vya kisasa vya kutolea huduma, Wahudumu wenye mishahara, motisha na maadili mazuri katika taaaluma zao ili kuboresha huduma za afya na Madawa ya kutosha ili kuboresha huduma za afya badala ya hali ilivya sasa kila ifikapo tarehe 2 ya kila mwezi dawa zimekwisha katika vituo vya huduma.

Kwa kutekeleza haya mambo matatu hapo juu kwa kweli tutahitaji tuzo na sisi tutaipokea kwa mikono miwili kwa kuwa tutakuwa tumestahili.

Mungu ibariki Tanzania na Watu wake.
 
napata mashaka na hata hao wanaozito hizo tuzo,au ni kwa ajenda za kisiasa.tuachane na danganya toto tujipange mambo yetu still yako hovyo na wala hatustahili tuzo hizo
 
mtiririko wa kutunukiwa udaktari, unaletwa mpaka kwenye mambo makubwa ya kitaifa. tunajifurahisha na tuzo wakati watu wanakufa, wanakosaelimu bara! nakubaliana na wewe mkuu, hizi tuzo ni hazina tija na ni uhuni tu
 
Back
Top Bottom