Tundu Lissu na Kiinimacho cha Muungano

Swali la Tatu: Je, Mkataba Ulijengwa kwa Nguvu Ganui ya Kisheria?

Jibu ni kwamba, Mkataba wa Muungano, 1964, ulichukua nafasi ya Sheria Mama, kwa matarajio kwamba, Muungano wetu utapewa nguvu za kikatiba ndani ya mwaka mmoja; Ni hapa ndugu Kobello unapoanza spins zako; Nitafafanua; Unaelezea vizuri sana yaliyojiri huku aidha kwa kujua au kutojua, unaruka mambo mengine muhimu zaidi ya kusaidia kufungua kiini macho hiki cha muungano; Kwa mfano, hoja yako kwamba Katiba ya Tanganyika ilikubaliwa ndio iwe Katiba ya Muda, hakuna anayebisha hili, mpaka hapa tupo sawa; Lakini hauelezei watanzania waliopo humu kwamba, ili hilo lifanikiwe, katiba ya Tanganyika ilitakiwa ifanyiwe marekebisha kwanza, bila ya hivyo, Mkataba wa Muungano, 1964 ungeendelea kuwa nguzo pekee ya kuhalalisha muungano;

Kwa makusudi au kwa kupitiwa, hautaki kujadili yaliyomo katika Mkataba wa Muungano, 1964, hasa pale unapoweka masharti juu ya matumizi ya Katiba ya Tanganyika kuwa Katiba ya Muda ya Jamhuri Mpya ya Muungano wa Tanzania (katika kipindi kisichozidi mwaka mmoja). Kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964, ibara ya tatu inasema hivi:

(iii) Katika kipindi cha mpito katiba ya Jamhuri ya Muungano itakuwa katiba ya Tanganyika iliyorekebishwa ili kuweka:
a) Chombo tofauti cha kutunga sheria na Serikali kwa ajili ya Zanzibar kwa mujibu wa sheria zilizopo za Zanzibar na vitakuwa na mamlaka ya mwisho katika Zanzibar kwa mambo yote isipokuwa yale tu yaliyo chini ya bunge na Serikali ya Jamhuri ya Muungano;
b) Nafasi ya makamo wawili wa Rais mmoja kati yao akiwa ni mkaazi wa Zanzibar atakuwa ndiye kiongozi wa Serikali iliyotajwa kwa ajili ya Zanzibar na atakuwa ndiye msaidizi mkuu wa rais wa Jamhuri ya Muungano katika utekelezaji wa kazi za Serikali kwa upande wa Zanzibar;
c) Uwakilishi wa Zanzibar katika bunge la Jamhuri ya Muungano;
d) Mambo mengine yatayofaa au kuhitajika ili kuipa nguvu Jamhuri ya Muungano na mkataba huu.

Bila ya Katiba ya Tanganyika kufanyiwa marekebisho katika maeneo haya, ili kuupatia Muungano wetu Uhalali na Nguvu ya Kikatiba, Katiba ya Tanganyika isingekuwa na uhalali au nguvu ya kutumika kama Katiba ya muda ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na badala yake, ingebakia na nguvu yake kwa upande wa Tanganyika, kama ilivyokuwa kabla ya Muungano baina ya taifa huru la Tanganyika na Zanzibar; Kwa maana hii, basi Mkataba wa Muungano, 1964, ungebakia kuwa ndio nyaraka peke yake ya kuhalalisha muungano wetu, hivyo kuendelea kuchukua nafasi ya Sheria mama katika kipindi cha mpito;

Mbali na marekebisho haya ya Katiba ya Tanganyika ili ipate nguvu za kikatiba kuendesha Muungano wakati wa kipindi cha mpito, pia kulikuwa na sharti lingine ndani ya Mkataba wa Muungano, 1964, sharti ambalo lilikuwa ni muhimu kuliko yote, kwa maana ya kuupatia Muungano wetu sasa nguvu kamili na uhalali wa kisheria wa kudumu; Sharti hili ambalo pia unakwepa kulijadili kwa mtindo wa ku-spin issues, lipo katika kipengelea cha saba cha Mkataba wa Muungano ambacho kinasema hivi:

vii) Rais wa Jamhuri ya Muungano kwa kukubaliana na Makamo wa Rais ambaye ni kiongozi wa serikali ya Zanzibar
a) Atateua tume kwa ajili ya kutoa mapendekezo kwa ajili ya katiba ya Jamhuri ya Muungano.
b) Ataitisha Baraza la kutunga katiba ikiwa na wawakilishi kutoka Tanganyika na Zanzibar katika idadi itakayoamuliwa likutane katika kipindi cha mwaka mmoja tokea kuanza kwa muungano kwa madhumuni ya kutafakarimapendekezo ya tume iliyotajwa juu na kupitisha katiba ya Jamhuri ya Muungano.

Nadhani sasa tupo tayari kudadisi kwa undani zaidi kuhusu Mkataba wa Muungano, 1964, na nguvu yake ya kisheria;
Mkataba kama unavyosema wewe wa mwaka 1964, siyo sheria, Sheria inaitwa "ACTS OFUNION OF TANGANYIKA AND ZANZIBAR, 1964."
Na hiyo act ni mjumuisho wa "Union
of Zanzibar and Tanganyika Law" kwa upande wa Zanzibar na "Union of Tanganyika and Zanzibar Act, 1964. hizi ndiyo sheria zilizoanzisha muungano.
Ukisema articles of the Union ni sheria, unakuwa upo kisiasa zaidi na si kisheria ... now lets go
 
Mkataba wa Muungano, 1964, umeweka wazi provision hii ya nchi kuwa na uwezo wa kujitoa; hii ndio essence ya federation, kwani chini ya unitary system, kama utajitoa, basi ni baada ya kupiga au kupigwa mabomu kama ilivyotokea north ireland; Kobello hataki kuamini kwamba Mkataba wa 1964 uliweka provision ya kujitoa, pale anapojenga hoja kwamba, hoja yangu kwamba Mkataba ule ulilenga a federation, anaita hoja yangu kwamba sio ya kweli na ni ya kisiasa;
Mkuu nadhani unaelewa vita iliyoua karibu watu millioni moja Marekani, ambayo ni Federation, please tuende kitaalam zaidi.
I want to learn, usiwe na hasira.
 
Mkuu Nguruvi3,

Nashukuru tena kwa mchango wako. Naomba niingie katika hoja zako tatu kuu kama ifuatavyo:

Kwanza - kuhusu matumizi ya neno "kiini macho"; Kimsingi naelewa hoja yako lakini naomba niwe muwazi kwamba – kwanza, kwangu mimi, uelewa na pia matumizi ya dhana hii ni kwamba, kiini macho au "false appearance", ingawa inaweza kuwa na synonyms nyingine ambazo zinatoa a negative connotation kama ulivyojadili; mimi nadhani ni suala la jinsi gani neno linatumika na katika mazingira yepi; Kwa mfano neno "MJINGA", it may not sound politically correct kwa mwanasiasa kupanda jukwaani na kusema

"ndugu wananchi, naombeni kura zenu kwa sababu nyinyi ni "WAJINGA", na mkinichagua, nawahakikishieni kwamba nitaenda bungeni kupigania maslahi yenu, ili mpunguze UJINGA mlio nao;"

Ingawa UJINGA ni moja ya maadui wakuu wa Maendeleo Tanzania, kwa kauli hii, kwa kweli kura hautapata; Hoja yangu ya msingi hapa ni kwamba, ni suala tu la matumizi to determine what is and what is not politically correct;

Vinginevyo, kwangu binafsi, kama nilivyosema hapo juu, kwa miaka mingi sana mimi navyoelewa neno illusion au kiini macho ni "FALSE APPEARANCE"; Sasa nilipomsikia Lissu bungeni akijenga hoja kwamba Muungano Wetu ni Kiini macho, moja kwa moja nikapata mwamko wa kwenda kuupitia tena Muungano wetu, KISHERIA ZAIDI, kwani huyu sio mwanasiasa bali Mwanasheria, kubaini zaidi the FALSE APPEARANCE relative to Mkataba wa Muungano, 1964; Kama kauli hiyo ingekuwa ya mwanasiasa, sidhani hata ningekuwa na uelewa juu ya muungano wetu kama nilivyo leo hii; kauli ya Lissu ilinisukuma nikafanye utafiti kwa miezi mitatu kabla ya kuja humu na kutoa hoja yangu hii;

Naomba uniwie radhi iwapo neno hili kidogo linakukera, lakini nia yangu ni kuliwakilisha kama lilivyowakilishwa na Mwanasheria, huku nikijaribu sana kulijadili kisheria; Vinginevyo, neno MATATIZO ya muungano, huleta mjadala uliokuwa na mwelekea wa kisiasa zaidi; Pengine sipo sahihi sana, lakini kwa kifupi, nia yangu ni kuchukua maneno ya Mwanasheria mwenye dhamana kama Waziri Kivuli wa Muungano; Naomba ieleweke kwamba sikutunga neno hili, bali nimeli ‘lift' kutoka kwa Lissu, na kwa vile yeye ni Mwanasheria, basi anajua alikuwa ana maana gani, na iwapo utasikia nimetiwa nguvuni kama mchochezi kwa matumizi ya neno hili, ndugu yangu nguruvi3, naomba uwe mtu wa kwanza kumtafuta Lissu aje kuniokoa ‘KISHERIA';

