Leo ni tarehe 5 na hakuna kinachoeleweka kuhusu mishahara ya wafanya kazi.Serikali kupitia raisi Kikwete ilitangaza kwamba ifikapo tarehe 26 ya kila mwezi wafanyakazi watakuwa wameshapata mishahara yao.Inashangaza kwamba mpaka leo wafanyakazi hawaja pata mishahara yao na serikali imekaa kimya kabisa kuhusu swala hili.Kwa ukimya huu sisi wafanyakazi tuna kila sababu ya kuaamini kwamba kuna jambo lisilo la kawaida, baya na la aibu ambalo limefanyika au linaendelea kufanyika, ndio maana serikali inasita kutoa tamko.Serikali ikumbuke kwamba wafanyakazi ni wanadamu ambao wanahitaji kula na kunywa na kupata haki zingine za msingi kama wanadamu wengine.Kuwa-nyima mishahara yao ni kuwanyima haki hizo kama wanadamu.Inashangaza kwamba serikali inaingia kwenye mikataba ya kimataifa ya kuwalinda wanyama lakini inashindwa kuwalinda wananchi wake hata katika yale mambo ya msingi kabisa.Katika hili naomba vikundi vya haki za binadamu viingilie kati kuishinikiza serikali iwalipe wafanyakazi mishahara yao,na kisha itoe tamko juu ya kile kilichotokea.Mwisho tunaitaka serikali ituombe radhi.