Tundu Lissu yuko sahihi: Majaji wengi hawajahitimu vyuo na elimu zao ni za mitandaoni

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Jun 12, 2012
4,572
26,868
Source Gazeti la Fahamu

Ule usemi wa Mbunge wa Singida Mashariki kuwa ujaji wa kuteuliwa na rais ni wa kirafiki zaidi na kujuana una ukweli ndani yake, na ulikuwa mwiba kwa serikali na mwanasheria mkuu wa serikali kuwa na ukweli kwamba majaji wengi hawana sifa za kuwa majaji na wengi wao elimi zao ni za kuungaunga. Ikitolewa mfano ya wa jaji ambaye kwa miaka minne kashindwa kuandika hukumu kumfatilia hana elimu ya degree na kwa muda huu anafanya degree ya kwanza online.

Narudia kusema Tundu Lissu yuko sahihi
 
Hilo halina ubishi mkuu,kwani Tundu lisu yuko makini sana katika kauli zake na kwamba huwa ana ushahidi anaposema kitu, cha ajabu magamba na vyombo vyake husika huwa hawapendi kuambiwa ukweli na hufurahi wakisiiwa kwa uongo.


Yaani hawa jamaa wana alergy ya kuambiwa ukweli! kila wakishushiwa vigongo wee mcheki Lukuvi, Werema, Wasira & co. wanavohangaika kutafuta mlango wa kutokea hata kama the room is made of a concrete wall!

Nilishangaa kuona Mwanasheria Mkuu anatoa matusi kwa Mbunge Lissu (Jembe) baada ya kuzidiwa. Hafu Job Ndugai nae eti anasema hakuna tatizo juu ya kauli ya AG kwa Lissu huku yalikuwa matusi na udhalilishaji wa wazi! Hivyo hata AG mwenyewe is questinable in terms of integrity and capacity!

Nilifurahia mchakato wa wenzetu Wakenya walivo wapata wakuu wa Idara ya Mahakama. Ilikua interview ya wazi na ilirushwa live KBC hivo hata wananchi walikua wanashuhudia nani alikua akionyesha uwezo mkubwa wakati wa usaili. Hata baada ya safari ndefu ya usaili, jamii ilishuhudia wale waliokua wakionyesha uelewa mkubwa wakiibuka kidedea na hakukua na dalili za mizengwe.

Sasa Werema and co. hatujui hata vigezo vilivyotumika juu yao kwani hawaonyeshi competency na professionalism badala yake ni watu wa kutetea uovu na wakizidiwa wanatukana. Natoa rai kwa Watanzania wenzangu, kwenye mchakato wa katiba mpya hili jambo lazima tuchangie kwamba Idara nyeti zote kuwe na public verting hata kwa kutumia wawakilishi wetu ita matter zaidi kuliko utaratibu wa sasa! Mungu ibariki Tanzania, walaani mafisadi!
 
Hivi mpaka leo tuna majaji wangapi na wanafanya nini? Maana ni kama kila baada ya miezi mitatu wanaapishwa majaji wapya
 
Hivi huyu Werema AG (SIC!), akisikia jambo kutoka kwa LS kwanini asijiridhishe kwa kufanya ka UTAFITI kidogo kuliko ku opt kumtukana LS?

Sasa hivi hata Idara ya mahakama inamchukia Werema, pale alipopinga hoja ya TL, kwamba budget ya mahakama itolewa in percetange 3%? au 2%, kama ilivyo Bunge na Vyama vya siasa hiyo ingesaidia kuondoa ukata ktk idara ya mahakama. Lakini Werema akapinga kwa HOJA YA NGUVU! As usual Magamba wenzake waka mu support. Idara ya mahakama inaona CDM wana VISION kuliko CCM!
 
Hilo halina ubishi mkuu,kwani Tundu lisu yuko makini sana katika kauli zake na kwamba huwa ana ushahidi anaposema kitu, cha ajabu magamba na vyombo vyake husika huwa hawapendi kuambiwa ukweli na hufurahi wakisiiwa kwa uongo.

Wamechezea Elimu na walimu , hii ndiyo inatucost , wewe unadhani watoto wanaomaliza darasa la saba na kwenda sekondari bila kujua kusoma na kuandika si watasoma na kuwa majaji . Ndio elimu yetu hiyo ndugu zangu bora wakijua kuropoka na kubwabwaja kuwa seriali yetu sikivu watakuwa majaji na mawaziri. Mwangalie Lukuvi ana kisomo gani , si waziri na wapo wengi wa haina iyo bora wamehitimu madrasa basi tutawapata wengi majaji wa Mahakama zetu hizi za Kadhi au gachacha . Nchi hii imeishakuwa ya ovyo . Huu ni mkakati wa siku nyingi kuua elimu , Tubaki na mahakama za Kadhi na majaji ndio hao tena
 
hatari tupu mzee, watakuitia RAMA.

Mkuu PhD, Kamanda wetu wa anga ametuhimiza tusiwe waoga la sivyo nchi hii haitakombolewa mikononi mwa mkoloni mweusi ccm (chama cha magamba, chama cha mafisadi, chama cha mabwepande chama cha majangili, nk.).
 
Wamechezea Elimu na walimu , hii ndiyo inatucost , wewe unadhani watoto wanaomaliza darasa la saba na kwenda sekondari bila kujua kusoma na kuandika si watasoma na kuwa majaji . Ndio elimu yetu hiyo ndugu zangu bora wakijua kuropoka na kubwabwaja kuwa seriali yetu sikivu watakuwa majaji na mawaziri. Mwangalie Lukuvi ana kisomo gani , si waziri na wapo wengi wa haina iyo bora wamehitimu madrasa basi tutawapata wengi majaji wa Mahakama zetu hizi za Kadhi au gachacha . Nchi hii imeishakuwa ya ovyo . Huu ni mkakati wa siku nyingi kuua elimu , Tubaki na mahakama za Kadhi na majaji ndio hao tena

Mkuu, Elimu ya tz. wameikolokochoa na kuondoa U-stereo wote, elimu inakoroma mziki wake haueleweki kabisa!!
 
Source Gazeti la Fahamu

Ule usemi wa Mbunge wa Singida Mashariki kuwa ujaji wa kuteuliwa na rais ni wa kirafiki zaidi na kujuana una ukweli ndani yake, na ulikuwa mwiba kwa serikali na mwanasheria mkuu wa serikali kuwa na ukweli kwamba majaji wengi hawana sifa za kuwa majaji na wengi wao elimi zao ni za kuungaunga. Ikitolewa mfano ya wa jaji ambaye kwa miaka minne kashindwa kuandika hukumu kumfatilia hana elimu ya degree na kwa muda huu anafanya degree ya kwanza online.

Narudia kusema Tundu Lissu yuko sahihi

Lissu akisema kitu huwa sina shaka haropoki maana ni lawyer anajua cha kusema
 
Binafsi navutiwa na hoja tetezi za ndg. Lissu ktk kutetea muhimili wa sheria nchini na uhuru wake; kuhusu uteuzi wa rais kwa majaji hapo sina la kuchangia kwani ni process ndefu mpaka rais anapotangaza mtu kuwa mteule wake wa ujaji.....

Mchango wangu ni kwa CJ na timu yake ya muhimili wa mahakama; imebainika wengi wa graduates wa tumaini ndio wanaopewa mamlaka za uongozi ktk muhimili wake lakini 80% yao licha ya kuwa na gpa nzuri hawako vizuri ki uweredi mahakamani na kutafsiri sheria na maamuzi yao, siwapigii debe udsm bali bado kuna gape kubwa ya kitaaluma na maadili ktk ya wahitimu wa tumaini ktk sheria na wa udsm....

Mahakama iangalie ajira za intake 2000-2006 kutoka vyuo hivyo, dosari hii ni kubwa na ya wazi, huenda udsm kwa kuwapatia gpa za kawaida wahitimu wake wametoa fursa kwa vyuo vingine kuzalisha kada hiyo isiyo kidhi haja lakini mwisho wa siku anayeumia ni mtanzania kutokana na maamuzi yasiyozingatia weredi wa kisheria wa mtoa haki.

Mahakama ijitathmini yenyewe kabla ya lissu hajawasemea bungeni, kuna dosari ambazo hata rais anakuwa na wakati mgumu ktk uteuzi na kujikuta anateua watu wengi nje ya mahakama. Nafasi wanayo bado, tuwape muda na ndio wanajipanga sasa kama independent muhimili kuanzia sasa.

Mengi yatapungua sana na nina imani wenye uwezo kimaamuzi mahakamani ndio wafikiriwe ktk nyadhifa ili kuipa sura chanya mahakama na siyo ukabila, udini, mahusiano hasi na kadhalika, si rahisi kuyathibitisha haya ila yapo ndani muhimili huo lakini taifa linakua na mahakama nayo inakua
 
Wanabodi, hivi hakuna namna yoyote tukapata hayo majina ya majaji waliopewa kishakaji na dhaifu bila vetting?
 
hatari tupu mzee, watakuitia RAMA.
Aa wapi RAMA UGHONDU anatafutwa na NGUVU ya UMMA yuko porini!! anajitibu kwa mitishamba!! kwa sababu hawezi kusogelea vituo vya afya NI WANTED!! popote. Usicheze na UMMA wa sasa!!
 
Tumesoma leo gazeti la jamhuri limetoa hata majina kwa mujibu wa lissu....how credible hii story ya jamhuri kwakweli sina hakika.....

Nunueni jamhuri
 
Ujaji wa kishikaji shikaji. Ipo siku utasikia, Mwantum Mahiza Jaji, hawa ndo MAGAMBA bwana, hakuna lolote acha wamalizie miaka yao huku umma ukijipanga kurudisha nchi ktk mikono salama ya CDM
 
FDR.Jr uko sahihi kaka, gpa za Tumaini kimeo, nimesoma nao law skul, wengi wanababaisha tu
 
Last edited by a moderator:
Hivi mpaka leo tuna majaji wangapi na wanafanya nini? Maana ni kama kila baada ya miezi mitatu wanaapishwa majaji wapya

:biggrin1: ni kweli lakini majaji wako wengi na hata hatuoni wanachofanya maana kesi zote kubwa serikali ndio mwamuzi wa mwisho sa sijui wao wako pale kufanya nini
 
Back
Top Bottom