Tupia imani ya kale uliyowahi kusikia

Kitovu cha mtoto kikikatika kisidondokee nanihino (hasa kwa mtoto wa kiume), vinginevyo mtoto atakuwa si rizki!
True or not, nilihakikisha hakidondoki vibaya kwa mwanangu, kwa kuwa sikuwa na cha kupoteza kwa kuhakikisha hakidondokei nanihino.......


kaka umenichekesha sanaaa.....ma wife alinidokeza kuhusu hii nikambishia nikamtega, nikamwambia tuache kimdondokee mwanetu ili tuprove hiyo kitu akawa mbogo.....hadi leo umekua wimbo oooh mwanao akikua ntamwambia ulivotaka kumfanyiaaa roho ya ubaya basi mi nacheeeeka
 
Kitovu cha mtoto kikikatika kisidondokee nanihino (hasa kwa mtoto wa kiume), vinginevyo mtoto atakuwa si rizki!

True or not, nilihakikisha hakidondoki vibaya kwa mwanangu, kwa kuwa sikuwa na cha kupoteza kwa kuhakikisha hakidondokei nanihino.......

Good work,machangu watamkoma.
 
Mkichanganya mikojo wakati wa kukojoa, mama zenu watakatika maziwa..
Mapaja ya kuku na maini ni kwa ajili ya baba...

Ukijamba mbele ya mzungu unapewa hela na huyo mzungu.

Watoto hawazaliwi kuna sehemu ambako huenda kununuliwa.

Ukimuona mtu na pikikipiki nyekundu ujue ni mnyonya damu.
 
Mkichanganya mikojo wakati wa kukojoa, mama zenu watakatika maziwa..
Mapaja ya kuku na maini ni kwa ajili ya baba...

Ukijamba mbele ya mzungu unapewa hela na huyo mzungu.

Watoto hawazaliwi kuna sehemu ambako huenda kununuliwa.

Ukimuona mtu na pikikipiki nyekundu ujue ni mnyonya damu.

Hii imenikumbusha baba mmoja mtaani kwetu alikuwa daktari wa mifugo, alikuwa na pikipiki nyekundu, siku moja alianguka nayo akiwa amebeba nyama, basi watoto tukaenda kuangalia, kukuta nyama zimesambaa chini, tukajua katoka kumyonya mtu damu kisha akamuua. Tulikimbia kila mtu kwao, na ndo ikawa stori mpk tumekuwa wakubwa
 
Ukiwa mwanachama wa CCM lazima uwe mkulima au mfanyakazi tena masikini.... siku hzi ni tofauti!!:ranger:
 
ukifagia usiku utaondoa baraka nyumbani.
ukiona mtoto mdogo anafagia ujue kunawageni watakuja.
ukitokewa na alama nyeupe kwenye kucha ujue shangazi yako ana mimba.
 
Mkichanganya mikojo wakati wa kukojoa, mama zenu watakatika maziwa..
Mapaja ya kuku na maini ni kwa ajili ya baba...

Ukijamba mbele ya mzungu unapewa hela na huyo mzungu.

Watoto hawazaliwi kuna sehemu ambako huenda kununuliwa.

Ukimuona mtu na pikikipiki nyekundu ujue ni mnyonya damu.
ukkalia Figa utapata jipu kalioni. Ukikomba mwiko mtoto wa kiume ukubwani utakosa mchumba. Ukitupia ungo kwenye kimbunga shetani atatokea. Ukinunua chumvi usiku usiite chumvi iite dawa ya jikoni. Timu pinzani ikipiga penati tushike nyeti zetu kwa kuzibana penati itakoswa. Goli la kichwa hues halirudishwi. (Any one to prove because some are still used up to now!!)
 
ukimuona bibi mwenye macho mekundu huyo mchawi
ukimkata mchawi akatoa damu unaisha
kutema mate chini ni kuepuka balaa pupupu
 
Hii imenikumbusha baba mmoja mtaani kwetu alikuwa daktari wa mifugo, alikuwa na pikipiki nyekundu, siku moja alianguka nayo akiwa amebeba nyama, basi watoto tukaenda kuangalia, kukuta nyama zimesambaa chini, tukajua katoka kumyonya mtu damu kisha akamuua. Tulikimbia kila mtu kwao, na ndo ikawa stori mpk tumekuwa wakubwa

ukimuona bibi mwenye macho mekundu huyo mchawi
ukimkata mchawi akatoa damu unaisha
kutema mate chini ni kuepuka balaa pupupu

umewai sikia hii
 
ukienda kwa jirani jioni kuomba chumvi husemi naomba chumvi bali unasema naomba dawa ya mboga
 
Back
Top Bottom