Tundu Lissu umetuangusha kwa nini hukuhudhuria vikao vya kamati za katiba

Status
Not open for further replies.
Pipijojo una hoja nzuri sana lakini "wapiganaji" wataingia humu kwa ugomvi na si kujibu hoja kisiasa. Hapo ndipo utapojuwa maana ya "upiganaji" ni nini.

Lissu kaudanganya umma wa Tanzania kautukana umma wa Tanzania kwa kuwaambia wanatawaliwa kifalme. Kashindwa hata kuheshimu kura alizopigiwa yeye na wapiga kura wake waliomfikisha bungeni.
 
kama hakuhudhuria vikao ulitaka akae kimya bungeni na kusinzia kama wengine...? tulimchagua ili atusemee.. popote, kama sio kwenye kamati basi bungeni na kama sio bungeni basi mikutanoni...

aluta kuntinua.. acha awaamshe watz, na sasa wameanza kuamka mmojammoja mpaka nchi nzima iamke..!
 
Pipijojo unanifanya niamini maneno ya muuliza swali mmoja katika mjadala wa "Tanzania tunayoita" kilichorushwa na Star TV jana... kwamba LISSU alipokea rushwa ya fedha ili awashawishi wenzake watoke Bungeni kwa lengo la kurahisisha muswada upite kwa urahisi japo yeye alikana na kusema kuwa hajawahi kufuatwa na mtu mwenye lengo la kumhongwa ukiachilia mbali kuhongwa kwenyewe.
 
uzuri wa chadema huwa hawakosei wala hawataki kurekebishwa

siasa zako naona unazilingznisha na ushabiki wa mpira wa miguu, hili suala la katiba liko wazi wala halihitaji hongera! Nyinyi ndo watanzania mnaotusababishia wengine tunatseka kutwa nzima huku ninyi mnaneemeka na kodi zetu, ila siku ipo tu, kama sio kwenu basi hata kwa wajukuu zenu.
 
Lisu ana haki kuwasilisha mawazo yake. Kwa wale unaoona anapiga kelele mmekosea. alichofanya Celina ni kumattack kujaribu kufunika uozo.. yani unaacha kujadili content unamjadili mtu tena unatafuta sababu dhaifu kabisa. alifanya sahihi kutokwenda. utashirikije wakati unajua watu tayari wamepanga mambo yaende wanavyotaka wao? angekuwa msindikizaji tu!!
 
tumeona sasa CCM wanajenga hoja kwamba alikimbia vikao vya kamati sasa ndio anaona ana maoni ya kubishana kipi kiwemo na kipi kisiwemo ni kama kweli Tundu hakuwajibika

hivi suala ni tundu lisu au katiba? Mbona akili zako ndogo sana?
 
chadema wameshikwa pabaya wabishi hao hata kwenye hoja iliyo wazi ni heri tusio na chama. kama mnabisha kuwa Tundu hakukosea basi hakuna haja ya kushika dola mtakuwa wabishi zaidi na hamtashaurika kama CCM


huyu pipijojo amekurupuka tena sana na wewe naona unaingia kwenye mtego wake halafu unajifanya eti huna chama.!!!!!! jana kwenye mdahalo kuna mtu aliuliza swali hilo na lissu alilijibu kwa ufasaha sana..
 
Aliulizwa pia kwamba CHADEMA wamepata nini kwa kutoka kwao Bungeni wakati muswada umepita? Jamaa alijikanyaga tu bila majibu ya kuridhisha. Mimi naona ni vyema wangewaomba radhi wananchi na wanachama wao kwa kutowawakilisha kwenye suala nyeti la katika ukizingatia hata yeye kwenye kamati uwakilishi wake ulikuwa butu.
 
Mnaongea ongea tu hamjui what real happened, Hebu mtafuteni Lissu ana majibu ya Uhakika!

hatutaki malumbano, lisu ameshapoteza hy haki yake ya kutoa maoni,, na kama ana niya njema na hoja yake kama italeta manufaa ya wengi aeleze watanzania na katika hilo atambue kuwa wapo watakao muunga na watakao mpinga, hivyo aamini kuwa na mawazo ya wengine pia ni muhimu. Asiwachongechonge sana wazanzibar na wala waliounda muungano hawana dhambi,. Asiwe mwanasiasa mchochezi.
 
Wakati wa kufunga muswada wa katiba, Waziri wa sheria na katiba Celina kombani alituambia watanzania kwamba anamshangaa Tundu Lissu anafunguka leo na kutoka bungeni na wanachadema wenzake wakati hakutokea kwenye vikao vya kamati ambako angeweza kutoa maoni yake. Kombani alisema, kwa mfano katika kikao cha mwezi juni, 2011 Lissu alikuwa Tarime wakati wajumbe wengine wakikutana kuandaa mchakato huo kwa ajili ya kuwakilishwa bungeni lakini pia Waziri alisema anayo orodha ya mahudhurio kuthibitisha kwamba Lissu hakuhudhuria. Katika hitimisho lake hilo Kombani alisema, wajumbe wengine kama Halima Mdee na wabunge wengine wa upinzani walihudhuria na walitoa maoni yao ambayo yamepokelewa na kufanyiwa kazi.

Kumbuka kamati hii iliundwa baada ya kukataliwa kwa muswada uliosomwa kwa mara ya kwanza ili kutatibu mchakato huo upya kabla hujasomwa kwa mara ya pili miongoni mwa wajumbe alikuwa Tundu Lissu ambaye taifa limetangaziwa kwamba hakuhudhuria vikao.


my take: 1. Ni kazi gani muhimu zilimbana Lissu kuliko unyeti wa katiba (moyo wa nchi)
2. lissu analetaje maoni yake bungeni wakati maoni hayo angeyatoa kwenye kamati
3. Lissu angehudhuria vikao vya kamati ya katiba angetuambia alitoa maoni gani ambayo hayakupokelewa.
4. Tundu Lissu huwezi kulitumia bunge kama kamati ndogo unawarudisha nyuma wengine.
5. Lissu tuombe radhi watanzania kwa kushindwa kutuwakilisha kwenye kamati
6. Lissu wewe ulikuwa muhimu sana kuanzia ngazi ya kamati ambako hukuhudhuria
7. tundu lissu ulitoa kipambele kwa mamabo mengine kuliko katiba?
magamba bwana!.....
 
pipijojo unaongea usicho kijua.hayo unayosema kombani hajayasema Bungeni bali aliyasema wakati startv alipowakutanisha yeye na lissu katika kpindi cha tuongee asubuhi ambapo lissu alimjibu na kumuuliza hasard ya waliyo yaongea lakini kombani akabaki akichekacheka pasipo jibu lolote.magamba mwaka huu mnalo. mia
 
huyu pipijojo amekurupuka tena sana na wewe naona unaingia kwenye mtego wake halafu unajifanya eti huna chama.!!!!!! jana kwenye mdahalo kuna mtu aliuliza swali hilo na lissu alilijibu kwa ufasaha sana..
Kwani alijibuje?
 
kuna watanzania huwa siwaelewi tukiisema CCM ni sawa chadema hapana ndio usitaarabu wa nchi ipi huu.
 
Katika hili sioni ni kwanini watu wanabisha wakati walisalitiwa na wabunge wa CHADEMA kwa kukosa uwakilishi Bungeni. Nadhani wanachadema wanatakiwa kuwaweka sawa wabunge wao na kuwataka watimize wajibu wao.
 
pipijojo unaongea usicho kijua.hayo unayosema kombani hajayasema Bungeni bali aliyasema wakati startv alipowakutanisha yeye na lissu katika kpindi cha tuongee asubuhi ambapo lissu alimjibu na kumuuliza hasard ya waliyo yaongea lakini kombani akabaki akichekacheka pasipo jibu lolote.magamba mwaka huu mnalo. mia


Kombani alisema bungeni mara tu baada ya mwanasheria mkuu Werema kumalisha na mimi nilisikia
 
hivi suala ni tundu lisu au katiba? Mbona akili zako ndogo sana?

Lissu ni mmoja wa viongozi wa chadema wanaotegemewa sana katika mchakato huu wa katiba kosa lake moja linaweza kukighalimu chama kukimbia vikao vyote ni lazima alisemee
 
hawa jamaa walifanya fujo jana kwenye mdahalo , naona bado wanaendeleza pumba humu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom