Tupeane mawazo wapendwa

Maty

JF-Expert Member
Aug 24, 2010
2,167
725
Huwa najiuliza mara nyingi lakini nakosa jibu zuri, naomba nipate mawazo tofauti tofauti, inaweza kutusaidia wengi wetu.

Wanandoa wengi hasa wa miaka ya sasa, wakikorofishana korofishana baada ya muda wanachoamua ni tuachane bwana kila mtu ataanza nataka niishi kwa amani, nahitaji furaha mimi maisha yenyewe mafupi haya. Ukute hiyo ndoa baba msomi ana kazi nzuri na mama vile vile ndio balaa, kila mtu anasema usinibabaishe ninaweza kumudu maisha.

Hapo kuna watoto mmezaa, lakini kila mtu utamsikia napenda kuishi kwa amani, ni vipi kuhusu watoto? Je hao hawatakiwi kuishi kwa furaha na amani wakiwa na baba na mama? Hivi hamuwezi kukaa mkazungumza na kuelewana ili mlee watoto pamoja badala yake mnafikiria kuachana?

Hivi kuachana ni suluhisho la matatizo yako? Na je ukiachana na mwenzio ndio kusema hutaki kuoa/kuolewa tena? Na je ukioa/olewa halafu huyo mwingine akawa na matatizo pia pengine kuliko uliyoyakimbia mwanzo utaachana nae pia? Au utavumilia?

Tushirikiane kupeana mawazo wandugu
 
Huwa najiuliza mara nyingi lakini nakosa jibu zuri, naomba nipate mawazo tofauti tofauti, inaweza kutusaidia wengi wetu.

Wanandoa wengi hasa wa miaka ya sasa, wakikorofishana korofishana baada ya muda wanachoamua ni tuachane bwana kila mtu ataanza nataka niishi kwa amani, nahitaji furaha mimi maisha yenyewe mafupi haya. Ukute hiyo ndoa baba msomi ana kazi nzuri na mama vile vile ndio balaa, kila mtu anasema usinibabaishe ninaweza kumudu maisha.

Hapo kuna watoto mmezaa, lakini kila mtu utamsikia napenda kuishi kwa amani, ni vipi kuhusu watoto? Je hao hawatakiwi kuishi kwa furaha na amani wakiwa na baba na mama? Hivi hamuwezi kukaa mkazungumza na kuelewana ili mlee watoto pamoja badala yake mnafikiria kuachana?

Hivi kuachana ni suluhisho la matatizo yako? Na je ukiachana na mwenzio ndio kusema hutaki kuoa/kuolewa tena? Na je ukioa/olewa halafu huyo mwingine akawa na matatizo pia pengine kuliko uliyoyakimbia mwanzo utaachana nae pia? Au utavumilia?

Tushirikiane kupeana mawazo wandugu

Kama umegundua mwenzio sio chaguo lako sahihi mnaachana tu kila abebe chake kuliko kukaa mnasoneneka.
Maisha mtu inabidi aishi kwa fraha na amani tele sio kuishi kama digi digi.
Ukiona umepata mme anakula bwibwi na wewe hupendezewi na tabia hizo piga chini tafuta chaguo lako sahihi.
 
Mie naungana na wanotaka kuachana mambo yanapokuwa magumu kwani maisha ya kuteseka c mazuri wakati unaweza kuishi kwa furaha.

Kuhusu watoto hiyo itakuwa ndio historia yao, but as long as nitataka kuishi maisha yanayo rizisha na wanagu ntajitahidi waishi hivyo.Amen
 
degree ya uvumilivu kwenye ndoa ni ndogo sana kwa maisha ya sasa
ukizingatia wana ndoa wengi wana'jua' haki zao na hakuna anayetaka kujiweka chini
haya yote nadhani yameletwa na utandawazi..na hii kitu equality wanawake tunaililia pia i think inachangia kwa namna moja au nyingine
hakuna mwanamke wa siku hizi anataka kunyenyekea, wote wana/tuna penda kujilinganisha na wanaume..
mbaya zaidi ukikuta mdada kasoma ndo kabisaa hapo ni maswala ya 'nini nini usinichoshe nisikuchoshe nataka amani'..
tofauti na mama zetu walikuwa ni wanyenyekevu wazuri sana na wao pia walikuwa wanaangalia consequences za kuachana kwa watoto
lifestyle imebadilika generation hii ni selfish haiangalii watoto

in a nutshell, anayeweza kuifanya ndoa iendelee kuwepo ni mwanamke, na mwanamke wa sasa si mvumilivu.

Ni mtazamo tu.
 
Huwa najiuliza mara nyingi lakini nakosa jibu zuri, naomba nipate mawazo tofauti tofauti, inaweza kutusaidia wengi wetu.

Ukute hiyo ndoa baba msomi ana kazi nzuri na mama vile vile ndio balaa, kila mtu anasema usinibabaishe ninaweza kumudu maisha.
[/FONT][/SIZE]

Ndoa nyingi za wasomi ndio huwa zina matatizo. Na matatizo mengi kwa kiasi kikubwa huwa yanasababishwa na akina mama, tena kama mama ana elimu kubwa au ana uwezo mkubwa wa kipesa kuliko baba hapo tena ndo balaa. Ule ubaba unakuwa hauna maana kabisa. Mama ndo atataka kutawala nyumba, ukisema hiki jibu lake usinibabaishe na visa kedekede. Jaribu kufanya kautafiti kadogo tu, hata viongozi na wasomi wengi wanawake aidha huwa hawana waume au ndoa zao huwa zina migogoro mikubwa sana.

Ninayo mifano mingi sana ambayo nimeishuhudia mimi mwenyewe ya wanandoa ambao mama aidha ana uwezo na elimu kubwa kuliko baba au wako sawa. Wengine huwa wanafikia hata hatua ya kulala vitanda tofauti, asubuhi kila mtu anaondoka na gari yake japo wanafanya kazi ofisi moja. Basi ilimradi vurumai.
Akina mama/dada jirekebisheni (siwatuhumu). Fedha na elimu haviwezi kununua mapenzi.
 
My dear
Tunarudi kulee
je mlioana kwa ajili gani?
Pesa,mlilazimishwa, matatizo, upendo wa kweli etc

Na kitu kingine kinacho changia
ni uhuru na sheria zinazotulinda..
ni ile unaniletea uzushi na mwita lawyer wangu..
system ziko hapo kutulinda lakini cheki tunavyo chukua advantage ...

Sababu nyingine ni kuwa mroho/selfish
mmezaa mnafamilia lakini bado unataka
kuishi maisha ya mtu singo.. nimesema
selfish sababu watu hawataki ku comprise vitu
fulani maishani na anajua hichi kitu kinaweza kusambaratisha
ndoa yangu..

Kuna sababu nyingi tu..
dahh ndoa nyingi USANII +SHOW OFF
 
Nyumba ndogo inahusika kushape nyumba kubwa kwa taarifa yako.[/QUOTE


jamani jamani jamani....hivi wewe Fidel180 upo over 18 kweli???,
hili jibu laweza kuwa jibu tata la kwanza kwangu kwa mwaka huu,
KIVIPI????,
Ila bado nina mashaka sana na age yako,
nahisi bado upo kwenye ile age ileeeeeeeeee.....
wakubwa wezangu nahisi mtanielewa....lol
 
Mapenzi ya siku hizi uongo/udanganyifu mwingi
tamaa imetawala kuliko upendo wa kweli
mke/mume mnajaribu kuongea haisaidi hakuna mabadiliko
unavumilia miaka na miaka mwishowe unapata
matatizo ya kiafya kwa nini usubiri upate ugonjwa wa moyo
bora kila mtu kuchukua hamsini zake.
 
nilidhani lbd ndoa za kilokole zinaweza kuwa na unafuu!!

Hivi juzi tu hata mwezi haujaisha dada mmoja mpiganaji kweli kweli na mwanamaombi aliolewa na kk mmoja mlokole mwenzie, kweli harusi ilikuwa nzuri!! wiki ile niliyofiwa akaja kunipa pole akiwa na mama mmoja mchungaji rafiki yangu, baada ya kuona muda umeenda sana, nilimuuliza nawewe unakesha?? akasema ndio, nikamuuliza shemeji vipi hata kasirika akasema tumeshaachana!! nilishika mdomo.

kumbe nasikia walitengana baada ya week 2 tu!! yule mama mchungaji aliniambia kuwa baada ya tu ya siku 2 za ndoa akaanza kusuluhisha kesi zao mpaka mwisho amechoka.

Nikasema duh!! kwakweli kuna haja ya kuendelea kuwa single mpaka kieleweke!!!
 
nilidhani lbd ndoa za kilokole zinaweza kuwa na unafuu!!

Hivi juzi tu hata mwezi haujaisha dada mmoja mpiganaji kweli kweli na mwanamaombi aliolewa na kk mmoja mlokole mwenzie, kweli harusi ilikuwa nzuri!! wiki ile niliyofiwa akaja kunipa pole akiwa na mama mmoja mchungaji rafiki yangu, baada ya kuona muda umeenda sana, nilimuuliza nawewe unakesha?? akasema ndio, nikamuuliza shemeji vipi hata kasirika akasema tumeshaachana!! nilishika mdomo.

kumbe nasikia walitengana baada ya week 2 tu!! yule mama mchungaji aliniambia kuwa baada ya tu ya siku 2 za ndoa akaanza kusuluhisha kesi zao mpaka mwisho amechoka.

Nikasema duh!! kwakweli kuna haja ya kuendelea kuwa single mpaka kieleweke!!!

Hapa ndio nimechoka kabisa lol
 
Back
Top Bottom