Tupunguze Idadi ya Wabunge ili Tusomeshe Watoto Wetu

Kubwajinga, Naunga mkono hoja yako ndugu yangu. Kuongeza idadi ya Wabubnge hakuongezi tija yoyote katika nchi yetu bali ni kuongeza tu gharama kubwa zisizo na msingi wowote.

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Shangingi ya Wabunge ni bil. 12.92/- [/FONT]

shangingi_1.jpg
[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Serikali imewapigia pande Wabunge wapya ya Jamhuri ya Muungano wa TZ jumla ya sh. bilioni 12.92 kwa ajili ya kununulia mashangingi mapyaa kama vitendea kazi majimboni kwao. [/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Katika pande hilo, kila mbunge aliyefanikiwa kutinga Dodoma atalamba jumla ya sh. milioni 40. [/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Bunge la Tanzania lina jumla ya Wabunge 323 na kwa mtaji huo mabilioni hayo yatamwangwa ili kuhakikisha Waheshimiwa Mama Rahimanino wanapatiwa michuma hiyo kuanza kazi zao rasmi. [/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Mshiko huo utatolewa kama mkopo na serikali ambapo Wabunge watatakiwa kulipa nusu ya fedha hizo yaani mil. 20 wakati mamilioni yaliyobakia yaani mil. 20 yatalipwa na serikali kama pande la kuongeza motisha ya kufanya kazi. [/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Utaratibu wa kukopesha Wabunge magari ulikuja baada ya utaratibu wa zamani wa kupatiwa magari kutoka Wilaya zao kuonekana unaongeza gharama kutokana na magari hayo kuharibika mara kwa mara kutokana na kutumika na wafanyakazi wengi kwa kubadilishana. [/FONT]

[FONT=Verdana, Arial, Helvetica, sans-serif]Akifagilia hatua hiyo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu -Bunge, Juma Akukweti alitonya kuwa utoaji mikopo umekuwa ukifanyika hivyo kwa Wabunge na serikali kuchangia gharama za michuma hiyo nusu kwa nusu ili kuwawezesha kuzungukia wapiga kura wao kiulaini. [/FONT]

Hii ni moja ya gharama za wabunge wetu. Hebu fikiria wakipungua mpaka 100 hivi tutaokoa mabilioni mangapi?
 
Sio wabunge tu wapo wengi kuna wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu kata, tarafa. hawana wanalolifanya hakuna maendeleo kwenye mikoa, wilaya, kata, tarafa na vijiji bora tujiendeshe wenyewe kuliko kuwa na hawa watu. Mkuu wa wilaya ndiye angekuwa mbunge kazi kwisha huku kubebana kusiko na faida kufikie mwisho wake. Tutaokoa pesa nyingi za walipa kodi na kuweza kujenga shule na kukarabati madarasa na hospitali na zahanati za sisi walala hoi.
 
si ajabu wanaulizana kwa nini sisi masikini, nimesoma dar wanataka kuiongezea wabunge kumi na saba piga isabu ya mishahara yao, marupupu yao na new shangingizi to each one si chini ya two billion shillings. halafu tukiambiwa waafrika wanatabia za umaskini, tunaona dharau. Hiyo hela ujajenga shule hata mbili hapo. Sisi si maskini wa hivyo bali tuna viongozi ambao si makini huo ndio ukweli wenyewe.
 
4802d1244659495-picha-itakayomsuta-jk-na-wabunge-wake-mamilionea-_igp9731.jpg

Zile milioni za kuongezea wabunge zingeisaidia sana hii shule.

Sio wabunge tu wapo wengi kuna wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu kata, tarafa. hawana wanalolifanya hakuna maendeleo kwenye mikoa, wilaya, kata, tarafa na vijiji bora tujiendeshe wenyewe kuliko kuwa na hawa watu. Mkuu wa wilaya ndiye angekuwa mbunge kazi kwisha huku kubebana kusiko na faida kufikie mwisho wake. Tutaokoa pesa nyingi za walipa kodi na kuweza kujenga shule na kukarabati madarasa na hospitali na zahanati za sisi walala hoi.

