Kuna matangazo kwenye radio yanayoelezea kuwa hata kulazimisha mapenzi kwa mkeo ni ukiukaji wa haki za binadamu, Hebu niambieni kuwa kuna watu wanabadilika jinsi ya kufanya mapenzi na wake zao kwa kusikia tu tangazo la radio au wanaolipia matangazo hayo wanaharibu pesa zao, Hivi wanafanya tathmini na kujua ni kiasi gani watu wanapokea hayo matangazo, Ambapo mengine yakitangazwa wengine wanafunga radio au wanaondoka kijanja. Kama fedha hizo ni za wafadhili hayo ni matusi na misaada ya aina hiyo haitatusogeza popote, Tutapewa misaada daima dumu lakini tutaendelea kuwa masikini na maendeleo duni. Hayo ni matumizi mabaya ya rasilimali