Kabwela
Member
- Feb 11, 2008
- 76
- 5
Ndugu Watanzania nilimepata fursa ya kuwa maeneo ya visiwa vya Mafia. Kuna Ujio wa Mafia Dance Festival (http://www.mafiadancefestival.com) ambayo inategemea kufanyika kuanzia tarehe 1 mpaka 15 Agosti 2010 na tamasha hilo linategemewa kuwa na washiriki 3,500 kutoka nchi mbalimbali duniani. Kwa ukubwa na miundombinu ya Kisiwa cha Mafia hasa makao makuu ya wilaya hiyo (mji wa kilindoni kwa wanoufahamu) ni vigumu kuweza kubeba idadi hiyo ya watu (yawezekana wataleta disposable equipments).
Tatizo kubwa hasa la tamasha hilo ni tofauti na lile la Jahazi Zanzibar ni kuwa mara ya mwisho lilifanyika Spain 2006 na limekatailwa nchi nyingine duniani kwa kuwa linahusisha sana ucheza uchi, uvutaji mkubwa wa vilevi na madawa ya kulevya pamoja na ngono holela popote washiriki wanapokuwepo kutokana na vilevi na mila za washiriki hasa wa nchi za ulaya. wazee wa Visiwa hivyo wanalalamika sana na kulikataa hilo tamasha na wakiuuliza uongozi wa wilaya wanasema hajataarifiwa na yeyote kuhusoiana nalo ingawa kwenye tovuti ya wawandaaji wanaonesha kuwa wanaandaa kwa ushirikiano na halmashauri ya wilaya wakiwa na baraka za wizara ya Maliasili na Utalii.
Kutokana na mchanganyiko huu nimelazimika kuwaomba waTZ hasa wahusika watupe majibu kwani hili tamasha likifanyika litaharibu taswira ya utalii kwenye visiwa hivyo kwani mahoteli yote yaliyo eneo la uhifadhi (Marine Park) kwa pamoja wamekataa kukubali kuwapa nafasi za malazi washiriki wa tamasha hilo ingawa waandaaji hasa waliopo Afrika ya kusini kuwafuata na kuwabembeleza sana lakini ilishindikana kuwashawishi.
Watanzania ni kweli tunapenda uwekezaji na maendeleo na kutambulika maeneo yetu ya utalii lakini hili la kucheza uchi, kufanya ngono hadharani, kubwia na kuvuta madawa ya kulevya holela halitotusaidia sana zaidi ya kuharibu watoto wetu. Wazee wa mafia wanasema serikali inataka kuwaletea Tsunami kama ilivyotokea Asia kutokana na mambo yalivyokuwa yakifanyika ufukweni.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.
Tatizo kubwa hasa la tamasha hilo ni tofauti na lile la Jahazi Zanzibar ni kuwa mara ya mwisho lilifanyika Spain 2006 na limekatailwa nchi nyingine duniani kwa kuwa linahusisha sana ucheza uchi, uvutaji mkubwa wa vilevi na madawa ya kulevya pamoja na ngono holela popote washiriki wanapokuwepo kutokana na vilevi na mila za washiriki hasa wa nchi za ulaya. wazee wa Visiwa hivyo wanalalamika sana na kulikataa hilo tamasha na wakiuuliza uongozi wa wilaya wanasema hajataarifiwa na yeyote kuhusoiana nalo ingawa kwenye tovuti ya wawandaaji wanaonesha kuwa wanaandaa kwa ushirikiano na halmashauri ya wilaya wakiwa na baraka za wizara ya Maliasili na Utalii.
Kutokana na mchanganyiko huu nimelazimika kuwaomba waTZ hasa wahusika watupe majibu kwani hili tamasha likifanyika litaharibu taswira ya utalii kwenye visiwa hivyo kwani mahoteli yote yaliyo eneo la uhifadhi (Marine Park) kwa pamoja wamekataa kukubali kuwapa nafasi za malazi washiriki wa tamasha hilo ingawa waandaaji hasa waliopo Afrika ya kusini kuwafuata na kuwabembeleza sana lakini ilishindikana kuwashawishi.
Watanzania ni kweli tunapenda uwekezaji na maendeleo na kutambulika maeneo yetu ya utalii lakini hili la kucheza uchi, kufanya ngono hadharani, kubwia na kuvuta madawa ya kulevya holela halitotusaidia sana zaidi ya kuharibu watoto wetu. Wazee wa mafia wanasema serikali inataka kuwaletea Tsunami kama ilivyotokea Asia kutokana na mambo yalivyokuwa yakifanyika ufukweni.
Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.