Pakawa,
Inaelekea tu mabingwa wa kuomba misaada na wataalamu wa kutumia hiyo misaada kwa mambo yasiyo na umuhimu.
 
mimi machozi yananitoka kuangalia hizi picha za shule,yaani ni kweli nimetokwa na machozi,mbona sisi ni wabaya zaidi ya wanyama?hata wanyama wanapendana.mbona hawa viongozi wetu wanapenda pesa hiviyo?yaani hawa angalii watoto wetu wanavyoteseka kwenye karne hii ya 21?au wao wako kule majuu?yaani eti sababu ni wabunge ndani ya ccm wansuguana so?basi hata watu mitaani wanasuguana,wapeni ubunge wote na hilo kumbi lenu litajaa.kama wanona hizo viti ni wazi,basi wazingoee,na wapeleke kule kwenye shule angalau watoto wetuy wafaidi.yaani tu nonesense reasons za ku defend very critical issues.nakuambia hii nchi tutakufa maskini mpaka mwisho wa dunia.miafrika ndivyo tulivyo....
 
mimi machozi yananitoka kuangalia hizi picha za shule,yaani ni kweli nimetokwa na machozi,mbona sisi ni wabaya zaidi ya wanyama?hata wanyama wanapendana.mbona hawa viongozi wetu wanapenda pesa hiviyo?yaani hawa angalii watoto wetu wanavyoteseka kwenye karne hii ya 21?au wao wako kule majuu?yaani eti sababu ni wabunge ndani ya ccm wansuguana so?basi hata watu mitaani wanasuguana,wapeni ubunge wote na hilo kumbi lenu litajaa.kama wanona hizo viti ni wazi,basi wazingoee,na wapeleke kule kwenye shule angalau watoto wetuy wafaidi.yaani tu nonesense reasons za ku defend very critical issues.nakuambia hii nchi tutakufa maskini mpaka mwisho wa dunia.miafrika ndivyo tulivyo....

Juakali-Chunya.jpg

Kunani Pale TGA,
Mifano ya kuliza ipo mingi. Angalia hii ya huko Chunya.

Hebu fikiria zile tu Milioni 20 anazopewa mbunge wao kununulia shangingi zingewanufaisha hawa watoto kwa kiasi gani. Halafu badala ya kupunguza wabunge (gharama), wao wanataka waongeze idadi ili wasigombane.

Wenzetu hawa wanene hawana huruma wala soni.
 
Naona wanataka kuwazidi Zanzibar kwa idadi ya viongozi . Zanzibar ni kisiwa cha viongozi na huu ukimwi unaingia Tanganyika.
 
Naona wanataka kuwazidi Zanzibar kwa idadi ya viongozi . Zanzibar ni kisiwa cha viongozi na huu ukimwi unaingia Tanganyika.

Wacha,
Inaelekea wanataka kila mtu kwenye mitandao yao awe ni mbunge. Lakini cha kushangaza ni kuwa hata upinzani nao wameshangilia. Hivi ndio inavyosemekana Dr. Slaa alisema.

Dr.W.Slaa as reported in The Citizen said:
Karatu MP Dr Wilbroad Slaa said review of constituency boundaries was a normal undertaking by the electoral commission as provided for under the Constitution.

"The timing is right and there is nothing wrong with that. This is the right time," he said.

Nitajaribu kumtumia pm kuomba maelezo yake.
 
Inasikitisha zaidi kuwa hata hao wa kutoka vyama vya upinzani hawaoni gharama zisizokuwa na mpango! Kwa mwendo huu tutafika kweli???
 
Nyie mnaleta utani nyie..,yani wabunge wale tunaowajua sisi..,wakae kwenye kikao chini ya spika sitta,waamue kwa pamoja kupunguza idadi yao kwa zaidi ya NUSU??!!too good to be true..,

I can bet my life on this,Under CCM,IT WILL NEVER HAPPEN!NEVER!

tungekuwa na wabunge wa aina hii hata kusingekuwa na haja ya kuwapunguza,maana wasingedai mamilioni kila mwisho wa term,wasingedai kupewa mashangingi ya mamilioni!!

hint:mmeshawahi kuliona BUNGE la china?!!wanakatibia 3000 wale,na wote wanatumia treni /mabasi kwenda vikaoni Beijing.Na upuuzi wa kulipwa haupo!
 
Nyie mnaleta utani nyie..,yani wabunge wale tunaowajua sisi..,wakae kwenye kikao chini ya spika sitta,waamue kwa pamoja kupunguza idadi yao kwa zaidi ya NUSU??!!too good to be true..,

I can bet my life on this,Under CCM,IT WILL NEVER HAPPEN!NEVER!

Kimweri,
Hapa nakubaliana na wewe kabisaa. Sio rahisi kwa wabunge kubadilisha hili.

Tatizo ni kuwa, kikatiba ni wao tu wenye uwezo wa kuibadilisha sheria ili majimbo yapunguzwe.

Bahati mbaya sasa hata wapinzani nao badala ya kulishikia hili suala bango, bungeni, kwenye mihadhara, maandamano n.k., baadhi yao wameshanena kuwa inaelekea wanalifurahia. Kweli hatuna pa kukimbilia.
 
NAMSHUKURU Mungu kwa kuwa ameendelea kuwa mwema maishani mwangu. Leo ningependa kuzungumzia hoja ambayo kwangu mimi imekuwa ikinitatiza kwa muda mrefu. Hivi karibuni, Bunge letu tukufu limekumbwa na kashfa ya matumizi mabaya ya pesa za serikali baada ya kubainika kuwa wawakilishi wetu huwa wanalipana posho mara mbili kwa vikao wanavyofanya nje. Kimantiki sitaki kuwa shabiki wa hili ila ninachotaka ni kujadili kwa kina na Watanzania wenzangu juu ya uhalali wa sakata hili...

Kwa mtazamo wa haraka, Bunge ni miongoni mwa nguzo kuu tatu za dola, na inapotokea likalegalega, basi serikali nzima lazima iyumbe. Naamini kuwa wananchi walipokuwa wanawapigia wabunge wao kura, walitaka wao ndio wawakilishe katika kuyafikisha matatizo yao serikalini. Walikuwa wanaamini kuwa wabunge hawa watafanya kila wanaloliweza kuhakikisha kuwa huduma za msingi kwa jamii zinapatikana kwa urahisi.

Baada ya kushika madaraka hali imekuwa tofauti sana kwa waheshimiwa hawa kiasi cha kunifanya nihoji, wakiwa bungeni wanamwakilisha nani? Yawezekana jibu likawa kuwa wanawawakilisha wapiga kura wao. Lakini bado kwa mtu mwenye fikra pevu atazidi kuhoji kuwa wanamwakilisha mwananchi katika misingi gani?

Wao wanachukua posho mara mbilimbili kwenye vikao vyao, wanatembelea magari ya bei mbaya, wamehama majimboni na kuhamia jijini wakiacha wananchi wao wakiteseka. Bado tunasema wanawawakilisha wananchi bungeni kwa misingi ipi?

Ukifanya utafiti jimbo hadi jimbo utagundua jinsi maisha ya Mtanzania yalivyo magumu. Huduma za msingi kama maji safi na salama, umeme wa kuaminika, hospitali na zahanati zenye vifaa vyote muhimu, shule zenye vifaa bora vya kufundishia na kujifunzia bado ni kitendawili kilichokosa majibu tangu enzi za uhuru. Watumishi wa sekta nyeti wanaoigusa jamii moja kwa moja kama wauguzi, walimu, wataalamu wa kilimo na wengineo, bado wamesahaulika licha ya kuwa wanapiga kelele kila kukicha.

Ukitazama kwa haraka haraka tofauti iliyopo kati ya posho anayopokea mbunge mmoja kwa siku, na mshahara anaolipwa mwalimu au muuguzi ambaye ndiye anafanya kazi ya kuihudumia jamii kwa mwezi mmoja, hakika utastaajabu. Kwa takwimu za haraka haraka, posho ya siku moja kwa mbunge inakadiriwa kufikia shilingi laki mbili na nusu (ukijumuisha gharama zote wanazolipwa) wakati mwalimu wa kawaida mshahara wake kwa mwezi haufikii fedha hiyo.

Ni nini kinachosababisha tofauti kubwa namna hii? Najiuliza kuwa inawezekana vipi kwa haya kutokea katika nchi ambayo imo kwenye orodha ya mataifa masikini zaidi duniani huku wananchi wake wengi wakikadiriwa kuishi chini ya dola moja ya Kimarekani kwa siku? Ni hili ndilo linalonifanya nihoji kuwa hawa wabunge tuliowachagua wanafanya kazi kwa maslahi ya nani? Inawezekana tukawa hatuujui ukweli mkubwa zaidi kuwa kumbe kila mbunge anatazama maslahi yake kwanza.

Ni wachache sana wanaoweza kuwatazama wananchi na kuwatatulia kero zao kabla ya kufikiria kujinufaisha wao kwanza na ndio maana wanakuwa wakali wanapotaka kuwajibishwa juu ya unyonyaji kama huu. Aliwahi kutoa hoja mbunge kutoka Jimbo la Karatu, Wilbrod Slaa kuwa anaona wabunge wanalipwa pesa nyingi sana. Alipoitoa, hakuna aliyemuunga mkono na ikafunikwa hadi leo. Huu ni ushahidi kuwa kumbe kila mtu yuko pale kwa manufaa yake binafsi.

Kiongozi ambaye anafahamu kuwa amewekwa madarakani na wananchi ili awatumikie kwa uadilifu, hawezi kukubali kupokea posho mara mbili ‘ilhali’ anajua kuwa wananchi wake hawana kisima hata kimoja cha maji safi au wakati hata shule za jimboni kwake hazina vitabu wala walimu.

Kama kweli mngekuwa mnatutumikia sisi wananchi, mngeliona hilo tangu awali na bila shaka mngependekeza kuwa badala ya kuendelea kufaidi “kuku” hizo pesa mngependekeza zitumike kununua vitabu na dawa kwenye shule na zahanati za vijijini, au kuboresha miundombinu kama barabara. Haya yalikuwa yanawezekana kwa kuwa yapo ndani ya uwezo wenu.

Kiongozi mzalendo, anayatanguliza maslahi ya wale anaowaongoza kwanza, kamwe hawezi kuishi kwa amani wakati anajua wapiga kura wake wanataabika na ugumu wa maisha. Badala ya kupoteza muda mwingi kwenye vikao na semina zenye posho lukuki, kiongozi mzalendo atatumia muda mwingi kukaa na wapiga kura wake ili azifahamu vizuri kero zao na kuangalia namna ya kuzitatua.

Najua ni vigumu kwa mkubwa kuomba radhi pale anapoteleza na kutoka nje ya maadili, lakini kwa hili naamini wabunge wetu wakikubali na kukiri kuwa walikuwa wanapokea posho mara mbili kimakosa, watarudisha imani yao kwa wananchi. Ni vigumu sana kumshawishi babu yangu aamini kuwa kupeana mamilioni ni takrima wakati huko kijijini hata shilingi mia moja ya mafuta ya taa ni tatizo kuipata. Kila mmoja huwa anakosea, na njia bora ya kukubali makosa yako ni kuomba radhi.

Tunapozidi kurefusha malumbano na kutafuta njia ya kukwepea kashfa hii nzito, tunapanda mbegu mbaya ya chuki ambayo itatumaliza. Ukisema kuwa mtu anawaonea wivu mnapolipana posho mara mbili kwa kazi moja, nadhani si sahihi kwa kuwa hakuna ambaye angelalamika iwapo huduma zote muhimu zingekuwa zinapatikana. Mnatufanya tuhisi kuwa kumbe nchi yetu si maskini bali wanaoiongoza wamekutana wote wajanja wanaozijua pesa kuliko thamani ya ubinadamu.

Busara zitumike na si kutuletea siasa za kibadhirifu wakati nchi inaangamia kwa uroho wa vigogo wachache wa kutaka kuyajaza matumbo yao kwanza. Kinyume na hapo wananchi wataendelea kuamini kuwa Tanzania ni ya wachache waliobahatika kupata uongozi serikalini. Lazima tufike mahali ambapo mtoto wa mbunge na yule wa mkulima wasome shule moja, waishi mtaa mmoja na wale chakula meza moja.

Haya yatawezekana kama kweli hawa tuliowapigia kura watakumbuka jukumu muhimu sana la kuwatumikia wananchi kwanza. Kama mbunge anaukaribu na wapiga kura wake, lazima atakuwa katika nafasi nzuri ya kuwatatulia kero zao kwani wananchi nao watamzoea na kuwasilisha matatizo yao bila wasiwasi wala woga kama ilivyo sasa. Tukiweza kuuziba ufa huu uliopo kati ya watawala na watawaliwa, hakika tutayafikia maendeleo ya kweli.

Inapotokea taasisi kama TAKUKURU inaona kuna ulazima wa kuwahoji wote watakaohisiwa kushiriki katika ubadhirifu wa kodi za walalahoi, basi taasisi hiyo ipewe nafasi ya kufanya kazi yake bila kubughudhiwa na mtu yeyote. Katiba ya nchi yetu inaeleza wazi kuwa hakuna ambaye yuko juu ya sheria. Kama sheria inatumika kumbana mtumishi wa chini anaposhukiwa kuwa amepokea rushwa ili kutoa huduma, ni lazima sheria hiyohiyo itumike kuwabana waheshimiwa wanaodai posho ili washiriki kwenye vikao vya wizara.

Tukiamua kulinyamazia suala hili kwa kuliita takrima, basi tuhalalishe hata vile vijisenti wanavyopewa matrafiki barabarani kwani nao hupewa ili wapate nguvu ya kuendelea kusimama kutwa nzima. Kama tunaona haifai, basi iwe haifai kwa wote, si kuwabana watu wa chini wakati vigogo nao wanacheza mchezo huo huo ila wanaubadilisha jina tu na kuita takrima au itifaki.

Kama kweli wapo kwa ajili ya maslahi ya wanachi waliowapigia kura, lazima wajisikie uchungu wa kutafuna kodi za wananchi bila huruma. Jipu limepasuka, siwezi kuwa adui kwa kusema kile ninachoamini kuwa ni ukweli!

http://www.globalpublisherstz.com/pasua_jipu/
 
ndugu zangu enough is enough tuache mambo ya kulaumu ccm tunapoteza muda kamwe hawatabadilika kitu pekee kinachoworth your time in this forum is to plot how to remove them from power
 
Je, Wabunge wanafanya kazi kwa ajili yetu?
Mambo nane kuhusu wabunge Tanzania.......

Soma utafiti wa UWAZI.ORG
 

Attachments

  • do_they_work_for_us.040210_final_swa_for_publication.pdf
    729 KB · Views: 29
Hivi ndivyo inavyokwenda na nchi zetu zilizojaa watu waliojazwa hofu na ujinga. Kama leo mama bado haoni sababu ya kumfanya mwanae apate elimu na kuamua kumuoza kwa mzee anayemiliki kiunga kidogo cha minazi ni lini haya yatagunduliwa na watu kusimama na kudai haki ya kumiliki na kutumia rasilimali zao kwa manufaa ya kijamii?
Napenda hoja hii Kubwajinga, lakini ni wachache tu wanasoma na katika hao wachache wanaosoma baadhi yao ni washiriki na wasaidizi wa hao wanaofuja na kutapanya rasilimali za nci yao kana kwamba wao wanaenda kuishi nchi nyingine! Tunao wabunge bwelele wasio na tija, wakilala tu bungeni, hata huko katika kamati zao hawana mchango wowote, bado tunao wengine wa kuambiwa wewe nenda huko ndani, bado hawawezi hata kumsaidia aliyewapeleka, aibu!
Keep it up!!!
 
Ukweli wa 6: Wabunge 72 hawajawahi kuuliza swali la msingi hata moja
[FONT=Calibri,Calibri][FONT=Calibri,Calibri]Njia kuu ya kuanzisha mjadala juu ya mada fulani ni kuwasilisha maswali ya msingi. Kama mchoro namba 5 unavyoonesha, wabunge 72 hawajawahi kuuliza swali moja la msingi. Wabunge hawa wengi ni wa CCM. UDP na CUF pia wana mbunge mmoja mmoja ambao hawajawahi kuuliza swali moja la msingi. (Angalia atachment kwa ajili ya mchoro) [/FONT]
[/FONT]
 
Ukweli wa 8: Mwinyi, Lowassa na Aziz wako mwisho katika ushiriki Bungeni
[FONT=Calibri,Calibri][FONT=Calibri,Calibri]Bunge lina wabunge watatu wa kuchaguliwa ambao hawajawahi kuchangia mijadala ya vikao hata mara moja kwa mujibu wa POLIS. Hawa ni Dk. Hussein Mwinyi, Edward Lowassa na Rostam Aziz. Kuna mbunge mwingine, Frederick Werema ambaye pia hajawahi kuchangia lakini hajawekwa kwenye jedwali na 2 kwa sababu ameteuliwa hivi karibuni tarehe 27 Oktoba 2009, kama Mbunge kutokana na cheo chake (Mwanasheria Mkuu wa Serikali). [/FONT]

[FONT=Calibri,Calibri]
1021.jpg
1042.jpg
1063.jpg
[/FONT]
[/FONT]
 
Ni bora idadi ya wabunge ikapungua ili tubane matumizi wapunguzwe wafikie at most 150 tu wanatosha,hawa viti maalumu wa tolewe wote
 
Back
Top Bottom