Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,489
- 86,005
Salaam Alyeikum
Tunakaribia kuanza mwezi mtukufu, mwezi wa toba na kumrudia Muumba, nikiwa kama Ndugu na jamaa wa karibu wa ndugu zangu waislamu nawatakia maandalizi mema na saumu njema kwenu.
Ombi langu kwenu kama ni lazima kuvunja jungu tukavunje kwa namna dini inavyoelekeza na sio kwa namna ilivyozoeleweka miongon mwa wengi ila hatimae saumu (swaumu) zetu zenye maana mbele za Mungu isije ikawa tumeshinda njaa bure na kujitesa bure. Ni imani yangu kuwa tutatenda mema kwa kipindi hiki na hata baada ya hapo ili kufunga kwetu kuwe na Maana.
Pia kwa nafasi zenu/zetu ningeomba tuikemee ile mihadhara yenu/yetu yenye nia ya kuanzisha na kujenga chuki na dharau dhidi ya dini za wengine kwa madai ya mwezi mtukufu lakini pia ile kuamshana asubuhi asubuhi kwenda kuswali kuwe na namna ya staha tukikkumbuka pia kuwa wenzetu nao wana namna ya kuabudu, tusijipende wenyewe.
Mwisho, nawatakia kuvunja jungu kwema na maandalizi mema ya mwezi wa Ramadhani unaoanza hivi karibuni. Waslaam (mtoto wa Mama'Mkubwa)
Tunakaribia kuanza mwezi mtukufu, mwezi wa toba na kumrudia Muumba, nikiwa kama Ndugu na jamaa wa karibu wa ndugu zangu waislamu nawatakia maandalizi mema na saumu njema kwenu.
Ombi langu kwenu kama ni lazima kuvunja jungu tukavunje kwa namna dini inavyoelekeza na sio kwa namna ilivyozoeleweka miongon mwa wengi ila hatimae saumu (swaumu) zetu zenye maana mbele za Mungu isije ikawa tumeshinda njaa bure na kujitesa bure. Ni imani yangu kuwa tutatenda mema kwa kipindi hiki na hata baada ya hapo ili kufunga kwetu kuwe na Maana.
Pia kwa nafasi zenu/zetu ningeomba tuikemee ile mihadhara yenu/yetu yenye nia ya kuanzisha na kujenga chuki na dharau dhidi ya dini za wengine kwa madai ya mwezi mtukufu lakini pia ile kuamshana asubuhi asubuhi kwenda kuswali kuwe na namna ya staha tukikkumbuka pia kuwa wenzetu nao wana namna ya kuabudu, tusijipende wenyewe.
Mwisho, nawatakia kuvunja jungu kwema na maandalizi mema ya mwezi wa Ramadhani unaoanza hivi karibuni. Waslaam (mtoto wa Mama'Mkubwa)