Tusikatishane tamaa kuhusu sekretarieti ya ajira

mwinukai

JF-Expert Member
May 3, 2011
1,447
630
Ni ukweli kuwa tupita kipindi kigumu sana katika kutafuta ajira, na maombi mengi tunayatuma na wala hatuitwi kuja kufanya interview, na wakati huohuo maisha ni magumu kwa namna hii mtu lazima alalamike, na kuona kwamba kuna tasisi au mtu anambania kazi, na hivyo kukata tamaa.

Mimi hadi kabla ya kuitwa kwenye interview pengine nilikuwa mtu wa fikra hizo, kwani nimetafuata ajira kwa mda mrefu sana, nimeandika barua nyingi, nimebadilisha CV za kila namna nikifikiri zitasanisaidia kupata kazi, lakini kwa muda mrefu kulikuwa na ukimya utadhani kama sijatuma kitu vile. kumbe ilikuwa ni suala la wakati kwani ikafikia kipindi nimeitwa na sekretarieti ya ajira nafasi tatu tofauti, na nimechaguliwa hapo jana katika interview ya kuanza tuu niliyoifanya katika maisha yangu hapo sekretarieti.

Cha msingi wenzangu tusikate tamaa, pale unapokataa tamaa ndipo ushindi wamwenzako unapoanzia, tusikatishane tamaa kuhusu Sekretariti ya ajira kwani kama kuna matatizo, hakuna taasisi yoyote hapa Tanzania ambayo haitafanya kazi bila matatizo, cha msingi Sekretariti imepunguza matatizo hayo. Cha msingi kuwa na sifa halafu uzitete sifa hizo kwenye interview utapita kama nilivyopita.


From Seniour job Seeker(As then was)
 
hahaha alakini hata ka-ukabila, rushwa na upendeleo wanao bhana, ukibisha tu naweka mfano, au kabla hujabisha ngoja niweke mambo wazi....Chuo cha Biashara-CBE Dodoma wapo waliotoa rushwa kwa hao maofisa na wakapata hizo ajira, sipo kwa majungu ila huo ndio ukweli, more to come..../
Ila kama wamejirekebisha basi ni jambo la heri, sina tatizo nalo wanahitaji kupongezwa.
 
Kaka Elli sisemi kuwa matatizo hayo hayapo, huenda yapo maana wote Tunaijua Tanzania, na unahaki ya kulalamika ili udhaifu huo uondoke, kwa mimi ninachosema licha ya hayo yote tusikate tamaa kutuma maombi kwani hata mimi mingekata tamaa singechaguliwa, kwa sisi ambao hatuna fedha au Ndugu silaha kubwa tuliyonao ni kutokata tamaa, kuwa na sifa na kuzitetea sifa hizo.
mwenzako nimetuma maombi zaidi ya 40, wala sikuitwa, na hayo uliyoyasema yalikuwa yakisemwa toka zamani, lakini kwa vile mimi nimepata wakati huu pamoja na senoiur job seekers wenzangu wengi wamepata napata tafsiri huenda tatizo limepungua.
 
naomba ninukuu yafutayo! soma mhubiri 9:11
[SUP]11 [/SUP]I returned, and saw under the sun, that the race is not to the swift, nor the battle to the strong, neither yet bread to the wise, nor yet riches to men of understanding, nor yet favour to men of skill; but time and chance happeneth to them all.

11 Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba mashindano si mwepesi, wala vita kwa nguvu, wala wenye hekima wapatao chakula, wala utajiri bado watu wa ufahamu, wala neema wenye ustadi; lakini wakati na bahati huwapata wote.



nawaomba vijana wenzangu haya maneno yawatie nguvu mnapoona mnakata tamaa ya kupata ajira!
 
Ni ukweli kuwa tupita kipindi kigumu sana katika kutafuta ajira, na maombi mengi tunayatuma na wala hatuitwi kuja kufanya interview, na wakati huohuo maisha ni magumu kwa namna hii mtu lazima alalamike, na kuona kwamba kuna tasisi au mtu anambania kazi, na hivyo kukata tamaa.

Mimi hadi kabla ya kuitwa kwenye interview pengine nilikuwa mtu wa fikra hizo, kwani nimetafuata ajira kwa mda mrefu sana, nimeandika barua nyingi, nimebadilisha CV za kila namna nikifikiri zitasanisaidia kupata kazi, lakini kwa muda mrefu kulikuwa na ukimya utadhani kama sijatuma kitu vile. kumbe ilikuwa ni suala la wakati kwani ikafikia kipindi nimeitwa na sekretarieti ya ajira nafasi tatu tofauti, na nimechaguliwa hapo jana katika interview ya kuanza tuu niliyoifanya katika maisha yangu hapo sekretarieti.

Cha msingi wenzangu tusikate tamaa, pale unapokataa tamaa ndipo ushindi wamwenzako unapoanzia, tusikatishane tamaa kuhusu Sekretariti ya ajira kwani kama kuna matatizo, hakuna taasisi yoyote hapa Tanzania ambayo haitafanya kazi bila matatizo, cha msingi Sekretariti imepunguza matatizo hayo. Cha msingi kuwa na sifa halafu uzitete sifa hizo kwenye interview utapita kama nilivyopita.


From Seniour job Seeker(As then was)

mkuu mie nko private nazuga ila future ya fani yangu naiona govt,so nasikilizia usail wa nov hebu nipe abc's za hayo maki2
 
Sure..mi ni mrugaruga tu wa kijijini huko,ktk kijiji na kata naweza kuwa ndo msomi(?)pekee...nimehangaika kupata kaz kwa mda sana,sikuwa na mtu wala sikuwa namfahamu mtu yoyote ktk mfumo wa nchi..kiufupi hata nlpokuja mjin kufanya interview nlfikia Guest kwa kukosa mwenyeji...lakn tume ya ajira imeniita,ikanisaili na kuniona nafaa..leo nipo ktk ofisi nyeti..masela wamebaki kudhania kuwa mimi eti Usalama wa Taifa..kumbe "mburulaaa" tu toka Nanjilinji nliyepata bahati kwa mgongo wa Tume ya Ajira
 
Kaka Elli sisemi kuwa matatizo hayo hayapo, huenda yapo maana wote Tunaijua Tanzania, na unahaki ya kulalamika ili udhaifu huo uondoke, kwa mimi ninachosema licha ya hayo yote tusikate tamaa kutuma maombi kwani hata mimi mingekata tamaa singechaguliwa, kwa sisi ambao hatuna fedha au Ndugu silaha kubwa tuliyonao ni kutokata tamaa, kuwa na sifa na kuzitetea sifa hizo.
mwenzako nimetuma maombi zaidi ya 40, wala sikuitwa, na hayo uliyoyasema yalikuwa yakisemwa toka zamani, lakini kwa vile mimi nimepata wakati huu pamoja na senoiur job seekers wenzangu wengi wamepata napata tafsiri huenda tatizo limepungua.
kwa mfano usingeitwa na hao sekretariet ya ajira ungesema hayo unayo sema? na unaweza kuonesha uhusiano wa kutokukata tamaa na kufanya uchaguliwe na kuitwa kwenye interview?
 
mim ntaendelea kusema huu ukweli pale kama huna unayemjua imekula kwako . nchi ya wajanja bwana wanachukua mtoto wa mkulima mmoja nafac 70 za kwao ili mjipe matumaini mbona yule jamaa kapata tutasubiri hadi tujute
 
mim ntaendelea kusema huu ukweli pale kama huna unayemjua imekula kwako . nchi ya wajanja bwana wanachukua mtoto wa mkulima mmoja nafac 70 za kwao ili mjipe matumaini mbona yule jamaa kapata tutasubiri hadi tujute

Unahitaji kuingia darasani ukasome vizuri somo la 'uvumilivu na kutokata tamaa'.
Kisha uende tution ya 'kupata bahati na kuajiriwa bila kumjua mtu'.

Baada ya hapo unaweza sasa kufanya mtihani wa kutafuta ajira.
 
Sure..mi ni mrugaruga tu wa kijijini huko,ktk kijiji na kata naweza kuwa ndo msomi(?)pekee...nimehangaika kupata kaz kwa mda sana,sikuwa na mtu wala sikuwa namfahamu mtu yoyote ktk mfumo wa nchi..kiufupi hata nlpokuja mjin kufanya interview nlfikia Guest kwa kukosa mwenyeji...lakn tume ya ajira imeniita,ikanisaili na kuniona nafaa..leo nipo ktk ofisi nyeti..masela wamebaki kudhania kuwa mimi eti Usalama wa Taifa..kumbe "mburulaaa" tu toka Nanjilinji nliyepata bahati kwa mgongo wa Tume ya Ajira

Sasa huku ni kusafishana na kuficha maovu, nani asiyejua madudu ya wakubwa ofisini kwa tanzania hii, hili la kusafishana kwa Tanzania ni kivutio mojawapo cha maajabu ya dunia tukipigie kura nacho. HATUDANGANYIKI!!
 
Sasa huku ni kusafishana na kuficha maovu, nani asiyejua madudu ya wakubwa ofisini kwa tanzania hii, hili la kusafishana kwa Tanzania ni kivutio mojawapo cha maajabu ya dunia tukipigie kura nacho. HATUDANGANYIKI!!

unafanya ofisi gani? ambapo kuna madudu ya wa kubwa?
ninacho jua mimi kuchafuana na kubambikiana ni tabia ya watu wasio na ueledi ofisini!
alafu great thinker unatuletea mawazo ya kupigia kura kivutio gani? yaani kama unapata nafasi ya kuandika vitu vya aina hii,basi ata kibaruani kwako utakuwa haya ndio mazungumzo yako
kitu cha msingi rudi kwenye heading ya thread! ACHA KUKATISHA WATU TAMAA!
Kukata tamaa ni dhambi kubwa sana yaani nikuto muamini MUNGU
 
unafanya ofisi gani? ambapo kuna madudu ya wa kubwa?
ninacho jua mimi kuchafuana na kubambikiana ni tabia ya watu wasio na ueledi ofisini!
alafu great thinker unatuletea mawazo ya kupigia kura kivutio gani? yaani kama unapata nafasi ya kuandika vitu vya aina hii,basi ata kibaruani kwako utakuwa haya ndio mazungumzo yako
kitu cha msingi rudi kwenye heading ya thread! ACHA KUKATISHA WATU TAMAA!
Kukata tamaa ni dhambi kubwa sana yaani nikuto muamini MUNGU

Acha unafiki wewe unaejiita Obama wa Bongo, inaelekia hata wewe ni walewale wanafiki wa kibongo mnafagilia kitu flan au mtu flani ili mpate kitu flani, hapa ni sehemu ya kujiachia kimawazo na kero zetu, mambo yanayofanyika ofisin kwa watu ni ya ajabu sana na hayajawahi kutokea kwingine ila Tanzania tu, vitisho, rushwa za wazi wazi, ukabila, udini, undugu, jikumbushie haya BOT, TANROADS, SENSA, hata huko sipakubali sana, mi nimejibu kutokana na huyu jamaa siwezi kurudi kwenye THREAD
quote_icon.png
By Ngaliba Dume
Sure..mi ni mrugaruga tu wa kijijini huko,ktk kijiji na kata naweza kuwa ndo msomi(?)pekee...nimehangaika kupata kaz kwa mda sana,sikuwa na mtu wala sikuwa namfahamu mtu yoyote ktk mfumo wa nchi..kiufupi hata nlpokuja mjin kufanya interview nlfikia Guest kwa kukosa mwenyeji...lakn tume ya ajira imeniita,ikanisaili na kuniona nafaa..leo nipo ktk ofisi nyeti..masela wamebaki kudhania kuwa mimi eti Usalama wa Taifa..kumbe "mburulaaa" tu toka Nanjilinji nliyepata bahati kwa mgongo wa Tume ya Ajira
 
sina comment ila kilichotokea usaili wa weo kwa mikoani ni aibu tupu eti haiwezekani ma intellectual na akili zao watufanyishe interview watu zaid ya 70 wachaguliwe 5 kuingia oral na 7 watoke kwenye 98 huu ni ubabaishaji na usumbufu.wanaochaguliwa mtoto wa mkulima 1 rejesha hatufichani bana zali likikudondoke mshukuru mungu na uwaombee mungu wenzioover.
mim ntaendelea kusema huu ukweli pale kama huna unayemjua imekula kwako . nchi ya wajanja bwana wanachukua mtoto wa mkulima mmoja nafac 70 za kwao ili mjipe matumaini mbona yule jamaa kapata tutasubiri hadi tujute
 
Mmhhhhh.......mimi napita tu kwani haya ya Sekretariat ya Ajira endeleeni nayo wenyewe. watu kila siku wanalalamika, hivi kuna mtu anaweza kuomba nafasi fulani ya ajira bila kuwa na sifa? Kama yupo huyo atakuwa taahira kwa kweli....kwa ushindani huu wa ajira sidhani kama intellectuals wanaweza kuumiza pesa zao kwa applications ktk nafasi usiyo-qualify, kama mpo badilikeni kabisaaa. Ila kwa wale wenye sifa sio siri hii Secretariat ya Ajira Bongo wanatakiwa kukumbushwa kuwa angalau wawaite watu wote wenye sifa ktk interviews na kuwapa nafasi ya kuwasikiliza ndio wawaengue. Ni mawazo yangu kwa hili jambo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom