Tanzania Utalii Dialogue
Member
- Jul 26, 2016
- 8
- 6
Tembo ni miongoni mwa wanyama pori wanaopatikana kwenye hifadhi nyingi hapa Tanzania ikiwemo hifadhi ya Ruaha
Ripoti zinasema kwamba mauaji ya Tembo yamezidi kuongezeka kwa kasi kubwa hasa maeneo ya hifadhi ya Ruaha, ambapo idadi ya Tembo dume imepungua sana kadri miaka inavyoendelea kwa kuwaua ili kupata pembe na meno na hivyo kufanya ongezeko la uhaba wa wanyama Hawa katika mbuga zetu.
Wadau wa masuala ya utalii bado wanaendelea na kampeni za kupinga ukatili wa tembo katika hifadhi zetu za Tanzania.
Kwa pamoja tuungane katika vita hiyo kwa kutoa elimu kwa wakazi wanaozunguka hifadhi za wanyama pori. Je nini kifanyike ili kutokomeza huu ukatili???