Watunduru
Senior Member
- Dec 29, 2011
- 170
- 39
wadau mimi kama mpenda amani,jana niliweka uzi hapa jamvini kuelezea matukio ya uchomaji moto mazizi ya nguruwe ambayo yameanza wiki 3 zilizopita.katika muendelezo wa matukio haya juzi makanisa mawili yalinusurika kuchomwa na leo hii tar 26/09/12 gari mbili zimechomwa moto moja ikiwa ya mchungaji na nyingine ni ya Mkristo wa kawaida,sambamba na hilo zizi ambalo lilikuwa na nguruwe 8 limeteketezwa.
Jambo la kustaajabisha pamoja na matukio haya kutishia amani na uwezekano wa kutokea machafuko ya kidini hakuna hatua inayochukuliwa na serikali wala hakuna kiongozi yoyote aliejitokeza kulaani jambo hili.
My take:
Mungu ibariki Tanzania.
Updates
Mkuu wa wilaya ameitisha mkutano kutoa tamko la serikali juu ya kadhia hii,hivyo kwa wale wafuatiliaji wa uzi huu,nitawajuza kinachoendelea baada ya mkutano kwisha
Jambo la kustaajabisha pamoja na matukio haya kutishia amani na uwezekano wa kutokea machafuko ya kidini hakuna hatua inayochukuliwa na serikali wala hakuna kiongozi yoyote aliejitokeza kulaani jambo hili.
My take:
Amani ni jambo jema kwa hiyo serikali ichukue hatua za haraka kukomesha hali hii kabla haijafika hatua ngumu maana wanaotendewa mambo haya nao sasa wanaanza kufikiria namna ya kulipa kisasi wenyewe baada ya kuona serikali haichukui hatua yoyote.
Mungu ibariki Tanzania.
Updates
Mkuu wa wilaya ameitisha mkutano kutoa tamko la serikali juu ya kadhia hii,hivyo kwa wale wafuatiliaji wa uzi huu,nitawajuza kinachoendelea baada ya mkutano kwisha