Kuna haja kila mtu siku ya sherehe ya miaka hamsini akatoka na bakuli kuelekea ofisi yoyote ya kimataifa iliyo karibu ili kutoa ujumbe kwa serikali na kwa watoa misaada kwamba watanzania hatufurahii hata kidogo na tendo la nchi yetu kuwa omba omba wakubwa kiasi hiki baada ya kujitawala kwa miaka hamsini. Kwamba viongozi wetu wanatudhalilisha sana wanapotembea na mabakuli ya kuombea misaada nje ya nchi ingawaje wao wanaona ni sawa tu. Kwamba wanatudhalilisha wanapokosa misaada walioahidiwa wanaanza kulia lia kama watoto wadogo.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.