Tuwe wakweli: Tatizo La Zanzibar sio Muungano, ni Udini

Status
Not open for further replies.
Sio kweli Mkiristu kwenye BLM ni Mwakanjuki pekee, alishakuwepo John Okello, Isack Sepetu na kuna wakristu wengi tuu wenye majina ya Kiislamu.

Hata kina Wolfgang Dourado, Agustino Ramadhani, Charles Hillary etc ni Wakristo Wanzanzibari!.

Kanisa lilianzia Zanzibar na Bagamoyo kufuatia kupigwa marufuku biashara ya utumwa. Soko lilikuwa Bagamoyo na Zanzibar, Kanisa liliwalipia fidia watumwa ili kuwagomboa na ndio Wakristu wa kwanza!.

Kiukweli udini halihawahi kuwa tatizo Zanzibar!.

Nakubaliana na wewe udini siyo tatizo kuu la ZNZ. Tatizo la Znz ni hali mbaya ya maisha inayochangiwa na ukosefu wa ajira n.k

Kijamii mtu anapokosa fursa muhimu za kujiendeleza kiuchumi, ili kujiliwaza ujiunga na wenzake kama yeye katika vikundi vya kidini, kikabila, kikanda n.k na kuona wote walio nje ya kundi lake kijamii kama maadui.
 
Udini ndio sera kubwa ya awamu ya Pili ya Kikwete nashangaa sana kuona nae ana toa tamko la kulani yaliyo tokea Zanzibar wakati Waislaam amekuwa akiwagawia fedha misikitini na hata Matamko kadhaa ya mabaya yaliyowai kutolewa na Waislaam na lile la Igunga alikuwa kimia!
 
Udini huo kwa mujibu wa mtazamo wako unaouona upo Zanzibar tu umeangalia upate wa pili wa kidole ukaangalia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Wakristo mpo wangapi? Tukichanganua Wizara za JK zaidi ya 70% ya mawaziri ni WAKRISTO !!! Wabunge wa bunge la jamhuri ya muungano Wakristo mpo wengi? Wakurugenzi wa taasisi za serikali almost 90% ni wakristo? Ajira vijana wengi wa kiislamu hawana kazi je nikuulize NCHI HII NI YA KIKRISTO!!!!! TUONDOSHEE UPUUZI WAKO HAPA

Mkuu usifanye asumption.

Interview zetu hatufanyi kuangalia divinity mtu kapata ngapi, hili ni kosa na pia tunahitaji watalamu na sio wachungaji kwenye system zetu wala hatuhitaji maasikofu au maimamu.

Interview zetu hatufanyi kwa kubalace idadi za kidini je wasio na dini na dini ndogo ndogo itakuwaje??, bali uwezo, uzoefu na elimu ya mtu. vinginevyo systems ziwe za kibenki au kimitambo itafeli kama suala ni kubalance idadi na sio taaluma.

Kusema tu waislamu wachache katika serikali ya jamhuri ya muungano haitoshi nikuchochea matatizo tu. mbona pale juu panadalili nzuri ya uiano mkuu!!!

Inawezekana kabisa mtu kuchoma nyumba yake sio ajabu, lakini huyo tunamwita kichaa. Makanisa 26 hawa wachungaji wote vichaa???, mabaa na maduka ya wabara wote vichaa?? wanaosema wabara waondoke hapo zenji kwani wabara vichaa wafukuzwee?? au wabara ndo wanapita mitaani kujitangaza wakuzwe?

Mkuu wangu ubaguzi na janjajanja ya kuukwepa ukweli itatuumiza siku zijazo.
 
Mkuu usifanye asumption.

Interview zetu hatufanyi kuangalia divinity mtu kapata ngapi, hili ni kosa na pia tunahitaji watalamu na sio wachungaji kwenye system zetu wala hatuhitaji maasikofu au maimamu.

Interview zetu hatufanyi kwa kubalace idadi za kidini je wasio na dini na dini ndogo ndogo itakuwaje??, bali uwezo, uzoefu na elimu ya mtu. vinginevyo systems ziwe za kibenki au kimitambo itafeli kama suala ni kubalance idadi na sio taaluma.

Kusema tu waislamu wachache katika serikali ya jamhuri ya muungano haitoshi nikuchochea matatizo tu. mbona pale juu panadalili nzuri ya uiano mkuu!!!

Inawezekana kabisa mtu kuchoma nyumba yake sio ajabu, lakini huyo tunamwita kichaa. Makanisa 26 hawa wachungaji wote vichaa???, mabaa na maduka ya wabara wote vichaa?? wanaosema wabara waondoke hapo zenji kwani wabara vichaa wafukuzwee?? au wabara ndo wanapita mitaani kujitangaza wakuzwe?

Mkuu wangu ubaguzi na janjajanja ya kuukwepa ukweli itatuumiza siku zijazo.

Mkuu,

Usikae ukaziamini statistics asilimia 100 hata siku moja zifanyie uchunguzi. Dhumuni la kuwepo taasisi za kidini ni kuangalia utendaji wa hiyo kazi ya ukusanyaji taarifa za sensa. Mfano umuhimu wa masheikh na maimamu ni kwamba wametapakaa Tanzania nzima kuliko hata wajumbe wa nyumba kumi. Na wao ndio watu walio karibu na jamii. Sasa wakiwa wanasimamia zoezi itahakikishwa kilamtu amehesabiwa nchini na sio swala la dini.

Kuhusu uwiano wa dini ni muhimu kwasababu wakristo tuwe honest wamekuwa wakidai kwa muda mrefu wao ni wengi hivyo the end justify the means ndio maana tunaona kuna mikataba mingi ya kifisadi kama lile dude la Memorandum of Understanding (MOU) ambapo waislamu wanafeli kwasababu the end justify the means. Sasa ikiwa waislamu ni wengi au wakristo wengi basi itaeleweka na sio kama kutatokea tatizo lolote. Shida ni pale unapozuia dini ya mtu isitambulike katika sensa wakati swala la umuhimu mkubwa sana nchini. Nchi za magharibi hadi kuomba kazi ukiitwa katika interview unapojaza forms zao unaulizwa dini yako sasa kwanini hapa iwe tatizo?
 
Tanzania has long way.....dhambi ya udini itatumaliza vizazi na vizazi na serikali yetu imelala kwa yanayotokea zanzibar.
 
Kama kuna kitu kimoja ambacho chdema wanakitamani basi ni kuuvunja muungano, maana huo ukiwepo wao madaraka hakuna kabisa. Kura za Waunguja na Wapemba watasikia redioni tu. Ndio maana nikawafungulia nyuzi kuwaambia waungane rasmi na uamsho.

Nilimuona juzi Lissu kwenye ITV akitetea hizo fujo na akitetea wanaotaka kuongelea kuvunjika muungano wapewe fursa. Kwi kwi kwi teh teh teh!

Chadema jiungeni tu na Uamsho msione haya. Maana huko visiwani hamna chenu.
 
Tunaloliona kuwa ni tatizo la Zanzibar, sio la Zanzibar pekee bali tatizo la Tanzania yote na kwa maneno ya wazi zaidi, TATIZO LA TANZANIA NI CCM.

La ZNZ linaonekana ni la kidini kwa sababu kule udini ndio mbolea nzuri la kupandikiza wanachotaka kupandikiza, na kwa Tanganyika mbali ya udini pia kuna mbolea ya "Uvunjaji wa Amani". Kila linapotokea suala mwiba kwa CCM, hutumia moja katika hayo ili" la kuwafanya Watanzania waelekeze macho yao huko na kuacha kujadili yanayotumaliza.

Kila linapokuja tatizo la kujadili mada muhimu kama vile Muungano,uchaguzi na sasa Katiba Mpya, CCM hutafuta ni wapi pako legege na kupatumia. Haya yote ni kiini macho, ni kufunika kombe ...upepo upite." Tusubiri lijalo.
 
Watajuta kuunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa maana CUF imeamua kuja "kivingine!"

ni kweli...i dont trust cuf at all..ina ugaidi ndani yake..yule hamad na lipumba ndio wao tu wanagombania urais sijui kwanini hawakai pembeni wawaachie watu wengine nao wagombanie hizo nafasi
 
Nafikiri mtoa bandiko imekupuruchuka. Zanzibar hakuwezi kuwa na UDINI hata siku moja sababu karibi 99.96% ya wazanzibari ni waislam. Dini nyengine ni less than 0.4%.

sasa udini utatoka wapi hapo kama karibu wote ni dini moja? Nakushauri fanya research yako vizuri kama si kudurusu historia ya Znz, Tanganyika na Tanzania (baada muungano) utajua nini cha kuandika na kuzungumza kwa wasomi.
 
Mkuu FJM,

Ni kweli Zanzibar ina tatizo la uongozi bora lakini hata huku Tanganyika tuna tatizo hilo hilo.


Tatizo la Zanzibar sio udini, it is lack of leadership. Basi.
 
Wa Tanganyika msitafute mchawi hapo na hizo propaganda. Wachawi ni nyie wenyewe kulazimisha kitu kisichotakiwa.
1. WaZnz wapo wazi kabisa kuwa wanataka kura ya maoni ya kuchagua au kukata muungano kabla kuanza kujadili katiba mpya a muungano.
2. Kwa mujibu wa Katiba ya Znz ya sasa Muungano huo ni HARAMU, sababu haujaridhiwa na Baraza la wawakilishi ili iwe kama sharia kutumika Znz. Umeridhiwa na Bunge la Muungano tu.
3. Kulazimisha kitu ambacho ni kinyume cha katiba ni kosa na kukubali kufuata ni ukondoo na usaliti ndio maana waZnz wapo wazi kabisa kulikemea hilo na kuliondosha kwa mikono yao wenyewe.
4. Znz hakuna UDINI kwani karibu 99.9% ni waislam. Udini upo Tanganyika na ndio unaolazimishiwa kuingia Znz kwa mwamvuli wa Muungano.

Hongera Znz , Hongera waZnz kwa kuondosha dhulma kwa mikono yenu
 
Tunaloliona kuwa ni tatizo la Zanzibar, sio la Zanzibar pekee bali tatizo la Tanzania yote na kwa maneno ya wazi zaidi, TATIZO LA TANZANIA NI CCM.

La ZNZ linaonekana ni la kidini kwa sababu kule udini ndio mbolea nzuri la kupandikiza wanachotaka kupandikiza, na kwa Tanganyika mbali ya udini pia kuna mbolea ya "Uvunjaji wa Amani". Kila linapotokea suala mwiba kwa CCM, hutumia moja katika hayo ili" la kuwafanya Watanzania waelekeze macho yao huko na kuacha kujadili yanayotumaliza.

Kila linapokuja tatizo la kujadili mada muhimu kama vile Muungano,uchaguzi na sasa Katiba Mpya, CCM hutafuta ni wapi pako legege na kupatumia. Haya yote ni kiini macho, ni kufunika kombe ...upepo upite." Tusubiri lijalo.

Nakubaliana na wewe Mkuu kuwa udini ni kama mbolea tu na tatizo hilo ni la tanzania nzima, ni wazi kuwa tanganyika idadi ya waislamu na wakristo ni almost 50:50 hivyo mbolea ya udini inakuwa ngumu kuotesha zao la vurugu, Zanzibar ina waislam wengi na ni rahisi kuwatumia kwa mwavuli wa dini kutekeleza agenda yoyote ile.

Viongozi waliopo madarakani sasa hivi pengine ni dhaifu sana au idara zao za intelijensia haziwapi mambo yaliyojificha nyuma ya kile kinachoitwa uamsho.

Uislam ni ule ule tangu lilipojengwa kanisa la anglikana na lile la wakatoliki la minara miwili katikati ya ngome kongwe, himaya ya uislam, yapata miaka zaidi ya mia moja iliyopita, je mbona makanisa hayo hayakuchomwa kwa muda huo wote, au waislam wana mafundisho ya mtume mpya zaidi ya Muhammad SAW
 
Nafikiri mtoa bandiko imekupuruchuka. Zanzibar hakuwezi kuwa na UDINI hata siku moja sababu karibi 99.96% ya wazanzibari ni waislam. Dini nyengine ni less than 0.4%.

sasa udini utatoka wapi hapo kama karibu wote ni dini moja? Nakushauri fanya research yako vizuri kama si kudurusu historia ya Znz, Tanganyika na Tanzania (baada muungano) utajua nini cha kuandika na kuzungumza kwa wasomi.

Tatizo la udini lipo kwani hao 0.4% ndiyo wanaochomewa makanisa, hao pia wana uhuru wa kuabudu kama walivyo 99.96%. kumbuka hata mkifanikiwa kuwamaliza hao mtaanza Shia na Sunni kama ilivyo Iraq,somalia na Libya. Nawapeni ushauri wa bure Msiwabague wakristo na kuwafanya waishi maisha ya dhiki katika nchi yao. Mungu wa kweli hasaidiwi katika kuchoma makanisa, hiyo ni kazi ya shetani Kuchinja kuua na kuharibu. Wanaofanya hivyo ni maajenti wa shetani na kama wameaminishwa kuwa wataiona pepo kwa kuwaua wakristo wamedanganywa na wao wamedanganyika. Nini tatizo kama ni muungano na tuachane tu kwa amani mbona tulikuwa na East African community tukaachana na baadaye tumerudiana tena na hatukuchomeana nyumba wala kupigana. Vipi leo tuchomeane nyumba za ibada wakati uhusiano wetu kibinafsi ni mkubwa sana. Binafsi sioni nafaidika nini na muungano kama biashara tunafanya na watu wa nchi mbalimbali.tukianzisha vurugu hata anayechoma kanisa pia hatapona vita vinavyohusisha imani ni hatari kuliko vya watusi na wahutu. Mungu apishe mbali na vurugu na kama ni kuvunja muungano na uvunjike kwa amani. Mungu wa amani tupitishe salama katika hili pia. Amen
 
ni kweli...i dont trust cuf at all..ina ugaidi ndani yake..yule hamad na lipumba ndio wao tu wanagombania urais sijui kwanini hawakai pembeni wawaachie watu wengine nao wagombanie hizo nafasi

wewe kwa sababu ni wa ubavu wa pili humuoni Slaa na DJ Mbowe katika mapambio yao.

Kila la kheir usisahau kutazama hapo uliposimama lakini.

 
Tatizo la udini lipo kwani hao 0.4% ndiyo wanaochomewa makanisa, hao pia wana uhuru wa kuabudu kama walivyo 99.96%. kumbuka hata mkifanikiwa kuwamaliza hao mtaanza Shia na Sunni kama ilivyo Iraq,somalia na Libya. Nawapeni ushauri wa bure Msiwabague wakristo na kuwafanya waishi maisha ya dhiki katika nchi yao. Mungu wa kweli hasaidiwi katika kuchoma makanisa, hiyo ni kazi ya shetani Kuchinja kuua na kuharibu. Wanaofanya hivyo ni maajenti wa shetani na kama wameaminishwa kuwa wataiona pepo kwa kuwaua wakristo wamedanganywa na wao wamedanganyika. Nini tatizo kama ni muungano na tuachane tu kwa amani mbona tulikuwa na East African community tukaachana na baadaye tumerudiana tena na hatukuchomeana nyumba wala kupigana. Vipi leo tuchomeane nyumba za ibada wakati uhusiano wetu kibinafsi ni mkubwa sana. Binafsi sioni nafaidika nini na muungano kama biashara tunafanya na watu wa nchi mbalimbali.tukianzisha vurugu hata anayechoma kanisa pia hatapona vita vinavyohusisha imani ni hatari kuliko vya watusi na wahutu. Mungu apishe mbali na vurugu na kama ni kuvunja muungano na uvunjike kwa amani. Mungu wa amani tupitishe salama katika hili pia. Amen

Kuna tofauti kubwa sana kati ya Kusoma na Kuelimika.

Nakushauri urudi Skuli ukaelimike.

Kwani kwa kuelimika utaweza
1. Kuchambua jambo lolote kwa mapana yake na kulijadili kwa kina kabla kufikia maamuzi.
2. Kuelewa baya na zuri ikiwemo uongo na ukweli.
3. Kuyafanyia research mambo kabla kutoa kauli.
4. Kuwa na maamuzi sahihi.


WaZnz wameelimika na sasa wameiona dhulma ambayo imechomekwa katika Katiba ya Muungano. sasa wameamua kuiondosha dhulma hiyo kwa mikono yao na kukwepa hizo propaganda zinazopandwa na wa Bara.

