Halisi
JF-Expert Member
- Jan 16, 2007
- 2,802
- 613
Tutafakari, nchi haiko sawa
John Bwire, Mhariri Raia Mwema Februari 11, 2009
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Jamhuri ya umoja ambayo iko chini ya demokrasia ya Bunge la vyama vingi vya siasa.
Ina nguzo tatu za utawala ambazo ni: Serikali, Mahakama na Bunge. Vyombo hivi vitatu vya utawala vina uwezo na madaraka ya kusimamia shughuli zote za umma.
Katika mfumo usio rasmi, vyombo vya habari navyo vimetajwa kama mhimili wa nne wa dola, na vimekuwa vikitoa mchango mkubwa katika mfumo mzima wa utawala bora na utoaji elimu na upashaji habari. Kwa muda mrefu vimetimiza wajibu wake.
Kwa kuwa mfumo wa vyama vingi vya siasa ndio uliokubalika na kutumika katika Tanzania, vyama vya siasa navyo vimekuwa na mchango mkubwa katika mustakabali wa taifa hili pamoja na kuwa ndani ya mhimili wa Bunge wamo wanasiasa wa vyama vyote.
Kwa utangulizi huo hapo juu, tuna kila sababu ya kushituka inapotokea kuwapo kwa kauli za kusigana katika mihimili rasmi na ule usio rasmi na kwa kuongezea katika matatizo hayo inatisha zaidi kuwapo matatizo ndani ya vyama vyote vya siasa na miongoni mwa vyama husika.
Hali hiyo inavigusa vyama vya upinzani na chama tawala cha CCM.
Taarifa za hivi karibuni kwamba Spika wa Bunge Samuel Sitta na Jaji Mkuu Augustino Ramadhan wametofautiana hadharani kuhusiana na mipaka ya vyombo vyao, ni mwangwi wa hali ilivyo sasa katika mfumo mzima wa utawala katika taifa letu.
Kama ilivyo katika utangulizi hapo juu hali hiyo haijaviacha vyombo vingine kama vile Serikali yenyewe ambako tumeshuhudia serikalini vyombo kama vile Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Jeshi la Polisi vikilumbana, na kuna wakati vyombo hivyo vimesikikika vikiilaumu Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kuhusiana na mwenendo wa kesi vinazochunguza.
Kadhalika, ndani na nje ya Bunge kumeripotiwa kuwapo taarifa za kuwapo mgawanyiko wa wazi wa vyama vya siasa na hata baadhi ya wanasiasa wa chama kimoja ikiwa ni pamoja na kuparaganyika kwa vyama vya upinzani na hata chama tawala cha CCM.
Kwa upande wa vyombo vya habari nako hali inaelekea si shwari tena kwa kuibuka malumbano ya wazi ambayo yanapotoeza mwelekeo na sasa kuhamia kuingiliwa kwa mambo binafsi zaidi huku hoja za msingi zinazolenga kuwakomboa Watanzania zikiachwa kwa makusudi kwa nia ya kubeba ajenda za watu wachache wanaotaka kujilinda.
Kama Taifa, hivi sasa Tanzania inaelekea imekuwa mithili ya mechi ya mpira wa miguu ambayo inachezwa bila ya kuwa na refa kutokana na mambo kwenda ovyo karibu katika kila eneo muhimu kwa mustakabli wa nchi hii.
Hali hii si njema kwa Taifa na ina hatari ya kuwafanya wananchi wa kawaida wakose mahali pa kukimbilia, jambo ambalo ni la hatari kwa amani na utulivu wa Taifa, tulivyorithi na tulivyovilinda kwa zaidi ya miaka 40 sasa.
Sisi tunatoa mwito kwamba sasa ni wakati muafaka wa kutafakari na kuchukua hatua za haraka.
SOURCE: Tutafakari, nchi haiko sawa
John Bwire, Mhariri Raia Mwema Februari 11, 2009
SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Jamhuri ya umoja ambayo iko chini ya demokrasia ya Bunge la vyama vingi vya siasa.
Ina nguzo tatu za utawala ambazo ni: Serikali, Mahakama na Bunge. Vyombo hivi vitatu vya utawala vina uwezo na madaraka ya kusimamia shughuli zote za umma.
Katika mfumo usio rasmi, vyombo vya habari navyo vimetajwa kama mhimili wa nne wa dola, na vimekuwa vikitoa mchango mkubwa katika mfumo mzima wa utawala bora na utoaji elimu na upashaji habari. Kwa muda mrefu vimetimiza wajibu wake.
Kwa kuwa mfumo wa vyama vingi vya siasa ndio uliokubalika na kutumika katika Tanzania, vyama vya siasa navyo vimekuwa na mchango mkubwa katika mustakabali wa taifa hili pamoja na kuwa ndani ya mhimili wa Bunge wamo wanasiasa wa vyama vyote.
Kwa utangulizi huo hapo juu, tuna kila sababu ya kushituka inapotokea kuwapo kwa kauli za kusigana katika mihimili rasmi na ule usio rasmi na kwa kuongezea katika matatizo hayo inatisha zaidi kuwapo matatizo ndani ya vyama vyote vya siasa na miongoni mwa vyama husika.
Hali hiyo inavigusa vyama vya upinzani na chama tawala cha CCM.
Taarifa za hivi karibuni kwamba Spika wa Bunge Samuel Sitta na Jaji Mkuu Augustino Ramadhan wametofautiana hadharani kuhusiana na mipaka ya vyombo vyao, ni mwangwi wa hali ilivyo sasa katika mfumo mzima wa utawala katika taifa letu.
Kama ilivyo katika utangulizi hapo juu hali hiyo haijaviacha vyombo vingine kama vile Serikali yenyewe ambako tumeshuhudia serikalini vyombo kama vile Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Jeshi la Polisi vikilumbana, na kuna wakati vyombo hivyo vimesikikika vikiilaumu Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kuhusiana na mwenendo wa kesi vinazochunguza.
Kadhalika, ndani na nje ya Bunge kumeripotiwa kuwapo taarifa za kuwapo mgawanyiko wa wazi wa vyama vya siasa na hata baadhi ya wanasiasa wa chama kimoja ikiwa ni pamoja na kuparaganyika kwa vyama vya upinzani na hata chama tawala cha CCM.
Kwa upande wa vyombo vya habari nako hali inaelekea si shwari tena kwa kuibuka malumbano ya wazi ambayo yanapotoeza mwelekeo na sasa kuhamia kuingiliwa kwa mambo binafsi zaidi huku hoja za msingi zinazolenga kuwakomboa Watanzania zikiachwa kwa makusudi kwa nia ya kubeba ajenda za watu wachache wanaotaka kujilinda.
Kama Taifa, hivi sasa Tanzania inaelekea imekuwa mithili ya mechi ya mpira wa miguu ambayo inachezwa bila ya kuwa na refa kutokana na mambo kwenda ovyo karibu katika kila eneo muhimu kwa mustakabli wa nchi hii.
Hali hii si njema kwa Taifa na ina hatari ya kuwafanya wananchi wa kawaida wakose mahali pa kukimbilia, jambo ambalo ni la hatari kwa amani na utulivu wa Taifa, tulivyorithi na tulivyovilinda kwa zaidi ya miaka 40 sasa.
Sisi tunatoa mwito kwamba sasa ni wakati muafaka wa kutafakari na kuchukua hatua za haraka.
SOURCE: Tutafakari, nchi haiko sawa