Tunda Man hakupata ajali, kwanini aliongopa?

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Nov 22, 2012
1,985
1,282


Mnajua kuwa inasemekana kuwa Tunda Man hakuwepo kwenye ile ajali iliyotokea hivi karibuni?

Kama alikuwepo inawezekanaje apone ikiwa hajafunga mkanda na waliofunga wameumia na kulazwa?

Iweje waseme simu na camera zimepotea alafu waje wakamatwe navyo Mikumi?

Au mshikaji aliyaka michango ya pole??? Kwa kujisingizia ajali? Kama kweli kaomba basi mshikaji ana roho ya kinyama sana.

Magazeti yakaandika eti dereva wake, wakati alikuwa msanii mwenzake ndio mwenye show. ALIYEKUFA SI DEREVA WA TUNDA, ni msanii.

Mtu hujafunga mkanda, na gari ndio kama linavyo onekana, unatokaje ukiwa mzima, hujavunjika wala kuchubuka, na hukulazwa hospital, TUNDA ACHA UWONGO.

Halafu Tunda Man ana roho mbaya sana.

Njano5
0622845394
 
You raise me up...so i can stand on mountainsyou raise me up to more that i can be..

Tundamna nae ndivyo alivyokuzwa
 

Tena tunda man anadai alikua siti ya nyuma katikati na hakufunga mkanda, hayo alisema katika E news ya chanel 5!
Ukiangalia utagundua yule dogo mwingine ambaye alikua camera man wa marehemu ambaye alikua siti ya nyuma alivyokua anahojiwa anaonesha kabisa ana kama stress flani bado na ana michubuko,lakini tunda man anahojiwa analeta masihala mengi kama na yupo club,
TUNDA MAN M$3G3^109999
 

Tena tunda man anadai alikua siti ya nyuma katikati na hakufunga mkanda, hayo alisema katika E news ya chanel 5!
Ukiangalia utagundua yule dogo mwingine ambaye alikua camera man wa marehemu ambaye alikua siti ya nyuma alivyokua anahojiwa anaonesha kabisa ana kama stress flani bado na ana michubuko,lakini tunda man anahojiwa analeta masihala mengi kama na yupo club,
TUNDA MAN M$3G3^109999
Kweli kabisa, alafu jiulize huyo dogo mkanda umemchubua hivyo na kumbana mbavu,,, lkn,,, yeye Tunda Kashika vichuma vya viti vya mbele,,,

Kwa mshituko wa gari,,, ule,,,

Mikono yake isingeweza kuhimili mshindo wa gari hata kama ajali aliiona,,, na kwakuwa ajali aliiona na kama mikono ilifanikiwa kuendelea kushikilia LAZIMA ingevunjika.

Hata hivyo,, hata uwe na nguvu kiasi gani kwa gari jinsi lilivyo,, hakuna ambaye angeweza kujizuia asipigwe na kurushwarushwa ndani ya gari kama HAJAFUNGA MKANDA.

tunda muongo, haiwezekani alofunga mkanda aumie na aongee kwa maumivu alafu yeye asiyefunga mkanda achangamke vile..

Na kwa urongo huo, Tunda atakuwa ameiba vitu vya marehemu, ili ni jambo baya, na baya zaidi msanii mwenzako unamwita dereva wako kisa underground, wakati mshikaj aliomba kampani yako na alikuwa anakulipa.

Kwa kujua marehemu hazungumzi, akasema alingia gari la marehemu wengine wakiwa wamelala, na marehemu tu ndio aliyekuwa macho. Kasingizia kapata ajali ili achangiwe fedha sijui na wasanii wenzake sijui kuua soo la kuiba vitu vya marehemu anajua mwenyewe.

Ila jambo alofanya Tunda si zuri na la kukemewa na ni kukandamizana na kukatishana tamaa, sasa huyu dogo.aliyepona atawachukiliake mastar? atafikiliaje fani hii ya muziki na kiu ya kufanikiwa ikiwa camera na vitu vyake vinaibiwa na mtu ambaye kimsigi alitakiwa ndio wa kumsaidia????? Ndio Diamond anaendelea sababu HANA ROHO MBAYA.
 
Tunda man nahc hajasema ukweli ukiangalia anavyohojiwa majibu anayoyatoa kama hayana ukweli ila naamin naye ni jipu...
 
Tunda man nahc hajasema ukweli ukiangalia anavyohojiwa majibu anayoyatoa kama hayana ukweli ila naamin naye ni jipu...
kutaka michango, huruma, au huenda kweli wameiba VITU vya marehemu,,,, hii ni aibu sana, kwan mshikaj mziki haumlipi hadi awe na njaa hiz?
 
Nani alikwambia kapata ajali?mbona huwa hampendi kusoma na kuelewa?hakuwemo kwenye hiyo gari yake bali promoter wake ndiye aliyekuwa akiiendesha
 
Unaniambia kuhojiwa studio au kwenye ajali?ajali itokee kwingine unaleta hekaya,mara roho mbaya mara hakufunga mkanda!ndiyo maana inaitwa ajali.unaweza ukapona kwenye ajali kubwa na ukaumia sana kwenye ajali ndogo
 
Sasa kama alikua kwenye ajali iweje akamatwe mbele huko akiwa na vifaa vya watu waliokuwemo kwenye gari iliyopata ajali? Aua yeye ilipotokea ajali akatoka akachukua vifaa akapanda gari nyingine wakaondoka wakawaacha wenzao walioumia? Huo ulikua ni mchoro na all people waliokuwemo kweli ile gari they needed to dead but badluck watu hawakufa wote mchoro umevuja. Jicho la tatu limetumika hapa, hidden spirit. Hako kajamaa ni shida katika upande wa pili
 
Tundaman alikuwa kwenye gari nyingine ,mbona dogo marijani anaeleza vizuri tu!km waliiba ni issue nyingine
 
Unaniambia kuhojiwa studio au kwenye ajali?ajali itokee kwingine unaleta hekaya,mara roho mbaya mara hakufunga mkanda!ndiyo maana inaitwa ajali.unaweza ukapona kwenye ajali kubwa na ukaumia sana kwenye ajali ndogo
Gari ya Tunda? Sasa kama hakupata ajali kama ulivyosema hapo awali hoja za kuponyeka unazileta za nini??? AJALI ile huwezi kuponyeka bila kuvunjika au kuchubuka,,,, VIDEO hiyo,,, Tunda angekuwa japo na mchubuko wa kucha angeuonesha sababu katika kujieleza kwake anaonekana anatumia nguvu kuthibitisha kuwa alikuwako katika gari ya ajali.

Sasa ni ajabu hana hata mchubuko wa kuonesha kuwa alipata ajali, hakukwenda hospitali kutibiwa zaid ya kumpeleka huyo aliyeumia.

Katika ajali kupona kupo, lkn si kwa ajalo hii,,, ajali hii bila mkanda kupona ni ngumu,,,, kwanini mfunga mkanda na waliokuwa wote siti ya nyuma aumie lkn TUNDA ambaye hakufunga MKANDA atoke bila mchubuko??? kwanini asingerushwa na kupigizwa ndani ya gari???
 
Tundaman alikuwa kwenye gari nyingine ,mbona dogo marijani anaeleza vizuri tu!km waliiba ni issue nyingine
SASA TUNDA ANASEMA YEYE ALIKUWA KATIKA GARI ILIYOPATA AJALI, na ya kwamba yeye alikuwa na marehemu gari moja,,, kwanini ang'ang'anize kuwa alipata AJALI??? tazama video....
 
Labda mwenzenu vampire alikuwepo kweli kwenye ajali ila akajirudi kupona....akiwaambia yeye vampire mtaamini???? Hahahahahha joking guys....In reality jamaa kadanganya kwamba ni miongoni mwa waliokuwamo ndani ya gari lililopata ajali but kwa maelezo yake SIO KWELI and honestly "I DON'T BELIEVE HIM"
 
Tobaaaa,Dogo aliepona atasema ukweli kama Tundaman alikuwepo ktk gari au laaa
TAZAMA video, dogo aliyekuwako ktk gari ya ajali kaumia lkn kapona na kasema tunda hakupata ajali,,,, TUNDA kasema alikuwako katika gari ya ajali, lkn hakufunga MKANDA,,, sasa kwanini ASIUMIE japo kwa kuchubuka tu??? ile ajali kwa asofunga mkanda kutoka kuwa mzima au bila kuumia NDOTOOOOOO, tunda muongo.
 
Back
Top Bottom