Mcheza Karate
JF-Expert Member
- Jun 30, 2011
- 690
- 350
(nimepiga hodi kule sebuleni). Wana JF leo nataka niwakumbushe wale wanaotazama makabila wakati wa kuoa. Hivi ni sahihi kuhukumu kabila zima? Mfano nimewahi kuambiwa mara kadhaa kuwa wanawake wa kichaga, kipare,kinyakyusa usioe ni wauaji wa mume mkishafanikiwa kama ilivyo kwa wazaramo, wadigo,wasambaana wabondei ambao huambiwa ni wavivu. Wahaya hushutumiwa kwa kale katabia ka kutoka nje ya ndoa. Je ni sahihi kuhukumu kabila? Mi nadhani si sahihi kwa vile tabia mbaya ni silika ya mtu huzaliwa nayo na kukuzwa nayo si kabila. Je mwana JF unasemaje?