Tuzo Kwa Mtanzania Aliyefanya Vyema

Nakubaliana na wale wanaosema isiitwe majina ya Wanasiasa. Wazo langu tuzo zinaweza kuwa na majina ya vivutio vyetu vya utalii. Hii itasaidia kutangaza vivutio vyetu vya utalii ndani na nje ya nchi.

Hapa kuna mfano yaweza itwa Serengeti (mbuga), Ngorongoro (mbuga), manyara (mbuga), Mikumi (mbuga) nk, ama yaweza itwa Amboni (machimbo ya kitalii), Mlingotini (eneo la utalii Bagamoyo), Kilwa (sehemu ya utalii). Pia tunaweza kutumia kutangaza maziwa, mfano Ziwa Victoria, Rukwa, Nyasa (tena hili ni muhimu manake wamalawi wanasema mpaka na TZ ni mwisho wa maji, na huliita Ziwa Malawi), Tanganyika, Singida, Kindai nk. Tunaweza kutangaza mito yetu kama Mara, Kagera, Ruvuma nk.
 
wandugu,

..nashukuru kuna ambao wameona hii trend ya kuwaenzi wanasiasa peke yao siyo nzuri, na inakwaza historia na michango ya wazalendo wengine.

..tuzo napendekeza itolewe kila mwaka. lakini kama, say, mwaka huo hakuna mwanamichezo aliyechomoza kweli kweli basi category ya mwanamichezo inaweza kurukwa.

..pia kila category iwe na Mtanzania anayeheshima ktk category hiyo ambaye atatoa wasifu wa mshindi na kumkabidhi tuzo.

..kwa mfano kama mshindi ni mwanamichezo, golikipa aliyechomoza kuliko wenzake, basi tutafute golikipa[pondamali,mwameja,mahadhi,..] mwenzake akabidhi tuzo.

..vilevile, kama mshindi kwa wanataaluma ni daktari mwanadada, basi tutafute daktari mwenzake[Dr.mrs.mwaikambo,Dr.mrs.masesa,...] amkabidhi tuzo.

..MC anaweza kuwa mtangazaji yeyote wa redio au television. pia wana kamati wanaweza kushirikishwa ktk hili.

..NAOMBA NIPENDEKEZE WANASIASA WASIPEWE TUZO HIYO. NASEMA HIVYO ILI MJIEPUSHE NA PRESSURES NA MIGOGORO YA KISIASA NA VYAMA.

NB:

..mfumwa nimependa mapendekezo yako kuhusu vivutio vya utalii.

..umeusahau mto Rufiji. nadhani huu ni kati ya mito mikubwa afrika mashariki.

.
 
TPN kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali Tanzania inapenda kupata maoni ya namna gani ya kutoa TUZO maalumu kwa Mtanzania ambaye atakuwa ametoa mchango mkubwa katika jitihada za kuboresha maisha ya Mtanzania wa kawaida katika kipindi husika.
Bandiko hili ni kuonyesha Sanctus Mtsimbe alikuwa mtu wa shukrani, appreciative, kukubali mafanikio ya wengine na kuwapatia tuzo.

Kwa maoni yangu, a deserving farewell kwa member wetu yoyote, aliyetangulia mbele ya haki ni kumuaga kupitia maandishi yake, threads zake ili kujikumbusha mawazo yake, maneno yake na matendo yake tukiendelea kuishi Tribute to Sanctus Mtsimbe: Sio tu ni smart kwa mavazi na muonekano, pia ni smart kwa mawazo, maneno, na matendo, na very smart upstairs!

RIP Comred Santus Mtsimbe, maandishi yako humu JF, yatakuishi milele!.

Umepigana vita vilivyo Vitakatifu,
Mwendo Umeumaliza, Imani umeilinda.

Bwana Ameleta, Bwana Ametwaa, Jina Lake Lihimidiwe!.

Paskali
 
Back
Top Bottom