Tuseme ni chuki au ndo udini wenyewe.

God bell

JF-Expert Member
May 13, 2011
590
210
Siku c nyingi zimepita kulikuwa na mkutano ulofanyika jijini Dar wa kujadili mambo ya uchumi kwa nchi za E.A na Africa kwa ujumla. Kwa kawaida mikutano hii huwa inafanyikia Arusha AICC au kwenye Hotel ya Ngordoto iliyoko Arusha. Lakini safari hii Rais JK aliamua kuhamishia Mkutano Dar kitu ambacho kilipelekea kuonekana kuwa anachuki na watu wa Arusha kwa kuwa % kubwa ya mji huo ilichukuliwa na upinzani. Na hii ilipelekea kutokea kwa tetesi kuwa vyombo vya usalama vilipata shida katika kuratibu maswala ya kiusalama. Pia kulikuwa na tetesi kuwa viongozi wengi walilalamika kuhusu hali ya joto kwani walikuwa wamezoea yale mazingira ya Arusha ambapo hii mikutano huwa inafanyika kila mwaka. Je JK haoni kuwa hiki kituo cha mikutano ya kimataifa AICC kinaweza kuhamishiwa ktk nchingine ya E.A kutokana na kushindwa kuratibu mambo kama inavyotakiwa.?
 
Back
Top Bottom