Tupunguze Idadi ya Wabunge ili Tusomeshe Watoto Wetu

Kubwajinga

JF-Expert Member
Jan 23, 2008
2,194
297
Tupunguze Idadi ya Wabunge ili Tusomeshe Watoto Wetu.

small-IMG_6453.JPG
Benno+Graduation2.JPG



Juzi nilisoma tamko la kushangaza na kusikitisha kwenye gazeti la Mwananchi lililotolewa na Makamu wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Jaji Omar Makungu, kuwa wana mpango wa kuongeza idadi ya wabunge ili kuondoa misuguano ndani ya vyama vya siasa.






Yaliyotamkwa;
  1. Inasemekana kuwa Dar es salaam itaongezewa wabunge na kuwa na jumla ya wabunge 17.
  2. Kisa kimojawapo kilichotajwa cha kuongeza wabunge eti ni kuwa, kuna baadhi ya wanene kwenye serikali ya JK ambao wanataka kugombea ubunge kwenye majimbo ambayo tayari yana wabunge wenzao wa CCM na hivyo italeta vurugu.
  3. Vigezo vilivyotajwa kutumika kuongeza wabunge ni pamoja na ukubwa wa ukumbi wa Jengo la Bunge kuwa bado lina nafasi ya viti 23, kama vile ni lazima ukumbi uliojengwa na wachina lazima ujazwe.
Swali ;
  1. Je, hivi kweli tunahitaji kuongeza idadi ya wabunge na hivyo kuongeza gharama kwa nchi au kuwapunguza wabunge ambao wingi wao haujaisaidia nchi?
  2. Kama tunaongeza, kwa nini tuongeze wabunge kwa vigezo laini kama vilivyotajwa badala ya kuangalia maslahi ya nchi hasa tukielewa kuwa uchumi wetu uko hoi?
Hoja ya Tunayofahamu:
  1. Kwa sasa hivi, nchi yetu iliyomasikini na yenye zaidi ya 50% ya bajeti inayotegemea misaada, ina Bunge la Muungano lenye wabunge 323, ambapo 232 ni wa majimboni na waliobaki wakiwa ni wa-mapambo. Pia TZ yetu ina watu karibu milioni 40 tu na ukubwa wa km za mraba 945,200.
  2. Ukilinganisha na Marekani wenye utajiri na mkubwa, nchi kubwa (mara kumi zaidi ya yakwetu = 9,827,000 Sq. km) na watu zaidi ya milioni 300, wao wana wabunge 435 tu. Kwa nini hatufuati sheria za kiuchumi zinazoeleza wazi kuwa unapokuwa hujitoshelezi kimapato, basi unatakiwa upunguze matumizi?
  3. Kwa nini tuongeze wabunge badala ya kuwapunguza? Kila Mbunge anatugharimu sio chini ya TShs. 15,000,000 kwa mwezi au TShs. 180,000,000 kwa mwaka (Dr. Slaa naomba msaada hapa). Hii gharama ya kumuweka bungeni mbunge Mmoja tu ni sawa na kusomesha UDSM waalimu 180 au mainjinia 150 au madaktari 150 kila mwaka. Lipi ni bora, kumstarehesha mbunge 1 au kusomesha mainjinia 150?
Maoni;
  1. Badala ya NEC (Tume ya Uchaguzi) kuiongezea nchi mzigo wa wanene, serikali kwa kushirikiana na Bunge, zipunguze majimbo ya ubunge na tufute kabisa wabunge wa kuteuliwa mpaka hapo uchumi wetu utakaponawiri. Ni wazi Serikali ya JK haiwezi kulikubali hili, sasa kwa nini wapinzani msilitumie hili kama wimbo wa kuwaimbia wananchi mapema mpaka walielewe hili?
  2. Kwa hali ya uchumi wetu, hatupaswi tuwe na zaidi ya wabunge 5 kwa kila mkoa, yaani tuwe na bunge la watu 100-125. Hakuna mbunge atakayeshindwa kuzungukia jimbo lake au hata mkoa mzima angalau mara 4 kwa mwaka.
  3. Bunge la watu 125 kwa makadirio ya haraka-haraka lingeokoa zaidi ya TShs.36,000,000,000. Hii ni sawa na Tution Fees ya Madakitari 24,000 kwa mwaka mzima au sawa na majengo 5 ya wadi ya watoto Muhimbili kila mwaka. Kwa nini tusipunguze wabunge tukapata pesa ya kusomesha?
  4. Hii tabia ya viongozi wetu Tanzania, ya kufuja vichache tulivyo navyo kwa kuendelea kujipangilia matumizi bila kuangalia hali yetu ya uchumi duni inapaswa ikome. Inapaswa tuanze kuwawajibisha wale wote wanaojipangilia matumizi bila kuangalia uwezo wa nchi au manufaa ya hayo matumizi kwa taifa. Ningeomba tuanze na hawa majaji wa NEC.
  5. Hatuhitaji nyongeza ya wabunge bali tungefurahi kama wakipunguzwa maana wingi wao haujaonesha kama unatusaidia.
  6. Badala yake, tutumie pesa yetu kiduchu tuliyonayo kuwekeza kwenye elimu ya watoto wetu ili tuache kuendelea kuogopa nchi jirani zetu waliotuzidi kielimu.
Mungu ibariki Tanzania. Naomba kutoa hoja wana-JF.


Soma Utafiti wa UWAZI.ORG
 
Na kama hiyo haitoshi, leo Marmo kasema wanaongeza idadi ya wabunge wa viti maalum (wanawake) eti wafikie 40% na kuwa hiyo ipo kwenye katiba. Hivi katiba inawazuia kufikia % hiyo kwa kugombea majimboni? Tatizo kubwa la serikali yetu ni vipaumbele!
 
Zanzibar pekee kuna Baraza la Wawakilishi, wapo 50 kama sikosei, halafu na wengine wanakuja kushiriki bunge la Jamhuri ya Muungano. Huwa najiuliza sana kama kuna mahitaji kiasi hicho!!
 
Ebwana hilo swala la kwamba wanataka kuongeza wabunge ili wajaze ukumbi unatania right?

Please say so!
 
101% right
Freetown,
Inabidi pia Tume ya Uchaguzi (NEC) kujiuzulu. Wawe wameshurutishwa kutoa hayo maamuzi au la sio hoja tena.

Kwa wao kutoa matamko ya kuwa wanaongeza wabunge ili kuondoa msuguano ndani ya CCM, ina maana hawafanyi kazi zao kwa manufaa ya Taifa bali wanawatumikia hao wachache ambao wanajiona kuwa ni lazima waingie bungeni hata ikibidi kwa kutengewa majimbo maalumu kwa ajili yao.
 
..kwa kweli hapa nakubaliana na wewe 100%.

..sasa basi viongozi wa vyama vya upinzani viyakatae mapendekezo haya.

..waandishi wa habari, na asasi z kijamii pia wanapaswa kulikemea suala hili.
 
Na kama hiyo haitoshi, leo Marmo kasema wanaongeza idadi ya wabunge wa viti maalum (wanawake) eti wafikie 40% na kuwa hiyo ipo kwenye katiba. Hivi katiba inawazuia kufikia % hiyo kwa kugombea? Tatizo kubwa la serikali yetu ni vipaumbele!

Hawa akina Marmo ndio wote wanaotakiwa kuachia ngazi sasa maana bongo zao zimeshapita expiration date.

Hawaangalii uwezo wa nchi kubeba hizo gharama za wabunge wapya na function ya hao wateule, wanachojadi ni kuwa na statistics tu watakazozitumia kujisifia kwenye makongamano nje ya nchi.

Zaidi ya hayo, nafasi zikiongezwa utasikia wanaopewa ni wake zao, vimada wao na watoto wao. Kwa nini starehe ziwe kwao nongwa watuachie sisi?
 
..wabunge wanawake wa viti maalum wawe wanateuliwa kwa term moja tu. baada ya hapo kama wanataka kuendelea kuwa wabunge basi wakagombee kwenye majimbo.
 
Hata Wabunge wakiwa 100 peke yao kama hakuna mikakati madhubuti ya Elimu,Afya n.k hali itakuwa mbaya tu...hoja hapa sio kuwa na wabunge wengi ama wachache.
 
..wabunge wanawake wa viti maalum wawe wanateuliwa kwa term moja tu. baada ya hapo kama wanataka kuendelea kuwa wabunge basi wakagombee kwenye majimbo.
Kwani wakipewa term moja idadi ya wabunge itapungua? Angalia hoja ya mleta mada; kupunguza idadi ya wabunge kuokoa fedha. Kupunguza term ya service ya mbunge ni jambo lingine, kwani hata huyo mpya atakayekuja atatumia fedha zile zile so tutakuwa hatujaokoa kitu.
 
Kazi kweli kweli dah umaskini unazidi kutawala si maisha yetu tu sasa mpaka akili zetu sijui lini wanasiasa wa watanzania wataweza kuongea ukweli na kutekeleza ukweli safari bado ndefu
 
Ebwana hilo swala la kwamba wanataka kuongeza wabunge ili wajaze ukumbi unatania right?

Please say so!

Ndio mahesabu yao kuwa kwa vile kuna viti vitupu basi wavijaze. Hawa wenzetu wamelewa madaraka.
 
Gabu said:
Kwani wakipewa term moja idadi ya wabunge itapungua? Angalia hoja ya mleta mada; kupunguza idadi ya wabunge kuokoa fedha. Kupunguza term ya service ya mbunge ni jambo lingine, kwani hata huyo mpya atakayekuja atatumia fedha zile zile so tutakuwa hatujaokoa kitu.

Gabu,

..kuna mchangiaji ameeleza kwamba Waziri Marmo amegusia kuhusu kuongezwa kwa idadi ya wabunge wa viti maalumu wanawake ili wafikie 40% ya bunge.

..sasa mimi nilikuwa naendeleza mjadala kuhusu wabunge wa viti maalum kwamba wapewe kipindi kimoja tu.

..kwa upande mwingine naungana na wengine wanaopendekeza kwamba idadi ya wabunge isiongezwe, na zaidi ingekuwa vema kama ingepunguzwa.

..zaidi, gharama za uendeshaji bunge letu, ikiwemo mishahara na marupurupu, zipunguzwe.
 
..kwa kweli hapa nakubaliana na wewe 100%.

..sasa basi viongozi wa vyama vya upinzani viyakatae mapendekezo haya.

..waandishi wa habari, na asasi z kijamii pia wanapaswa kulikemea suala hili.

JokaKuu,
Labda waandishi wa habari na asasi za kijamii ndio wasaidie kulizima hili, maana The Citizen limeripoti kuwa wabunge wa CCM na wa upinzani wote wanaelekea kukubaliana na huo uamuzi.
 
JokaKuu,
Labda waandishi wa habari na asasi za kijamii ndio wasaidie kulizima hili, maana The Citizen limeripoti kuwa wabunge wa CCM na wa upinzani wote wanaelekea kukubaliana na huo uamuzi.
Waandishi wa habari hao hao wakishapata popularity wanachukua form kugombea ubunge, unategemea watalizima hili? Nasikia Mkamia anapasha misuli kuwania Dodoma, sasa sijui ni mjini au kwa mzee JSM !!
 
MPs welcome review of constituency boundaries
Bernard James, Dodoma

Members of Parliament have overwhelmingly supported the announcement by the National Electoral Commission (NEC) for a review and a possible split-up of some constituency boundaries.

However, the MPs attending the 18th Parliamentary session, warned that the intended exercise could frustrate the whole electoral process if the move was politically motivated to favour some candidates.

Their stand is in stark difference to comments aired by some members of society, who saw the exercise as the wastage of the much needed national resources.

Former University of Dar es Salaam lecturer, Prof Mwesiga Baregu, said the sudden announcement of what is depicted as mandatory exercise, brands the whole exercise as politically motivated in order to further weaken the opposition.

�This is the continuation by the government to withhold information by design and suddenly release them to the surprise of everybody involved,� he said.

Many MPs also urged for strict adherence of criteria set out in the Constitution when conducting the exercise.

But an insider yesterday confided to The Citizen that the number of new constituencies after the split-up exercise, would not exceed four.

And minister of State in the Prime Minister�s Office (Policy, Coordination and Parliamentary Affairs), Mr Philip Marmo, said there was a �very narrow possibility� of adding many constituencies due to many factors including the limited capacity of the House debating chamber.

�This is a constitutional exercise and review. It does not mean the split-up of many constituencies. There are many things to consider including the capacity of the House to accommodate MPs,� he said.

MPs from both the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM) and the opposition, said there was nothing bad with the plan.

�It is a good idea although the timing is wrong. I thing it is the right decision to review constitutional boundaries according to population quarter,� Vunjo MP Aloyce Kimaro (CCM) said.

There has been speculation that the intended exercise was a plan by the ruling CCM to avert possible split up of voters in the constituencies with stiff competition among its members eyeing parliamentary seats.

But Mr Kimaro said he did not believe in the suggestion saying: �The competition is going to be stiff even in those new constituencies. What is supposed to be done is for CCM leaders to adhere to rules and regulations governing party elections.�

Karatu MP Dr Wilbroad Slaa said review of constituency boundaries was a normal undertaking by the electoral commission as provided for under the Constitution.

�The timing is right and there is nothing wrong with that. This is the right time,� he said.

The outspoken Same East MP, Mrs Anne Kilango Malecela (CCM), warmly welcomed the suggestion.

�To me the idea is good so long as the criteria for doing so will be followed. It will help people to get social services and bring MPs close to the people. The role of the MP is to serve the people,� she said.

Mr John Momose Cheyo (Bariadi East-UDP) strongly supported the idea, but called for fully involvement of the people in the exercise.

Mr Cheyo who is also chairman of the opposition United Democratic Party (UDP), said he was ready to see his constituency divided.

Muleba North MP, Mr Wilson Masilingi, said he was shocked and surprised with the announcement. �We want more explanation on what exactly NEC want to achieve,� he said.

But he was not critical of the idea. �I would like to have even five more constituencies out of Muleba North. I would be happy if I get an MP in every ward. Are Zanzibaris not happy with their MPs?� he asked.

The current Parliament has 323 MPs and the capacity of House debating chamber is only 346 legislators.

Mr James Lembeli, MP for Kahama (CCM), said the idea is good although he could not imagine how would more MPs seat comfortably in the current House.

Making a reference from his own constituency with not less than 500,000 people, 4,000 square miles and about 20 wards, the MP said some other legislators were being overburdened.

NEC said on Monday it was receiving applications to have constituencies split-up. NEC deputy chairman Justice Omar Makungu, told reporters that the deadline for applying is February 29, 2010, and NEC is expected to have completed the review by the end of April.
SOURCE: The Citizen 2010-01-27 08:38:00

Hivi ndio wanavyofikiria wabunge wetu. Hakuna hata mmoja anayeuliza gharama za hiyo shughuli zitabebwa na nani.
 
PIX.jpg
[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]Makabe primary school standard two pupils doing their schoolwork sitting on the floor due to shortage of desks, as captured by photographer Peter Mgongo, in Dar es Salaam on Tuesday.[/FONT]
Hii ndio hali halisi ya shule zetu. Wanafunzi wanasomea chini. Hivi tunawaanda hawa malaika kuwa wanasayansi kweli kkwa staili hii?
Idadi ya Wabunge ipunguzwe na pia kuwepo na mkakati mahsusi wa kuendeleza elimu yetu hapa nchini
 
PIX.jpg

[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]Makabe primary school standard two pupils doing their schoolwork sitting on the floor due to shortage of desks, as captured by photographer Peter Mgongo, in Dar es Salaam on Tuesday.[/FONT]​

Obi,
Umeweka picha inayotueleza mengi sana.

Wabunge wapunguzwe kulingana na uwezo wetu. Pale uchumi utakapokua basi ndio tufikirie kati ya kujenga shule, hospitali na kuongeza wabunge.

Hivi sasa tuna wabunge wengi ambao kwenye majimbo yao hakuna shule wala hospitali za maana, lakini gharama za kuwahudumia hao wabunge zinazidi gharama za kujenga hospitali na shule majimboni mwao.

Ni vema tukaangalia upya wapi tunatumia pesa yetu badala ya kuwakubalia hawa wanene wanaotaka kuongeza wanene wengine kati yao.
 
Tupunguze Idadi ya Wabunge ili Tusomeshe Watoto Wetu.


small-IMG_6453.JPG
Benno+Graduation2.JPG


Juzi nilisoma tamko la kushangaza na kusikitisha kwenye gazeti la Mwananchi lililotolewa na Makamu wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (NEC), Jaji Omar Makungu, kuwa wana mpango wa kuongeza idadi ya wabunge ili kuondoa misuguano ndani ya vyama vya siasa.





Yaliyotamkwa;
  1. Inasemekana kuwa Dar es salaam itaongezewa wabunge na kuwa na jumla ya wabunge 17.
  2. Kisa kimojawapo kilichotajwa cha kuongeza wabunge eti ni kuwa, kuna baadhi ya wanene kwenye serikali ya JK ambao wanataka kugombea ubunge kwenye majimbo ambayo tayari yana wabunge wenzao wa CCM na hivyo italeta vurugu.
  3. Vigezo vilivyotajwa kutumika kuongeza wabunge ni pamoja na ukubwa wa ukumbi wa Jengo la Bunge kuwa bado lina nafasi ya viti 23, kama vile ni lazima ukumbi uliojengwa na wachina lazima ujazwe.
Swali ;
  1. Je, hivi kweli tunahitaji kuongeza idadi ya wabunge na hivyo kuongeza gharama kwa nchi au kuwapunguza wabunge ambao wingi wao haujaisaidia nchi?
  2. Kama tunaongeza, kwa nini tuongeze wabunge kwa vigezo laini kama vilivyotajwa badala ya kuangalia maslahi ya nchi hasa tukielewa kuwa uchumi wetu uko hoi?
Hoja ya Tunayofahamu:
  1. Kwa sasa hivi, nchi yetu iliyomasikini na yenye zaidi ya 50% ya bajeti inayotegemea misaada, ina Bunge la Muungano lenye wabunge 323, ambapo 232 ni wa majimboni na waliobaki wakiwa ni wa-mapambo. Pia TZ yetu ina watu karibu milioni 40 tu na ukubwa wa km za mraba 945,200.
  2. Ukilinganisha na Marekani wenye utajiri na mkubwa, nchi kubwa (mara kumi zaidi ya yakwetu = 9,827,000 Sq. km) na watu zaidi ya milioni 300, wao wana wabunge 435 tu. Kwa nini hatufuati sheria za kiuchumi zinazoeleza wazi kuwa unapokuwa hujitoshelezi kimapato, basi unatakiwa upunguze matumizi?
  3. Kwa nini tuongeze wabunge badala ya kuwapunguza? Kila Mbunge anatugharimu sio chini ya TShs. 15,000,000 kwa mwezi au TShs. 180,000,000 kwa mwaka (Dr. Slaa naomba msaada hapa). Hii gharama ya kumuweka bungeni mbunge Mmoja tu ni sawa na kusomesha UDSM waalimu 180 au mainjinia 150 au madaktari 150 kila mwaka. Lipi ni bora, kumstarehesha mbunge 1 au kusomesha mainjinia 150?
Maoni;
  1. Badala ya NEC (Tume ya Uchaguzi) kuiongezea nchi mzigo wa wanene, serikali kwa kushirikiana na Bunge, zipunguze majimbo ya ubunge na tufute kabisa wabunge wa kuteuliwa mpaka hapo uchumi wetu utakaponawiri. Ni wazi Serikali ya JK haiwezi kulikubali hili, sasa kwa nini wapinzani msilitumie hili kama wimbo wa kuwaimbia wananchi mapema mpaka walielewe hili?
  2. Kwa hali ya uchumi wetu, hatupaswi tuwe na zaidi ya wabunge 5 kwa kila mkoa, yaani tuwe na bunge la watu 100-125. Hakuna mbunge atakayeshindwa kuzungukia jimbo lake au hata mkoa mzima angalau mara 4 kwa mwaka.
  3. Bunge la watu 125 kwa makadirio ya haraka-haraka lingeokoa zaidi ya TShs.36,000,000,000. Hii ni sawa na Tution Fees ya Madakitari 24,000 kwa mwaka mzima au sawa na majengo 5 ya wadi ya watoto Muhimbili kila mwaka. Kwa nini tusipunguze wabunge tukapata pesa ya kusomesha?
  4. Hii tabia ya viongozi wetu Tanzania, ya kufuja vichache tulivyo navyo kwa kuendelea kujipangilia matumizi bila kuangalia hali yetu ya uchumi duni inapaswa ikome. Inapaswa tuanze kuwawajibisha wale wote wanaojipangilia matumizi bila kuangalia uwezo wa nchi au manufaa ya hayo matumizi kwa taifa. Ningeomba tuanze na hawa majaji wa NEC.
  5. Hatuhitaji nyongeza ya wabunge bali tungefurahi kama wakipunguzwa maana wingi wao haujaonesha kama unatusaidia.
  6. Badala yake, tutumie pesa yetu kiduchu tuliyonayo kuwekeza kwenye elimu ya watoto wetu ili tuache kuendelea kuogopa nchi jirani zetu waliotuzidi kielimu.
Mungu ibariki Tanzania. Naomba kutoa hoja wana-JF.

Kubwajinga, Naunga mkono hoja yako ndugu yangu. Kuongeza idadi ya Wabubnge hakuongezi tija yoyote katika nchi yetu bali ni kuongeza tu gharama kubwa zisizo na msingi wowote. Bunge lenyewe ni Bunge butu liko pale kuhalalisha sera za chama tawala hata kama sera hizo hazileti maenedeleo yoyote kwa nchi yetu. Ukiangalia tangu bunge hili lichaguliwe 2005 hakuna chochote walichokifanya ambacho tunaweza kuwapongeza na hata wakiongeza idadi zaidi ya Wabunge hakuna chochote watakachofanikisha maana wameweka mbele maslahi yao binafsi, ya chama chao (ccm) badala ya yale ya Taifa.
 
Back
Top Bottom