Omulangi
JF-Expert Member
- Feb 12, 2008
- 1,036
- 265
Bora wewe umeliona hili na kulileta hapa jamvin.Ipo haja kwa hiyo intelijensia kufuatilia mambo ya msingi kama haya na sio kuvunja maandamano ya aman.Radio Iman+gazet la Al nur ni vyombo vya habari vya kichochezi na visivyokuwa na maadili.Binafsi nimekuwa nikifuatilia habari zao hasa wakati wa kampeni,kwa kweli inasikitisha,sijui kwa nini yanazidi kukumbatiwa!
Kuna rafiki yangu mmoja wa Rwanda ambaye alikuwepo huko kabla na wakati wa mauaji ya kimballi huko juzi ameniambia hali inayoanza kutokea Tanzania ni ile ile iliyokuwa huko kwao kabla ya genocide. Jambo la kushangaza ni jinsi serkali inavyochochea tofauti hizi na kutia mafuta katika fukuto hili la kidini kwa maslahi yake. Kwa vile sasa watawala wanaona hawakubaliki kama zamani wanafikiri ni bora kuigawa jamii katika udini ili angalau wawe na mtetezi!!! Lakini kwa vile malengo haya tunayajua ni vizuri sasa data zianze kukusanywa na ushahidi wa magazeti, kanda n.k n.k Pia ni vizuri kuwa alert mapema mahakama ya kimataifa ili damu zikishamwagwa waliohusika na uchochezi huu pamoja na walio engineer wakumbane na mkono wa sheria.