Unaishi sayari ipi wewe? Hao majaji ni malaika?mahakama ya tanzania iko imara na haitikisiki
Mahakama ni muhimili uliyo imara na haungiliki kama baadhi ya wanasiasa wanavyodai.
Unaishi sayari ipi wewe? Hao majaji ni malaika?mahakama ya tanzania iko imara na haitikisiki
Mahakama ni muhimili uliyo imara na haungiliki kama baadhi ya wanasiasa wanavyodai.
jamhuri ni gazeti la lowassa,nadhani inatosha kueleza nini kinaendelea,pia tuwe makini juu ya suala la kuwaponda ama kutowaponda majaji wetu
Mwandishi nakubaliana na wewe 100 kwa 100, hasa nikifanya reference zile hukumu mbili za kihistoria 1. Majaji saba including Jaji mkuu, a.k.a Mgombea binafsi na 2. Hukumu ya Godbless Lema, mashtaka udhalilishaji hukumu kushiriki vitendo vya rushwa. Salaaale!!!mahakama ya tanzania iko imara na haitikisiki
watanzania amkeni, sio porojo zote zinazoandikwa magazetini bila kufuata maadili ni ukweli. Tujaribu kujitafutia taarifa sisi wenyewe bila kuwategemea wale wanaotoa tafsiri zao za sheria. Tujisomee hukumu sisi wenyewe na tusisubiri wanasiasa watutafsirie hukumu za mahakama kisiasa na na maslahi ya kisiasa.
Mahakama ni muhimili uliyo imara na haungiliki kama baadhi ya wanasiasa wanavyodai.
Mkuu Jogi,
1. kwanza nakushukuru kutambua kuwa Spika Anna Makinda, alichaguliwa na kuridhiwa na bunge, ila usichojua wewe
ni alipendekezwa na nani, who was behind Anna Makindas speakership?, hoa ndio who pays the piper, na
anachofanya Makinda is just to play the tune ambayo imekuwa called by the one who paid for it!.
2. Mimi ni mtu ninayeamini on "principles of natural justice", kwa vile Chenge, hajashitakiwa popote kwa kosa lolote,
he is a clean man, na hana uchafu wowote!, so do EL, ndio maana mimi niko wazi katika kumsupport EL!.Kama JK
alidiriki kupanda jukwaani na kumnadi Basil Mramba mwenye kesi mahakamani, then Chenge na EL ni malaika kabisa
mbele ya macho ya CCM!.
3. Umeniomba "Nikubaalie japo mara hii tu kuwa, tatizo linalotumaliza ni zimwi CCM". Samahani sana, sikukubalii,
tatizo sio CCM, CCM is just the vehicle, haikujiweka hapo ilipo, imewekwa, hivyo tatizo sio CCM iliyowekwa, bali
tatizo ni walioiweka CCM hapo ilipo!. That simply means, tatizo ni sisi Watanzania tulioiweka CCM madarakani and it
plays games on us again and again na sisi tukiendelea kuiweka madarakani again and again na sitashangaa kama
hata 2015, tukairudisha tena!.
4. Hii dhana ya kudhania adui mkubwa wa Tanzania ni CCM, is a wrong concerpt, na ndilo kosa kubwa la wapinzani,
katika chaguzi zote za nyuma kuelekeza mashambulizi yote CCM wakijihesabu ndie adui yao mkubwa, hivyo ku miss
the target ya adui halisi ni nani!.
5. CUF baada ya kujaribu mara 3 ikashindwa, ikaamua kutumia principle ya "if you can't beat them, join them", kwa
mara ya 4 katika uchaguzi wa 2010, ikakubali yaishe, ikawajoin ndani ya SUK katika ndoa ya kukubali kutekeleza
ilani ya uchaguzi ya CCM, at the same time, its fighting from within, and is hitting them very hard kwa mtindo wa
"kikulacho" na kikundi cha "uamsho" ni matokeo chanya ya kipigo from within, hivyo kwa 2015 upande wa Zanzibar
CUF ni njia nyeupe!.
6. Naishukuru Chadema, kupitia M4C, imeshagundua adui halisi anayewakosesha ushindi, na sasa imejielekeza kwa
wananchi. Mara baada ya uchaguzi wa 2010 na mafanikio makubwa upande wa Chadema, niliwaeleza kuwa bado
hawajipanga mkao wa kushika dola, kwa sasa kupitia M4C, wanaonyesha wanajipanga, ila udhaifu mwingine mkubwa
wa chadema niliousemea ni ule "umimi" kujiamini kupita kiasi kuwa peke yao wataweza!, nilisema peke yao
hawawezi, na leo nasema te na na tena, "Chadema peke yao hawawezi!", lazima wa join forces kutafuta how they
work together hata na watu wasiokubaliana nao!.
7. Japo CUF ni mke wa CCM kwa upande wa Zanzibar, hiyo ni "marriage of convinience", hivyo inavunjika wakati
wowote "conveniences" zikimalizika, hivyo Chadema inacho kibarua kigumu cha kumtongoza huyu mke wa mtu
kumhakikishia akikubali kutoka nje ya ndoa, yeye sasa hatakuwa mke tena, bali atageuka mume na 2015 ni yeye
sasa ndie atageuka kidume na kumuoa huyo mume aliyenae sasa kwa sababu mume huyo ategeuzwa mke!.
8. Hakuna ubishi kuhusu nguvu ya CUF kule Zanzibar na Chadema itake isitake, ipende isipende, ili kujihakikishia njia
nyeupe ya kuwa mpangaji wa magogoni kwa 2015, ni lazima ikubali kuisupport ya CUF kwa upande Zanzibar ili CUF
nao wakubali kuisupport Chadema huku bara!. Chadema wakae chini na CUF, waainishe maeneo ya strong holds za
kila mmoja na kuachiana maeneo hayo ili 2015, kuepuka kumfaidisha kunguru kwa vita vya panzi!.
Wasalaam.
Pasco.
Hii ilikuwa Agosti 19, 2012!.Kiukweli hapa Tanzania, hatuna kabisa "The doctrine of Separation of powers" kilichopo ni kiini macho, na alichokifanya Tundu Lissu ni kuuthibitisha tuu udhaifu huu!.
Kazi ya bunge zaidi ya kutunga sheria, pia ni kuisimamia serikali, na kuithibiti mahakama!. Kazi ya Mahakama ni kutafsiri sheria, kuithibiti serikali na kulidhibiti bunge, na kazi ya serikali ni to provide kwa bunge na mahakama na kuendesha nchi kwa mujibu wa sheria zilizotungwa na bunge, na kusimamiwa na mahakama!. Hivyo kila chombo ni big brother aki watch over and above mhimili mwingine ili kujenga hizo checks and balance, lakini kwa Tanzania ni shaghala bagala, Serikali ndio kila kitu, ikifuatiwa na bunge na mwisho ni mahakama!.
Rais wetu ni sehemu ya bunge, anaweza kulivunjilia mbali bunge as he pleases!, bunge likishatunga sheria, sheria hiyo haiwi sheria mpaka rais aikubali, na akiikataa bunge halina uwezo wa kufanya lolote, kwa sababu rais anaweza kulivunjilia mbali anytime!. Hivyo mbele ya rais, bunge si lolote sii chochote!.
Rais ndiye anayemteua Jaji Mkuu, bila any imput toka bunge, mahakama ikitoa capital punishment, adhabu hiyo haitekelezwi mpaka rais airidhie, rais anaweza kuamua kutotekeleza adhabu yoyote, kuwasamehe wafunga wowote, na kwa Tanzania hata kuzuia wahalifu kama ile mijizi ya EPA kupewa msamaha bila kufikishwa mahakamani ambapo ni uvunjaji wa katiba ya JMT, lakini hakuna mwenye uwezo wa kumfanya chochote rais, hivyo mbele ya rais, mahakama sii lolote, sii chochote!.
Kwa mtaji huo, Lissu is very right, bunge linapaswa kuidhibiti mahakama na ilipaswa jaji mkuu aridhiwe na bunge kama anavyoridhiwa waziri mkuu!. Bunge pia ndilo lilipaswa liwe supreme kwa sababu ndilo lililochaguliwa na watu, na sio serikali!. Hapa kwetu serikali ndio kila kitu, rais wetu ni Alfa na Omega!.
Pasco.
Ilikuwa ni wakati ule ambao hata ungeuliza lile swali lako "je bunge linajipendekeza ... ??" usingeitwa DodomaHii ilikuwa Agosti 19, 2012!.
P