samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Jana chama cha wananchi CUF kiliitisha maandamano ya kuwasilisha mapendekezo ya katiba mpya. Licha ya maandamano hayo kuzuiwa na polisi dakika za mwisho wanachama wa CUF waliendelea na maandamano hayo kitendo ambacho kilisababisha taharuki baada ya askari polisi kutumia mabomu ya machozi na risasi za moto kuwatawanya wana CUF. Jambo lililonisikisha ni kitendo cha wana jamii forum kubeza harakati hizo za kudai katiba mpya. Wengi wametoa manenö ya kejeli na kudai inakuaje polisi wanawapiga ndugu zao na CCM. Wana JF wanaona harakati hizo za CUF hazina mchango wowote katika mapambano ya kudai katiba mpya kwa sababu CUF wako kwenye serikali ya mseto kule zanzibar. Mtu mwenye mtazamo huo hastahili kujiita great thinker. Ni vizuri wale wote wenye mtazamo hasi dhidi ya CUF ni vema akafahamu kwamba harakati za madai ya katiba mpya sio za CHADEMA peke yao bali ni ya watanzania wote bila kujali itikadi za vyama vya siasa au dini. CHADEMA PEKE YAN HAWAWEZI KUTUPATIA KATIBA MPYA. Hivyo basi ni muhimu tuunge mkono harakati zinazofanywa na makundi mbalimbali ili kufanikisha upatikanaji wa katiba mpya. Kitu kingine naomba tuache tabia ya kuwashabikia polisi wanapokua wakiwandunda wananchi wakati wa kutekeleza haki zao za kikatiba kama wana JF wengi walivyofanya baada ya polisi kuwadunda wanafunzi wa UDOM na jana baada ya kuwatawanya wana CUF. Tunapochangia ndani ya JF tuache kufuata mkumbo.