Wandugu, katika utawala wa CCM awamu ya nne, Mungu alituinulia watu miongoni mwetu akatuonyesha jinsi serikali ya CCM inavyotenda maovu, akatuonyesha ufisadi mkubwa kama wa EPA, Meremeta radar nk. Katika ufisadi ule hakuna aliyekana kuhusika ikwemo serikali yenyewe.
Cha kushangaza wezi walewale wakaja kutuomba watuongoze(kipindi hiki cha pili), wakaja na khanga, wali, tshirt na kofia. Mwisho wa siku tukaamua kuwachagua wezi watuongoze. Kitendo hiki kilimkasirisha sana Mungu wetu, aliyekuwa ametuwekea kila kitu tuamue. Baada ya hapo akaamua kuondoka maana hatukumtii. Wezi tuliochagua ni wa shetani, wala si wa Mungu.
Na hizi ndizo ishara za kuachwa na Mungu: Mabalaa mengi kama ajali za majini, angani na nchi kavu, njaa, kukosa huduma muhimu kama mahospitalini, umeme, maji na nyingine nyingi. Hata wana wa Israeli kipimo chao cha kumkosea Mungu ni adhabu na mabalaa makubwa, hadi walipotubu na kumwangukia tena.
Kwa Mawazo yangu ni kuwa Mungu ameondoka ameenda Rwanda. Hili ndilo taifa lililotubu baada ya mabalaa makubwa. Na sasa ameifanya Rwanda kuwa taifa la mfano ulimwenguni.
Kwa hiyo tuyavumilie,tuliyataka wenyewe, tunahitaji toba ya kweli, ikiwemo kuwaondoa viongozi na chama hiki dhaifu na kumtii Mungu kwa kuchagua viongozi waadilifu.
Vinginevyo taifa litaangamia.
Cha kushangaza wezi walewale wakaja kutuomba watuongoze(kipindi hiki cha pili), wakaja na khanga, wali, tshirt na kofia. Mwisho wa siku tukaamua kuwachagua wezi watuongoze. Kitendo hiki kilimkasirisha sana Mungu wetu, aliyekuwa ametuwekea kila kitu tuamue. Baada ya hapo akaamua kuondoka maana hatukumtii. Wezi tuliochagua ni wa shetani, wala si wa Mungu.
Na hizi ndizo ishara za kuachwa na Mungu: Mabalaa mengi kama ajali za majini, angani na nchi kavu, njaa, kukosa huduma muhimu kama mahospitalini, umeme, maji na nyingine nyingi. Hata wana wa Israeli kipimo chao cha kumkosea Mungu ni adhabu na mabalaa makubwa, hadi walipotubu na kumwangukia tena.
Kwa Mawazo yangu ni kuwa Mungu ameondoka ameenda Rwanda. Hili ndilo taifa lililotubu baada ya mabalaa makubwa. Na sasa ameifanya Rwanda kuwa taifa la mfano ulimwenguni.
Kwa hiyo tuyavumilie,tuliyataka wenyewe, tunahitaji toba ya kweli, ikiwemo kuwaondoa viongozi na chama hiki dhaifu na kumtii Mungu kwa kuchagua viongozi waadilifu.
Vinginevyo taifa litaangamia.