Anna Makinda ameshindwa kuliendesha bunge, anakipendelea chama cha zamani ki waziwazi.
Ndugu Zangu,
Nimekuwa nikisema kila siku kwamba tunajadili then what!!, tutaumia kwa machungu, kwa sasa nchi hii haina uongozi kabisaaaaaa,
JK - Msaniii,
Makinda - Msanii
Mawaziri – Wengi wao Wasanii
Wabunge wa CCM,NCCR,CUF,UDP,TLP - wengi wao Wasanii,
Wabunge waliobaki kutetea wananchi kiukweli ni Wachadema tu.
Sasa tumebaki na viongozi makini amabo ni wabunge toka Chadema, wanajaribu kupambana kwa maslahi ya nchi hii na wanachi kwa ujumla, lakini sisi wananchi tunaopenda mabadiliko tunawasaidiaje hawa wapambanaji wachache wa Chadema?. Tufanye nini kuwaunga mkono ?
Yaani ukisikiliza Bunge unaona kinachoongelewa ni kupoteza muda na pesa ya walipa kodi wa nchi hii, yaani bunge lote limekaa mguu pande kuangalia Chadema wanakuja na nini ili wapambane nao, wapo kwa ajili ya kuangalia maslahi yao! na wanawaona Chadema kama adui anayetaka kuchukua maslahi yao na familia zao.
Kama mijadala yenyewe ya bunge ndio hivi kunasababu gani ya wabunge kwenda kutumia gharama kubwa na ilihali majibu yote ya mawaziri Makinda anayajua!?, hivi perdiem za wabunge ni shilingi ngapi (hope si chini ya tsh 120,000/=)kwa siku, naomba kusahihishwa kama sio hivyo, zidisha idadi ya wabunge, zidisha siku wanazokaa pale, plus gharama nyingine na gharama watendaji wengine wa serikali nawa Bunge Lenyewe, where is value for money, can they justify this, je kwa gharama hizi ni zahanati zingejengwa na Magari mangapi ya wagonjwa yangenunuliwa?
Ndugu zangu; nchi hii kwa viongozi hawa waliopo hawatafanya lolote la maana kwa manufaa ya nchi, wao bado wanaamini sisi wananchi hatujui kitu na tukisikiliza bunge tu tunaamini, Sipendi tabia ya mawaziri na wabunge wa CCM kuwazarau wananchi kwa kiasi hiki, Ni bora Vita, Vurugu na baadae tushikishane adabu, maana hizi kauli za amani na utulivu na zarau za namna hii hazifai.
Watu wale wale ndio wanamiliki ardhi, kuna watu wanaardhi ukubwa wa wilaya, yote hiyo wewe mtu mmoja ya nini?, ina maana kaburi lako litakuwa kubwa hivyo, jamani hii nchi inatia aibu na hasira sana, ni dhambi gani watanzania tumefanya mpaka kuwa na viongozi wabnafsi kama hawa, hawana mipango yoyote ya kumkomboa matanzania, kila kitu hovyo, jamani nendeni kwa Kagame anavyo kimbia kimaendeleo na hii ni baada ya kuchinjana kwanza ndio adabu imekuja, angalia majirani zetu Kenya baada ya kuchinjana sasa adabu! waziri akikosa tu anajiuzuru maana ndivyo katiba inavyoongoza, angalia majirani zetu karibu wote wamefanya mabadiliko ya chama cha kuongoza nchi na sasa kunaadabu kwani kinachoongoza kinajua kikivurunda kinajiweka pabaya uchaguzi unaofuata.
Sasa sisi tunataka mabadiliko lakini watawala hawataki na sisi tumekaa tuasubiri mabadiliko yaletwe na nani!? JK? Makinda? CCM? Wabunge wa CCM? jamani sisi ndio wenye nchi hii na sisi ndio tutaamua mwelekeo wa taifa hili.