Hoja yako ya Pili - kwamba Muungano wetu ni beyond repair, kwa kum-quote Joka Kuu; Ni kweli kuna dalili nyingi na kubwa sana kwamba tumefikia hali hiyo; Lakini kama nilivyosema awali, nadhani ili tufikie final analysis juu ya hilo, ni muhimu Referendum iitishwe haraka ili tujue moja; Vinginevyo naelewa juu ya sentiments and views hizi kupitia mtu mmoja mmoja, lakini naheshimu zaidi uamuzi wa UMMA, na kwa maana hii, referendum;

Kama ulivyojadili, "NIA" ya Mwalimu Nyerere na Karume ilikuwa ni njema kabisa at the outset, na kama tatizo lilijitokeza, basi ilikuwa on the "MEANS: Vinginevyo until nipate confirmation Watanzania wanasema nini juu ya hatima ya muungano, kwa njia ya ‘Referendum', nitaendelea kutetea muungano wetu, LAKINI Per Articles of the Union(1964), not Per Katiba ya Tanzania (1977), kwani katiba ya Tanzania (1977), kwa MTAZAMO WA KISHERIA, haina mema kwa muungano wetu; Wema uliopo mle, kama upo, basi ni KISIASA tu;

Suala la Mwisho na muhimu sana ni hoja ya kuvunja muungano; Mantiki ya hoja hii naielewa vizuri sana, na sipingani nayo bila maelezo, kwani maelezo yangu ni hayo hapo juu kwamba, ili nijiunge na Kambi hii, mimi nahitaji kwanza kuona matokeo ya Referendum juu ya suala hili; Ningependa kumalizia kwa maswali yafuatayo ambayo naomba nipate mtazamo wako tafadhali, na again, maswali haya ni kutokana na approach yangu kwa muungano huu kisheria zaidi kuliko kisiasa, ingawa nakubaliana na wewe there is a thin line….:


  • Je, Muungano wetu uliundwa kwa sheria ipi? Kwani kama sheria ipo, basi kuna mawili: aidha iwe rectified, or revoked all together, ili tupate tena Tanganyika yetu;

  • Je, tunaweza kuachana na Zanzibar bila ya kufufua Tanganyika?

  • Kwa vile Tanganyika ilivunjwa kwa mujibu wa sheria ya bunge la JMT, sheria namba 24, 1967; Je, ili kurudisha Tanganyika, tunahitaji ku rectify sheria hii? Revoke? Au kutunga nyingine bila ya haya mawili?

  • Sote tulishuhudia mwaka 1995jinsi gani hoja ya Tanganyika ilizimwa, iliposhika kasi ndani ya bunge la JMT; Hoja ya kuzimwa kwake tunazijua Kwahiyo sina haja za kuzirudia, hasa kwamba - kwamba – uamuzi ule ulitakiwa ufanyike ndani ya vikao vya CCM, sio Bungeni; Je, hii ina maana kwamba kuanzisha hoja ya Tanganyika lazima ipitie vikao vya CCM, na sio chama kingine chochote cha siasa au mchakato mwingine wowote? Kama inahitaji referendum, kwanini hili halikusemwa mwaka 1995, wakati nchi ilikuwa tayari ni ya mfumo wa vyama vingi kama ilivyo leo?

Ha hah aha ha...Kama nilivyo kuambia kule nyuma , nilijua utaamsha hisia za Bw Nguruvi3. Sasa kaanza na kukuchagulia maneno ya kusema. Mimi binafsi naamini kuwa huu Muungano ni kiini macho or whatever you may call it. Kisheria Muungano unakasoro nyingi ambazo zimeelezwa na wanasheria mbali mabali.

Kisiasa , Muungano umekuwa na kero zenye kuzaa makero yasiyo na ufumbuzi. Kuirudisha Tanganyika ni muhimu kama kweli wapo watanganyika wenye kuami Muungano wa kweli.
 
