Hivi karibuni tumeshuhudia upepo mbaya wa mahusiano ya kidini kufuatia kukojolewa kwa msahafu wa waislamu na kisha kuchomwa moto makanisa na mali zingine kuharibiwa.Kilichofuatia baada ya tukio hilo ni kauli nzito za kimsimamo zilizotolewa na pande mbili zinazohasimiana,waislamuj na wakristo.Nimepata fursa ya kutosha kusoma matamko ya kila upande kwa makini.Kwa jumla wakristo(Maaskofu KKKT) wanalalamikia ukimya wa Serikali kuchukua hatua kufuatia vitendo vya muda mrefu vya wailamu kuingilia mamlaka ya nchi,kama kugomea sensa,kushinikiza waliogomea sensa na kukamatwa waachiwe,kuchomwa makanisa Zanziba,mahakamaya kadhi,kukataa ubalozi fulani nk.
Kwa upande wa waislamu wanalalamikia Kuonewa kwa muda mrefu na bila Serikali kuchukua hatua,kama,kuchomwa moto misahafu yao,kukamatwa na polisi,kunyimwa mahakama ya kadhi,kubaguliwa nafasi za uongozi na hili la kukojolewa msahafu,nk.Aidha wanaamini kuwa migogoro ya kisiasa ,migomo na maandamano kama ni mbinu za wakristo kumuhujumu Rais kabla hajamaliza kipindi chake,zinazoongozwa na CDM. Ili mradi kila mmoja anaona hatendewi haki na serikali(ya kikwete)
Kwa muono wangu,ni kweli Serikali imezembea sana kuchukua hatua kukomesha udini mara tu dalili zilipoanza kujitokeza.(Sisemi kuna upande wowote ulioonewa)..Udini na Ukabila ni sumu mbaya inayopaswa kukomeshwa katika hatua za awali kabisa. Kwa Tanzania udini umeshakomaa,tumechelewa,pande zote haziaminiani tena ,na hawaiamini serikali yao.HAKUNA ALIE SAFI MWENYE UBAVU WA KUWAWEKA CHINI PANDE HIZI MBILI NA KUZIKEMEA,ACHILIA MBALI KUSULUHISHA,TWAHITAJI MTU NEUTRAL WA KUFANYA KAZI HIYO.
MUNGU IREHEMU TANZANIA.
Kwa upande wa waislamu wanalalamikia Kuonewa kwa muda mrefu na bila Serikali kuchukua hatua,kama,kuchomwa moto misahafu yao,kukamatwa na polisi,kunyimwa mahakama ya kadhi,kubaguliwa nafasi za uongozi na hili la kukojolewa msahafu,nk.Aidha wanaamini kuwa migogoro ya kisiasa ,migomo na maandamano kama ni mbinu za wakristo kumuhujumu Rais kabla hajamaliza kipindi chake,zinazoongozwa na CDM. Ili mradi kila mmoja anaona hatendewi haki na serikali(ya kikwete)
Kwa muono wangu,ni kweli Serikali imezembea sana kuchukua hatua kukomesha udini mara tu dalili zilipoanza kujitokeza.(Sisemi kuna upande wowote ulioonewa)..Udini na Ukabila ni sumu mbaya inayopaswa kukomeshwa katika hatua za awali kabisa. Kwa Tanzania udini umeshakomaa,tumechelewa,pande zote haziaminiani tena ,na hawaiamini serikali yao.HAKUNA ALIE SAFI MWENYE UBAVU WA KUWAWEKA CHINI PANDE HIZI MBILI NA KUZIKEMEA,ACHILIA MBALI KUSULUHISHA,TWAHITAJI MTU NEUTRAL WA KUFANYA KAZI HIYO.
MUNGU IREHEMU TANZANIA.