Tusisubiri Mtetezi suala la Pensheni atoke nje ya wafanyakazi!

Mjomba wa taifa

JF-Expert Member
Apr 20, 2012
231
161
"Ukicheka na Nyani utavuna mabua". Usemi huu unazidi kudhihirika katika nchi yetu hasa katika suala la wafanyakazi kuendelea kukandamizwa bila ya kuwa na mtetezi. Wafanyakazi hawa ndio wamekuwa walipa kodi kwa serikali kwa asilimia 100 kuliko chanzo kingine chochote cha kodi. Hili serikali imefanikiwa kuwanyamazisha wafanyakazi.

Sasa kanakwamba hilo la kodi halitoshi, Serikali imeamua kuwatikisa tena wafanyakazi kwa kuwalazimisha kusubiri pesa zao za akiba mpaka ufike umri wa kustaafu. Hivi kwanini serikali inapanga maisha ya mtu mmojammoja. Kesho itakuja na sheria nyingine ya matumizi ya mshahara.

Kwa hili tafadhali wafanyakazi wasitarajie kupata mtetezi asiyekuwamfanyakazi na anaeumizwa moja kwa moja na sheria hii. Sheria hii imepitishwa Bungeni kwa urahisi kabisa pasipo kuzua mijadala na ndio maana watanzania wengi wameshtuka na kushangaa kusikia sheria hiyo ilipitishwa muda mrefu Bungeni, April mwaka huu.

Kama ni suala la kuweka akiba, mfanyakazi wa leo anajua kuna mabenki mengi nchini atakwenda kuhifadhi pesa za watoto wake. Kumekuwa na utetezi potofu juu ya sheria hii kuwa itasaidia mfanyakazi kukopa Nyumba. Je, mahitaji ya wafanyakazi ni nyumba tu? kuna ambao tayari wameshajenga kwa njia wanazozijua wenyewe na mahitaji yao si nyumba tena.

Na kama suala ni kumlinda mfanyakazi asijekudhalilika uzeeni, basi suala hili liwe ni hiari ya mfanyakazi mwenyewe lakini kwa wanaotaka kuchukua pesa zao, waachwe wachukue. Kwa hili serikali ndio inajifanya kuwajali wafanyakazi, mbona wazee wa iliyokuwa Jumuiya ya Afrika Mashariki mpaka leo wapo wamelala pale makao makuu ya stesheni Dar wanaokoteleza vyakula, serikali haiwaoni? Mafao yao yako wapi?

Wafanyakazi ujumbe ni kuwa "ukicheka na Nyani utavuna Mabua".
 
suala hilo likiwagusa na wabunge pia ndo litafanyiwa marekebisho,hv hv ni tantalila tu,nao waambiwe kama hawajafikisha hy miaka no pension uone ukali wao
 
Hivi mimi mpaka leo najiuliza hivi ni kweli hii sheria imepitishwa Bungeni? Kama imepitishwa kweli bungeni naanza kuwa na shaka na wabunge wote bila kumuondoa hata mmoja hata wale niliowaamini wa upinzani.

Ilikuwaje ikapita kimyakimya tusisikie hata kelele kwa akina Mnyika, Mkosamali, Filikunjombe, Lissu wote kweli mkanyamaza kimya watanzania tunapitishiwa sheria ya kutuumiza kiasi hiki?
 
Kama sheria hii itapita nadhani njia pekee ya kuja kujikomboa ni kuchagua chama cha upinzani ili kije kibadili sheria hii. kama Raisi alivyosema sihitaji kura za wafanyakazi basi nadhani na sisi wafanyakazi wa private sector tuungane hiyo 2015 kuhakikisha CCM hairudi tena hapo ndo utakua ukombozi wetu, vinginevyo imekula kwetu
 
Najiuliza hivi huo mwezi wa nne wakati hii sheria inapitishwa ya kuzuia wafanyakazi kulipwa pesa yake
mpaka afikishe umri wa miaka 55 au zaidi, hivi wabunge walikuwepo bungeni na wakakubali?
Cha kushangaza hakukuwa na hata tetesi kuwa kuna hii sheria inapitishwa,je wabunge
wote mpaka wa upinzani hawakuwa wameona madhara ya hili!

Maana kama wangeliona hili lazima kelele za kupinga zingesikika.Hivi kwa hali ya maisha ya sasa ni watanzania wangapi wana uhakika wa kufika miaka 55? au mtu anaacha au kuachishwa kazi na hataki kuajiriwa let say ana miaka 40 asubiri mpaka miaka 15 ijayo ndipo alipwe pesa zake!!

Hii inaingia akilini? Cha kushangaza hakuna mbunge wala kiongozi yoyote aliongelea au anaongelea juu ya hili, mnataka watanzania tuamini kuwa wote mlinyamazishwa kama Mgaya na TUCTA yake walivyonyamazishwa?
 
kulalamika hivi hakutoshi...do something....hili ni jaribu la mwisho kwa watanzan hasa wafanyakazi
 
REMSA So long as haiwagusi wao, hawaoni shida yoyote. Wote wanapigaania matumbo yao tu.
 