Kobello,

The Republic of Tanganyika and the Peoples' Republic of Zanzibar shall be united in one Sovereign Republic.
Naomba niyarudie maneno hayo hapo juu, kwa Kiswahili kwa mujibu wa Mkataba wa Muungano, 1964:

Kwahivyo IMEKUBALIWA baina ya Serikali ya Jamhuri ya Tanganyika na ya watu wa Zanzibar kama ifuatavyo:


  1. Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar Zitaungana na Kuwa Jamhuri Huru Moja

Ukiamua kuwa makini hapa Kobello, utagundua kwamba mjadala hapa sio JAMHURI KUWA MOJA bali SERIKALI KUWA MOJA, MBILI au TATU; Kwahiyo kama suala ni JAMHURI MOJA, tupo sawa mpaka hapo, sina shida na hilo, lakini je:

Ndani ya Jamhuri hiyo Moja ya Tanzania, Mkataba wa Muungano, 1964, ulilenga uwepo wa Serikali ya Namna gani? MOJA? MBILI? TATU?

Ili tuweze kupata mwanga juu ya hili, ndio maana katika bandiko langu namba 94, nikakuwekea maelezo juu ya aina kuu za ushirikiano wa mataifa ambazo ni tatu:

1. Serikali Moja
2. Matangamano ya Serikali Za Majimbo
3. Mfumo wa Shirikisho

Nikajitahidi kufafanua kila mfumo, huku nikikuuliza swali baada ya kumaliza ufafanuzi wa kila mfumo, na nilitegemea ungenijia na majibu, hasa juu ya maoni yangu kwanini Mkataba wa Muungano, 1964, ulilenga Shirikisho;

Vinginevyo, kuhusu mifano yako miwili, wa kwanza nimeshaujibu hapo juu i.e. hoja kuhusu JAMHURI MOJA, na naomba usijaribu ku-spin hili;

Mfano wako wa Scotland nimeupenda ka kitu kimoja: Umeonyesha IDENTITY ya SCOTLAND REMAINING INTACT,licha ya Treaty of the Union in the 16th Century; Leo hii ukienda UK, kuna watu who identify themselves as Scottish; Kwanini hatuna hili kwa TANGANYIKA?

Kumbuka kwamba, mbali ya jina SCOTLAND Kuendelea kuwepo, huku wananchi wa muungano ule wakikuelezea kwa furaha kabisa kwamba UK is made up of N.Ireland, Scotland, Wales and Britain, wote hawa, lakini hasa Scotland [kwa vile ndio umetolea mfano], they have autonomy katika masuala yafuatayo:

-Legal System;
-Education na Religious Institutions;
-Home Affairs; etc

Na usisahau kwamba in 2014, kuna referendum inakuja ya kutafuta independence kutoka UK;

Naomba turejee kwenye bandiko langu la 94, na unijibu maswali yangu yaliyopo chini ya maelezo yangu kwa kila aina ya ushirikiano wa mataifa;
 
Mkuu nadhani unaelewa vita iliyoua karibu watu millioni moja Marekani, ambayo ni Federation, please tuende kitaalam zaidi.
I want to learn, usiwe na hasira.

Vita ilitokana na mfumo mbovu wa confederation, marekani ilikuja kuwa federation baada ya vita hivi; Sina hasira mkuu, samahani kama nakukwaza;
 
Kuirudisha Tanganyika ni muhimu kama kweli wapo watanganyika wenye kuami Muungano wa kweli.

Asante sana mkuu, natumaini wengi zaidi wataliona hili, kwa mantiki rahisi kabisa, hasa per articles of the union, 1964;
 
Tatizo sisi Waafrika bado tunapenda kukumbatia sana matatizo na kuogopa kuchukua maamuzi magumu. Tukiwa na tatizo huwa tunajifanya kama vile hakuna tatizo kabisa. Angalia mgogoro wa Ziwa Nyasa. Mgogoro umekuwepo muda mrefu lakini tukaufimbia macho. Sasa ndiyo tumeshtuka na kuanza kutafuta nyaraka.

Hivyo hivyo kwa suala la muungano. Inaonekana wazi kabisa kuwa kuna matatizo kwenye huu muungano lakini hakieleweki nini kinafanyika. Viongozi wamekaa kimya kama vile huu muungano uko perfect or made from heaven. Yaani kuongelea suala la muungano unachukuliwa kama unatenda kosa la treason. Wakati sisi tunafumbia macho matatizo ya muungano, wenzetu wanatatua ya kwao kabla mambo hayajaharibika.

Scottish independence: 'Deal agreed' on referendum

The basis of a deal has been reached between the UK and Scottish governments over the independence referendum. In a joint statement Deputy First Minister Nicola Sturgeon and Scottish Secretary Michael Moore said "substantial progress" had been made. But the BBC understands that although a few minor details need to be ironed out, a package of measures has been agreed.

It paves the way for a meeting between David Cameron and Alex Salmond. This is expected to take place on Monday in Edinburgh. The prime minister and the first minister are expected to agree on a plan which will involve a referendum which asks a single yes/no question on whether Scotland should leave the United Kingdom.

It is understood the agreement will also extend the vote to include those aged over 16 in Scotland. Mr Moore, who is currently on holiday, and Ms Sturgeon spoke on the phone on Monday night and are due to do so again on Friday.

'Further work'

It follows a series of face-to-face meetings and negotiations between the pair in recent weeks. A joint statement issued by the Scottish government and the Scotland Office after Mr Moore and Ms Sturgeon's latest conversation said: "Further substantial progress towards agreement was reached this afternoon between the Deputy First Minister Nicola Sturgeon and the Secretary of State Michael Moore.

"Officials have now been tasked with doing some further work on the final detail of the agreement. We are however on track for the full agreement, including the terms of a section 30 order, to be presented to the First Minister and the Prime Minister over the next few days."

The BBC's political editor, Nick Robinson, said the deal - if it is finalised - will be presented as "a compromise involving concessions by both sides". The SNP is understood to have accepted a single question referendum, as opposed to two questions including one on greater powers for the Scottish Parliament, whilst the UK government has abandoned its opposition to giving 16 and 17-year-olds a vote.

One question

Scotland Office Minister, David Mundell, who has been involved in the negotiations, told the BBC there will be one question and confirmed the vote will be held before the end of 2014. He said: "It won't automatically be the case that 16 and 17-year-olds can vote in the referendum. "The UK government, certainly the Conservative party, oppose that change. It will be up to Scottish Parliament to determine who can vote in the referendum in Scotland, and also the date and the nature of the question."

Scottish Finance Secretary John Swinney said progress had been made but "further ground" had to be covered before a final agreement is reached. He added: "The Scottish government has always made clear that we preferred to have a single question on whether Scotland should become an independent country.

"But we also recognised that some people in Scotland want to consider other options to strengthen the powers of the parliament. That is a question we have consulted upon, it is one we have discussed and it has been an important part of the discussions with the UK government, but throughout all of this our preference has been to have a single question."

When a final agreement between the two governments is formalised legislation to set up the referendum is expected go before both the Westminster and Holyrood parliaments.

BBC News - Scottish independence: 'Deal agreed' on referendum
 
Mkataba kama unavyosema wewe wa mwaka 1964, siyo sheria, Sheria inaitwa "ACTS OFUNION OF TANGANYIKA AND ZANZIBAR, 1964."
Na hiyo act ni mjumuisho wa "Union
of Zanzibar and Tanganyika Law" kwa upande wa Zanzibar na "Union of Tanganyika and Zanzibar Act, 1964. hizi ndiyo sheria zilizoanzisha muungano.
Ukisema articles of the Union ni sheria, unakuwa upo kisiasa zaidi na si kisheria ... now lets go

Kumbuka, i am reasoning not to win an argument but to seek the truth; Ulichokisema hapo juu hakijatilia maanani niliyoyasema ingawa umeya quote kama yalivyo; jaribu kuangalia conditions za Mkataba zilikuwa zipi, na kama hazikuwa met, then nini kilibakia kuwa legally binding when it came to the Union;
 
Kumbuka, i am reasoning not to win an argument but to seek the truth; Ulichokisema hapo juu hakijatilia maanani niliyoyasema ingawa umeya quote kama yalivyo; jaribu kuangalia conditions za Mkataba zilikuwa zipi, na kama hazikuwa met, then nini kilibakia kuwa legally binding when it came to the Union;
Kwa sababu kila sheria huwa na "Definitions" au "Explanation of terms" kwa hiyo ukichukulia articles of the union pekee bila kuwa kama sheria i.e the ratified agreement by both the Revolutionary council na national Assemby of Tanganyika utakua unaishia kwenye conclussions ambazo wewe ndiyo utakuwa unazitafsiri na siyo jinsi sheria ilivyokuwa inatafsiri. Hii ni muhimu sana.
So, please when we talk about "Law" let's refer to Parliamentary acts.
You have to be surgical with this, otherwise utakuwa unakosea.
 
Mkuu Kobello,

So far, whats your position juu ya mada iliyopo mbele yetu, je kuna kiini macho au kitu kinachofanania na hilo? In other words, kwa mtazamo wako, sababu kuu za muungano wetu kuwa na dhoruba ni nini?

