cheusimangala
JF-Expert Member
- Feb 27, 2010
- 2,585
- 496
Nawatakieni nyote heri ya mwaka mpya.Mungu akaufanye mwaka huu kuwa mwaka wenu wa kuvuna yote mnayomuomba.
Nikiwa kama mzazi mtarajiwa,nimeona sio mbaya sisi wazazi tukikumbushana au kufunguana macho ktk mambo mbalimbali yatakayozidisha usalama wa watoto wetu.
Ni kawaida sana sisi watanzania kuishi na ndugu zetu wengi ktk nyumba zetu,utakuta mfano mtu una watoto wako lkn pia una ndugu zako na ndugu wa mkeo mnaishi nao pamoja kwa lengo la kuwasaidia ili siku moja nao wawe na maisha yao.Hii inasababisha watoto wetu wa kiume washee vyumba na ndugu zetu wa kiume yaani baba zao wadogo au wajomba zao na watoto wetu wa kike washee vyumba na mama zao wadogo/wakubwa au shangazi zao na housegirl.
Ni jambo zuri kuishi na ndugu zetu lakini naombeni mniamini kuwa sio vizuri watoto wetu walale na ndugu zetu watu wazima hasa wa kiume,nina uhakika na ninachokiongea,nina shuhuda nyingi juu ya watoto wengi wa kiume walivyokua sexualy abused na ndugu wa kiume wa wazazi wao wanaolala nao pamoja.Na inakuwa vigumu kwa mtoto kusema maana hawa molesters wanajua jinsi ya kumtisha mtoto ili asiseme.
Hata watoto wa kike ni vizuri waachwe walale wenyewe maana pia nimeshashuhudia watoto wadogo wa kike wakifanyishwa vitu vya ajabu na ndugu wa kike wa wazazi wao.Kuna mtoto mmoja hivi tunavyoongea anatibiwa fungus mdomoni sababu alikua "analambishwa chumvi" na mama yake mdogo kila siku usiku wakilala.
Najua labda mtaniona mwehu sababu tunawapenda ndugu zetu hivyo hatuwezi kamwe kudhania kuwa wanaweza kufanya hivi,lakini laiti ungeshuhudia niliyoshuhudia ungechukua tahadhari.Dunia imeharibika sana.wanadamu hatuna tena woga,sijasema muwafukuze ndugu zenu,ila ningeshauri hasa kwa watoto wa kiume kuliko wakalala na ndugu wakubwa wa kiume ni bora ndugu hao walale sebuleni kwenye magodoro.
Vile vile kina mama wenzangu naomba niwaonye,kama una tabia ya kuwaambia ndugu zako wa kiume wamsafishe mtoto akiwa amejisaidia uache sio vizuri.Hii tabia ya kumwambia mjomba au baba mdogo wa mtoto akusafishie mtoto ni ya hatari sababu,mwanao anaweza chomekwa vidole sehemu sehemu na wewe ukiona wala usishitukie.Na kama uncle anamfanyia mtoto mambo haya wakati anamsafisha basi akipata upenyo wkt mwingine pia atafanya.
Vile vile najua JF ni kama msafara wa mamba ambao ndani yako kuna mijusi na kenge,najua kabisa wengi wa JF memberz ni watu wazuri sana na wenye hekima lakini nataka niongee na wale wachache wetu wenye tabia za kifataki.Nyie ambao ni watu wazima lakini kutwa kurubuni watoto wadogo,definition ya fataki ni mtu mzima anayewarubuni kimapenzi watoto wadogo.
Nina amini mtu yeyote mwenye tabia za kifataki anaweza kujirekebisha,hivyo naombeni muache tabia za kutuharibia watoto/wadogo zetu.Kama wewe ni mbaba unayefanya hivi hebu jiulize je mtu mzima wa umri wako akikaharibu kale katoto kako unakokapenda utafurahi?Jibu ni hutafurahi,vile vile na wazazi wa hao watoto mnaowarubuni hawafurahi.
Na nyie wanaume mnaotongoza watoto wetu wa kiume nawaombeni hofu ya Mungu iwaingie muache maana siku za hivi karibuni hiki kimchezo kimepamba moto.
Pia kuna kina mama wanaharibu watoto,na maanisha kuna mafataki wa kike pia,wengi tu,kuna mama mmoja amesababisha mtoto wa mwenzake aache shule,huyu mama alikua anamfata mtoto shule ya boarding anakosoma anamtorosha wanakwenda kupanga hotel mwishowe mtoto akashindwa masomo na ameambukizwa ukimwi japo huyo mama anadai yeye mzima lkn muda si mrefu na yeye atachekiwa.
Pia kuna kina mama wasagaji wanaharibu watoto wa kike,labda hili ni geni kwetu lakini wapo na hivi vitendo vipo na shuhuda ninazo.Hivyo naomba mwaka huu ili Mungu awaondolee mikosi na mabalaa na aweze kuwapatia yale mnayohitaji hebu nyie mnaofanya hivi vitendo vichafu amueni kubadilika maana inawezekana.
Amini usiamini kama unafanya hivi vitendo lazima tu Mungu anakuadhibu lakini wewe hujui,unaweza kuwa tajiri una kila kitu lakini ukapewa ugonjwa utakaofanya hata usifurahie hizo mali zako.
Okay wazazi wenzangu najua labda sio wote mtakaonielewa hasa ktk kipengele cha ndugu lakini hata kama kuna mmoja atanielewa post hii itakuwa imefanikiwa.
Wimbo huu wazazi nasindikizia huu ujumbe wangu,ni wimbo mzuri sana,kama una watoto wanaosoma ni vizuri uwawekee wausikilize,una ujumbe ambao Tanzania inahitaji kwa sasa.
