Tundu Lissu aibuka kidedea!!

TUKUTUKU

JF-Expert Member
Sep 14, 2010
11,765
4,033
Mahakama kuu kanda ya Dodoma ,jana ilitupilia mbali kesi iliyokuwa ikimkabili Mbunge wa singida mashariki Tundu Lissu (CHADEMA) na kusema kuwa kesi hiyo iliyofunguliwa kimakosa hivyo haiwezi kuendelea kusikilizwa.
Jaji Sivangilwa Mwagesi,alisema kuwa kesi hiyo ilikuwa na kasoro nyingi kutokana na vifungu vya kisheria na akasema haiwezezi kuendelea kusikilizwa mahakamani hapo.
Kesi hiyo ilifunguliwa na wanachama wawili wa CCM,Shaban Itambu na Pascal Hallu ambao wamewafungulia kesi ya kupinga matokeo Mbunge wa singida mashariki Tundu LISSU,msimamizi wa uchaguzi na mwanasheria wa serikali.
Hata hivyo wakati kesi hiyo ikifutwa jana,Lissu mwenyewe hakuwapo mahakamani baada ya kuelezwa kuwa aliharibikiwa na gari akiwa njiani kuja Dodoma ambapo aliwakilishwa na Ndugu yake Samson Mkotya ambaye alisema kuwa mbunge huyo alikuwa Morogoro baada ya juzi kuharibikiwa na gari lake.
Kufutwa kwa kesi hiyo ni ushindi kwa Tundu lissu ambaye tangu mwanzo wa kesi hiyo alionekana kujiamini zaidi na kusema kuwa kesi hiyo ingeishia katika hatua za mwanzo bila ya kufika mbali.
"Mimi nasema kuwa,kesi hii naisimamia mwenyewe na ninatambua kuwa haiwezi kufika mahali popote kwa kuwa imejaa makosa mengi ya kisheria ambayo kimsingi kama jaji ataamua kufuata haki hakuna kesi hapa,"alisema Lissu siku alipowasilisha ombi la kufutwa kwa kesi hiyo.
Mbunge huyo ambaye kitaaluma ni mwanasheria aliwasilisha kumbukumbu za hukumu za kesi nyingi ambazo zilifunguliwa kwa mtindo huo ambazo alisema kuwa yeye(Lissu) alizisimamia lakini alishindwa.
Baadhi ya kesi alizozinukuu Lissu ni pamoja na kesi ya John Mnyika na Charles Keenja,Joyce Chitende na Zainab Gama,John Jombi na Christopher Ole Sendeka ambazo alisema kuwa zote zilifunguliwa kwa mtindo huo lakini zilishindwa kuendelea.
Jana Jaji Silivangira alisema licha ya kifungu cha 111(b) ambacho Lissu alisema kuwa kimekosewa kutokuwa na mapungufu ya moja kwa moja,lakini kwa kutumia sheria hiyo katika kifungu 112(a),(b) bado ufunguaji wa kesi hiyo ulionekana kuwa na makosa.(Chanzo cha habari:Mwananchi 9 machi 2011,pp3).

Nawasilisha
 
Ilikuwa ni kupotezeana muda tu, Bora wangeendelea na shughuli zao kuliko kushinda mahakamani kwa kitu kisichofaa
 
Hivyo vijamaa vinapinga matokeo vimetoka wapi? Vilale mbele hukoooo....:Lissu endelea na kazi yako kusaidia jimbo letu masikini la Singida Mashariki.
Tuko pamoja, tulikuchagua wenyewe, tutakuunga mkono pia.....njaghamba iuhoma ilolo wang'u.........keep it up!
 
Hivyo vijamaa vinapinga matokeo vimetoka wapi? Vilale mbele hukoooo....:Lissu endelea na kazi yako kusaidia jimbo letu masikini la Singida Mashariki.
Tuko pamoja, tulikuchagua wenyewe, tutakuunga mkono pia.....njaghamba iuhoma ilolo wang'u.........keep it up!
Sio bure watakuwa walitumwa na watu wakubwa!!
 
Mahakama kuu kanda ya Dodoma ,jana ilitupilia mbali kesi iliyokuwa ikimkabili Mbunge wa singida mashariki Tundu Lissu (CHADEMA) na kusema kuwa kesi hiyo iliyofunguliwa kimakosa hivyo haiwezi kuendelea kusikilizwa.
Jaji Sivangilwa Mwagesi,alisema kuwa kesi hiyo ilikuwa na kasoro nyingi kutokana na vifungu vya kisheria na akasema haiwezezi kuendelea kusikilizwa mahakamani hapo.
Kesi hiyo ilifunguliwa na wanachama wawili wa CCM,Shaban Itambu na Pascal Hallu ambao wamewafungulia kesi ya kupinga matokeo Mbunge wa singida mashariki Tundu LISSU,msimamizi wa uchaguzi na mwanasheria wa serikali.
Hata hivyo wakati kesi hiyo ikifutwa jana,Lissu mwenyewe hakuwapo mahakamani baada ya kuelezwa kuwa aliharibikiwa na gari akiwa njiani kuja Dodoma ambapo aliwakilishwa na Ndugu yake Samson Mkotya ambaye alisema kuwa mbunge huyo alikuwa Morogoro baada ya juzi kuharibikiwa na gari lake.
Kufutwa kwa kesi hiyo ni ushindi kwa Tundu lissu ambaye tangu mwanzo wa kesi hiyo alionekana kujiamini zaidi na kusema kuwa kesi hiyo ingeishia katika hatua za mwanzo bila ya kufika mbali.
Mimi nasema kuwa,kesi hii naisimamia mwenyewe na ninatambua kuwa haiwezi kufika mahali popote kwa kuwa imejaa makosa mengi ya kisheria ambayo kimsingi kama jaji ataamua kufuata haki hakuna kesi hapa,alisema Lissu siku alipowasilisha ombi la kufutwa kwa kesi hiyo.
Mbunge huyo ambaye kitaaluma ni mwanasheria aliwasilisha kumbukumbu za hukumu za kesi nyingi ambazo zilifunguliwa kwa mtindo huo ambazo alisema kuwa yeye(Lissu) alizisimamia lakini alishindwa.
Baadhi ya kesi alizozinukuu Lissu ni pamoja na kesi ya John Mnyika na Charles Keenja,Joyce Chitende na Zainab Gama,John Jombi na Christopher Ole Sendeka ambazo alisema kuwa zote zilifunguliwa kwa mtindo huo lakini zilishindwa kuendelea.
Jana Jaji Silivangira alisema licha ya kifungu cha 111(b) ambacho Lissu alisema kuwa kimekosewa kutokuwa na mapungufu ya moja kwa moja,lakini kwa kutumia sheria hiyo katika kifungu 112(a),(b) bado ufunguaji wa kesi hiyo ulionekana kuwa na makosa.(Chanzo cha habari:Mwananchi 9 machi 2011,pp3).

Nawasilisha

Comrade Lissu, pamoja sana!!
 
Back
Top Bottom