Upo sahihi kuhusu Sheria ambayo ndiyo ilithibitisha muungano, lakini sheria hii ililenga kufanikisha masharti yaliyopo kwenye Mkataba, na masharti hayo hayakufuatwa; kwa maana nyingine, chanzo cha mgogoro wa muungano sio kukiukwa sheria ya muungano, bali mkataba wa muungano; Na kinachobakia kuwa nguzo kuu ya muungano leo ni Mkataba wa Muungano, 1964, sio sheria ya Muungano 1964;
 
Vita ilitokana na mfumo mbovu wa confederation, marekani ilikuja kuwa federation baada ya vita hivi; Sina hasira mkuu, samahani kama nakukwaza;
Kama kuna historia ya nchi ambayo nimeangaikia sana kuisoma (kiulazima ) nadhani US ni mojawapo. Marekani ilkuwa ni Federation kabla ya civil war na baada ya civil war. Nia yangu ni kuondoa imani kuwa unitary governments hazivunjiki bila mtutu wa bunduki. Chukua hata mfano wa Czechoslovakia, ilivunjika kwa amani na US ilwalazimisha confederate states kubaki kwenye Union.
 
Kwa sababu kila sheria huwa na "Definitions" au "Explanation of terms" kwa hiyo ukichukulia articles of the union pekee bila kuwa kama sheria i.e the ratified agreement by both the Revolutionary council na national Assemby of Tanganyika utakua unaishia kwenye conclussions ambazo wewe ndiyo utakuwa unazitafsiri na siyo jinsi sheria ilivyokuwa inatafsiri. Hii ni muhimu sana.
So, please when we talk about "Law" let's refer to Parliamentary acts.
You have to be surgical with this, otherwise utakuwa unakosea.

Sheria ya muungano kazi yake ilikuwa tu kuthibitisha Mkataba wa muungano ili uwe na nguvu ya kisheria; Upo hapo?
 
Kama kuna historia ya nchi ambayo nimeangaikia sana kuisoma (kiulazima ) nadhani US ni mojawapo. Marekani ilkuwa ni Federation kabla ya civil war na baada ya civil war. Nia yangu ni kuondoa imani kuwa unitary governments hazivunjiki bila mtutu wa bunduki. Chukua hata mfano wa Czechoslovakia, ilivunjika kwa amani na US ilwalazimisha confederate states kubaki kwenye Union.

Sija double check kuhusu federation versus confederation US, but you might be right about that; Ila nachojua ni kwamba muungano ule ulipata dhoruba kutokana na matatizo ya autonomy; Civil war whether ilitokea under federation or not, source ya vita hivi had nothing to do na migogoro ya muungano, bali ilichangiwa sana conflicting interests between the elites wa north na south in the context of slavery;

Suala la mtutu wa bunduki, hoja yangu ya msingi ilikuwa kwamba, under federation kuna urahisi zaidi wa kutoka kuliko under unitary system, kwani under federation, hiyo provision ipo wazi zaidi; otherwise upo sahihi kwamba sio lazima unitary struggles ziendane na mtutu wa bunduki;
 
Mkuu Kobello,

So far, whats your position juu ya mada iliyopo mbele yetu, je kuna kiini macho au kitu kinachofanania na hilo? In other words, kwa mtazamo wako, sababu kuu za muungano wetu kuwa na dhoruba ni nini?

Upo sahihi kuhusu Sheria ambayo ndiyo ilithibitisha muungano, lakini sheria hii ililenga kufanikisha masharti yaliyopo kwenye Mkataba, na masharti hayo hayakufuatwa; kwa maana nyingine, chanzo cha mgogoro wa muungano sio kukiukwa sheria ya muungano, bali mkataba wa muungano; Na kinachobakia kuwa nguzo kuu ya muungano leo ni Mkataba wa Muungano, 1964, sio sheria ya Muungano 1964;
Mkuu, mimi ni mtanganyika, mtanzania na mwafrika.
Haya yote ni majina tu ambayo karne moja na nusu iliyopita (ukiondoa Africa) mababu zetu wala hawakujua maana yake.
Nataka Tanganyika iwe Tanganyika. Na hicho kiini macho unachozungumzia, kisilaumiwe CCM, ilaumiwe serikali ya Zanzibar na baadhi ya Wazanzibari.
Serikali ya Zanzibar ilitaka wale Polisi mia nne kutoka bara wasiondoke, Tanganyika ilitaka kuwepo na muungano wa serikali moja, hilo ndiyo lengo letu.
Lengo la zanzibar siyo kuungana na Tanganyika. Na sitakubali Tanganyika iungane na Zanzibar nusu kwa nusu kwa sababu hatuko nusu kwa nusu, ni lazima watuambie "Electorate" ya Tanzania itakuwaje? We are majority, so we should have majority representation ... kitu ambacho nina uhakika hawatakubali.
Tusiwe waoga, tumechoka na huu muungano kwa sababu Zanzibar hawautaki, na sasa hivi sisi hatuutaki.
Mkuu Mchambuzi tusimtafute mchawi, it's so obvious.
 
Ok Mchambuzi,nimepata hicho kipengele,hapo chini...Kutoka kitabu cha "Mwalimu Julius K.Nyerere",cha William Edgett Smith,kilichotafsiriwa na Paul Sozigwa(uk. 154)



Hapo nimetafsiri kwamba bila ya shinikizo kutoka nje,wakitaka kuvunja muungano,basi hana shida na hatoweza kuwapiga mabomu wazanzibari,again, i stand to be corrected,pengine ni utafsiri wangu?

Kumbe mwalimu alikuwa ameweka wazi hayo maneno.. sasa kwanini CCM sasa hivi hawataki kusikia hoja za muungano

Wanaficha mambo gani nyuma ya muungano..?

Na hawa CUF plus wazanzibar kwanini bado wanaikataa chadema while chadema wanaweza na wana nia ya kuwapa hilo wanalo taka.. Zanzibar yenye mamlaka kamili?

Siwaelewi hawa watu,
 
Sheria ya muungano kazi yake ilikuwa tu kuthibitisha Mkataba wa muungano ili uwe na nguvu ya kisheria; Upo hapo?
Nipo! na ninayop copy yake hapa, sasa tuangalie maana ya Interim constitution na turelate na hoja yako ya mwaka mmoja na commission. Ila tuende taratibu, kwa sababu nataka kuonyesha nguvu aliyoitoa Karume kwa National Assembly ya Tanganyika, na President of Tanganyika.
 
Kumbe mwalimu alikuwa ameweka wazi hayo maneno.. sasa kwanini CCM sasa hivi hawataki kusikia hoja za muungano

Wanaficha mambo gani nyuma ya muungano..?

Na hawa CUF plus wazanzibar kwanini bado wanaikataa chadema while chadema wanaweza na wana nia ya kuwapa hilo wanalo taka.. Zanzibar yenye mamlaka kamili?

Siwaelewi hawa watu,
Labda wanaamini kuna shinikizo kutoka nje?
 
Nipo! na ninayop copy yake hapa, sasa tuangalie maana ya Interim constitution na turelate na hoja yako ya mwaka mmoja na commission. Ila tuende taratibu, kwa sababu nataka kuonyesha nguvu aliyoitoa Karume kwa National Assembly ya Tanganyika, na President of Tanganyika.

Pengine ungeniongoza kwa hoja, kipengele kwa kipengele, kwani nimekuwa nafanya hivyo kwa muda huku wewe ukichukua upande wa kupinga au kuhoji;
 
Mimibaba,

Nashukuru kwa mchango wako mzuri na vile vile pongezi zako kwangu, bila ya kusahau ushauri;

Maudhui na madhumuni ya thread yako yananitatiza kwa sababu sielewi unachotaka kuanikisha kwenye huu mjadala kama umekipata basi ujue baadhi yetu hususan mimi binafsi umeniacha bila cha kushika cha kusonga nacho mbele.

Imenichukua miezi kama miwili kujiandaa na mada hii; Hii ni kwa sababu, siku zote nilikuwa nachukulia kero za muungano kwa mtazamo wa kisiasa zaidi; Lakini baada ya Lissu, ambae ni Mwanasheria by profession, kutoa hotuba yake Bungeni Mwezi Juni, 2012, na kutumia neno ‘kiini macho’, hii ilikuwa ni wake up call kwangu kwamba pengine mgogoro huu utaeleweka zaidi iwapo utaangaliwa kisheria zaidi kuliko kisiasa; Hivyo nikaamua kujifanyia utafiti wangu wa hapa na pale taratibu, na niliporidhika na facts nilizopata, nikaja na mada hii, chini ya title inayolenga kuendeleza neno “kiini macho”, ili kuipa longevity hoja ya Lissu ambayo nadhani ilikuwa ni muhimu sana lakini ikafa upesi sana;

Kama umekuwa unanisoma, hasa katika majibu yangu kwa washiriki wengine humu, najaribu sana kukwepa matumizi ya siasa katika kujenga hoja, na badala yake kujaribu kutumia zaidi hoja za kisheria, ingawa mimi sio mwanasheria; Nina amini kwamba, kuangalia mkataba huu kisheria ndio njia pekee ya kuelewa kiini macho hiki kipo wapi, lakini pia ndio njia pekee ya kuirudisha Tanganyika yetu, kwani haikufa kwa SIASA bali kwa SHERIA, kwa mujibu wa sheria ya bunge namba 24, 1967, na kupewa jina jipya la TANZANIA;

Kwahiyo mimibaba, maudhui yangu ndio hayo – kudadisi mgogoro uliopo kwa mtazamo wa kisheria zaidi, kwa imani kwamba tutaweza kuelewa chanzo cha mgogoro, lakini pia jinsi ya kuutatua mgogoro huu, ikiwa ni pamoja na kuifufua Tanganyika yetu;

Pamoja na yote, hujagusia kukosekana kwa hotuba ya TL kwenye Hansard, sijui ndiyo umeridhika au funika kombe.

Nilijadili kidogo suala hili, lakini kwa mtazamo wako, nini cha ziada ambacho ningeweza kukifanya? Kwa mamlaka gani niliyo nayo? Nadhani kitendo cha kuliweka hili hadharani ‘ON A HEAVY NOTE’, kilitosha kuamsha wadau wengine juu ya hilo, ili nao waje na mawazo juu ya jinsi gani ya kutatua tatizo hili, na kama watakuwa na muda, basi waanzishe uzi wao wa mjadala, kwani tutashiriki katika mjadala huo; Vinginevyo sikwenda mbali sana na hoja hii, hasa kutokana na mdau mwenzetu EMT kutuletea hotuba ile ambayo ipo kwenye ukurasa wa kwanza wa uzi huu, bandiko namba ‘8’;

Unapopewa changamoto na ambao wanakerwa na michango yako, tushirikishe nasi tuwachome zaidi maana hii fursa ni ya members na wageni kama hao wafaidike au wajitazame walivyo kama wanavyojitazama kwenye kioo.
Nimejaribu kwa namna mbali mbali kushirikisha wadau humu, hasa kwa kutumia maneno from time time kama vile – natumaini wadau wengine humu watapima mawazo kama haya na kukubaliana na mimi au lah; natumaini hoja yako kwamba hoja zangu zimejaa ushabiki kuliko sheria, itapimwa na wadau wengine, na wao ndio wanaweza kutusaidia zaidi katika kubaini hilo, n.k;

Nadhani tatizo hapa ni kwamba huwa naweka maombi yako haya katikati ya mabandiko yenye maelezo marefu, hivyo kumezwa na hoja husika; kwa ushauri wako, nifanyeje ili kufanikisha hili kwani nahitaji sana msaada kutoka kwa watu wanaokubaliana na mtazamo wangu, ingawa pia wale wanaopingana nao KISHERIA, kama wapo, nao watatusaidia sana katika kufanikisha maudhui na madhumuni ya mada hii, maudhui ambayo nimejaribu kuyafafanua hapo juu;

Nashauri utoe majumuisho kama update ili angalau tuende na maoni ya wengi.

Upo sahihi katika hili, pengine ni kweli nimechelewa kufanya hili, lakini naomba uelewe sababu ya hilo kutokea:
Kwanza, Sijapata maoni ya kutosha kutoka pande zote mbili yenye mtazamo wa kisheria (rejea maudhui na madhumuni yangu);

Pili, katika mijadala na hoja zangu, I am reasoning NOT TO WIN ARGUMENTS, BUT, TO FIND THE TRUTH; Kwa sababu hii, inawezekana nimekuwa dragged sana into searching for truth, kuliko kutengeneza notes za majumuisho;

Nitafanya hivyo muda sio mrefu;
 
Imetajwa katika ibara 98(1)(b) kuwa moja ya mambo ambayo mabadiliko yake yahitaji kuungwa mkono na mbili ya Wabunge wote kutoka Tanzania Bara na theluthi mbili ya Wabunge wote kutoka Tanzania Visiwani ni kuwapo kwa Jamhuri ya Muungano.

Ina maana Baraza la Wawakilishi Zanzibar halina mamlaka ya ku-repeal the UNION OF ZANZIBAR AND TANGANYIKA LAW 1964? Is the UNION OF ZANZIBAR AND TANGANYIKA LAW 1964 simply a statute with the same force as any other or a statute with a special status (eg. a constitutional Act) which could be repealed only with a special procedure?
 
Back
Top Bottom