Tunashuhudia amani kwa mara ya mwisho Tanzania

Tatizo tulilo nalo kwa sasa ni kwamba viongozi wetu wakuu wanapenda sana udini na wanaulea. Na sijui wanafanya hivi kwa maslahi ya nani.Sheikh Ponda kaanza uchokozi siku nyingi lakini akina mwema wamekuwa wakimchekea tu. Anatukana Wakristo lakini Mwema na viongozi wengine wa juu wanamchekea tu. Uamusho nao wameanza uchochezi muda mrefu lakini si Rais wa Jamhuri wa wa Zanzibar aliyewakemea. Wameachwa mpaka amani ya nchi inatishiwa. Lakini viongozi wamekuwa hawachukui hatua zozote. Jamani hii nchi viongozi mnaipeleka wapi? Mnataka Watanzania wachinjane? Mnaongoza kwa kufuata katiba ipi ambayo mliapa kuilinda? aaT
Viongozi wa kasheshe hizi sio wazawa kumbe wa TZ ??? Mhh kweli changanya na zako. Mimi naamini bado tunaweza kuilinda amani yetu. Ila ukweli kabisa serikali inahusika kabisa kuvuraga amani hii. Lazima wote tuheshimu sheria za nchi na uhuru wa kuabudu. Vikundi vyote vya kichochezi na ambavyo havifanyi kazi kwa mujibu ya maombi ya usajili wao vifutwe. Na wale wote wanaotumia dini kuvunja sheria waathibiwe kwa kosa lao sio kosa la kidini. Mungu atusaidie kwani wote walianza hivi hivi mwisho wakimbizi. Hauna sehemu nzuri ya kuishi kama TZ kama hamwamini leteni kasheshe tuwe wakimbizi halafu tutasomanamba.
 
Kumbe Nyerere alikuwa Dokta?!! Aisee huyu mzee hakupenda kabisa kujikweza

DSCF0031.JPG DSCF0032.JPG
 
Jana asubuhi kulikuwa na ripoti za kijana wa kiislamu huko zanzibar aliyekojolea q'uran na kumvalisha mbwa tasbihi(?) Nataka kujua tu ni lini tutaandamana kulaani tukio hilo na kuchoma majumba ya ibada??!
 
ukione hivyo ujue kwamba ubepari ni hatari sana hasa kwa taifa ambalo linasemekana ni la kijamaa.vitusho,mauaji,ujambazi,dhuruma,ugaidi na utekaji nyara ni vitu vya kawaida kabisa kwa mataifa ya kibepari.yahitaji moyo wa ujasiri maana joto litazidi kupanda kuelekea 2015.
 
Niliumia sana wakati nasikiliza hii makala hasa pale walipokuwa wanachangia raia Burundi baada ya kuongea kwa uchungu sana na kutuonea huruma,nitamnukuu mmoja wao:"Tanzania 2liyokuwa 2naiona kisiwa cha amani sasa wameanza machafukio,ninawaonea huruma sana"!kwa kweli kwa ha2a 2liyofikia serikali inabidi ivunje ukimya wake wa muda mrefu wa kuto ku "comment" chochote kile kuhusu dini!.
 
Jana asubuhi kulikuwa na ripoti za kijana wa kiislamu huko zanzibar aliyekojolea q'uran na kumvalisha mbwa tasbihi(?) Nataka kujua tu ni lini tutaandamana kulaani tukio hilo na kuchoma majumba ya ibada??!