Hoja zao hizi hapa.
1. WaZnz wapo wazi kabisa kuwa wanataka kura ya maoni ya kuchagua au kukata muungano kabla kuanza kujadili katiba mpya a muungano.
2. Kwa mujibu wa Katiba ya Znz ya sasa Muungano huo ni HARAMU, sababu haujaridhiwa na Baraza la wawakilishi ili iwe kama sharia kutumika Znz. Umeridhiwa na Bunge la Muungano tu.
3. Kulazimisha kitu ambacho ni kinyume cha katiba ni kosa na kukubali kufuata ni ukondoo na usaliti ndio maana waZnz wapo wazi kabisa kulikemea hilo na kuliondosha kwa mikono yao wenyewe.
4. Znz hakuna UDINI kwani karibu 99.9% ni waislam. Udini upo Tanganyika na ndio unaolazimishiwa kuingia Znz kwa mwamvuli wa Muungano.
 
kuna tofauti kubwa sana kati ya kusoma na kuelimika.

Nakushauri urudi skuli ukaelimike.

Kwani kwa kuelimika utaweza
1. Kuchambua jambo lolote kwa mapana yake na kulijadili kwa kina kabla kufikia maamuzi.
2. Kuelewa baya na zuri ikiwemo uongo na ukweli.
3. Kuyafanyia research mambo kabla kutoa kauli.
4. Kuwa na maamuzi sahihi.


Waznz wameelimika na sasa wameiona dhulma ambayo imechomekwa katika katiba ya muungano. Sasa wameamua kuiondosha dhulma hiyo kwa mikono yao na kukwepa hizo propaganda zinazopandwa na wa bara.

Hoja zao hizi hapa.
1. Waznz wapo wazi kabisa kuwa wanataka kura ya maoni ya kuchagua au kukata muungano kabla kuanza kujadili katiba mpya a muungano.
2. Kwa mujibu wa katiba ya znz ya sasa muungano huo ni haramu, sababu haujaridhiwa na baraza la wawakilishi ili iwe kama sharia kutumika znz. Umeridhiwa na bunge la muungano tu.
3. Kulazimisha kitu ambacho ni kinyume cha katiba ni kosa na kukubali kufuata ni ukondoo na usaliti ndio maana waznz wapo wazi kabisa kulikemea hilo na kuliondosha kwa mikono yao wenyewe.
4. Znz hakuna udini kwani karibu 99.9% ni waislam. Udini upo tanganyika na ndio unaolazimishiwa kuingia znz kwa mwamvuli wa muungano.

sipingi hoja zako ninachopinga ni strategies ambazo zinatumika ikiwa ni pamoja na kuwaumiza watu wasiohusika na hata kufaidika na huo muungano. Vita havina macho vitahusisha walio waislamu na wasio waislamu watoto wanawake na hata wazee.
 
Bado nauliza kama zanzibar hakuna ubaguzi wa dini mbona sipati majibu muaafaka. Nataka atakayejibu haya maswali aweke jazba na matusi pembeni, atumie hekima na busara katika kujibu na siyo nakule nahuku, na wao nataka kuelimishwa maana hata huku bara dini zipo zote kama huko zanzibar. Ni kweli hawa wachungaji vichaa kuchoma na kuharibu mali zao kama mnavyotaka kutuaminisha?

1. Nimisikiti mingapi imechomwa au kuhalibiwa dhidi ya makanisa 26

2. umesikia wapi huku tanzania bara ubaguzi wa wapemba au wanguja au wakifukuzwa mifano tafadhari!!

3. Kama suala ni waislam kubaguliwa hususani hapo zanzibar 99% ya viongozi wa serikali ni waislamu je wanawabaguwa waislamu wenzao wenzao?

4. Kama nyerere aliwakosea wazanzibar na baadhi ya waislam wanaoamini hivyo mpaka sasa Tanzania imeongozwa na marais wanne. Hawa ndiyo maamiri jeshi na wenyemaamuzi ya mwisho achiliambali waziri anataka nini mfano kikwete kavunja baraza la mawazili kama mara moja na kulikarabati mara mojo hivi majuzi.

