Tunduru: Gari ya mchungaji, mfuasi wake pamoja na nguruwe 6 wachomwa moto

Watunduru

Senior Member
Dec 29, 2011
170
39
wadau mimi kama mpenda amani,jana niliweka uzi hapa jamvini kuelezea matukio ya uchomaji moto mazizi ya nguruwe ambayo yameanza wiki 3 zilizopita.katika muendelezo wa matukio haya juzi makanisa mawili yalinusurika kuchomwa na leo hii tar 26/09/12 gari mbili zimechomwa moto moja ikiwa ya mchungaji na nyingine ni ya Mkristo wa kawaida,sambamba na hilo zizi ambalo lilikuwa na nguruwe 8 limeteketezwa.

Jambo la kustaajabisha pamoja na matukio haya kutishia amani na uwezekano wa kutokea machafuko ya kidini hakuna hatua inayochukuliwa na serikali wala hakuna kiongozi yoyote aliejitokeza kulaani jambo hili.

My take:
Amani ni jambo jema kwa hiyo serikali ichukue hatua za haraka kukomesha hali hii kabla haijafika hatua ngumu maana wanaotendewa mambo haya nao sasa wanaanza kufikiria namna ya kulipa kisasi wenyewe baada ya kuona serikali haichukui hatua yoyote.

Mungu ibariki Tanzania.

Updates
Mkuu wa wilaya ameitisha mkutano kutoa tamko la serikali juu ya kadhia hii,hivyo kwa wale wafuatiliaji wa uzi huu,nitawajuza kinachoendelea baada ya mkutano kwisha
 
Watunduru Kwa hali hii naona hakuna serikali kabisa, najaribu kupata picha uvumilivu utakapowashinda wakristo hali itakuwaje tunduru. Muda si mrefu tutashuhudia vurugu kubwa
 
Last edited by a moderator:
Kwa hali hii naona hakuna serikali kabisa, najaribu kupata picha uvumilivu utakapowashinda wakristo hali itakuwaje tunduru. Muda si mrefu tutashuhudia vurugu kubwa
Wasiwasi unaanzia hapo kwani nao wameshaanza kukaa vikao kujadili mustakbali wao.hadi muda huu polisi wanaomba wapelekewe taarifa mezani toka kwa raia wema,ni kama upelelezi umewashinda.
 
Kama ingekuwa tukio kama hilo limetokea kwa upande wa waislamu, mara moja FFU wangefika kwenye tukio kwa gharama zote, maana waislam wanasema wanataka kukomesha mfumo Kristo Tanzania. Uharaka huo ni kwa sababu Rais na Makamo wake na Mkuu wa Polisi ni wenzao. Wakristo hawajali hayo ndo maana wako kimya, lakini isitafsiriwe kwamba ni wapumbavu. Wangejua, waislam wangeonyana, kwa sababu Kristo si mtu wa vurugu isipokuwa akikosa uvumilivu matokeo yake ni mkishindo. Alipigwa na kudharauliwa khata kufa msalabani lakini alikaa kimya. Kumbuka alivyowafurusha waliofanya biashara nyumbani mwa baba yake utajua kwamba kumbe naye uvumilivu hakuwa nao milele kwa wachokozi wa makusudi.

Uislam nilidhani ni amani kama wanavyohubiri wenyewe, lakini wanapotenda hawafanani na wanaotaka amani. Wakidai wanatii na kufuata maagizo ya Mtume wao, lakini akitokea leo Mtume huyo atawakataza kama alivyowakataza enzi za uhai wake wale waliokuwa na jazba ya kuua wasioamini kama wao. Nani atawatetea? Uislam wa leo nadhani ni NGO ya vurugu ambayo hata muasisi wa jina hilo asingependa kusikia. Mtume wa Mungu hupenda amani. Asiyeamini Mungu ni kundi la Shetani bila shaka. Tusifike huko, vita ya kiroho hupiganwa kiroho sio kwa ncha ya upanga. Chonde chondeeee!
 
wadau mimi kama mpenda amani,jana niliweka uzi hapa jamvini kuelezea matukio ya uchomaji moto mazizi ya nguruwe ambayo yameanza wiki 3 zilizopita.katika muendelezo wa matukio haya juzi makanisa mawili yalinusurika kuchomwa na leo hii tar 26/09/12 gari mbili zimechomwa moto moja ikiwa ya mchungaji na nyingine ni ya mkristo wa kawaida,sambamba na hilo zizi ambalo lilikuwa na nguruwe 8 limeteketezwa.
Jambo la kustaajabisha pamoja na matukio haya kutishia amani na uwezekano wa kutokea machafuko ya kidini hakuna hatua inayochukuliwa na serikali wala hakuna kiongozi yoyote aliejitokeza kulaani jambo hili,
My take:amani ni jambo jema kwa hiyo serikali ichukue hatua za haraka kukomesha hali hii kabla haijafika hatua ngumu maana wanaotendewa mambo haya nao sasa wanaanza kufikiria namna ya kulipa kisasi wenyewe baada ya kuona serikali haichukui hatua yoyote.
Mungu ibariki tanzania.



mkuu asante kwa taarifa, lakini ungedodosa pia ukatuambia sababu za vurugu hizo hasa ni nini, ili tuwe na taarifa zilizokamilika. Ni maoni tu mkuu!
 
Sijui ni dini gani inafundisha chuki kali kama hizi dhidi ya binadamu mwenzio, hii lazima itakuwa ni dini ya kishetani!
 
mkuu asante kwa taarifa, lakini ungedodosa pia ukatuambia sababu za vurugu hizo hasa ni nini, ili tuwe na taarifa zilizokamilika. Ni maoni tu mkuu!

Hawa jamaa hawana sababu wala hoja yoyote ya msingi isipokuwa wana kiu ya kumwaga damu.wanadai eti wamedhulumiwa sana na eti sasa basi sijui wamedhulumiwa kitu gani na hao nguruwe wanaowaua!kimsingi huu ni mtandao wa kigaidi sawa tu na wale uamsho n.k wanatishia hadi kujitoa muhanga.serikali isipowa crackdown mapema hali itazidi kuwa mbaya.
 
Kelele zote hizi ni kwa ajili ya nguruwe tuuu? Afterall nguruwe toka Moshi Tunduru kaenda kufanya nini?
 
nadhani hawajui wanchokiabudu maana kama wangejua kuwa waliumbwa na Mungu wangemwabudu mungu aliyehai lakun bahati mbaya hawajui lolote juu ya wanachoamini.
 
wadau mimi kama mpenda amani,jana niliweka uzi hapa jamvini kuelezea matukio ya uchomaji moto mazizi ya nguruwe ambayo yameanza wiki 3 zilizopita.katika muendelezo wa matukio haya juzi makanisa mawili yalinusurika kuchomwa na leo hii tar 26/09/12 gari mbili zimechomwa moto moja ikiwa ya mchungaji na nyingine ni ya mkristo wa kawaida,sambamba na hilo zizi ambalo lilikuwa na nguruwe 8 limeteketezwa.
Jambo la kustaajabisha pamoja na matukio haya kutishia amani na uwezekano wa kutokea machafuko ya kidini hakuna hatua inayochukuliwa na serikali wala hakuna kiongozi yoyote aliejitokeza kulaani jambo hili,
My take:amani ni jambo jema kwa hiyo serikali ichukue hatua za haraka kukomesha hali hii kabla haijafika hatua ngumu maana wanaotendewa mambo haya nao sasa wanaanza kufikiria namna ya kulipa kisasi wenyewe baada ya kuona serikali haichukui hatua yoyote.
Mungu ibariki tanzania.

Bado tupo kwenye vikao vya chaguzi za ndani, mtuache kwanza.
 
Hawa watu wabaya sana kushinda hata mafrimason.Influence ya shetan inawadhuru sana.

Hawa kimsingi hawako kwa ajili ya dini kwa sababu uislam unafundisha amani,upendo na kuvumiliana,hawa si waislamu,mtume alipigana vita kujihami na kwa kuwa alizuiwa kuabudu na alinyanyasika kwa sababu ya dini,hawa ansar sunna hawajakatazwa kuabudu na hawana sababu ya msingi kuleta machafuko,isipokuwa hawa ni magaidi na hawana uhusiano wowote na dini tukufu ya islam iliyosheheni mafundisho ya kistaarabu,hawa sio dini,hawa sio siasa,hawa ni wauaji.
 
kelele zote hizi ni kwa ajili ya nguruwe tuuu? Afterall nguruwe toka moshi tunduru kaenda kufanya nini?

kwa tundulu nguruwe hu ni mnya wa polini hafugwa na binadam kama ameuwawa basi aliwafuata maadui zake nguruwe hufugwa mbeya moshi dar.. Pia akionekana nguruwe mtaani pia atauwawa ndio maana wafugaji wa nguruwe huka mbali na mjilani hakyna anae penda halufu ya shwahini .....
 
jamani tutumie busara kdg, hakuna anaependa udini awe muislam au mkristo.
Mleta mada toa ufafanuzi tafadhali, hayo matukio yameanza lini, chanzo ni nini?
Ungetufafanulia manake binafsi hizo taarifa sijazisikia hata kwenye chombo kimoja cha habari.
Siamini kama kuna mtu yoyote mwenye akili timamu anaeweza akafanya hayo uloeleza bila sababu.0ungetoa taarifa kamili bila upendeleo tuweze kujadili vzr manake taarifa yako ya awali inaonekana kuelemea upande mmoja.

Pili hakuna sehemu yoyote katika mafundisho ya uislam panapofundisha kudhulumu, kuharibu mali ya mtu au kuu asie na hatia.
Anaefanya hivyo kakiuka misingi ya uislam na anapaswa ahukumiwe kama mhalifu mwingine na si kuhukumu dini yake kwani uislam haufundishi hivyo.
 
Kelele zote hizi ni kwa ajili ya nguruwe tuuu? Afterall nguruwe toka Moshi Tunduru kaenda kufanya nini?

Mkuu naomba ungesoma vizuri taarifa hii! Hayo magari nayo ni nguruwe siku hizi? Halafu kwani Moshi ndo wanafuga nguruwe peke yao?
 
kwa tundulu nguruwe hu ni mnya wa polini hafugwa na binadam kama ameuwawa basi aliwafuata maadui zake nguruwe hufugwa mbeya moshi dar.. Pia akionekana nguruwe mtaani pia atauwawa ndio maana wafugaji wa nguruwe huka mbali na mjilani hakyna anae penda halufu ya shwahini .....

Aiseee! Kwa hiyo nguruwe pori wanafugwa kwenye zizi huko tunduru? Unawafahamu nguruwe pori au unawasikia?
 
Back
Top Bottom