Tundu Lissu: Mpambanaji aliyeuanza uanaharakati utotoni

Serekali iweke mapato na matumizi yote na katika kila wizara ili wananchi waweze kufanya perfomance evaluation kwanzia kitongoji kijiji mpk hapo kwa mkubwa ikulu hapo tutaenda sawa...
 
Kumbe hela zipo kila mwaka,wananchi wana lazimishwa kuchangia gharama za kuendesha shule,....mwishoni hela zinarudishwa hazina eti zimebaki,kweli?

Msome Tundu Lissu

Akirejea takwimu za mahesabu ya Tamisemi, alisema kwa mwaka wa fedha 2008/2009 na 2009/2010 zaidi ya shilingi bilioni 30 zilizotengwa na Bunge kwa shughuli za maendeleo zilirudishwa hazina.
“Tungependa kujua… nafikiri wananchi wa Tanzania wanapenda kujua hizi fedha zimerudi kweli hazina au zimetumika kwa mambo mengine tusiyoyajua.
“…Na ni sababu gani zilizofanya zisitumike wakati Watanzania nchi nzima wanachangishwa fedha kwa nguvu bila kuwepo sheria, bila kuwepo utaratibu wowote unaotambuliwa na sheria za nchi hii ili kujenga na kuendesha mashule.
“Hii ni moja ya sababu ya kupeleka hoja binafsi ya kutaka Bunge liichunguze hii ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ili Bunge linalotoa fedha liridhike kwamba kweli hizi fedha hazijatumika kweli au zimetumika kwa mambo mengine,” alisema

Kweli Tanzania ni zaidi ya uijuavyo. kumbe serikali ina madudu mengi sana. Najiuliza maswali kibao hapa wakati hizo hela zina tengwa sikuna miradi ililengwa , kwani huwezi mpamtu helabila sababu je hiyo miradi haikufanyika?na je hakuna mtu kama miradi imefanyika ama laa? sielewi inakuaje hela zinarudi wakati sis tunapata shida huku mtaani
 
kha halafu, kwani yale matundu ya choo kule msoga yaliyobadilishwa kuwa ghorofa la rz1 pale msamvu yalikuwa kwenye MTEF?
 
Ninavyoambiwa kuhusu huyu mtu, slaa hayuko bumngeni lakini cha moto watetezi wa mafisadi watakipata!
 
Hongera sana Tundu Lissu. Nchi inahitaji kina Lissu wengi na kina Hiza wachache zaidi mno!
 
Hiki kichwa bana.........I concur kabisa 100%


Akitangua kesi ya Dowans na kuokoa hizo billions zinazoibiwa nitamwamini zaidi. Ila kwa hilo nampa pongezi kwa umakini na nia njema ya kuinua maisha ya wana-Singapore!!!
 
Nakumbuka wakati wa kampeni T.Lissu aliwakataza wanasingida kulipa kodi holela za biashara na mazao,pia aling'oa vizuizi ya kulipia kodi barabari. Hapo alikuwa anaomba kura,je akikabidhiwa rungu kama mbunge inakuwaje?na tayari amekuwa mbunge,na hapo sinema inaanza!
 
Ili wabunge waweze kuifuatilia bajeti ya serikali kikamilifu na kisha waweze kuibana, ni muhimu kuomba serikali iwe inapatia wabunge vitabu vinavyoitwa Medium Term Expenditure Framework (MTEF). Vitabu ambavyo huwasilishwa kwa wabunge ni vile vye jumla kuu na wala siyo budget details. Hivyo wabunge hupitisha matumizi mabaya bila wao kujua, kisha mambo yakishafanyika eanahoji nani aliidhinisha.

Pili, wabunge wapewe vitabu vya bajeti at least 21 days kabla ya kikao cha bajeti, kama ilivyoelekezwa kwenye kanuni za kudumu za bunge. Hii itawapa fursa ya kuichambua bajeti na kuihoji badala ya kugonga meza na kuuliza maswali ambayo hayarejei bajeti.

Kwa mfano mbunge anauliza, ni lini daraja la mto X litajengwa, kwenye mjadala wa wizara ya miundombinu, wakati hilo ni swala la TAMISEMI. Au mbunge anauliza lini jimbo lake litaunganishwa kwenye gridi ya taifa badala ya kuelekeza waziri apunguze pesa kwenye kifungu fulani ili zitengwe kuunganisha jimbo lake kwenye gridi ya taifa.

Nachojaribu kusema ni kwamba, matatizo hayo mawili waliyoyataja Tundu na John, na matatizo mengine, yamesababishwa na wabunge kutokuwa makini wakati wa mijadala ya bajeti. Manunuzi ya mashangingi hupitishwa na wabunge. Safari za kifahari za viongozi hupitishwa na bunge. Kisha wabunge wanalalamika serikali inatumia pesa kwa matumizi yasiyo muhimu!!!

Nashukuru kwa mchango wako.

Pia wabunge wasaidie Wizara kwa sababu hata mwaka mmoja hazijawahi kutolewa pesa zote zilizoombwa kwenye bajeti. Ndiyo maana kuna kamchezo kanaitwa Funga Mwaka pesa zinatolewa mwezi wa mwisho kabla ya bajeti ambazo hazilingani na absorbtion ya Wizara. Wajanja wanazitafuna; huko wkenye Halmashauri wanazirudisha. Nadhani wabunge wafanye tathmini ya vitendo siyo ya makabrasha ambayo ni utaalamu tu wa uandishi na siyo hali halisi.

Kuna mchezo mwingine waku"negotiate" na maofisa wa hazina kuhusu upatikanaji wa fedha hata za wafadhili. Ni uppuuzi kwa sababu kama bunge limepitisha bajeti, basi itolewe kama ilivyoombwa na wabunge wahakikishe zimetumika ilivyokusudiwa wakati wote na hasa wakati wa kuomba bajeti ya mwaka unaofuata. Asipewe mtu ppesa mpaka maelezo yajitosheleze. Kurudisha fedha hazina enzi za mkoloni adhabu yake ni kufukuzwa kazi katibu mkuu na waziri wake.
 
Juzi nimeona tbc1 hospital ya mlandizi haina shuka hata moja,wagonjwa wanalalia plastic covers,halafu wanarejesha pesa hazina!
 
Siyo TAMISEM tuu mkuu kula mahali pesa inarudigi hazina tena nyingi mno!!! huku afya ndo utashangaa, hosp mbovu, vitanda vibovu, hamna dawa and working tools, mpaka wamama wanakuja kujifungua na vitu vyao!! But mkienda kwenye vikao vya budget unaambiwa mamilioni yamerudishwa tressury sa unajiuliza why the money zisinge tumika kufund some project hata tusolve tatizo moja moja kila mwaka unaambiwa sio matumizi yake!!

So what is the use of that money now! just kuzunguka ie kuja huku and kurudi hazina??? this is crazy yani the chronic one..! doesnt ring a bell kabisaa! Matatizo tunayo afu hela zinarudishwa hazina ni ukichaa ama ni nini..!

LISSU TUKO NYUMA YAKO HEBU LIJENGEE HOJA NZITO HILI KWA MAKINI HUU UOZO UMETUCHOSHA...!!

:shock:
 
Akirejea takwimu za mahesabu ya Tamisemi, alisema kwa mwaka wa fedha 2008/2009 na 2009/2010 zaidi ya shilingi bilioni 30 zilizotengwa na Bunge kwa shughuli za maendeleo zilirudishwa hazina.

"Tungependa kujua… nafikiri wananchi wa Tanzania wanapenda kujua hizi fedha zimerudi kweli hazina au zimetumika kwa mambo mengine tusiyoyajua.

"…Na ni sababu gani zilizofanya zisitumike wakati Watanzania nchi nzima wanachangishwa fedha kwa nguvu bila kuwepo sheria, bila kuwepo utaratibu wowote unaotambuliwa na sheria za nchi hii ili kujenga na kuendesha mashule.

"Hii ni moja ya sababu ya kupeleka hoja binafsi ya kutaka Bunge liichunguze hii ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa ili Bunge linalotoa fedha liridhike kwamba kweli hizi fedha hazijatumika kweli au zimetumika kwa mambo mengine," alisema

Mheshimiwa Pinda

Vote of no confidence inakunyemelea haswaaaaa hufurukuti na kujihami tena kama mambo ndio hayo wajuwa wananchi wengi wanakuwa excited with kind of this stories kwani serikali yetu haiwafanyi mambo ya kuwafanya wananchi wafuatilie hatua za maendeleo kwa wananchi wao.

Kila kukicha ni kuvurunda tuuuu hata kama wakifanya mazuri kesho limeharibika inakuwa ni kuuzunguka mbuyu kila kukicha. Kwanini nimesema hayo, kwani pia Jana kipindi cha marudio TBC1 waandishi wa habari wakiongea na Nchimbi na Nchimbi kusema waandishi waandike stories kwa umakini lakini ukirudi nyuma serikali yenyewe hajipangi vyema ni inavurunda na ndio kila kukicha nao wanajikuta kwa mabango.

Kuna siri nyingi wanazificha na kulipeleka taifa pasipo na kutulazimisha tukubaliane nao ndio hayo sasa Tundu Lisu anayasema Bil 30 zililudi ili iweje sasa ????
 
Angalia tbc kuna viroja bi.kiroboto amechakachua kura za maamuzi sasa wanaitxa majina juu ya marekebisho ya vifungu kwenye mswada wa sheria maadili ya mahakama
 
Bi.kiroboto alipoona ccm waliondani wanashindwa amegonga kengere ili waliotoroka warudi na wamerudi na watashinda
 
Back
Top Bottom