WITH LOVE ,CHEUSIE.
Nikiwa kama mzazi mtarajiwa,nimeona sio mbaya sisi wazazi tukikumbushana au kufunguana macho ktk mambo mbalimbali yatakayozidisha usalama wa watoto wetu.
Ni kawaida sana sisi watanzania kuishi na ndugu zetu wengi ktk nyumba zetu,utakuta mfano mtu una watoto wako lkn pia una ndugu zako na ndugu wa mkeo mnaishi nao pamoja kwa lengo la kuwasaidia ili siku moja nao wawe na maisha yao.Hii inasababisha watoto wetu wa kiume washee vyumba na ndugu zetu wa kiume yaani baba zao wadogo au wajomba zao na watoto wetu wa kike washee vyumba na mama zao wadogo/wakubwa au shangazi zao na housegirl.
Ni jambo zuri kuishi na ndugu zetu lakini naombeni mniamini kuwa sio vizuri watoto wetu walale na ndugu zetu watu wazima hasa wa kiume,nina uhakika na ninachokiongea,nina shuhuda nyingi juu ya watoto wengi wa kiume walivyokua sexualy abused na ndugu wa kiume wa wazazi wao wanaolala nao pamoja.Na inakuwa vigumu kwa mtoto kusema maana hawa molesters wanajua jinsi ya kumtisha mtoto ili asiseme.
Hata watoto wa kike ni vizuri waachwe walale wenyewe maana pia nimeshashuhudia watoto wadogo wa kike wakifanyishwa vitu vya ajabu na ndugu wa kike wa wazazi wao.Kuna mtoto mmoja hivi tunavyoongea anatibiwa fungus mdomoni sababu alikua "analambishwa chumvi" na mama yake mdogo kila siku usiku wakilala.
Najua labda mtaniona mwehu sababu tunawapenda ndugu zetu hivyo hatuwezi kamwe kudhania kuwa wanaweza kufanya hivi,lakini laiti ungeshuhudia niliyoshuhudia ungechukua tahadhari.Dunia imeharibika sana.wanadamu hatuna tena woga,sijasema muwafukuze ndugu zenu,ila ningeshauri hasa kwa watoto wa kiume kuliko wakalala na ndugu wakubwa wa kiume ni bora ndugu hao walale sebuleni kwenye magodoro.
Vile vile kina mama wenzangu naomba niwaonye,kama una tabia ya kuwaambia ndugu zako wa kiume wamsafishe mtoto akiwa amejisaidia uache sio vizuri.Hii tabia ya kumwambia mjomba au baba mdogo wa mtoto akusafishie mtoto ni ya hatari sababu,mwanao anaweza chomekwa vidole sehemu sehemu na wewe ukiona wala usishitukie.Na kama uncle anamfanyia mtoto mambo haya wakati anamsafisha basi akipata upenyo wkt mwingine pia atafanya.
Vile vile najua JF ni kama msafara wa mamba ambao ndani yako kuna mijusi na kenge,najua kabisa wengi wa JF memberz ni watu wazuri sana na wenye hekima lakini nataka niongee na wale wachache wetu wenye tabia za kifataki.Nyie ambao ni watu wazima lakini kutwa kurubuni watoto wadogo,definition ya fataki ni mtu mzima anayewarubuni kimapenzi watoto wadogo.
Nina amini mtu yeyote mwenye tabia za kifataki anaweza kujirekebisha,hivyo naombeni muache tabia za kutuharibia watoto/wadogo zetu.Kama wewe ni mbaba unayefanya hivi hebu jiulize je mtu mzima wa umri wako akikaharibu kale katoto kako unakokapenda utafurahi?Jibu ni hutafurahi,vile vile na wazazi wa hao watoto mnaowarubuni hawafurahi.
Na nyie wanaume mnaotongoza watoto wetu wa kiume nawaombeni hofu ya Mungu iwaingie muache maana siku za hivi karibuni hiki kimchezo kimepamba moto.
Pia kuna kina mama wanaharibu watoto,na maanisha kuna mafataki wa kike pia,wengi tu,kuna mama mmoja amesababisha mtoto wa mwenzake aache shule,huyu mama alikua anamfata mtoto shule ya boarding anakosoma anamtorosha wanakwenda kupanga hotel mwishowe mtoto akashindwa masomo na ameambukizwa ukimwi japo huyo mama anadai yeye mzima lkn muda si mrefu na yeye atachekiwa.
Pia kuna kina mama wasagaji wanaharibu watoto wa kike,labda hili ni geni kwetu lakini wapo na hivi vitendo vipo na shuhuda ninazo.Hivyo naomba mwaka huu ili Mungu awaondolee mikosi na mabalaa na aweze kuwapatia yale mnayohitaji hebu nyie mnaofanya hivi vitendo vichafu amueni kubadilika maana inawezekana.
Amini usiamini kama unafanya hivi vitendo lazima tu Mungu anakuadhibu lakini wewe hujui,unaweza kuwa tajiri una kila kitu lakini ukapewa ugonjwa utakaofanya hata usifurahie hizo mali zako.
Okay wazazi wenzangu najua labda sio wote mtakaonielewa hasa ktk kipengele cha ndugu lakini hata kama kuna mmoja atanielewa post hii itakuwa imefanikiwa.
Wimbo huu wazazi nasindikizia huu ujumbe wangu,ni wimbo mzuri sana,kama una watoto wanaosoma ni vizuri uwawekee wausikilize,una ujumbe ambao Tanzania inahitaji kwa sasa.
WITH LOVE ,CHEUSIE.
Last edited by a moderator: