Tutakapopata uelewa sahihi wa demokrasia na Market Economy

Habari Mkuu wangu Mkandara, ni kitambo sana kimepita!

Sijakuelewa kabisa kwenye uzi huu, kwanini unang'ata pande zote mbili? Mwanzoni kabisa umeonesha kuafikiana sana na alichodai mtoa mada, lakini papohapo unakuja kuafikiana tena na imani ya MgonjwaUkimwi ambayo imebezwa haswaa na mtoa mada, unasimama wapi? Maana hoja zao zipo mbalimbali kabisa, Africanism Vs Umagharibi. Unasimama wapi? Kumbuka kuwa kuna watu wengi nyuma yako, waoneshe pa kusimama usiwaache dailema!

Sisi sio vipofu wa utandawazi, bali hatupaswi kabisaaaa kuugeukia! USIMTUPE MBUZI MTONI KWA KUMUONA NG'OMBE AMEVUKA, UTAMUUA hata kama nae ana kwato!

Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani. Anaita sasa!
Mkuu wangu habari nzuri tu, mimi hupitia hapa kijiweni japo mara moja kwa wiki kuwasoma wanafalsafa kama nyie.

Labda nikufahamishe tu ya kwamba nimeyaunga mawazo yote mawili kwa sababu maalum ambazo zote zinafuata ukweli wa hali halisi iliyopo sasa hivi na pili hatuna haja ya kuendelea kuaminishwa hivo.

Niseme tu ya kwamba kizazi hiki ni VIPOFU kwa maana ya kwamba hawajui UKOLONI MAMBOLEO unafanya kazi vipi japo wanajua maana yake kwa elimu walofundishwa.

Pengine sii ajabu kabisa leo hii hakuna mtu anajua maana ya Ukoloni Mamboleo hivyo tunazidi kutopea ktk lindi la kutawaliwa kiuchumi pasipo kujua. Kuna kipande hiki kinachosema hivi:-

1. Neo Colonialism - Whereby multinational corporations continue to exploit the natural resources of the former colonies; that such economic control is inherently neo-colonial, and thus is akin to the imperial and hegemonic varieties of colonialism practiced by the empires of Great Britain, the United States, France, and other European countries...

Ningependa sana kumsikia Rais au mwanasiasa yeyote atakayeweza kusimama na kuzungumzia Neo - Colonialism, kisha tupime tulipo leo kama haitakuwa tumefanya kama walivyotaka wakoloni tufanye ama tume hivyo!..Nina hakika hadi napoandika hivi wakoloni tayari wameisha fika wanapotaka..

Labda kisome kipande hiki kidogo ambacho Kwame Nkurumah alikizungumzia kuhusu Ukoloni Mamboleo halafu nambie Je, hatufanyi watakavyo?.

Neo colonialism
1. Political control that can be exercised economically, linguistically, and culturally, whereby promotion of the culture of the neo-colonist country facilitates the cultural assimilation of the colonised people and thus opens the national economy to the multinational corporations of the neo-colonial country.
 
Mkandara

Asante Mkuu wangu! Nakupata haswaa hasa unaposema sisi ni mbumbumbu wa namna ya Ukoloni Mamboleo unavyofanya kazi, ni kweli katika hilo sisi ni vipofu japo tuna macho. Ukoloni Mamboleo nyenzo yake kuu ni Utandawazi, ambao kutumia neno upofu nao ni sahihi kabisa, lakini nahisi kama halibebi uzito unaohtajika! Ndio maana nimesema Hatupaswi kabisa kuugekia, ni MWIKO na HARAMU kuu kabisa!

Sasa Democratization ni sehemu ya Utandawazi, nao ndio Ukoloni Mamboleo! Mtoa mada ameshauri tupiganie kuuimarisha Demokrasia wakati tunajua ni nyenzo kuu na bora ya Ukoloni tajwa, MgonjwaUkimwi yeye anasema tutafute namna yetu ya kuendesha siasa zetu, wewe Mkuu Mkandara unasimama wapi? Ni kweli kilichosemwa ni kitu halisi, lakini, Je, tuipiganie Demokrasia na Market Economy tukijua wazi Ukoloni mamboleo umetega miba yake yenye sumu humo, au tupiganie kubuni namna ya mifumo yetu kulingana na Mazingira yetu na Nayakati zetu, yaani Mahususi kwetu!

Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani. Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Ha ha..sound km vile una suggest tuendelee kujifungua kwa wakunga kwa vile kuna watu wana iba dawa hospital....whatever you say mimi naongelea democracy na market economy hapa..ila kilichonivuta kuandika haya ni kwamba..watu hawaelewi haya..na hivyo hawajitumi kufanya yale yote yanayosaidi democrasy na market economy kutumika to the best.

Nicholas, napata wakati mgumu kujua unataka kusema nini in relation to my argument. I can't put your argument in one or two lines. I really cannot. As such it weighs me difficult to respond. My doubt is we are not on the same page regarding the form and functioning of market economy and liberal democracy.

I would suggest you solidify your understanding of the two before we proceed with the topic. Unlike siasa topics this topic requires a good grasp of Science particularly political economy and economics. Short of that we can simply go back to the usual stuff of chadema vs ccm; the stuff that require nothing but working keyboard and healthy typing hands.
 
Asante Mkuu wangu! Nakupata haswaa hasa unaposema sisi ni mbumbumbu wa namna ya Ukoloni Mamboleo unavyofanya kazi, ni kweli katika hilo sisi ni vipofu japo tuna macho. Ukoloni Mamboleo nyenzo yake kuu ni Utandawazi, ambao kutumia neno upofu nao ni sahihi kabisa, lakini nahisi kama halibebi uzito unaohtajika! Ndio maana nimesema Hatupaswi kabisa kuugekia, ni MWIKO na HARAMU kuu kabisa!

Sasa Democratization ni sehemu ya Utandawazi, nao ndio Ukoloni Mamboleo! Mtoa mada ameshauri tupiganie kuuimarisha Demokrasia wakati tunajua ni nyenzo kuu na bora ya Ukoloni tajwa, MgonjwaUkimwi yeye anasema tutafute namna yetu ya kuendesha siasa zetu, wewe Mkuu Mkandara unasimama wapi? Ni kweli kilichosemwa ni kitu halisi, lakini, Je, tuipiganie Demokrasia na Market Economy tukijua wazi Ukoloni mamboleo umetega miba yake yenye sumu humo, au tupiganie kubuni namna ya mifumo yetu kulingana na Mazingira yetu na Nayakati zetu, yaani Mahususi kwetu!

Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani. Anaita sasa!
Mkuu, kwanza nisaidie moja. Kila napoandika hapa JF button ya enter kutenganisha sentasi haikubali, hivyo kila nachoandika hakina paragraph kama ulivyoona hapo juu - Nifanyeje?...Ni JF tu inatokea..
 
Mkuu, kwanza nisaidie moja. Kila napoandika hapa JF button ya enter kutenganisha sentasi haikubali, hivyo kila nachoandika hakina paragraph kama ulivyoona hapo juu - Nifanyeje?...Ni JF tu inatokea..

Utaniwia radhi Mkuu wangu, sijajua hapo tatizo ni nini. Kwa sasa navmia simu ya kawaida, nashindwa kuona hata mpangilio wa aya, japo ninapotumia pc sijawahi pata tatizo kama hilo!
Labda ni tatizo la settings au badilisha kifaa kuhakiki zaidi! Pole sana!
 
Asante Mkuu wangu! Nakupata haswaa hasa unaposema sisi ni mbumbumbu wa namna ya Ukoloni Mamboleo unavyofanya kazi, ni kweli katika hilo sisi ni vipofu japo tuna macho. Ukoloni Mamboleo nyenzo yake kuu ni Utandawazi, ambao kutumia neno upofu nao ni sahihi kabisa, lakini nahisi kama halibebi uzito unaohtajika! Ndio maana nimesema Hatupaswi kabisa kuugekia, ni MWIKO na HARAMU kuu kabisa!

Sasa Democratization ni sehemu ya Utandawazi, nao ndio Ukoloni Mamboleo! Mtoa mada ameshauri tupiganie kuuimarisha Demokrasia wakati tunajua ni nyenzo kuu na bora ya Ukoloni tajwa, MgonjwaUkimwi yeye anasema tutafute namna yetu ya kuendesha siasa zetu, wewe Mkuu Mkandara unasimama wapi? Ni kweli kilichosemwa ni kitu halisi, lakini, Je, tuipiganie Demokrasia na Market Economy tukijua wazi Ukoloni mamboleo umetega miba yake yenye sumu humo, au tupiganie kubuni namna ya mifumo yetu kulingana na Mazingira yetu na Nayakati zetu, yaani Mahususi kwetu!

Mungu wetu yu tayari kutupigania vitani. Anaita sasa!
Nimeweza badilisha kule kwenye setting kwa hiyo mambo mswano.

Turudi kwenye mada, umeniuliza mimi nimesimama wapi ktk mjadala huu wenye kutokubaliana baina ya Nicolas na MgonjwaUkimwi..
Nadhani hoja kubwa zaidi ni hili neon Demokrasia na matumizi yake. Bila shaka kila mmoja wao ana tafsiri yake ktk hili na nadharia kubwa nayosimamia miye ni ile ya Upofu ambapo vipofu unawapa neno kama tembo halafu unawauliza ukubwa wake au hata maumbile yake na ndio maana umenikuta nakubaliana na wote wakati huo huo napingana nao ki-aina kwa sababu binafsi yangu naaminiDemokrasiaau market economy vinaweza kuwa na mazuri au madhara ikiwa tu utazingatia kwanza tunamzungumzia nani azitumie..na kulingana na mada hii jibu ni MTANZANIA.. je huyu Mtanzania ni mtu wa aina gani? ana uwezo gani, ana mapungufu gani, yupo ktk mazingira gani? kasha ndio hapo unaweza kuvipenyeza hizi nyenzo za kukuza uchumi kulingana na watu wenyewe..

Tatizo sio demokrasia au market economy, isipokuwa SISI Watanzania ndio kikwazo cha yote sasa iwe imetokana na kukoloniwa, Ujamaa au Ujinga lakini tuna kilema na kwa bahati mbaya tunasahau ulemavu huu hivyo badala ya kwanza kujitibu na Ulemavu tunajaribu sana kutumia nyenzo ambazo mlemavu hawezi kuzitumia japo nyenzo hizo hizo zimewafaidisha wengine walokuwa wazima pasi ulemavu.

Kuna msemo usemao ya kwamba 'Ukitafuta kweli, usitazame nje ya nafsi yako" wadhungu wanasema - When searching for truth look no further than Yourself! haya ni maneno mazito sana kwetu na ndipo tunapotakiwa kuanzia kabla kabisa ya kubishana juu ya Demokrasia au Market Economy maana hizi ni nyenzo tu kama vile wasemavyio waswahili -mkulima mpe jembe akalime lkn ukweli bado unabakia ktk hali, imani na uwezo wa huyo unayemwita mkulima. Jembe halilimi, mkulima ndiye hulima!

Kwa hiyo tujitazame kwanza sisi, na nimesema sisi VIPOFU kwa maana ya kwamba sisi ni WAJINGA ktk dunia hii ya Utandawazi.. hakuna tunaloliona, kusikia kihisia zaidi ya Ulemavu wetu na ndio maana tunaanza na sisi kuwa Taifa la OMBA OMBA...Toka uongozi wa familia zetu hadi uongozi wa nchi tumejijengea utamaduni wa kuamini ulemavu hivyo tunastahili kusaidiwa ama kusaidiana. na nitakupa mifano ya hali halisi hapa chini:-

1.Marais wetu wanapokwenda nchi za nje, huenda huomba MISAADA... kwa nini? kwa nini isiwe wanaenda kuweka makubaliano ya kiuchumi (Kuandika makubaliano ya kibiashara - Trade agreements)badala yake tumekuwa omba omba tena hujisifia kwa misaada tuloahidiwa iwe Millenium goal ama ujinga mwingine wowote unaozidisha kutulemaza kifikra kwa kuamini kwamba sisi ni maskini tunaohitaji kusaidiwa! Tena kwa ubaya zaidi sisi ndio wenye dhahabu, Almasi, gasi, na vitu vingine wanavyovihitaji wao kwa matumizi yao ya kila siku. Iweje sisi tuwe waombaji kwao ilihali sisi sote tunahitajiana?..

2. Tazama Familia zetu, ukifanikiwa kimaisha waswahili wanasema UKITOKA!, basi kila ndugu, rafiki na majirani zako watakutegemea wewe pia uwatoe wao. Na ajabu ni kwamba wewe mwenyewe hukutolewa na mtu yeyote kati ya ndugu, marafiki au majirani isipokuwa jitihada zako nje ya ulingo wa familia na displine ya fedha. Hivyo tumejilemaza ktk lindi la Umaskini kwa kutegemea kuaidiwa japo tumezungukwa na utajiri mkubwa..

Kwa hiyo, huu ulemavu iwe umetokana na Kukoloniwa,Utumwa au Ujamaa na Kujitegemea maana wapo watu wanaodai hivyo basi tujiepushe na utamaduni huu wa kuwa TEGEMEZI au OMBAOMBA. Ndio maana nikasema kipofu kumpa fimbo hujamsaidia bado isipokuwa ni kumlemaza zaidi ikiwa hukutafuta mbinu ama dawa ya kuondoa upofu wake. Kwa kukubali hii misaada wakati sisi wenyewe ndio matajiri wenye malighafi na sio hizo karatasi zinazotengenezwa viwandani na kuitwa Dollar vikapewa thamani kubwa kuliko dhahabu, ama korosho yetu.

Iweje leo hii sisi tunajua waz kabisa kwamba soko la dhahabu na vito liko Asia (ndia na China) lakini tutawapa wawekezaji wa Ulaya waje wachimbe malighafi bure ila kwa misaada na ruzuku wakati tukijua wao huvisafisha na kuviuza Asia?. Kwa nini sisi mazao yetu kama Korosho tunayauza India wakati tunajua fika kwamba soko la Korosho liko Ulaya na Marekani badala yake India leo ndio exporter wakubwa duniani wa Korosho?..Haya ni maswali ya kujiuliza sisi wenyewe kwanza badala ya kutazama nje kutafuta wachawi.

Watanzania pia tuna tatizo kubwa la kutokuwa na Malengo, Kutoaminiana na Unafiki. Na kusema kweli hulka hii ndio iloniondoa miye ktk ukumbi wa siasa na siasa za Tanzania. Demokrasia inaweza kuwa nzuri ikiwa sisi tutaitazama kwa manufaa yetu maana lengo kubwa la Demokrasia sio kugawa watu ktk imani za kitikadi bali matumizi ya itikadi ktk ujenzi wa Jumuiya hiyo hiyo. Kwetu sisi, Ukisema wewe CCM au Chadema basi tayari unawekwa ktk kundi la watu Fulani tofauti wakati huko Ulaya na Marekani hakuna kundi la watu wanaoitwa Wajamaa wala Wahafidhina na wakaishi maisha yao Kijamaa au Kihafidhina bali huzitumia tu siasa hizi kufikia malengo yao ya kiuchumi na Kijamii.. Sisi Demokrasia imekuja kutugawa ili tutawaliwe. Na tunatawaliwa sasa sielewi kama chimbuko lake ni Ukoloni, Ujinga ama basi tu Ulimbukeni wetu. Kwa hiyo mkuu wangu nadhani nimegusia sehemu zote muhimu na hoja yangu kubwa haipo HAIKUTANGULIWA na Demokrasia wala Market economic isipokuwa sisi wenyewe na tukiweza kutatua na kujitambua sisi kwanza hayo yote maswala ya Demokrasia na Market Economy yatajijaza kwa nafasi zake..

- Once we balance ourselves, only then can we balance the world around us.
- Only when we require no approval from outside ourselves,can we own ourselves.

SAY NO TO AID
 
Last edited by a moderator:
Duh! Mkuu wangu Mkandara, naona una hasira za kutosha juu ya kinachoendelea. Nimekupata vyema kabisa, ni kweli kabisa kwamba, regardless of chanzo, sisi ni mbumbumbu wa dunia ya leo!

Binafsi ninapoitafakari Demokrasia na yake Free Economy, ninaona UA zuuuurii sana, lakini ndiniye limebeba nyuki wakali sana, na hao nyuki ni sehemu ya hilo UA.

Ninapozitafakari nchi ambazo zimefanikiwa kupitia Demokrasia na Soko Huria, sioni namna yoyote ya kuweza kwao kufanikiwa kama Ujinga wetu usingekuwepo! Gharama za kuisimamisha Demokrasia na Uchumi Huria, ni kwa wazi kabisa zinabebwa na Ujinga wetu.

Kwa sababu ya hilo, nasi kama tunataka kuisimamisha Demokrasia na Uchumi Huria, vituongoze kufikia mafanikio, ni lazima tumtafute Mjinga wa kubeba gharama zake. Awe wa kumtengeneza ama laa, ni lazima awepo kwanza! Nikizungumza kama Mtanzania, basi nimfanye mwana-Malawi ama Kenya, ama Burundi, Kongo, Angola, n.k kuwa mjinga abebe gharama za Demokrasia.

Ninapozungumza kama mwana-Afrika, hapa ni lazima nimtafute Mmarekani, European, Asian n.k nimfanye mjinga, na ujinga wake ubebe gharama za Demokrasia yetu Afrika.

Katika hilo sioni namna ya kukwepa dunia yenye HILA na VISASI. Unyonge wetu hautaisha milele.

Ni lazima tutafute njia yetu tofauti. Tukae chini tumize vichwa, tutafakari na kubuni namna bora na sahihi ya kuendesha Uchumi wetu, Siasa na Tamaduni zetu, kulingana na Mazingira na Nyakati(FIKRA) zetu mahususi! Hiyo ndio namna pekee ya kusema sisi si wajinga tena! Kila la heri Mkuu.

Anaita sasa!
 
Last edited by a moderator:
Duh! Mkuu wangu Mkandara, naona una hasira za kutosha juu ya kinachoendelea. Nimekupata vyema kabisa, ni kweli kabisa kwamba, regardless of chanzo, sisi ni mbumbumbu wa dunia ya leo!

Binafsi ninapoitafakari Demokrasia na yake Free Economy, ninaona UA zuuuurii sana, lakini ndiniye limebeba nyuki wakali sana, na hao nyuki ni sehemu ya hilo UA.

Ninapozitafakari nchi ambazo zimefanikiwa kupitia Demokrasia na Soko Huria, sioni namna yoyote ya kuweza kwao kufanikiwa kama Ujinga wetu usingekuwepo! Gharama za kuisimamisha Demokrasia na Uchumi Huria, ni kwa wazi kabisa zinabebwa na Ujinga wetu.

Kwa sababu ya hilo, nasi kama tunataka kuisimamisha Demokrasia na Uchumi Huria, vituongoze kufikia mafanikio, ni lazima tumtafute Mjinga wa kubeba gharama zake. Awe wa kumtengeneza ama laa, ni lazima awepo kwanza! Nikizungumza kama Mtanzania, basi nimfanye mwana-Malawi ama Kenya, ama Burundi, Kongo, Angola, n.k kuwa mjinga abebe gharama za Demokrasia.

Ninapozungumza kama mwana-Afrika, hapa ni lazima nimtafute Mmarekani, European, Asian n.k nimfanye mjinga, na ujinga wake ubebe gharama za Demokrasia yetu Afrika.

Katika hilo sioni namna ya kukwepa dunia yenye HILA na VISASI. Unyonge wetu hautaisha milele.

Ni lazima tutafute njia yetu tofauti. Tukae chini tumize vichwa, tutafakari na kubuni namna bora na sahihi ya kuendesha Uchumi wetu, Siasa na Tamaduni zetu, kulingana na Mazingira na Nyakati(FIKRA) zetu mahususi! Hiyo ndio namna pekee ya kusema sisi si wajinga tena! Kila la heri Mkuu.

Anaita sasa!
Nakusikia sana mkuu, na sii kwamba njia hazipo - Njia ZIPO!
Na sii kweli lazima kumtafuta MJINGA mwingine maana fomula inayotakiwa ni kuwepo mjinga na mwerevu. Huyo huyo mwerevu tunamhitaji kutokana na tofauti ya mazingira yetu kwani hayafanani. Waswahili wanasema penye miti hakuna wajenzi ndilo balaa linalotukuta sisi, hivyo wao kuja kata miti wakajenga kwao haina maana sisi hatuwezi kujenga hadi tutafute wajinga wengine tukakate miti yao. Miti tunayo kinachioytakiwa ni sisi kuwa wajenzi na ndio ELIMU tunayotakiwa kuitafuta. Hatuna haja wala sababu ya kuiga mila na desturi za watu wa Ulaya wasiokuwa na miti ya ujenzi ili tufanikiwe. Tujifunze kukataa methali hiyo ili nasi tuwe wajenzi..

kwa bahati kubwa sana leo ni siku ya kumkumbuka Mwl.Nyerere, baba wa Taifa, kiongozi ambaye kwa hakika alitufuta tongotongo mapema sana lakini kwa ujinga na uvivu wetu sisi tukarudi usingizini. Na alisema nini basi kuhusu Demokrasia?. ni wazi ya kwamba Demokrasia yetu sii lazima iwe ya vyama bali tutachagua viongozi wetu kutokana na vision zao, uwezo wao kwa maana ya kwamba demokrasia ni pale wengi wanapomchagua kiongozi wampendaye na sii lazima iwe vyama wavipendavho.

Binafsi yangu naamini kabisa ya kwamba demokrasia haina muundo mmoja utokanao na mazingira ya Ulaya, Amerika ama Asia bali demokrasia huundwa kutokana na muundo wa JUMUIYA ya watu na UHURU wao wa kuchagua, hakuna Uhuru wa bara mbili unaofanana wala hakuna Jamii ya watu zinazofanana kimila na kitamaduni. Hakuan kitu kibaya sana kama kuiga dawa ya kitu pasipo kutanguliwa na sababu ya maradhi. Nikiwa na maana ya kwamba huwezi kuitafuta demokrasia ikiwa hapakuwepo na tatizo la uongozi ama Kiutawala. Hivyo basi ukitazama kwa makini matokeo ya hii demokrasia tuloiga kutoka Ulaya imetugawa badala ya kutuunganisha.

Wakati wa Mwl.Nyerere tulikuwa na Ukabila, tukaufuta, Udini tukaufuta, kwa kila tatizo letu tulilitafutia njia yetu ambayo sii Ulaya wala Asia waliifuata ama kulazimishwa waifuate. Na hakika tulijiona sisi ni Watanzania, wamoja na sii kwamba tulipigania UHURU wa Bendera ili watu wasitawaliwe na mkoloni bali nia hasa ilikuwa UHURU wetu KIUCHUMI na kuunda jamii moja ya Mwafrika. Hatuutaka UHURU wetu kwa fikra za mtu mweusi ndiye anayefaa kukaa IKULU bali tulipigania UHURU kwa sababu mali yetu ilikuwa ikichukuliwa nje kukuza chumi za nchi za magharibi ilihali maendeleo tulopewa sisi yalikuwa ktk kurahisisha uzalishaji,uvunaji na usafiri wa mali zetu kwa faida ya wakoloni. Ndio maana baada ya kupandisha bendera zetu za Uhuru tulijikuta tumeachiwa nyenzo zao iwe mashamba, reli, bandari, shirika la ndege, na viwanda ambavyo vyote vilimikiwa na wao na kwa mahitaji yao wenyewe huko Ulaya, Hapakuwwa na benki kuu, bond wala mfuko wa hifadhi. Hakuna kitu hata kimoja kilichotengenezwa na mkoloni kwa mahitaji ya mwafrika zaidi ya kutuweka hai na wenye afya na nguvu ya kuzalisha ili kukidhi mahitaji yao.

Maajabu ya Mussa leo hi tumerudi kule kule ktk kuwamilikisha wageni (wakoloni) mali zetu kwa mahitaji yao na kuupoteza Uhuru wetu wa kiuchumi kwa kupewa ruzuku na ahadi za misaada ya pump za maji,vyandarua na kadhalika halafu kwa madaha kabisa tunadai kuwa nchi yetu iko HURU? huo Uhuru wanaozungumzia ni wa bendera ama wa Kiuchumi?. Je, hawa watawala wetu wamesahau haswa nia na malengo ya baba na mababu zetu kuutafuta Uhuru wa kiuchumi ikiwa leo tunarudi kuwamilikisha kile tulokipigania? Au fikra zao zinawaambia uhuru tuliopigania na kutotawaliwa na wazungu au waarabu maana dunia ya kesho tutakuwa na wazungu na waarabu wazawa -born and raise kwa karne zaidi ya tano.

Hivyo basi ktk swala la Demokrasia, tujiulize tumejifunza nini?. Je, kweli demokrasia ya vyama inawezekana kwa watu maskini, wajinga na wehitaji ama inawezekana tu kwa Taifa linaloendeleza Ubeberu na ukoloni mamboleo. Haiwezekani Mbwa mwitu akaiga maisha ya Mbwako au Jibwa kwa sababu tu wana asili moja, na itakuwa ujinga mkubwa mtu kufikiria waweza kumfuga mbwa mwitu ktk mazingira ya mbwa ama kinyume na akafanikisha kumgeuza mbwa hiuyo kuwa mwingineyo. Tukumbuke tu ya kwamba hawa wazungu walifikiria hii nadharia ya Demokrasia kutokana na kwamba wao tawala zao walitanguliwa na vita baina ya watawala wao kutawala eneo moja pasi ridhaa ya wananchi.

Wakagawanyika within, na mwenye nguvu ndiye alotawala japo wamoja wakati sisi Tawala zetu zilikuwa za kurithiana kimakabila na kuheshimu mipaka yetu toka enzi. Hakuna Mtawala wala Chief hata mmoja alotaka kuitawala Tanganyika nzima,ama kutawala nje ya kabila lake isipokuwa walipigana vita ktk kulinda rasilimali na maliasili zao ktk mipaka ya makabila..Na zilikuwepo sababu za kijamii ktk vita baina ya makabila yetu hakuna historia ya nguvu mbili kupigana vita kutawala kabila moja.

Kwa hiyo demokrasia ya wenzetu ilikuja kuondoa vita ya kugombania kuwa mtawala kwa maana ya kwamba mwenye nguvu ndiye atakaye kaa IKULU. Baada ya Uhuru wa Bendera wakachagua Demokrasia ili kuwapa wananchi uwezo wa kumchagua kiongozi wao badala ya vita vilivyokuwa vikiwaangamiza watoto, wale na wananchi kwa Ujumla. Sisi Waafrika hatukupitia huko na ndio maana demokrasia hii imekuwa sii Muarobaini bali imetugawa ktk makundi na kuzua chuki ambayo haikutakiwa kuwepo. Dawa siku zote kwa maradhi yake huwezi kunywa Panadol wakati tatizo lako ni ujauzito.

Free economy pia ina matatizo yake na Mwl. Nyerere alilizungumzia vizuri sana lakini bahati mbaya Ukoloni Mamboleo umeshinda fikra zile kama vile ushetani anavyoweza kuturubuni tukaenda kunywa pombe Bar lakini tukakosa ada ya shule kwa motto. Tunaweka nguvu kubwa ktk harusi na mazishi ya mtu alokwisha kufa lakini sii ktk kumwezesha ndugu au rafiki kulima shamba lake la mahindi ama kumpeleka mwanae akasome. Ndio tukasema Penye miti hakuna wajenzi! lakini bado hatujajifunza kutokana na UJINGA wa mtu mweusi.

Ni maajabu makubwa sisi wenye dhahabu na madini yote ambayo hao wazungu wanayahitaji leo tumekuwa ombaomba wa misaada yao. Na hatujiulizi hata kidogo imekuwaje nchi kama Marekani matajiri wao ndio wana madeni ya nchi kama China, India na Asia kwa matrillioni ya dollar kutokana na matumizi ya hii Free economy? Marekani ndiye amekuwa Teja mkubwa wa mali za Asia wala sii kwa sababu ya cheap labor ati wao Marekani wamefungua viwanda vyao Asia bali ukweli ni kwamba mali zinazotoka Asia ni bei rahisi kwao na zimewalenga walalahoi wengi (asilimia 90)ya wananchi wa nchi hizo tajiri. Hivyo pamoja na kwamba nchi tajiri zimeendelea bado wamehakikisha asilimia 90 ya maskini wao inaweza kumudu maisha kwa kununua mahitaji yao kwa bei nafuu wakifanya kazi kuzalisha mali kwa tekonologia ya juu itakayo uzwa tena nchi za Asia na Afrika kwa faida kubwa. Katika mzunguko huu sisi Waafrika tunabakia mateja kwa sababu urithi wetu tumeisha uuza kwa wageni na hivyo kupoteza Uhuru wa kiuchumi. Sisi ndio mateja hatuidai Marekani, Ulaya wala Asia bali tunadaiwa na madeni hayo kamwe hatutaweza kuyalipa maana tumeisha uza uhuru wetu wa kiuchumi.

Nitaachia hapo kwa leo...
 
Last edited by a moderator:
Nakusikia sana mkuu, na sii kwamba njia hazipo - Njia ZIPO!
Na sii kweli lazima kumtafuta MJINGA mwingine maana fomula inayotakiwa ni kuwepo mjinga na mwerevu. Huyo huyo mwerevu tunamhitaji kutokana na tofauti ya mazingira yetu kwani hayafanani. Waswahili wanasema penye miti hakuna wajenzi ndilo balaa linalotukuta sisi, hivyo wao kuja kata miti wakajenga kwao haina maana sisi hatuwezi kujenga hadi tutafute wajinga wengine tukakate miti yao. Miti tunayo kinachioytakiwa ni sisi kuwa wajenzi na ndio ELIMU tunayotakiwa kuitafuta. Hatuna haja wala sababu ya kuiga mila na desturi za watu wa Ulaya wasiokuwa na miti ya ujenzi ili tufanikiwe. Tujifunze kukataa methali hiyo ili nasi tuwe wajenzi..

kwa bahati kubwa sana leo ni siku ya kumkumbuka Mwl.Nyerere, baba wa Taifa, kiongozi ambaye kwa hakika alitufuta tongotongo mapema sana lakini kwa ujinga na uvivu wetu sisi tukarudi usingizini. Na alisema nini basi kuhusu Demokrasia?. ni wazi ya kwamba Demokrasia yetu sii lazima iwe ya vyama bali tutachagua viongozi wetu kutokana na vision zao, uwezo wao kwa maana ya kwamba demokrasia ni pale wengi wanapomchagua kiongozi wampendaye na sii lazima iwe vyama wavipendavho.

Binafsi yangu naamini kabisa ya kwamba demokrasia haina muundo mmoja utokanao na mazingira ya Ulaya, Amerika ama Asia bali demokrasia huundwa kutokana na muundo wa JUMUIYA ya watu na UHURU wao wa kuchagua, hakuna Uhuru wa bara mbili unaofanana wala hakuna Jamii ya watu zinazofanana kimila na kitamaduni. Hakuan kitu kibaya sana kama kuiga dawa ya kitu pasipo kutanguliwa na sababu ya maradhi. Nikiwa na maana ya kwamba huwezi kuitafuta demokrasia ikiwa hapakuwepo na tatizo la uongozi ama Kiutawala. Hivyo basi ukitazama kwa makini matokeo ya hii demokrasia tuloiga kutoka Ulaya imetugawa badala ya kutuunganisha.

Wakati wa Mwl.Nyerere tulikuwa na Ukabila, tukaufuta, Udini tukaufuta, kwa kila tatizo letu tulilitafutia njia yetu ambayo sii Ulaya wala Asia waliifuata ama kulazimishwa waifuate. Na hakika tulijiona sisi ni Watanzania, wamoja na sii kwamba tulipigania UHURU wa Bendera ili watu wasitawaliwe na mkoloni bali nia hasa ilikuwa UHURU wetu KIUCHUMI na kuunda jamii moja ya Mwafrika. Hatuutaka UHURU wetu kwa fikra za mtu mweusi ndiye anayefaa kukaa IKULU bali tulipigania UHURU kwa sababu mali yetu ilikuwa ikichukuliwa nje kukuza chumi za nchi za magharibi ilihali maendeleo tulopewa sisi yalikuwa ktk kurahisisha uzalishaji,uvunaji na usafiri wa mali zetu kwa faida ya wakoloni. Ndio maana baada ya kupandisha bendera zetu za Uhuru tulijikuta tumeachiwa nyenzo zao iwe mashamba, reli, bandari, shirika la ndege, na viwanda ambavyo vyote vilimikiwa na wao na kwa mahitaji yao wenyewe huko Ulaya, Hapakuwwa na benki kuu, bond wala mfuko wa hifadhi. Hakuna kitu hata kimoja kilichotengenezwa na mkoloni kwa mahitaji ya mwafrika zaidi ya kutuweka hai na wenye afya na nguvu ya kuzalisha ili kukidhi mahitaji yao.

Maajabu ya Mussa leo hi tumerudi kule kule ktk kuwamilikisha wageni (wakoloni) mali zetu kwa mahitaji yao na kuupoteza Uhuru wetu wa kiuchumi kwa kupewa ruzuku na ahadi za misaada ya pump za maji,vyandarua na kadhalika halafu kwa madaha kabisa tunadai kuwa nchi yetu iko HURU? huo Uhuru wanaozungumzia ni wa bendera ama wa Kiuchumi?. Je, hawa watawala wetu wamesahau haswa nia na malengo ya baba na mababu zetu kuutafuta Uhuru wa kiuchumi ikiwa leo tunarudi kuwamilikisha kile tulokipigania? Au fikra zao zinawaambia uhuru tuliopigania na kutotawaliwa na wazungu au waarabu maana dunia ya kesho tutakuwa na wazungu na waarabu wazawa -born and raise kwa karne zaidi ya tano.

Hivyo basi ktk swala la Demokrasia, tujiulize tumejifunza nini?. Je, kweli demokrasia ya vyama inawezekana kwa watu maskini, wajinga na wehitaji ama inawezekana tu kwa Taifa linaloendeleza Ubeberu na ukoloni mamboleo. Haiwezekani Mbwa mwitu akaiga maisha ya Mbwako au Jibwa kwa sababu tu wana asili moja, na itakuwa ujinga mkubwa mtu kufikiria waweza kumfuga mbwa mwitu ktk mazingira ya mbwa ama kinyume na akafanikisha kumgeuza mbwa hiuyo kuwa mwingineyo. Tukumbuke tu ya kwamba hawa wazungu walifikiria hii nadharia ya Demokrasia kutokana na kwamba wao tawala zao walitanguliwa na vita baina ya watawala wao kutawala eneo moja pasi ridhaa ya wananchi.

Wakagawanyika within, na mwenye nguvu ndiye alotawala japo wamoja wakati sisi Tawala zetu zilikuwa za kurithiana kimakabila na kuheshimu mipaka yetu toka enzi. Hakuna Mtawala wala Chief hata mmoja alotaka kuitawala Tanganyika nzima,ama kutawala nje ya kabila lake isipokuwa walipigana vita ktk kulinda rasilimali na maliasili zao ktk mipaka ya makabila..Na zilikuwepo sababu za kijamii ktk vita baina ya makabila yetu hakuna historia ya nguvu mbili kupigana vita kutawala kabila moja.

Kwa hiyo demokrasia ya wenzetu ilikuja kuondoa vita ya kugombania kuwa mtawala kwa maana ya kwamba mwenye nguvu ndiye atakaye kaa IKULU. Baada ya Uhuru wa Bendera wakachagua Demokrasia ili kuwapa wananchi uwezo wa kumchagua kiongozi wao badala ya vita vilivyokuwa vikiwaangamiza watoto, wale na wananchi kwa Ujumla. Sisi Waafrika hatukupitia huko na ndio maana demokrasia hii imekuwa sii Muarobaini bali imetugawa ktk makundi na kuzua chuki ambayo haikutakiwa kuwepo. Dawa siku zote kwa maradhi yake huwezi kunywa Panadol wakati tatizo lako ni ujauzito.

Free economy pia ina matatizo yake na Mwl. Nyerere alilizungumzia vizuri sana lakini bahati mbaya Ukoloni Mamboleo umeshinda fikra zile kama vile ushetani anavyoweza kuturubuni tukaenda kunywa pombe Bar lakini tukakosa ada ya shule kwa motto. Tunaweka nguvu kubwa ktk harusi na mazishi ya mtu alokwisha kufa lakini sii ktk kumwezesha ndugu au rafiki kulima shamba lake la mahindi ama kumpeleka mwanae akasome. Ndio tukasema Penye miti hakuna wajenzi! lakini bado hatujajifunza kutokana na UJINGA wa mtu mweusi.

Ni maajabu makubwa sisi wenye dhahabu na madini yote ambayo hao wazungu wanayahitaji leo tumekuwa ombaomba wa misaada yao. Na hatujiulizi hata kidogo imekuwaje nchi kama Marekani matajiri wao ndio wana madeni ya nchi kama China, India na Asia kwa matrillioni ya dollar kutokana na matumizi ya hii Free economy? Marekani ndiye amekuwa Teja mkubwa wa mali za Asia wala sii kwa sababu ya cheap labor ati wao Marekani wamefungua viwanda vyao Asia bali ukweli ni kwamba mali zinazotoka Asia ni bei rahisi kwao na zimewalenga walalahoi wengi (asilimia 90)ya wananchi wa nchi hizo tajiri. Hivyo pamoja na kwamba nchi tajiri zimeendelea bado wamehakikisha asilimia 90 ya maskini wao inaweza kumudu maisha kwa kununua mahitaji yao kwa bei nafuu wakifanya kazi kuzalisha mali kwa tekonologia ya juu itakayo uzwa tena nchi za Asia na Afrika kwa faida kubwa. Katika mzunguko huu sisi Waafrika tunabakia mateja kwa sababu urithi wetu tumeisha uuza kwa wageni na hivyo kupoteza Uhuru wa kiuchumi. Sisi ndio mateja hatuidai Marekani, Ulaya wala Asia bali tunadaiwa na madeni hayo kamwe hatutaweza kuyalipa maana tumeisha uza uhuru wetu wa kiuchumi.

Nitaachia hapo kwa leo...

Kama kawaida yetu JF tumeibaka mada hii na kupoteza kile kilichokusudiwa. Mada inataka tuwe na uelewa sahihi wa demokrasia na uchumi wa soko huria. Ajabu wachangiaji wengi wanakwepa kutupa uelewa wao wa haya mambo mawili na applicability yake Tz na badala yake wanaongea matatizo ya Tz. Hii topic kwangu naona imepoteza mwelekeo na malengo ya mwanzilishi. Tuambieni kwanza demokrasia na free market ni vitu gani katika form na substance ili tuupate huo uelewa sahihi anaotaka mwanzilishi wa mada hii tuufahamu. Tuko nje ya mstari kwa kila namna.
 
Kama kawaida yetu JF tumeibaka mada hii na kupoteza kile kilichokusudiwa. Mada inataka tuwe na uelewa sahihi wa demokrasia na uchumi wa soko huria. Ajabu wachangiaji wengi wanakwepa kutupa uelewa wao wa haya mambo mawili na applicability yake Tz na badala yake wanaongea matatizo ya Tz. Hii topic kwangu naona imepoteza mwelekeo na malengo ya mwanzilishi. Tuambieni kwanza demokrasia na free market ni vitu gani katika form na substance ili tuupate huo uelewa sahihi anaotaka mwanzilishi wa mada hii tuufahamu. Tuko nje ya mstari kwa kila namna.
Mkuu maana ipo pale pale labda wewe ndio hujatusoma vizuri...

Labda nigusie tu ya kwamba Demokrasia sii yetu sisi, chimbuko lake limetokana na kuwepo watu waheshimiwa (The Elite)wenye nguvu ya kiuchumi (matajiri) wakichagua viongozi kutawala raia wengi walokuwa maskini. Historia inajieleza wazi iwe Ugiriki ama Uingereza kote Demokrasia ilianza na kundi la watu fulani wenye uwezo waloshikilia njia kuu za uchumi kupewa mamlaka kutumia influuence yao kifedha (Lobbying) kuchagua viongozi ambao watalinda sii tu mipaka ya nchi zao bali pia na muhimu zaidi MALI ZAO - UTAJIRI wao. Utajiri kwao ni wa watu sii wa nchi. Unaweza kata ama kupingana name lkn huu ndio ukweli wa kihistoria.

Sasa Sisi tuloingia Demokrasia wakati kundi lote la wananchi ni maskini ilihali nchi ndio tajiri ktk mfumo huu wa uchumi wa soko huria, unajiuliza Je, lengo letu haswa ni lipi?. Hawa lobbiest kwetu ni kina nani na watakuwa na nafasi gani kisiasa na kiuchumi?.. Hivi kweli inawezekana kuwepo demokrasia ya kweli kwa watu maskini kuchagua viongozi pasipo kuzingatia kwanza nafasi za wananchi wake? Je,inawezekana kweli maskini kumchagua maskini mwenzake kulinda Uhuru na zaidi ya yote UTAJIRI wao wa kuiga mfumo wa Demokrasia ya Ulaya?..

Labda wewe nambie maana nijuavyo miye hii demokrasia na Uchumi wa soko Huria vinaenda sambamba kwa lengo kuu la Kulinda UCHUMI na Uhuru wa WATU wake. Hivyo, ni muhimu kuijenga demokrasia itakayo walinda WATU na MALI ZAO. Maadam sisi hatuna Matajiri, hao waheshimiwa kiasili tulitakiwa kuchagua viongozi watakao linda Uhuru, maliasili na rasilimali zetu badala yake tunakazana kuunda kundi la waheshimiwa - The elite ili kuwatajirisha na kuwalinda hadi tuwe kama nchi za Ulaya.
 
Demokrasia na uchumi wa soko huria vilikuwapo kabla ya wakoloni. But I think that is a topic of its own.

I will reiterate what I said previous in an attempt to strengthen my point. Demecracy existed before colonialism in Africa. It was nonpartisan direct democracy. In this a person could belong to a multiple interest and political groups. In it people where equal by default and voting was employed to reach a decission. Like in the modern democracy, votes carried equal weight across voters. Like in modern representative democracy, accountability, majority rule and free election were in full effects. Notable difference was the fact that one could belong to as many political groups as he/she could. This was indeed a democracy that was designed special for Africa.

Likewise market economy existed before colonialism. Batter trade is case in point. Nothing actually explains better the functioning of free market economy that batter trade system. That gets me to think the scholars of market economy like Adam Smith and Ricardo built their theories on batter system. Notable difference between African free market economy and today's modern free market is that the former factored in human face elements to its function. Equilibrium value would actually move around both market and social values.

When we got independent we adopted new free market and democracy from the west. We did that at a wholesale value. We pay for it dearly in terms of equal distribution of goods and services, political instability and total destruction of social fabric and values.
 
Demokrasia na uchumi wa soko huria vilikuwapo kabla ya wakoloni. But I think that is a topic of its own.

I will reiterate what I said previous in an attempt to strengthen my point. Demecracy existed before colonialism in Africa. It was nonpartisan direct democracy. In this a person could belong to a multiple interest and political groups. In it people where equal by default and voting was employed to reach a decission. Like in the modern democracy, votes carried equal weight across voters. Like in modern representative democracy, accountability, majority rule and free election were in full effects. Notable difference was the fact that one could belong to as many political groups as he/she could. This was indeed a democracy that was designed special for Africa.

Likewise market economy existed before colonialism. Batter trade is case in point. Nothing actually explains better the functioning of free market economy that batter trade system. That gets me to think the scholars of market economy like Adam Smith and Ricardo built their theories on batter system. Notable difference between African free market economy and today's modern free market is that the former factored in human face elements to its function. Equilibrium value would actually move around both market and social values.

When we got independent we adopted new free market and democracy from the west. We did that at a wholesale value. We pay for it dearly in terms of equal distribution of goods and services, political instability and total destruction of social fabric and values.

Sijui unaongelea ukoloni upi.ila kwa haraka tuu ni kwamba ukoloni ulikuwepo pia kipindi cha nyuma kwa dola mbalimbali, kabla ya democrasia, km unadhani kuwa democrasia na soko huria vilikuwepo kabla ya wakoloni ni kuonyesh ajinis gani huna fikra ya "Relative".Ukooloni ulikuwepo miaka mingi kabla ya Kristu,kabla ya democrasia ya Ugiriki...wakati wa Yesu warumi walikuwa wakoloni wa Israel, na Biblia inasema miaka mingi tuu ya wayahudi kutumikishwa.au kutawaliwa ktk nchi yao.Democrasi ya leo ni pana sana kuliko ya miaka mingi iliyopita.

Soko huria halikuwa hi kuwepo miaka mingi kihivyo kwani kipidni kicho kulikuwa na piracy, utawala na watumwa au kupeana zawadi, hilo soko huria unaongelea juzi wakati wagiriki wakiwa wasomi na warumi wakiwa wakoloni.Ni ngumu kuliita huria ingawa watu waliuza na kununua.

barter trade haikuwa market economy km unavyotaka tudanganya,prices zilikuwa determined kwa vita,ujanja ujanja, etc...hao akina Adama smith wameishi juzi baada ya Christ wakati ukoloni kwa dola za zamani ulikuwepo kwa miaka kadhaa.
 
Nicholas mkuu, wewe ndio unaongea juu ya ukoloni. Mimi nimeongelea democracy na uchumi wa soko huru. Ili unielewe vizuri ni lazima ujue maana ya haya mambo mawili na jinsi yanavyofanya kazi. Yajuwe sio kwa kubahatisha. Sasa ukileta mambo ya ukoloni kwenye analysis inayolenga kuonyesha kwamba market economy na democracy vilikuwapo kabla ya ukoloni nashindwa hata nianzie wapi kukujibu. Nachoongea siongei kwa kubahatisha hivyo sitaki nibahatishe uelewa wangu kwa kile ulichokiandika hapa.
 
Nicholas mkuu, wewe ndio unaongea juu ya ukoloni. Mimi nimeongelea democracy na uchumi wa soko huru. Ili unielewe vizuri ni lazima ujue maana ya haya mambo mawili na jinsi yanavyofanya kazi. Yajuwe sio kwa kubahatisha. Sasa ukileta mambo ya ukoloni kwenye analysis inayolenga kuonyesha kwamba market economy na democracy vilikuwapo kabla ya ukoloni nashindwa hata nianzie wapi kukujibu. Nachoongea siongei kwa kubahatisha hivyo sitaki nibahatishe uelewa wangu kwa kile ulichokiandika hapa.
Sasa sidhani km unajua unachoongea hapa...hembu kaondoe fikra za kijamaa..za kila kitu wao ni victims wa Capitalism...mimi ndio naongelea democracy na market economy ,wewe ndio umeingiza ukoloni sasa unachemsha unaamu kunihukumu kwa matatizo yako...kwani utake play victim?Hizo ni sifa za magaidi na wajamaa kwani wote ni evils...wana halalisha uovu wao kwa kujifanya victims.Haulimi na kujituma ktk kazi .....hujui bargain ili upate best price, una watu zaidi ya nusu hawazalishi waliwanyonya wengine km viongozi, na wengine wanaozalisha chini ya 50% kwanini msididimie? Marketing economy ilikuwepo long time before ukoloni,watu walikuwa wachuuzi,na bei ya market ilibase ktk demand and supply..
 
Nicholas na MgonjwaUkimwi,
Daaah wakuu zangu bado hoja hii inaendelea? sikuwapata kujua hadi nimeona likes ndio nimejikuta najikumbusha ya miaka mingi. Hata hivyo jamani ebu tupige break kidogo, Iwe demokrasia na Market economy vilikuwepo/havikuwepo kabla ya Ukoloni inatusaidia nini kubishana juu ya hili ikiwa leo tunataka kuelewa matumizi yake yatatusaidia vipi katika kuijenga Jamii yetu.

Nadhani ni bora sana mliweke kando hili la mambo yalopita na tugange yaliyopo maana kidogo hata mimi elimu ya historia yetu kabla ya kukoloniwa siifahamu zaidi ya kuelewa tu kwamba wageni walikuja nchini kutafuta bidhaa walozihitaji lakini sijasoma kwa wenyeji wetu kwenda nchi zao kuuza ama kutafuta bidhaa. Sijui kuhusu demokrasia zaidi ya Wafalme na mengineyo yalohusu Utawala wa kimila. Tupeni darasa juu ya matumizi ya hivi vyombo ktk mazingira haya tuliyopo.
 
Nashukuru kwa somo zuri.

katika uchumi kunakitu kitu kinaitwa PERFECT Market, lakini mpaka sasa this is unrealistic theory, yaani ni kitu ambacho hakiwezekani kuwepo practicaly.
sasa masikini waafrika tunalazimisha DEMOCRASIA ingawa kwa hesabu za kiuchumi ni sawa na kutwanga maji kwenye
kinu.
 
Last edited by a moderator:
Nicholas na MgonjwaUkimwi,
Daaah wakuu zangu bado hoja hii inaendelea? sikuwapata kujua hadi nimeona likes ndio nimejikuta najikumbusha ya miaka mingi. Hata hivyo jamani ebu tupige break kidogo, Iwe demokrasia na Market economy vilikuwepo/havikuwepo kabla ya Ukoloni inatusaidia nini kubishana juu ya hili ikiwa leo tunataka kuelewa matumizi yake yatatusaidia vipi katika kuijenga Jamii yetu.

Nadhani ni bora sana mliweke kando hili la mambo yalopita na kugange yaliyopo maana kidogo hata mimi elimu ya historia yetu kabla ya kukoloniwa siifahamu zaidi ya kuelewa tu kwamba wageni walikuja nchini kutafuta bidhaa walozihitaji lakini sijasoma kwa wenyeji wetu kwenda nchi kuuza ama kutafuta bidhaa. Sijui kuhusu demokrasia nzaidi ya Wafalme na mengineyo. Tupeni darasa juu ya matumizi ya hivi vyombo ktk mazingira haya tuliyopo.

Mkuu Mkandara habari za miaka tele!

Ngumu kuanza kujadili demokrasia na market economy vitatusaidiaje kabla hatujajuwa vitu hivi ni vitu gani na vimetoka wapi na je vina fit vipi kwenye jamii yetu. Rejea kwenye kichwa cha habari cha mada hii.
 
Last edited by a moderator:
Nchi haiwezi kukuwa na wasomi kibao kila mmoja anafikiri kuiba ndio uchumi na kuwapelekea wengine waweke akidhani ni uchumi, wengine wansahau waliopelekewa wameisoma Injil ,na mfano wa Yesu wa walioachiwa hela na kibopa aliyesafiri, waliozifanyia kazi walifaidi riba na kuongezewa juu,walioziweka kwa roho mbaya walinyang`angywa hata kidogo walichopewa.Hawa hawa wasomi na viongozi ili wapate faida wanaiba tena.Maana yake ni kwamba..Wataiba hadi wamalize na kukosa cha kuiba...Sifa hii ni ya mwizi asiye competent..mwoga na hatari.Mwizo asiye competent,mzee au aliyeanza karibia kufa huiba nyumbani, na mwisho huishia hata kubaka jamaa zake nyumbani.
 
As we liberalize the economy, we must also liberalize our politics. As we ambrace pluralism in market economy we should also embrace political pluralism wholeheartdely. Mazingaombwe katika mfumo wa vyama vingi kama ilivyo sasa hayatatufikisha popote. Lazima wananchi na viongozi wa siasa tuache usanii wa kisiasa.
The issue ni kwamba watu km nyie muanze liberate akili zenu kwanza.Halafu mu aim high na mfanye vitu mnavyoamini ktk mioyo kuwa ni sahihi kwa best understanding yako ,in reference to all community standards at least.Wewe unahitaji political liberation kwa upinzani au kwa chama tawala?Pia ungeanza wewe kuacha mazingaombwe ndipo ungenishawishi kuwa una uelewwa kutosha kujadili ninachokisema hapa.Sasa km machapisho yako yamejaaa ujanja ujanja wa kutaka Mtengeneza super hero kwa kumbandika sifa mwanasiasa unayemtamani awe juu ya kila kitu ,badala ya kum tame awe hivyo.Ni vipi sasa unajadili hii mada?Au unataka leta poison za UDSM zilizochafua na kuifanya Africa iwe comfused.
 
As we liberalize the economy, we must also liberalize our politics. As we ambrace pluralism in market economy we should also embrace political pluralism wholeheartdely. Mazingaombwe katika mfumo wa vyama vingi kama ilivyo sasa hayatatufikisha popote. Lazima wananchi na viongozi wa siasa tuache usanii wa kisiasa.
Shida yako Muzee sasa hivi prof ni kwamba your too biased na driven by emotions and wishes...Kwanini umefix akili yako kwamba Yai ndilo linaweza leta kuku tuu na Kuku naye anaweza leta yai?China is shaped by economic revolution zaidi ya political.Sasa km akili yako imekuwa locked ktk harisa zako dhidi ya CDM haitochukua muda utajikuta hata undergraudate wanandika paper zitakazokuwa your envy.Nimewawahi wasikia sana wewe na maprof wengine..mkiwa ktk media enzi zile mkiwa na soko.Mlikuwa mara zote mnaweka kwapani mlichokuwa mkitaka ongea baada ya kusikia vya wengine.na mwinsho kuishia jifanya wasuluhishi kuliko watu wenye view na philosophy ambayo inaweza kuwa defined km the alternative views.Bahati mbaya sana hata machapisho ya UDSM siko zote ni mchanganyiko wa Popular Voculbraries that explain contemporary issues and mostly unrelated and opposing.Ila machapisho yenu huwa yanajumlisha as if hayo mambo yanakaa chung moja.Ndio maana Wajamaa ni Chaos duniani.Mnataka kila kitu kizuri kiwa chenu.Lini nyumba moja ikawa na madirisha yote mazuri duniani?
 
Back
Top Bottom