-JK nyerere, mkristu
-Ally Hassan Mwinyi, mwislam
-Benjamin W. Mkapa Mkristu
-J.M Kikwete Mwislau
Ratio 2:2 = 1

a) Mnauaminishaje umma wa watanzania kwamba waislam mnaonewa sana? Je Mwinyi na kikwete wanawaonea pia?
b) Kila jambo na kosa ni la nyerere mbona Mzee karume halaumiwi au nyerere alikaa peke yake kuusain muugano?

Matusi na jaziba hapana, mwenye majibu anielimishe. Maswali ni manne sio moja tafadhari amjibu yaendane na idadi.
 
Mkuu,

Usikae ukaziamini statistics asilimia 100 hata siku moja zifanyie uchunguzi. Dhumuni la kuwepo taasisi za kidini ni kuangalia utendaji wa hiyo kazi ya ukusanyaji taarifa za sensa. Mfano umuhimu wa masheikh na maimamu ni kwamba wametapakaa Tanzania nzima kuliko hata wajumbe wa nyumba kumi. Na wao ndio watu walio karibu na jamii. Sasa wakiwa wanasimamia zoezi itahakikishwa kilamtu amehesabiwa nchini na sio swala la dini.

Kuhusu uwiano wa dini ni muhimu kwasababu wakristo tuwe honest wamekuwa wakidai kwa muda mrefu wao ni wengi hivyo the end justify the means ndio maana tunaona kuna mikataba mingi ya kifisadi kama lile dude la Memorandum of Understanding (MOU) ambapo waislamu wanafeli kwasababu the end justify the means. Sasa ikiwa waislamu ni wengi au wakristo wengi basi itaeleweka na sio kama kutatokea tatizo lolote. Shida ni pale unapozuia dini ya mtu isitambulike katika sensa wakati swala la umuhimu mkubwa sana nchini. Nchi za magharibi hadi kuomba kazi ukiitwa katika interview unapojaza forms zao unaulizwa dini yako sasa kwanini hapa iwe tatizo?
Hapa ndo penye tatizo kubwa sana hapa!!

Hivi waislamu wakiwa wengi au wakristo wakiwa wengi nini maana yake katika maisha ya Mtanzania?

Au ni league, kwamba sisi tupo wengi........halafu mkiwa wengi inakuaje?
:crazy::crazy:
 
Bigirita umenena

Hapa ndo penye tatizo kubwa sana hapa!!

Hivi waislamu wakiwa wengi au wakristo wakiwa wengi nini maana yake katika maisha ya Mtanzania?

Au ni league, kwamba sisi tupo wengi........halafu mkiwa wengi inakuaje?
:crazy::crazy:
 

Hoja zao hizi hapa.
1. WaZnz wapo wazi kabisa kuwa wanataka kura ya maoni ya kuchagua au kukata muungano kabla kuanza kujadili katiba mpya a muungano.


Very good........kwahiyo wale vijana walioandamana ndio waZnz? wanawakilisha mawazo ya waZnz wote??.......

2. Kwa mujibu wa Katiba ya Znz ya sasa Muungano huo ni HARAMU, sababu haujaridhiwa na Baraza la wawakilishi ili iwe kama sharia kutumika Znz. Umeridhiwa na Bunge la Muungano tu.
Katiba iliyoukubali Muungano sio hii ya sasa............kwanini mmetengeneza katiba ISIYOUKUBALI MUUNGANO??
Hapa ndo chokochoko zinapoanzia sasa!!!


3. Kulazimisha kitu ambacho ni kinyume cha katiba ni kosa na kukubali kufuata ni ukondoo na usaliti ndio maana waZnz wapo wazi kabisa kulikemea hilo nakuliondosha kwa mikono yao wenyewe.
unamaanisha nini???
4. Znz hakuna UDINI kwani karibu 99.9% ni waislam. Udini upo Tanganyika na ndio unaolazimishiwa kuingia Znz kwa mwamvuli wa Muungano

Sasa unasomeka loud and clear!!! Watanganyika ndio wadini........Mtapata mnachikata, lakini hamtakuwa salama hata kidogo!!!!

Sisi tutawaangalia tu!!!
Endeleeni kujifanya hamnazo!!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom