Tundu Lissu on KLH News Exclusive!

Status
Not open for further replies.
tatizo ni wewe kuassume kuwa nisingelimuuliza kuhusu mtazamo wa kisiasa au mimi sifahamu kuwa ni Mkurugenzi wa Idara ya Sheria ya Chadema. Kama ungesikiliza hadi mwisho halafu ungekuta sijamuuliza basi ulikuwa na sababu ya kulalamika. Next time, kosoa baada ya matangazo, lakini kuassume kuwa kwa sababu fulani nisingewaambia watu kuwa Lissu ni kiongozi wa Chadema pia ni kuniunderestimate.. kuna vitu vingine unaviweka kama dramatic portion of the show..

Mwanakijiji,

Labda standard za wengine ziko juu sana na hapo ndipo tatizo linapoanzia. Wengine haya mambo ya conflict of interests kila mwaka lazima uyasoma ili kulinda maslahi ya kampuni.

Nitashangaa kweli kuona mwandishi yeyote wa chombo cha maana ambaye angeacha kusema Lindu pia ni mkurugenzi wa sheria, haki na katiba wa CHADEMA.

Kama unaona ulivyofanya ni SAHIHI, sawa endelea. Hapa tunajifunza na kufundishana, hakuna viboko kwa asiyeelewa na wala zawadi kwa anayeelewa, badala yake viboko ni dunia yetu.

Mimi sikuwa concerned na wewe kumuuliza mtazamo wake wa kisiasa. Concerned yangu ilikuwa kuhakikisha unawapa wasikilizaji wako info zote muhimu kuhusu Lisu pale mwanzoni ili wajue yeye anaongea kama nani.

Kushindwa kuelewa na kufuata mambo madogo madogo ndiko kumetufanya tuwe na mafisadi, aambaye hasemi ukweli kwenye jambo dogo huishia kuongopa kwenye jambo kubwa.

Any way wote tunaongelea uongozi bora lakini level ya huo uongozi bora iko tofauti sana. Binafsi ningetaka sisi ambao tunaongoza kuishambulia serikali, kuwashambulia akina Rweyemamu basi tuwe whitter than white inapokuja kwenye matendo yetu. Lakini nikiangalia yanayotokea hapa JF siko optmistic.
 
hivi hili tishio la ufisadi imekuwa kama fimbo ambayo watu huwa watashikiwa kuwa mtu asipofanya hivi au vile na yeye atakuwa fisadi?
 
Kwa wale waliokosa kusikiliza mahojiano yangu na Bw. Tundu Lissu mnaweza kusikiliza mahojiano hayo kwa kwenda kwenye KLH News hapa chini.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom