~*~ Tunawaudhi ~*~

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Ndiyo Tunawaudhi!!

Wanakaa chini na kujiuliza kwanini tunawafuata fuata! Wanakereka tunapoandika na kuwajadili na wanaona tunawaandama pasipo sababu ya msingi. Wanachukia na wangekuwa na uwezo wangesha tubamiza kama mtu anavyobamiza nzi ukutani!

Tumekuwa kwao kero isiyokoma, wasumbufu waliotumwa, na watu wenye wivu na maendeleo "yao". Wanakasirika na kununa, wanachukia na kuchukizwa! Tukipita wanatema mate pembeni, na tukiwasalimia hadharani wananyosha mkono kibahili! Wameudhika!!

Tumewaudhi kwa sababu suala la EPA lilitakiwa limalizwe kimya kimya, na sakata la Richmond lilikuwa limeshatolewa "maelezo". Tumewaudhi kwa sababu suala la Kiwira linamhusu "Rais Mstaafu" ambaye tuliambiewa tumuache "mzee wetu astaafu kwa amani". Wameudhika, na tena wamekereka.

Tumewaudhi kwa sababu tumeenndelea kuwahoji hata baada ya kuambiwa mtu kafa; Na tunaendelea kuwaudhi kwa sababu inaonekana tumekuwa watukutu tusiosikia, hatuelewi majibu yao na zaidi ya yote tumekuwa kama luba tumewang'ang'ania kwenye miguu yao ikimbiliayo maovu na ifanyayo haraka kuharibu!

Ndugu zangu, tumewaudhi na tunaendelea kuwakera; wakikaa ofisini kusaini mikataba mipya wanafikiria mara mbili sasa; wakitangaza tenda wanaulizana kama kuna maslahi binafsi yaliyofichwa; Wamebaki wenyewe kushukiana na kuhisiana ubaya na sasa wanazungukana kama watoto wanaocheza "kioo kioo"! Ajulikani nani hasa kakivunja! Wamebakia kuulizana huku wengine wamejificha "tiari bado"?!

Ndio wanakerwa na uwepo wetu, wanachukizwa na uthubutu wetu, wangelikuwa na uwezo kama wa paka kumrukia panya wangedaka mawazo yetu, kuyararua na kuyaweka kiporo ili wayachezee kesho yake! Wangekuwa na uwezo wangetukwapua kama kinyonga akwapuavyo vipepeo na kutubamiza kwenye ndimi zao za moto, na kufumba vinywa vyao kwa ghafla kama mamba wafanyavyo pembezoni mwa Rufiji!

Wanajiuliza kwanini tunawafuatafuata, kwanini hatuwaachi wafanye "kazi", kwanini tunafuatilia matendo na maneno yao wakati wao ndio "viongozi"? Wanashangaa kwanini wakisema mambo ya "vijisenti" kauli zao zinakuzwa kama kwa baragumu! Hawaelewi, wamebakia kuchukizwa na kukerwa!

Ndiposa, sisi sote tunaitwa kufanya uamuzi; aidha kusalimu amri na kuwaacha wapumue kidogo? au kukaza uzi ule ule. Tuna uamuzi wa kukubali maelezo yao ya juu juu au kuendelea kuwachimba kwa maswali ya ziada; tuna uamuzi wa aidha kuwaonea huruma kwa sababu familia zao na jamaa zao wamefadhaishwa na kufedheheshwa au kuendelea kwa sababu kwa maamuzi yao wametufadhaisha na kutufedhehesha sisi kama taifa! Tukubali majibu yao ya awali na turidhike?

Tunaitwa kufanya uamuzi; kujipanga mstari na kupiga makofi na kuwaimbia nyimbo za shangwe au kukaa kimya na kusubiri tuone wanachofanya nini ili tuamue sawasawa. Tunaitwa kufanya uamuzi wa kukubali kutawaliwa nao jinsi wapendavyo, au kuwalazimisha kutambua tunavyopenda kutawaliwa nao! Yes! Tunaoumauzi pia wa hata kuamua kama tunataka waendelee kututawala tena au hii ndiyo iwe ngwe ya mwisho kwao!

Kama wewe ni Mtanzania na mzalendo wa kweli, bila kujali hali yako ya maisha, elimu yako au nafasi yako ya kisiasa na kijamii, bila kujali kama wewe ni mfurukutwa au mkeretwa, bila kujali kama unafuata mrengo wa kulia au wa kushoto au kama itikadi yako ni ya kijamaa au ya kibepari; kama kweli una mapenzi na taifa lako, kama kweli unataka Tanzania ije kusimama kama Taifa la watu walio huru kweli na sawa; Taifa ambalo ndani yake kila mmoja ana nafasi sawa ya kufanikiwa; Taifa ambalo ndani yake wana na mabinti wake wanaona fahari kulitumikia na siyo kulitumia, kuliendeleza na sio kulitelekeza, kuliinua na siyo kulifumua! Taifa la kisasa, Taifa la Kiafrika, na Taifa ambalo kwa mafanikio na fahari litasimama katika jamii ya Mataifa ya ulimwengu!

Basi tunaitwa kufanya uamuzi, na uamuzi huo kwa hakika utakuwa ni wa kuwaudhi na kuwakera watu fulani fulani. Je uko tayari kuwaudhi mafisadi? Je uko tayari kuwakera waliokwiba fedha za Taifa letu? Je uko tayari kuwasumbua usiku kucha waliobaka raslimali za Taifa letu huku wanatuchekelea na kujilamba vinywa vyao huku wakipangusa ala zao?

Najua mimi niko tayari! sijui wewe.. lakini huko tunakokwenda, ni wale walio tayari kusimama peke yao na pweke ndio wataliinua Taifa letu na kulifanya liwe jinsi ile tulitamanivyo liwe! Stand up and be counted otherwise sit down and be forgotten!
 
nothing new ! yooooote yameongelewa kwenye threads lukuki humu, whats new ? NOTHING.... sasa propaganda kama kawaida ! haya wazee msifieni saddam hussein huyoooooooooooooo.....anakuja ! muimbieni nyimbo nzuri nzuri na mumtupie maua ili afurahi !
 
Ndiyo Tunawaudhi!!

Wanakaa chini na kujiuliza kwanini tunawafuata fuata! Wanakereka tunapoandika na kuwajadili na wanaona tunawaandama pasipo sababu ya msingi. Wanachukia na wangekuwa na uwezo wangesha tubamiza kama mtu anavyobamiza nzi ukutani!

Tumekuwa kwao kero isiyokoma, wasumbufu waliotumwa, na watu wenye wivu na maendeleo "yao". Wanakasirika na kununa, wanachukia na kuchukizwa! Tukipita wanatema mate pembeni, na tukiwasalimia hadharani wananyosha mkono kibahili! Wameudhika!!

Tumewaudhi kwa sababu suala la EPA lilitakiwa limalizwe kimya kimya, na sakata la Richmond lilikuwa limeshatolewa "maelezo". Tumewaudhi kwa sababu suala la Kiwira linamhusu "Rais Mstaafu" ambaye tuliambiewa tumuache "mzee wetu astaafu kwa amani". Wameudhika, na tena wamekereka.

Tumewaudhi kwa sababu tumeenndelea kuwahoji hata baada ya kuambiwa mtu kafa; Na tunaendelea kuwaudhi kwa sababu inaonekana tumekuwa watukufu hatusikii, hatuelewi majibu yao na zaidi ya yote tumekuwa kama luba tumewang'ang'ani kweny miguu yao ikimbiliayo maovu!

Ndugu zangu, tumewaudhi na tunaendelea kuwakera; wakikaa ofisini kusaini mikataba wanafikiria mara mbili sasa; wakitangaza tenda wanaulizana kama kuna maslahi binafsi yaliyofichwa; Wamebaki wenyewe kushukiana na kuhisiana kuwa wanazungukana kama watoto wanaocheza "kioo kioo"! Ajulikani nani hasa kakivunja!

Ndio wanakerwa na uwepo wetu, wanachukizwa na uthubutu wetu, wangelikuwa na uwezo kama wa paka kumrukia panya wangedaka mawazo yetu, kuyararua na kuyaweka kiporo ili wayachezee kesho yake! Wangekuwa na uwezo wangetukwapua kama kinyonga akwapuavyo vipepeo!

Wanajiuliza kwanini tunawafuatafuata, kwanini hatuwaachi wafanye "kazi", kwanini tunafuatilia matendo na maneno yao wakati wao ndio "viongozi"? Wanashangaa kwanini wakisema mambo ya "vijisenti" kauli zao zinakuzwa kama kwa baragumu! Hawaelewi, wamebakia kuchukizwa na kukerwa!

Ndiposa, sisi sote tunaitwa kufanya uamuzi; aidha kusalimu amri na kuwaacha wapumue? au kukaza uzi ule ule. Tuna uamuzi wa kukubali maelezo yao ya juu au kuendelea kuwachimba kwa maswali ya ziada; tuna uamuzi wa aidha kuwaonea huruma kwa sababu familia zao na jamaa zao wamefadhaishwa na kufedheheshwa au kuendelea kwa sababu kwa maamuzi yao wametufadhaisha na kutufedhehesha sisi kama taifa!

Tunaitwa kufanya uamuzi; kujipanga mstari na kupiga makofi na kuwaimbia nyimbo za shangwe au kukaa kimya na kusubiri tuone wanachofanya nini ili tuamue sawasawa. Tunaitwa kufanya uamuzi wa kukubali kutawaliwa nao jinsi wapendavyo, au kuwalazimisha kutambua tunavyopenda kutawaliwa nao! Yes! Tunaoumauzi pia wa hata kuamua kama tunataka waendelee kututawala tena au hii ndiyo iwe ngwe ya mwisho kwao!

Kama wewe ni Mtanzania na mzalendo wa kweli, bila kujali hali yako ya maisha, elimu yako au nafasi yako ya kisiasa na kijamii, bila kujali kama wewe ni mfurukutwa au mkeretwa, bila kujali kama unafuata mrengo wa kulia au wa kushoto au kama itikadi yako ni ya kijamaa au ya kibepari; kama kweli una mapenzi na taifa lako, kama kweli unataka Tanzania ije kusimama kama Taifa la watu walio huru kweli na sawa; Taifa ambalo ndani yake kila mmoja ana nafasi sawa ya kufanikiwa; Taifa ambalo ndani yake wana na mabinti wake wanaona fahari kulitumikia na siyo kulitumia, kuliendeleza na sio kulitelekeza, kuliinua na siyo kulifumua! Taifa la kisasa, Taifa la Kiafrika, na Taifa ambalo kwa mafanikio na fahari litasimama katika jamii ya Mataifa ya ulimwengu!

Basi tunaitwa kufanya uamuzi, na uamuzi huo kwa hakika utakuwa ni wa kuwaudhi na kuwakera watu fulani fulani. Je uko tayari kuwaudhi mafisadi? Je uko tayari kuwakera waliokwiba fedha za Taifa letu? Je uko tayari kuwasumbua usiku kucha waliobaka raslimali za Taifa letu?

Najua mimi niko tayari! sijui wewe.. lakini huko tunakokwenda, ni wale walio tayari kusimama peke yao na pweke ndio wataliinua Taifa letu na kulifanya liwe jinsi ile tulitamanivyo liwe!

Inawaumiza wakiona hatugive up, inawaumiza wakiona kila asubuhi, mchana na jioni tuko hapa kuyafukua mambo yao. Inawaumiza kuona kuwa kwa sasa kuna ushirikiano mkubwa kati yetu na media ya bongo. Inawatia kiwewe na woga, wanalala wakijiuliza, hivi ni kesho watanzania wote wataandamana kudai haki zao?

Huu ni mwanzo, najua inagharimu kupiga simu, najua inagharimu kuendesha site kama hii, najua inagharimu kutafuta mikataba ya siri na kuiweka hapa. lakini huu ni mwanzo tu, ni mwanzo wa kukomboa taifa letu, ni mwanzo wa kurudisha ardhi na mali yetu toka mikononi mwa wezi na watu wasio na hay.

Hata kama wakitumia fujo na nguvu ya dola, bado haki ya mnyonge itatetewa na wenye moyo na nia thabiti. Huu ni mwanzo mzuri mwanakijiji, MUNGU yuko upande wa haki na upande wetu..... mwishoni tutashinda!
 
mke wa saddam huyooooooo ........... nae atupiwe maua jamani na mumuimbie nyimbo nzuri ili afurahi !!

PROPAGANDA HAILALI HADI IELEWEKE !!
 
mke wa saddam huyooooooo ........... nae atupiwe maua jamani na mumuimbie nyimbo nzuri ili afurahi !!

PROPAGANDA HAILALI HADI IELEWEKE !!

Kada,
Tupe solution yako. Tanzania leo siyo nchi ya asali na maziwa. Hivyo vimeshanyakuliwa na wajanja wachache wakishirikiana na akina Sinclair.
Tupe jibu, badala ya kukebehi maoni ya wenzako ambao wanatafuta ufumbuzi kwa Tanzania tunayoitaka.
 
Kada,
Tupe solution yako. Tanzania leo siyo nchi ya asali na maziwa. Hivyo vimeshanyakuliwa na wajanja wachache wakishirikiana na akina Sinclair.
Tupe jibu, badala ya kukebehi maoni ya wenzako ambao wanatafuta ufumbuzi kwa Tanzania tunayoitaka.

sijakebehi, ila ninachosema ni kwamba, yooote aliyogusia HAMNA JIPYA, na kama unaandika kitu basi lazima uwe AIM ya kuandika, hadi hivi sasa sijaona chochote kipya, na kama solutions nadhani zilishatolewa before katika threads husika !

asante !
 
KM,
Hata kama hamna jipya kuna haja ya kujikumbusha hapa tulipo ili tuweze kubuni hatua inayostahili kuchukuliwa ili tujikwamue.
 
KM,
Hata kama hamna jipya kuna haja ya kujikumbusha hapa tulipo ili tuweze kubuni hatua inayostahili kuchukuliwa ili tujikwamue.

Nimekupata, basi nitaanza kumwagia maua na kuimba nyimbo ili saddam afurahi au sio bila ya kumsahau na bi. saddam ...!lol. anyway tupo pamoja !
 
Mwanakijiji

Unaona jinsi SI's wanavyohaha, Tanzania ni ya WTZ wote na sio kwa wale wanaofikiri kwamba wameteuliwa kutafuna pesa ya walipa kodi na vikaragosi vyao. wataulizwa na kuwajibishwa - Pesa ya walipa kodi sio ya kuichezea upatu.
 
Mwanakijiji

Unaona jinsi SI's wanavyohaha, Tanzania ni ya WTZ wote na sio kwa wale wanaofikiri kwamba wameteuliwa kutafuna pesa ya walipa kodi na vikaragosi vyao. wataulizwa na kuwajibishwa - Pesa ya walipa kodi sio ya kuichezea upatu.

wee unalipa kodi wapi ?? wangapi humu jf mnalipa kodi tanzania ??
 
Dua.. hakuna kitu kibaya kama mazoea. Mazoea ndiyo yaliyotufikisha hapa na kujaribu kubadili mawazo au mwelekeo watu hujikuta wanakabiliwa na changamoto ya kuachana na mazoea. Kwa wengine hilo ni unthinkable. Wanataka tufanye mambo vile vile na ni wepesi kukebehi ukweli hata ukiwakodolea macho.

Lakini yote ni sehemu ya mapambano ya fikra ambayo mwanzo wake ni kujiamini. Watanzania pole pole wameanza kujiamini na kutambua kuwa Taifa hili si la watu wachache (kama alivyosema mama Malecela) na ya kuwa kikundi cha watu wachache hawawezi hata kidogo kumiliki nchi nzima kana kwamba wanamshikia mtoto kitu halafu wanammegea kidogo kidogo.

Hivyo mawazo yanayotolewa na jamii kama JF, vyombo vya habari, taasisi huru na mashirika binafsi vimeanza kuwa kero. Na sasa tumefikia mahali mstari unaanza kuchorwa vizuri kabisa kati ya serikali na CCM kiasi kwamba CCM kama chama kimeanza kugawanyika ndani kwa ndani huku serikali ikijaribu kwa kila namna kutafuta nafasi yake katika Tanzania yetu mpya.

Haya ni mabadiliko ya lazima. Hivyo hata wale ambao wanachaguliwa au kuteuliwa kushika nafasi yoyote sasa wanajikuta wanapokea kwa wasiwasi kwa sababu wanajua darubini za watanzania na kurunzi zao zimeelekezwa kwao.
 
yellow_flowers_T1684.jpg


fresh tulips kwa mheshimiwa saddam hussein ! mwenye nyimbo amtungie shairi sasa hivi kabla hajakasirika kabla hajaamuwa watu wawe executed(kufungiwa)!
 
wee unalipa kodi wapi ?? wangapi humu jf mnalipa kodi tanzania ??

Nalipa kodi Tanzania au unataka nikupe namba yangu? Hivi unafikiri ukikaa nje ndio hulipi kodi? Hii ni karne ya 21 sio ya 19 amka! Hayo ni mawazo ya kufilisika na kuishiwa na hoja badala yake unaleta viroja. Unataka nikutangazie? Naona limekuuma hili hivi na wewe ni moja wa wale wanaotafuna pesa ya walipa kodi?
 
Nalipa kodi Tanzania au unataka nikupe namba yangu? Hivi unafikiri ukikaa nje ndio hulipi kodi? Hii ni karne ya 21 sio ya 19 amka! Hayo ni mawazo ya kufilisika na kuishiwa na hoja badala yake unaleta viroja. Unataka nikutangazie? Naona limekuuma hili hivi na wewe ni moja wa wale wanaotafuna pesa ya walipa kodi?

ndio nipe info zote ! NIHAKIKISHE ! pesa yako ya box sina haja nayo ! lete ma-info hayo watu tumeki shua kama unalipa kodi, kama hulipi basi argument yako mdebwedo !

usiponipa hizo namba/info NAWE FISADI PIA !
 
ndio nipe info zote ! NIHAKIKISHE ! pesa yako ya box sina haja nayo ! lete ma-info hayo watu tumeki shua kama unalipa kodi, kama hulipi basi argument yako mdebwedo !

Nikupe wewe kama nani? Mtetezi wa mafisadi? SIKUPU NG'O ....Hapa umehola unafikiri mimi kama wewe? Endelea kutafuna pesa ya walipa kodi lakini kumbuka utakapokuwa Keko wakati ukifika utakumbuka haya maneno.

Hivi ujuzi wako wote huwezi kuona swali lililoulizwa....Au ina maana gani?Jifunze kiswahili fasaha kabla hujarukia keybord hatuko kwenye kilabu cha walevi hapa.
 
Nikupe wewe kama nani? Mtetezi wa mafisadi? Hapa umehola unafikiri mimi kama wewe? Endelea kutafuna pesa ya walipa kodi lakini kumbuka utakapokuwa Keko wakati ukifika utakumbuka haya maneno.

Hivi ujuzi wako wote huwezi kuona swali lililoulizwa....Au ina maana gani?Jifunze kiswahili fasaha kabla hujarukia keybord hatuko kwenye kilabu cha walevi hapa.

Nalipa kodi Tanzania au unataka nikupe namba yangu? Hivi unafikiri ukikaa nje ndio hulipi kodi? Hii ni karne ya 21 sio ya 19 amka! Hayo ni mawazo ya kufilisika na kuishiwa na hoja badala yake unaleta viroja. Unataka nikutangazie? Naona limekuuma hili hivi na wewe ni moja wa wale wanaotafuna pesa ya walipa kodi?

maskini wee, si umeuliza mwenyewe kama unipe nikasema NDIO NIPE sasa unatoa jazba, wewe mtu wa wapi lakini ?? au ulikuwa unadhani nitakwambia unavyotaka wewe kusikia (kwamba usinipe)!! TOA NAMBA HIYO ! USIPOTOA WEWE FISADI ! umesema mwenyewe dua !

kama pesa zako za kodi hazitumiwi kama unavyotaka, (in this case hulipi kodi tanzania) then wakabe shati viongozi wa nchi husika unayolipa kodi/.
punguza jazba babu hii sio ligi !
 
Nikupe wewe kama nani? Mtetezi wa mafisadi? Hapa umehola unafikiri mimi kama wewe? Endelea kutafuna pesa ya walipa kodi lakini kumbuka utakapokuwa Keko wakati ukifika utakumbuka haya maneno.

Hivi ujuzi wako wote huwezi kuona swali lililoulizwa....Au ina maana gani?Jifunze kiswahili fasaha kabla hujarukia keybord hatuko kwenye kilabu cha walevi hapa.

Dua,

mwenzako hajui kuwa hii statement ni swali, hakuona hiyo alama ya kuuliza;

Dua said:
Nalipa kodi Tanzania au unataka nikupe namba yangu?
 
Nalipa kodi kubwa kuliko mafisadi wote wa Tanzania. Ndio Nimesema. Kodi ninayolipa tena kihalali bila hata kufuatwa ni kubwa kuliko wanayolipa Mafisadi

kila mtu anaweza kusema unachosema wewe ! au unataka humu watu waanze mchezo wa kusema, "me toooooo"(kwamba nao pia wanalipa)..........proove plz kwamba unalipa kodi ??
 
Back
Top Bottom