Last edited by a moderator:
vyama vya wafanyakaz vifanye kaz kwny hilo suala la wafanyakazi
LHRC wameamua kufungua kesi ingawa kwa mahakama zetu hatujui itachukua miongo mingapi kuamuliwa. Ifunguliwe kwa hati ya dharura kama inawezekana na wapeni msaada wanaohitaji. Hivi vyama vya wafanyakazi ni ulaji tu.
 
Hivi mimi mpaka leo najiuliza hivi ni kweli hii sheria imepitishwa Bungeni? Kama imepitishwa kweli bungeni naanza kuwa na shaka na wabunge wote bila kumuondoa hata mmoja hata wale niliowaamini wa upinzani.

Ilikuwaje ikapita kimyakimya tusisikie hata kelele kwa akina Mnyika, Mkosamali, Filikunjombe, Lissu wote kweli mkanyamaza kimya watanzania tunapitishiwa sheria ya kutuumiza kiasi hiki?
[/QUOTwE]
wao wakimaliza kipindi chao wanapata marupuru kibao so hata wakisubiri mpaka miaka 55 hawana tatizo... katika bunge la sasa hakuna mwenye nia ya kweli katika kuyafanya maisha ya watanznia kuwa mazuri.. wako kimaslahi zaidi si ccm peke yake hata hawa wanaojiita wanaharakati wa chadema na nccr
 
Mi nilichoka tu nilipoambiwa kwamba ukiacha kazi leo huku akiba yako ni milioni 2 na una miaka 30, utalipwa milioni 2 ile ile wakati una miaka 50 (20 years later). Huu ni upuuzi wa hali ya juu sana na nimeamini wabunge WOTE ni wanafiki tu
 
Hivi mimi mpaka leo najiuliza hivi ni kweli hii sheria imepitishwa Bungeni? Kama imepitishwa kweli bungeni naanza kuwa na shaka na wabunge wote bila kumuondoa hata mmoja hata wale niliowaamini wa upinzani.

Ilikuwaje ikapita kimyakimya tusisikie hata kelele kwa akina Mnyika, Mkosamali, Filikunjombe, Lissu wote kweli mkanyamaza kimya watanzania tunapitishiwa sheria ya kutuumiza kiasi hiki?

ilishapita mkuu...
 
48. The principle act is ammended by repealing section 18 and substitung for it the following new sections

RECOVERY OF CONTRIBUTION CAP 33



18.(1) Every statutory contribution due to the fund may be recovered by way of summary suit under order XXXV of civil procedure code at any time after the date which it is due
18. (2) where an offense is committed by reason of non payement of statutory contribution no prosecution shall be commenced without consent of director of public prosecution

49. The principle act is ammended in section 20 by adding iimediately after subsection 3 the following new subsections

(4) Without prejudice to subsection 1, 2, and 3 benefit for entitled person may be used as collateral for home mortgage for a member who has not attained the age of retirement

Wanasheria hebu tupeni uelewa juu ya order XXXV of civil procedure code, na haya mambo ya mortgage hapo sielewi elewi! kwanini iwe collateral kwa home mortgage tuu isiwe collateral labda ya kuombea mikopo benki!!!
 
Siasa za Tanzania ni za kijinga sana hakuna cha Magamba wala magwanda wote ni wanafiki tu wanatafuta ulaji. ni kama mchezo wa kombolela mmoja analinda goli mwingine anafichama
 
Siasa za Tanzania ni za kijinga sana hakuna cha Magamba wala magwanda wote ni wanafiki tu wanatafuta ulaji. ni kama mchezo wa kombolela mmoja analinda goli mwingine anafichama

Igwe like this.......
 
Hivi mimi mpaka leo najiuliza hivi ni kweli hii sheria imepitishwa Bungeni? Kama imepitishwa kweli bungeni naanza kuwa na shaka na wabunge wote bila kumuondoa hata mmoja hata wale niliowaamini wa upinzani.

Ilikuwaje ikapita kimyakimya tusisikie hata kelele kwa akina Mnyika, Mkosamali, Filikunjombe, Lissu wote kweli mkanyamaza kimya watanzania tunapitishiwa sheria ya kutuumiza kiasi hiki?

Hayo waliyopigia kelele hatua gani ulichukua? shughulikia kwanza hayo kabla hujawauliza kwa nini hawakupiga kelele kwa hili!
 
REMSA So long as haiwagusi wao, hawaoni shida yoyote. Wote wanapigaania matumbo yao tu.

Ni kweli ktk hili sielewi tunakwenda wapi,maana mfanyakazi ukiacha au kuachishwa kazi hulipwi pesa zako
na wala huatapeleka michango wala mwajiri hatapeleka tena,ukisubiri mpaka kufika huo umri wa kustaafu
hiyo pesa utalipwa kwa thamani ipi ya toka ulipoacha kuchangia au ya wakati huo.Mbele giza!!!!!!!!!
 
Hayo waliyopigia kelele hatua gani ulichukua? shughulikia kwanza hayo kabla hujawauliza kwa nini hawakupiga kelele kwa hili!

Hata kama tusingekuwa na la kufanya lakini tungejua kuwa wametutetea,na sijui una maanisha nini kusema nishughulikie
hayo waliyopigia kelele,nikiwa mwananchi wa kawaida ndio maana nimemtuma mwakilishi bungeni akaielekeze serikali
nini ifanye kwa ajili yangu.
 
Back
Top Bottom