Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,555
- 19,430
Rushwa ni fadhila zitolewazao au kupokelewa ili kutokee upendeleo fulani. Zamani sana ningali shule ya msingi nilikuwa nimeakaririshwa ahadi, imani na madhumuni ya TANU; mojawapo ilikuwa inasema hivi:
"Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa."
Katika sheria za Tanzania, kuna sheria zinazoharamisha rushwa, na ndiyo maana kuna kitengo maalum cha serikali kinachopambana na rushwa. Mwanzoni mwa utawala wa Mkapa, kulikuwa na tume ya kuchunguza tatizo la rushwa nchini. Yote hayo ni kuonyesha kuwa Taifa letu linatambua wazi ubaya wa rushwa.
Hhata hivyo, inaonekana kuwa bado hatujajua namna ya kupambana na rushwa sawasawa, ndiyo maana beneficiaries wengi wa rushwa hawajawahi kutiwa hatiani kwa makosa hayo. Katika kosa la rushwa, mtoaji na mpokeaji kwa pamoja wanavunja sheria. Hata hivyo, kisheria inabidi washikwe na mtu wa pembeni na athibitishe kuwa watu hao walikuwa wakipeana rushwa ili kuwe na upendeleo wa aina fulani, vinginevyo hakuna njia rahisi ya kuwashika watumia rushwa hasa kama wote wamekubaliana. Mara kwa mara wapokea rushwa wamekuwa wakishikwa pale tu ambapo mtu aliyeombwa rushwa anaona kuwa hana haja ya yeye kutoa rushwa hiyo ili apate haki yake; na watoa rushwa wamekuwa wakishikwa pale wanapotoa rushwa ndogo sana kiasi kuwa mpewa rushwa anaona kuwa hatapata faida yoyote kwa kupokea rushwa hiyo. Njia rahisi ya kushika watumia rushwa waliokubaliana ni kutoa msamaha na kumtisha mmoja hasa yule aliyeshawishiwa kujihusisha na rushwa hiyo ili atoe ushahidi dhidi ya yule aliyeshawishi rushwa kumtia hatiani na yeye shahidi aachiwe huru. Kwa vyovyote sheria zetu dhidi ya rushwa bado ni dhaifu sana.
Kuanzia miaka ya themanini wakati wa "Mikingamo" wapokea na watoa rushwa walianzisha njia nyingine ya kufanya hivyo kwa kupitia "wakaa kati." Yaani ama mtoa rushwa au mpokea rushwa au wote wawili wanatumia watu wengine kuomba, kutoa au kupokea rushwa hiyo ili upendeleo ufanyike baina ya wahusika. Kwa vile sheria zetu bado zinataka ithibitike kuwa anayeshitakiwa ndiye aliyehusika na rushwa ile moja kwa moja, ni wazi kuwa haziwezi kufanya lolote kuhusiana na rushwa zinazohusisha wakaa kati.
Kwa wanaojua sheria, je tufanye nini katika sheria zetu ili kukabiliana na rushwa zinazotumia wakaa kati? Yaania kumtia hatiani yeyote aliyehusika kama mkaa kati wa rushwa na wale beneficiaries wa rushwa inaytumia wakaa kati.
"Rushwa ni adui wa haki, sitapokea wala kutoa rushwa."
Katika sheria za Tanzania, kuna sheria zinazoharamisha rushwa, na ndiyo maana kuna kitengo maalum cha serikali kinachopambana na rushwa. Mwanzoni mwa utawala wa Mkapa, kulikuwa na tume ya kuchunguza tatizo la rushwa nchini. Yote hayo ni kuonyesha kuwa Taifa letu linatambua wazi ubaya wa rushwa.
Hhata hivyo, inaonekana kuwa bado hatujajua namna ya kupambana na rushwa sawasawa, ndiyo maana beneficiaries wengi wa rushwa hawajawahi kutiwa hatiani kwa makosa hayo. Katika kosa la rushwa, mtoaji na mpokeaji kwa pamoja wanavunja sheria. Hata hivyo, kisheria inabidi washikwe na mtu wa pembeni na athibitishe kuwa watu hao walikuwa wakipeana rushwa ili kuwe na upendeleo wa aina fulani, vinginevyo hakuna njia rahisi ya kuwashika watumia rushwa hasa kama wote wamekubaliana. Mara kwa mara wapokea rushwa wamekuwa wakishikwa pale tu ambapo mtu aliyeombwa rushwa anaona kuwa hana haja ya yeye kutoa rushwa hiyo ili apate haki yake; na watoa rushwa wamekuwa wakishikwa pale wanapotoa rushwa ndogo sana kiasi kuwa mpewa rushwa anaona kuwa hatapata faida yoyote kwa kupokea rushwa hiyo. Njia rahisi ya kushika watumia rushwa waliokubaliana ni kutoa msamaha na kumtisha mmoja hasa yule aliyeshawishiwa kujihusisha na rushwa hiyo ili atoe ushahidi dhidi ya yule aliyeshawishi rushwa kumtia hatiani na yeye shahidi aachiwe huru. Kwa vyovyote sheria zetu dhidi ya rushwa bado ni dhaifu sana.
Kuanzia miaka ya themanini wakati wa "Mikingamo" wapokea na watoa rushwa walianzisha njia nyingine ya kufanya hivyo kwa kupitia "wakaa kati." Yaani ama mtoa rushwa au mpokea rushwa au wote wawili wanatumia watu wengine kuomba, kutoa au kupokea rushwa hiyo ili upendeleo ufanyike baina ya wahusika. Kwa vile sheria zetu bado zinataka ithibitike kuwa anayeshitakiwa ndiye aliyehusika na rushwa ile moja kwa moja, ni wazi kuwa haziwezi kufanya lolote kuhusiana na rushwa zinazohusisha wakaa kati.
Kwa wanaojua sheria, je tufanye nini katika sheria zetu ili kukabiliana na rushwa zinazotumia wakaa kati? Yaania kumtia hatiani yeyote aliyehusika kama mkaa kati wa rushwa na wale beneficiaries wa rushwa inaytumia wakaa kati.