Huo ni uzushi au kwa habari zaidi waulize radio wapo
 
hakuna anayemkumbuka nyerere kwani pamoja na uzuri wake katenda mabaya mengi sana na yeye ndio muasisi wa udini tanzania na chuki za kidini, laanatullah na aendelee kupata adhabu huko aliko, angeweka utawala usiokuwa na upendeleo wa upande mmoja wala tusingechukiana, ila yeye kabase sana kanisani na amefanya kanisa ndio serikali na kutudidimiza waislamu, so sidhani kama ni wakukumbukwa cha kufanya ni kuomba dua azidi kuadhibiwa
 
tanzania haina amani kwa kuw wapo watu wameshiba wengine wana njaa halafu wenye njaa wanabezwa eti hawajaenda shule eti wanaenda tu madrasa mbona watu wako biased kiasi hk halafu useme kuna amani
 
[h=5][SUB]Mwenye dhamana ya kulinda amani ni mimi mwenyewe, wewe mwenyewe na yeye bila kujali itikadi zetu za dini. Serikali haiwezi kutulindia amani kwa maana nayo inaongozwa na binadamu ambao pia wanaweza kuwa na mioyo mizuri au mibaya! Amani inalindwa na mimi, wewe na yule na si serikali #Nakupenda Tanzania.[/SUB][/h]
 
Kawaida kila mlinzi huwa ana japo kijisilaha/kilindio, je, wewe unashauri tutumie silaha gani kuilinda hiyo amani ya Tanzania.
 
[SUB]Mwenye dhamana ya kulinda amani ni mimi mwenyewe, wewe mwenyewe na yeye bila kujali itikadi zetu za dini. Serikali haiwezi kutulindia amani kwa maana nayo inaongozwa na binadamu ambao pia wanaweza kuwa na mioyo mizuri au mibaya! Amani inalindwa na mimi, wewe na yule na si serikali #Nakupenda Tanzania.[/SUB]
Mkuu Logo umetoa wazo zuri sana na nimelipenda, lakini lenye walakini mkubwa katika nia hasa ya kulinda amani na wajibu wa nani anajukumu la kulinda amani na kivipi,
Ninakubaliana na wewe kwamba kila mtu anajukumu la kulinda amani, Lakini unaposema kuwa serikali haina jukumu la kulinda amani, ni wazi unakuwa unajaribu kujipofusha macho kimakusudi na kujaribu kutetea serikali ukiwa umefumba macho.
Labda nikuulize swali moja tu, kunapotokea dalili za au viashiria vya amami kutoweka ni nani mwenye mamlaka halali ya kuchukua hatua kama sio serikali?.
Nina kila sababu ya kuamini kuwa umekurupuka.
 
Mkuu Logo umetoa wazo zuri sana na nimelipenda, lakini lenye walakini mkubwa katika nia hasa ya kulinda amani na wajibu wa nani anajukumu la kulinda amani na kivipi,
Ninakubaliana na wewe kwamba kila mtu anajukumu la kulinda amani, Lakini unaposema kuwa serikali haina jukumu la kulinda amani, ni wazi unakuwa unajaribu kujipofusha macho kimakusudi na kujaribu kutetea serikali ukiwa umefumba macho.
Labda nikuulize swali moja tu, kunapotokea dalili za au viashiria vya amami kutoweka ni nani mwenye mamlaka halali ya kuchukua hatua kama sio serikali?.
Nina kila sababu ya kuamini kuwa umekurupuka.

Kwanza nakupongeza wewe ni msomi comment yako imenifurahisha, sukari...sukari...sukari..chumvi...chumvi...na baadaye chunguuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu ahahahah!

Ukweli ni kwamba nimekosea tu mkuu, lengo langu lilikuwa "Tusikae kusubiri serikali itutekeleezee kutulindia amani, kwani nayo inawatu kama sisi wenye mioyo mizuri au mibaya so jukumu lenye kuleta faida litoke kwetu sisi" Ya serikali ni matokeo.
 
Kwanza nakupongeza wewe ni msomi comment yako imenifurahisha, sukari...sukari...sukari..chumvi...chumvi...na baadaye chunguuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu ahahahah!

Ukweli ni kwamba nimekosea tu mkuu, lengo langu lilikuwa "Tusikae kusubiri serikali itutekeleezee kutulindia amani, kwani nayo inawatu kama sisi wenye mioyo mizuri au mibaya so jukumu lenye kuleta faida litoke kwetu sisi" Ya serikali ni matokeo.
Mkuu sana Logo, japo nimecheka kwenye sukariii, chumvii na kisha chunguu,(teh, teh, teh)lakini avha tuendelee,
Watanzania hawana tatizo kabisa kuhusu kulinda amani ya nchi yao, wamekuwa wavumilivu mno hata kwa kutowajibika kwa serikali kwa nia tu ya kulinda amani ya nchi yao iliyoasisiwa na muasisi wa taifa letu Mwalimu JK Nyerere,
Kwa mfano kuhusu suala la udini kwa sasa, Tanzania ilikuwa shwari mpaka ulipoingia utawala wa awamu ya nne, al maarufu utawala dhaifu
ndipo tunapoona sasa nyufa za udini, chama cha mapinduzi baada ya kuona kina face fierce opposition, kilitumia mbinu mbalimbali ikiwamo ya udini, kilinadi sera za udini kama vile mahakama ya kadhi na kutumia kete ya upadri wa Dr Slaa kuwahadaa waislamu wasimchague,
Kwenye suala la kuhusu kuchinja vitoweo, ni serikali ambayo imeshindwa kusimamia katiba ya nchi kwa sababu za udini, inayoleta machafuko na kuishia kumung'unya maneno, pale inapotakiwa kutoa msimamo. Kwa nini sasa kama kweli unaipenda Tanzania usiseme ukweli kwamba serikali ndio chanzo chakuchochea vurugu kwa kutoa amri kinyume cha katiba?(kuzuia wakristo kuchinja vitoweo), na badala yake una intend kuitetea?
 
Mkuu sana Logo, japo nimecheka kwenye sukariii, chumvii na kisha chunguu,(teh, teh, teh)lakini avha tuendelee,
Watanzania hawana tatizo kabisa kuhusu kulinda amani ya nchi yao, wamekuwa wavumilivu mno hata kwa kutowajibika kwa serikali kwa nia tu ya kulinda amani ya nchi yao iliyoasisiwa na muasisi wa taifa letu Mwalimu JK Nyerere,
Kwa mfano kuhusu suala la udini kwa sasa, Tanzania ilikuwa shwari mpaka ulipoingia utawala wa awamu ya nne, al maarufu utawala dhaifu
ndipo tunapoona sasa nyufa za udini, chama cha mapinduzi baada ya kuona kina face fierce opposition, kilitumia mbinu mbalimbali ikiwamo ya udini, kilinadi sera za udini kama vile mahakama ya kadhi na kutumia kete ya upadri wa Dr Slaa kuwahadaa waislamu wasimchague,
Kwenye suala la kuhusu kuchinja vitoweo, ni serikali ambayo imeshindwa kusimamia katiba ya nchi kwa sababu za udini, inayoleta machafuko na kuishia kumung'unya maneno, pale inapotakiwa kutoa msimamo. Kwa nini sasa kama kweli unaipenda Tanzania usiseme ukweli kwamba serikali ndio chanzo chakuchochea vurugu kwa kutoa amri kinyume cha katiba?(kuzuia wakristo kuchinja vitoweo), na badala yake una intend kuitetea?

nimefurahi umeongea pointi ya nguvu sana! Ila hii serikali sidhani kama itatusaidia mpaka hili tatizo litatulike labda kama Dr. W Slaa atakuja kuwa Rais hapo sawa! Ila waliomo saivi.......
 
nimefurahi umeongea pointi ya nguvu sana! Ila hii serikali sidhani kama itatusaidia mpaka hili tatizo litatulike labda kama Dr. W Slaa atakuja kuwa Rais hapo sawa! Ila waliomo saivi.......
Hili suala mimi sioni kama ni gumu kulitatua, unless kama serikali inanufaika na mgogoro, najiuliza, kwanini wasichunguze hata nchi zingine wanafanyaje?, Kwa sababu tumezoea kukopi nchi za magharibi tujiulize kwa mfano, Uingereza wanafanyaje?, Wakristo hawaruhusiwi kuchinja?, kama wanachinja je, waislamu wa UK wanakula vibudu?, so simple,
Serikali ikitamka rasmi kama enzi za mzee ruksa kwamba ni ruksa kwa mtu yeyote kuchinja kitoweo bila kujali imani yake, itakuwa ndio mwisho wa vurugu, maana baadhi wanapata nguvu ya kufanya vurugu baada ya kugundua kuwa serikali inakigugumizi.
 
Watanzania tumekuwa tukishuhudia matukio kadhaa ambayo kwangu mimi ni upandaji wa mbegu ya uvunjifu wa amani ambao matokeo yake sidhani kama watu wengi tunafahamu.

Tukiachilia mambo mengi ambayo yapo Mahakamani ambayo nisingependa kuyaongelea hapa...tujikumbushe matukio ya Dr. Ulimboka, Mwangosi, Rushwa Barabarani, Rushwa za ukwepaji wa Kodi, Rushwa Hospitalini, Rushwa Mahakamani,Kero za kupata huduma katika ofisi za umma ikiwemo urasimu kwenye ofisi kama Nssf na nyinginezo za jinsi hiyo, mishahara ya walimu na watumishi wengineo wa ngazi za chini, upendeleo katika ajira, ukosefu wa ajira, kurithisha wanafamilia katika mifumo nyeti ya serikalini, vyama vya siasa, taasisi za fedha,ufisadi mkubwa na wa wazi bila wahusika kuchukuliwa hatua zinazofaa kisheria, ugomvi na malumbano yasiyo na tija Bungeni, watoto kufeli kidato cha nne na kadhalika (wadau wataongeza hapa chini kwenye michango yao) ni vema viongozi wetu wakafahamu kuwa wao ni chanzo muhimu sana cha kuelekeza jahazi la nchi yetu kuelekea tusikotaka kwenda.


Nilikua naangalia chombo kimoja cha habari na nilimuona Mzee wetu Reginald Mengi akiwaasa waandishi wa habari waache kushabikia mambo ambayo yanaweza kuleta uvunjifu wa Amani. Yeye kama mzalendo na muwekezaji sikuwa na shaka yoyote ile nilipomuona akifanya hivyo. Tatizo langu siku zote wakati midahalo ya Amani imekuwa ikihubiriwa sijawahi sikia mtu akisimama kwa ujasiri akiainisha vyanzo vya uvunjifu wa amani na kuanza kutupia lawama vyombo vya habari ama waandishi wake.


Kujisahau kwa viongozi wetu kushughulikia kero hizi ama ni kwa makusudi ama ni kwa kutokuwa na uwezo wa kuongoza kunaipeleka nchi pabaya. Inasikitisha kuona wazi wazi kabisa miaka miwili kabla ya uchaguzi wa wabunge na Kiongozi wa juu wa nchi kuanza watu wameanza siasa za makundi, fitna na ninashawishika pia kuwepo kwa mipango mikubwa ya kifisadi ya kukusanya fedha ama kwa hiari au lazima ili kuingia madarakani. Hii nia aibu kubwa kwa taifa kwa sababu wananchi wa kawaida tunapata shaka kubwa kuwa madaraka yanayokimbiliwa kwa nguvu namna hiyo nini maana yake achilia mbali waliopewa sumu nakadhalika.


Tunapopiga kelele kuhusu amani tusipoteze muda, tuwaweke bayana waziwazi watu wa jinsi hiyo ili wasiwe sehemu ya watu katika jamii wanaoheshimika. Ni vema pia viongozi wetu wakafahamu pia kuwa kwenye njaa hakuna amani.


Kuijenga nchi yenye amani si kitu cha lele mama na kama inafikiriwa ni rahisi kiasi hicho wakafanye ziara zao Somalia watajifunza Mengi kuliko kuelekea mabara ya Ulaya.

Wakuu naomba kutoa Hoja!!!
 
Back
Top Bottom